Chama kikiwafukuza Wabunge Viti Maalum CHADEMA itakuwaje?

Chama kikiwafukuza Wabunge Viti Maalum CHADEMA itakuwaje?

Kwani wamepishwa bila wenyewe kuwepo je wenyewe wanasemaje je mwenyekiti anasemaje!
Mwenyekiti tayar ashapewa deposit ya kiasi kadhaa cha pesa ili awasimamie hawa kina dada. So Mnyika, Lisu na magenge yao humu JF wanajisumbua na kupoteza muda wao bure sabab mwkt ameshaamua iwe na itakuwa
 
Mwenyekiti tayar ashapewa deposit ya kiasi kadhaa cha pesa ili awasimamie hawa kina dada. So Mnyika, Lisu na magenge yao humu JF wanajisumbua na kupoteza muda wao bure sabab mwkt ameshaamua iwe na itakuwa
Wewe unasema tunapoteza muda.....hao Mdee na group lake wameua tayari mambo yote waliofanyie chama na nchi kwa ujinga mmoja tu
 
Mfalme Sulemani, anayesadikiwa kujaliwa akili nyingi kuliko watawala wote waliowahi kuishi alisema, "Mwenye kutawala akisikiliza uongo; Basi watumishi wake wote watakuwa waovu." Mithali 29:12.
 
Bunge na mfumo mzima wa uongozi wa serekali ya Tanzania wanawahitaji wabunge wa CHADEMA kuliko wanavyomuhitaji Magufuli na ndiyo maana mpaka Nusrat ameenda kuchomolewa mahabusu katika kesi isiyokuwa na dhamana
Chagua moja jela au ubunge.Ujasiri pekee wa kuendelea kukaa jela anao Jesus alone
 
Walipovunjwa mikono na askari magereza kwa kipigo haukuwa unyanyasaji?Wanafiki wakubwa nyie.
Wangevunjwa mikono halafu wakapata uwezo wa kusaini kwa ule wino mbele ya sipika?? Acha unyanyasaji wa kijinsia, na wivu ulionao mke wako ataendelea kuuza chipsi pale shule msingi adi uzeenii. Mumewakomalia tuuu wake za watuuuu, oneniii aibuuuuu.
 
Chadema inapofuata katiba yake kutoa maamuzi yoyote yale haijawahi kujiuliza itakuwaje , bali wengi waliowahi kutimuliwa na Chadema waliishia kudharauliwa hata na mifugo yao
 
Wee kapuku hujui kitu kuhusu Chadema , masikini mkubwa wee !
Makamanda halisi wameshaa apaa, wake zenuuu wamekosaa, njoooniii kijiweni makapuku na umbwe na we we uwemooo. Kwakua wakee zenu hawamo baada ya nyie kugaragazwaa sasa mnatapatapa
 
Habari wanajamvi.

CDM kupitia KM wao wanasema hawakupeleka orodha ya majina ya Wabunge wa viti maalumu NEC. Tumeshuhudia Wabunge wateuliwa wa viti maalumu 19 wakiapishwa.

Tetesi ni kwamba Bunge linalazimisha uwepo wa kambi rasmi ya upinzani Bungeni ili wapate pesa kutoka kwa wahisani wetu Triliioni 2. Bila hizo pesa inasemekana Bunge litakuwa kapuku, Wabunge wataishi kama Walimu na huenda wakaibana serikali kisawasawa.

Sasa najaribu kujiuliza maswali ambayo nayaleta kwenu tujiulize kwa pamoja.

CDM wakiweka ngumu na kuwafukuza uanachama hao wateule 19 ambapo kisheria watakuwa wamepoteza uhalali wa kuwa Wabunge. Je, Bunge na serikali watafanya nini ili kunusulu hizo Trillions za pesa zisipoteee?

Wanaweza kufukuza Wabunge kadhaa wa CCM ili warudi kwenye uchaguzi na kuielekeza tume iwapitishe wapinzani kuwa Wabunge?

Je, huu uhusiano wa kambi rasmi ya upinzani Bungeni na msaada wa hayo mapesa haukujadiliwa kabla ya uchaguzi? Walijisahau au walishindwa vipi hata kupitisha Wabunge kadhaa hata wa chama kingine tofauti na CDM ili wakaunde kambi rasmi ya upinzani. I think it was simple Technic kuliko sasa hivi tunapoonekana watu wasiostaarabika.
Ccm ulifanya uchafuzi na madudu Sana uchaguzi huu hivi hawakujua hayo
 
Badala ya kulalamika na kutukana na vilevile waandishi wetu kuogopa na kukaa chini sisi...Tumefanya utafiti mdogo kwanini ghafla Bunge na mfumo mzima wa uongozi wa serkali ya Tanzania ghafla wanawahitaji hao wabunge wa CHADEMA.

MASHARTI YA PESA TOKA NJE (DONORS)
Kama mnaelewa bunge letu hakuna pesa la kuliendesha na ndo maana kuna wabunge tumesikia wamelalamika hawajapewa pesa za magari. Kwahiyo Bunge linahitaji pesa toka nje na wameandika maombi kwa donors wao wakubwa na wameletewa mashariti madogo ili hiyo pesa ipatikane.

Diversity and Inclusion in Tanzania Parliament
Pamoja na demokrasia mbovu iliyozaa hilo bunge,Donors wamesema wanaweza kutoa hizo pesa kama tu shariti la bunge kuwa diversity and inclusivity (sijapata maneno mazuri kwa Kiswahili).Bunge diversity and inclusivity kwa mujibu wa donors ni Bunge lenye;

1.Wabunge toka vyama mbalimbali vya kisiasa

2.Wabunge wanawake toka vyama mbalimbali vya kisiasa au makundi ya kijamii.

Bunge la Tanzania linatakiwa kukizi 4 protected characteristics kati ya 9 za kawaida ambazo ni 1.Age 2 gender 3.sex orientation na 4 disability

JOB NDUGAI
Huyu anaelewa kinachoendelea na anautaalam mzuri wa mabunge ya madola na Zaidi zaidi anazihitaji hizo pesa kwa nguvu zote ili kuendesha bunge na anawahitaji kwa nguvu zote wale wanamama wa chadema ili kutiki box zote za mashariti ya pesa,sasa ni rafiki mzuri sana wa Halima Mdee.

HALIMA MDEE
Huyu ni muhimu sana kwa Ndugai na mfumo mzima kwasababu yeye anaweza kutiki box zote hapo juu.
Mkuu wakati u dhalimu ule ukifanyika hawakuona consequences zake?!Wasomi wote washauri wa system hawakuepo? Kule kwetu kuna watu huitwa "Abhasololi " je Serikali haina watu Hao mpaka tufikie sarakasi hizi za aibu? ° hakna jambo ambalo katika siasa halina umuhimu. Mnaposema maendeleo hayana vyama mpaka mkarigg election kwanini sasa vyama vimeonekana vinaumhim bungeni?Wasomi tunaowaita Prof kweny system hamuoni mnasalit nchi kukwepa wajibu wenu wa kushauri ya kesho??

Sent from my SM-G920F using JamiiForums mobile app
 
Mkuu wakati u dhalimu ule ukifanyika hawakuona consequences zake?!Wasomi wote washauri wa system hawakuepo? Kule kwetu kuna watu huitwa "Abhasololi " je Serikali haina watu Hao mpaka tufikie sarakasi hizi za aibu? ° hakna jambo ambalo katika siasa halina umuhimu. Mnaposema maendeleo hayana vyama mpaka mkarigg election kwanini sasa vyama vimeonekana vinaumhim bungeni?Wasomi tunaowaita Prof kweny system hamuoni mnasalit nchi kukwepa wajibu wenu wa kushauri ya kesho??

Sent from my SM-G920F using JamiiForums mobile app
Uchafuzi siyo mpango wa kitaasisi bali ulikuwa mkakati wa dharura ulioratibiwa na vyombo. Inavyoelekea mpango huu dharura uliandaliwa kuadhibu ma kukomesha uhuru uliopitiliza uliojitokeza wakati wa kampeni. Jambo kubwa kwa vyombo vyetu ilikuwa kuondoa upinzani na kung'oa mbegu yote iliyopandwa wakati wa kampeni. Vyombo vilivyopewa jukumu la kufanilisha uchafuzi hawama weledi wa kuangalia athari za kutokuwa na upinzani na haikuwa kazi yao.
 
Chadema kukubali kupeleka wabunge wa viti maalum ni sawa na kukubaliana na zoezi zima la uchaguzi, jambo ambalo linawapa changamoto kubwa katika kufanya maamuzi. Ni vema taasisi za serikali zikajikita katika mifumo yenye uwazi mkubwa katika chaguzi zetu ili kutuepusha na migogoro ya aina hii siku zijazo..
 
Back
Top Bottom