Pre GE2025 Chama Tawala na Vyama vya upinzani vimeshindwa kutuletea mabadiliko na ustawi. Wananchi tufanye nini?

Pre GE2025 Chama Tawala na Vyama vya upinzani vimeshindwa kutuletea mabadiliko na ustawi. Wananchi tufanye nini?

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Tuwarudishe wakoloni (Mabeberu) direct waje waendeleze pale walipoishia,

Ni afadhal mara 100 tutayaona maendeleo ya kweli kuliko hawa watawala wa kiafrica waganga njaa.

Sio chama tawala wala upinzani watakaoleta maendeleo ya kwel africa wote ni wale wale tu.
 
Endelea kuwanyeyekea wanasiasa, wana siasa wakuletee ajira? haohao wanasiasa ndo wanakaa bungeni kusema kiswahili kitumike kufundisha shuleni wakati watoto wao wanasoma nje ya nchi, ndo unawategemea? achana na mawazo ya nchi kuuzwa umeshasikia nchi gani imeuzwa? kama Mungu amekupa ajira, fanya kwa bidii kwa ajili ya kizazi chako, hata usipokuwepo watajua uliwapigania, Hao hao wanasiasa wanakuambia jiajirini wakat wao wanapigania hizo ajira hata kwa kuroga. Amka usingizini

Hao wanasiasa hawana msimamo kila kukicha kila mtu anapigania tumbo lake. Yesu mwenye alisema "enyi wanawake wa Yerusalem jililieni ninyi na watoto wenu"
Una kiwango cha chini mno cha uelewa, Marekani Serikali ndio inatengeneza ajira sembuse Tanzania? Hizi akili Mavi mnazitoga wapi?

Unajua kwa nini Serikali inakusanya kodi? nyie ndio wale huduma za haki yenu mnapata kwa kupiga magoti au kuhonga make hakuna mnacho kijua.

Pia rambua Siangalii kama mimi nina ajira pia naumia kuona wengine hawana ajira, nina uwezo wa kkujitibu ila naumia kuona watu wanavyo kosa huduma ya Afya. Taifa limejaa wajinga sana.

Nyie ndio wale mnafurahisa sana shida za wenzenu, nazani ukiona wenzako hawana ajira unafura sana.

Mwisho tambua ni jukumu la Serikali kutoa huduma za afya kwa raia wake, kutoa ajira kuhakikisha raia wake wana ajira.

Okay umejiajiri, unazani kama kundi kubwa halina ajira huo ujasiriamali wako utawauzia wakina nani? Kama kundi kubwa halina afya wataweza kuzalisha ili kuwe ba mzunguko wa pesa?

Huna unacho jua na hii ni coment ya mwishi kwako.
 
Nimekuwa nikifuatilia mwenendo wa chama tawala CCM na pia Vyama vya Upinzani, nimegundua hakuna chama kinachoweza kutuletea mabadiliko ya kweli. Matokeo yake akina Msigwa,Mwita Waitara,Prof Mkumbo, Mashinji, Gekul, Kitambi nk kuhama na kutafuta maslahi binafsi zaidi. Upande wa pili CCM inatafuta kila njia ya kutumia kodi za wananchi kwenye mambo yasiyo na maslahi ya wananchi zaidi ya kufuja raslimali za nchi na kujinufaisha wao wenyewe. je tufanye nini sasa iwapo upinzani ni tatizo na Chama Tawala tatizo. Tukimblie wapi.Nisaidieni kupata suluhisho na mwafaka.
Ulitaka vyama vya siasa vije vikushikie jembe vikakulimie ukiwa umekaa hapo nyumbani unaangalia tv ya baba yako.

Umezungukwa na mito ya maji na shamba kubwa la baba yako? Bashe akitangaza mbolea ya ruzuku uko bize kubeti. SGR inaisha, hujiulizi utakuwq unapeleka nini Dsm kibiashara
 
Na ndio ujinga mkubwa, et utegemee wanasiasa.

Kuna kijiji nimekipenda huko Rukwa, wao kwenye shughuli za kujenga madarasa kwa ajili ya watoto wao, kila mwanakijiji anachangia tofali 200, na fedha taslimu, yaani wameamua kujipambania wenyewe, ukingoja mwanasiasa atapika mboyoyo tu
Ni wajimga hao kama wewe, Unajua ni pesa kiasi gani zinapotea kwa ufisadi? usha ona wanasiasa wanatoa pesa hata za kukimbiza mwenge?

Hao wanao changa wanalipa kodi au hawalipi kodi? nini kazi ya kodi wanayo lipa? Kuchangia shughuri za maendeleo ni ujinga mkubwa sana labda kama watu hawalipi kodi.

Pia Tambua hao hawachangi kwa hiari wana lazimishwa na serikali ya kijiji na asie changa anakamatiwa hadi kuku.

Taifa la Mazezeta wanachangishana huku watawala wakitembelea magari ya milion 600, ujinga hautaisja nchi hii kamwe.Watawala wanaishi kwa anasa wajinga wanachangishana.
 
Back
Top Bottom