Chama Kipya: New York Metropolitan Tanzanians Community

Mimi bado sijaelewa kwa nini mlioona umuhimu wa kutafuta baraka za baadhi ya potential members. Hamuoni kwa kufanya hivyo mmeishaanza kuweka tabaka za wale walio muhimu kwa chama na wanachama wa kawaida? Kwani Chama kingeathirika vipi kama pasingekuwepo hizo baraka? Kwa kufanya mlivyofanya mnampa uwezo huyo aliyowapa baraka kuweza kuondoa baraka zake. Kitu muhimu katika chama chochote ni wanachama wake wote kuwa sawa bila kujali nafasi zao, uwezo wao wakipesa, umri wao, jinsia yao n.k. Kwa kufanya mlivyofanya mnaonekana kuwa bado mnakumbatia imani ya ki-imla ambayo kwa kiasi kikubwa imetufikisha hapa tulipo.

Amandla......
 
- Ahsante sana ndugu kwa ushauri wako mzito sana, ndio maana tukaja hapa kwenye Great Thinkers ni ili kupata ushauri mzito kama huu wako.

Ahsante.

William.
Malecela,
Magnificent responce to some artful contrieved and provocating arguments.

However, we ought not to forget that the last time NYokers tried to form an association, the move failed due to some elements of tribalism.

What I am seeing in this new movie, is an effort to make sort of gov/CCM contolled association led by the same names we meet at the embassy or their associates.
  1. Can't the Tanzanians form an association that is not influenced by those in power?
  2. Kwa nini watu wa ubalozini wasiondolewe kwenye kuongoza hiki chama?
 
KJ ru serious?Unaweza kutuhabarisha ilikuwa vipi?Mkuu Malecela vipi kuhusu huo ukabila,bado upo ama nao umebarikiwa mkuu?
 



Mkuu,
Kama unashindwa kuelewa maana ya alama mbali mbali katika lugha,sasa nikuelewe vipi.

Kwa kukuelewesha tu...Alama ? =alama ya kuuliza(qstn mark)

Alama !=Mshangao

So mimi sikushangaa bali niliuliza maana ya maneno niliyo-quote frm your post.Maanake nilitaka kueleweshwa.Acha kukurupuka mkuu,una safari ndefu sana kama huelewi hata tofauti ya alama ndogo kama hizo.Sitaki kubishana na wewe,lol
 

Kama hutaki kubishana unachofanya ni nini?Acha ligi za mchangani wewe,unatoa wapi muda kuandika upupu?Unapojibu post nzima kwa questions mark siwezi kujua nini haswa unachouliza,mbona unaweweseka bila sababu?
Sina muda mchafu FYI
 

- so far wazee wote waliokuwa consulted ni watu mahiri sana katika proffesionals zao ambazo zinagusa uanzishwaji wa chama, uongozaji wa chama na uimarishaji wa chama, sasa unapoanza kulima mahindi ni shurti uende kwanza kwa walima mahindi kupoata ushauri na dnio hasa alichokifanaya Mwenyekiti wa muda Ndugu Khajim, kupata ushauri wa waliobobea na hizo fani kwanza, ndio baadaye ashukle kila kunakotakiwa.

Ahsante Sana.


William : CO na msemaji wa chama (Interim).
 

- Mwenyekiti wa muda Khaji ni anatokea visiwani, mimi ninatokea Dodoma, katibu mkuu anatokea Kigoma, katika viongozi wote wa muda tulionao hakuna mfanyakazi wa ubalozi wowote uwe wa nchi au nyumba kumi kumi na wala hakuna influence ya yoyote kutoka anywhere, unless kama unawafahamu unaweza kuwasema kwa majina yao ili tuweze kujiangalia ndani ya chama chetu kama wapo bila sisi wenyewe kujua. Ya chama cha zamani hayatuhusu sisi tunajali chama cha sasa.

Ahsante Sana.


William.CO
 

Vipi kwa wale ndugu zetu waliojilipua wanaoishi NY, je wanayo sifa ya kuwa wanachama?
 

Bado Mkuu haujanijibu. Kutafuta baraka na ushauri ni vitu viwili tofauti. Halafu inabidi mtambue chama chenu kiko katika context tofauti na zile ambazo hao wazee mahiri walipata uzoefu wao. Mngeanzisha chama alafu muwakaribise wachangie kama wanacama wengine. Kujaribu kukamilisha kila kitu kabla hata chama chenyewe hakijaanzishwa ndiyo mwanzo wa kukosa transparency. Maamuzi yote muhimu ilibidi na inabidi yafanywe kwa uwazi na ushirikiswaji wa wanachama. Hivi vikao vya ushauri vya jikoni ndiyo mwanzo wa kuwafanya wanachama wakose imani na nyie viongozi wao.

Amandla......
 

- Tumekwenda kwa wazee kama tulivyokuja hapa Jf, principle ni ile ile kutafuta ushauri, haina maana kwamba kwa vile tumekuja hapa JF sasa hiki chama kitakuwa na mkono wa JF hapana, kila tulikokwenda na tunakokwenda sasa hivi na hapa tulipo yaani JF, tunachotafuta ni ushauri, mawaidha na mawazo na hasa kutoka kwa pros wa mambo ya vyama.

- Kuja kwetu hapa JF hakukifanyi hiki chama kuwa na influence ya JF katika uhai wake huko mbele ya safari na wala sio kukosa transparency, isipokuwa ni simply kutafuta ushauri tu na mkuu ni matumaini yangu kwamba utajiunga na hiki chama ni chama cha kila mwananchi.

Ahsante Sana.


William : (CO).
 

- Mkuu maneno mazito sana haya, sasa vipi ukitoa ushahidi kwamba chama kina watu wa ubalozi ukiwataja wka majina utasaidia sana, na kama huna ushahidi ni vyema ukaomba radhi kwa kuwa mzushi!

Respect.


FMEs!
 
Ningependa kujiunga na hiki Chama,ingawa sasa hivi sipo New York. Kwa hiyo tafadhali niweke katika orodha ya wanachama,mimi Andrew Nyerere.
 
Hiki ni chama au jumuiya? Kama ni jumuiya naomba kujiunga. Ila kama ni chama mimi simo!
 
Ningependa kujiunga na hiki Chama,ingawa sasa hivi sipo New York. Kwa hiyo tafadhali niweke katika orodha ya wanachama,mimi Andrew Nyerere.

- Ndugu yangu vipi ulifika salama sana safari yako ya kurudi nyumbani? Unakaribishwa sana kujiunga mambo yatakapokuwa tayari sasa hivi bado tuko kwenye awali za kuanzishwa lakini karibu sana ndugu Andrew.

Ahsante.

William. (CO)
 
Hiki ni chama au jumuiya? Kama ni jumuiya naomba kujiunga. Ila kama ni chama mimi simo!

- Unaona sasa ndio maana tulikuja hapa kwenye wazoefu wa hizi shughuli, binafsi sikujua tofauti maana nllipoona neno Community kwenye jina la chama nilifikiri lina-present Jumuiya na kwa kawaida tumezoea kuita Community kuwa ni chama ingawa ninaamini ni Jumuiya, ahsante kwa marekebisho mkuu hii ni Jumuiya, tunaita chama kwa sababu ya mazoea tu, na karibu sana mkuu tutahitaji sana kuwa na viongozi wenye upeo wa juu sana kielimu kama wako.

Ahsante.


William. (CO)
 
- Mkuu Kubwajinga bado tunasubiri ushahidi wako kwamba hii Jumuiya ina ubalozi ndani yake, toa ushahidi mkuuu maana hapa kila kitu kiko wazi! kama huna kubali kwamba ni mzushi!

Respect.

FMEs!
 

Mwanajumuia, kuna mawili matatu ya kujifunza kutoka kwenye jumuia hii ya Watanzania huko Edinburgh, Uskochi: http://www.tzeca.org.uk/
 
Kama hutaki kubishana unachofanya ni nini?Acha ligi za mchangani wewe,unatoa wapi muda kuandika upupu?Unapojibu post nzima kwa questions mark siwezi kujua nini haswa unachouliza,mbona unaweweseka bila sababu?
Sina muda mchafu FYI


Mhhh,Let me ignore you kwa maslahi ya huu mjadala na wachangiaji wake.

Kama hujui tofauti ya (?) na (!) ,ni dhahiri huna tija hapa ktk debate
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…