Chama gani cha upinzani Tanzania angalau kina sera na uelekeo wa kuaminika kwa sasa?

Chama gani cha upinzani Tanzania angalau kina sera na uelekeo wa kuaminika kwa sasa?

Tanzania kuna vyama vya kisiasa zaidi ya 20 vyenye usajili wa kudumu. hata hivyo, vipo zaidi ya hivyo vyenye usajili wa muda kwa mujibu wa sheria ya vyama vya siasa...

Je, ni kipi kwa maoni yako,
miongoni mwa vya vyama vya siasa vya upinzani, chenye usajili wa kudumu, ambacho kipo hai, chenye muundo imara na mzuri wa kitaasisi, chenye uongozi unao eleweka kwa awamu, chenye katiba nzuri, chenye wanachama wengi zaidi ya mashabiki, chenye sera nzuri mbadala, chenye mikakati ya kuvutia wananchi, chenye mipango na uelekeo wa chama cha upinzani kweli, na ambacho angalau kina aminika kwa wananchi kwa sasa?

kitaje na useme kidogo kwanini hicho 🐒
Mbona sera zenu zimeshindwa kuinua kipato cha mtu mmojammoja? Mnanikumbusha kuhusu ukahaba
 
Mbona sera zenu zimeshindwa kuinua kipato cha mtu mmojammoja? Mnanikumbusha kuhusu ukahaba
sera za chama gani cha upinzani zimeshindwa kuinua kipato cha mtu moja moja, gentleman?🐒
 
Sijakiona chama chochote cha kutuvusha na kutupeleka kule tunakotaka kwenda..wote wapo kufaidisha matumbo yao
kwahiyo unataka kusema wapinzani wapo wapo tu, hawajui wanataka nini au wanaelekea wapi, right?🐒
 
CHADEMA ilimeremeta na inameremeta na itaendelea kumeremeta mpaka mwisho wa dunia kwa sababu ilianza na Mungu,na inalindwa na Mungu japo ccm,vyombo vya ulinzi na usalama pamoja na machawa wanapambana usiku kucha kila siku kuivuruga lakini nuru yake bado inawaka na Mungu ataendelea kuilinda CHADEMA kwa sababu inaamini katika WATU walioumbwa kwa mfano wake na haiamini katika Mapinduzi kama jirani zao wanavyofanya kizuri kinakuwa kibaya na kibaya kinakuwa kizuri.Chama cha dhuluma,utapeli,ujambazi,rushwa na kuishi kwa kutegemea watawala.
licha ya kwamba bado wanaendelea kugawanyika na kuvurugana miongoni mwao, wao kwa wao lakini bado wapo tu, right?🐒
 
Sera ndio zingekuwa zinatoa uongozi kwa chama, tungeongelea sera kama kigezo Cha wananchi kukubali chama fulani. Lakini kwa hizi chaguzi za kishenzi unawezaje kuongelea sera kama kipimo Cha chama kukubalika na wananchi?
gentleman 🐒
uchaguzi tutaongelea siku ingine kwa kirefu,
ni chama gani cha upinzani nchini angalau kina sera na walau mipango inayoweza kuvutia na kubeba matumaini ya wananchi?🐒

usiogope wala usione aibu kutaja, be free kamanda 🐒
 
Hana anachojua huyo.Ushabiki tu.

sera za chama gani cha upinzani zimeshindwa kuinua kipato cha mtu moja moja, gentleman?🐒
You can implement national policies with working government machineries even companies and other organizations have policies but national policies are intended to support welfare of the citizens
 
Back
Top Bottom