Chama cha Wananchi CUF chaweka Historia kwa Kumchagua Katibu Mkuu Bi Husna Mohamed Abdallah

Chama cha Wananchi CUF chaweka Historia kwa Kumchagua Katibu Mkuu Bi Husna Mohamed Abdallah

Boveta

JF-Expert Member
Joined
Jul 23, 2019
Posts
3,174
Reaction score
3,804
Chama Cha Wananchi CUF jana kupitia Baraza Kuu la Uongozi lilimchagua Bi. Husna Abdallah kuwa katibu mkuu wa chama hicho.

Hivyo katika medani za siasa hapa Tanzania, Bibi Husna anakuwa ndio Mwanamama wa Kwanza kushika nafasi hiyo lakini pia hii inaonyesha jinsi Chama Cha Wananchi (CUF) kilivyo na uwazi inapotokea mwanachama mwenye sifa anapotaka kugombea nafasi yoyote.

Aidha Bi. Husna alishinda kwa kura 19 wakati mpinzani wake ndugu Ali Abarani alipata kura 11.
Chama cha Wananchi (CUF) kimedhamiria kufanya mambo makubwa katika Uchaguzi ujao wa Uraisi, Wabunge na Madiwani October Mwaka huu.​
 
Kipo hiki chama?
Aisee,niliisha kisahau.
 
Chama Cha Wananchi CUF jana kupitia Baraza Kuu la Uongozi lilimchagua Bi. Husna Abdallah kuwa katibu mkuu wa chama hicho.

Hivyo katika medani za siasa hapa Tanzania, Bibi Husna anakuwa ndio Mwanamama wa Kwanza kushika nafasi hiyo lakini pia hii inaonyesha jinsi Chama Cha Wananchi (CUF) kilivyo na uwazi inapotokea mwanachama mwenye sifa anapotaka kugombea nafasi yoyote.

Aidha Bi. Husna alishinda kwa kura 19 wakati mpinzani wake ndugu Ali Abarani alipata kura 11.
Chama cha Wananchi (CUF) kimedhamiria kufanya mambo makubwa katika Uchaguzi ujao wa Uraisi, Wabunge na Madiwani October Mwaka huu.​
Kwa kweli wanastahili pongezi. Wakicheza karata zao vizuri watapata wabunge na madiwani wengi zaidi katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu.

Amandla...
 
Hamna chama hapo.
Labda "chama" kama kikundi cha watu wanaokunywa pombe pamoja kilabuni.
 
Back
Top Bottom