Chama na Onyango Watafute Timu, Msimu Ujao Hatuwataki

demigod

JF-Expert Member
Joined
Jan 2, 2015
Posts
8,292
Reaction score
15,250
Kuna wachezaji Klabuni kwetu wana mikosi. Onyango ndio kila akipewa pasi mapigo ya moyo yanakimbia mithili treni ya SGR.

Onyango ataendelea kutu-cost kwenye mechi kubwa siku zote mpaka pale atakapo fariki.

Yes tunampenda Chama ila tukubali ukweli kuwa dogo hamfikii mchezaji kiungo wa Utopolo (Aziz Ki). Aziz anafunga bao la kuwapeleka Uto robo, huku Chama anakosa penati.

Tutafute namba 10 mwingine, ikiwezekana tumvute Feisal Salum.

Hata hivyo, licha ya kukosa penati jamaa ni mzito sana, hata ukimbiaji wake wakati wa kaunta ataki ni kama ana majipu kwapani.

Boss MO avunje benki msimu ujao aondoe hawa.
 
🤣🤣🤣🤣🤣🤣😂😂
 
Sina deni Simba wamepambana kiasi Fulani ref.. amechangia kupoteza wachezaji hadi Muda Fulani wakifika kwenye 18 wanaogopa kumkaba mpinzani.
 
Unajisikiaje pale unapokuwa shabiki wa Yanga hlf unaiandikia Simba kwamba ifanye jambo fulani, huwa hauoni aibu?
 
Kwakweli simba inapaswa tufanye usajili wa maana bora twende congo hapo kuna wachezaji wazuri sana..na bei nzuri tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…