Changamoto gani utakutana nazo kwa kuoa au kuishi na Mwanamke mwenye mtoto?

Changamoto gani utakutana nazo kwa kuoa au kuishi na Mwanamke mwenye mtoto?

Ujue namimi najiuliza kama wewe, haya mambo yanaendaje? Ndiyo maana nikakuuliza ingekuwa ni wewe ungemuacha mtoto wako mazima kwa mwanaume mwingine? I wish tungepata ka-testimony

Paragraph ya mwisho imeniwazisha mweeh. Imagine baba mzazi ana ndoto za mtoto wake asome Feza labda, afu mama alipoolewa kule baba uwezo wake ni St Mary's maybe; ndiyo yale kila mtoto atakwenda shule kutokana na uwezo wa baba yake au? Mind you yule ni mtoto wake, ana ndoto juu ya mtoto wake na ana uwezo wa kuzitimiza; je azikatishe na kukaa chonjo kisa mtoto anaishi kwenye paa ya mwanaume mwingine? (Naongelea kwenye situation ambazo maybe ni salama zaidi mtoto kukaa na mama, imeshindikana kukaa na baba). Au kwa single mom with multiple baby daddies, na kila baba anahudumia mtoto wake kwa uwezo wake.

Mtazamo wangu upo hivi kulingana na scenarios tofauti tofauti, sijui kwa wengine...

1. Nikiamua kuoa mwanamke ambaye ni single mom, basi hata mwanaye/wanaye watakuwa chini ya himaya yangu kwa kila kitu...

2. Endapo mimi ni mwanaume niliyemzalisha mwanamke na mwanamama huyo akaolewa na mwanaume mwingine, nitamfungulia mtoto akaunti na hela yake nitaweka huko. Akiwa mkubwa atakutana nayo...
 
Teenagers ndiyo wenye kiburi cha kusema sioi/siishi na mwanamke asiye na mtoto, kwakua wana uhakika wa kupata mwanamke chuchu konzi ambaye bado hajazaa.

Wanaume wenye umri kuanzia miaka 35+, ni nadra kupata mwanamke hajazaa, kwakua wanawake saizi yao wanakua wameshazaa.

Hizi kauli za sioi mwanamke aliyezaa, ni za vijana wa umri mdogo, watu wazima oeni tu mwanamke aliyezaa, hakuna namna
 
Teenagers ndiyo wenye kiburi cha kusema sioi/siishi na mwanamke asiye na mtoto, kwakua wana uhakika wa kupata mwanamke chuchu konzi ambaye bado hajazaa.

Wanaume wenye umri kuanzia miaka 35+, ni nadra kupata mwanamke hajazaa, kwakua wanawake saizi yake wanakua wameshazaa.

Hizi kauli za sioi na mwanamke aliyezaa, ni za vijana wa umri mdogo, watu wazima oeni tu na mwanamke aliyezaa, hakuna namna
Kuongea rahisi tu
 
Kwanini umuolee mwenzio mke wake?
Unaona raha kuishi katika ugoni maisha yako yote?

Vile wanaume wakipenda wanawaprotect wake zao
Hakuna anayeweza kumuolea mwanaume mwenzie mke wake labda huyo mwenye mke awe ameamua kuipoteza nafasi yake mwenyewe
 
Habari wakuu,
Hapa nakusudia mwanamke mwenye mtoto ambaye si wako, Mtoto ambaye kwa kiasi kikubwa bado anahitaji ukaribu na mama yake.

Nimeshuhudia ndoa ya Jirani yangu ikiyumba baada ya mtoto wa miaka takribani miwili na nusu au mitatu Kuletwa nyumbani na mkewe kwani wamekaa wastani wa miezi 3 bila ya mtoto huyo kuwepo.

Tatizo ninaloliona ni utundu wa huyo mtoto ambao wakati mwingine unasababishwa na kudekezwa na mama yake.

Mfano siku moja aliiburuza chini Iphone ya baba yake mlezi, akafokewa na baba huyo, Jambo hilo lilisababisha mama akasirike kwa madai kuwa baba hampendi mtoto.

Je changamoto gani nyingine za kuoa mwanamke mwenye mtoto mdogo?
kuoa mwanamke mwenye mtoto hapo kuna mawili..
1. Baba mtoto achague kutomuona tena mtoto wake na athibitishe hilo kwa baba mlezi.
2. Amchukue mtoto wake amlee yeye
 
Labda tunapishana mitazamo...

Najaribu tu kufikiri, inakuaje mwanaume ana mtoto na anaishi chini ya dari ya nyumba ya mwanaume mwingine, halafu kitu pekee anachofanya ni kutuma hela za matumizi/ada n.k

Yaani mwanaume mwingine ampe chakula, malazi na malezi, halafu baba mzazi ujifanye upo responsible kwa kutoa fedha sijui ya matumizi...

Kama mwanamke umeamua kuolewa ilihali una mtoto, ni vyema huyo anayekuoa apende ua na boga lake, hiyo itajenga heshima na kuleta maana nzima ya familia...

Hii ni sawa mwanamke umeolewa na wanaume wawili wenye majukumu tofauti

Exactly hili hua nawaeleza watu kwamba hapo ni sawa na wanaume wawili mnaendeshwa na mwanamke mmoja yaani kwako atake pesa na kule atataka pesa sasa ni either aliyemuoa ahudumie na mtoto au akuachie mtoto umlee mwenyewe na utimize majukumu yote ukiwa nae.
 
Teenagers ndiyo wenye kiburi cha kusema sioi/siishi na mwanamke asiye na mtoto, kwakua wana uhakika wa kupata mwanamke chuchu konzi ambaye bado hajazaa.

Wanaume wenye umri kuanzia miaka 35+, ni nadra kupata mwanamke hajazaa, kwakua wanawake saizi yao wanakua wameshazaa.

Hizi kauli za sioi mwanamke aliyezaa, ni za vijana wa umri mdogo, watu wazima oeni tu mwanamke aliyezaa, hakuna namna
Ukiwa huna pesa utaoa aliyezaa maana nae hana option ukiwa nazo unapata binti mbichi kabisa hata bikra unaoa.
 
Habari wakuu,
Hapa nakusudia mwanamke mwenye mtoto ambaye si wako, Mtoto ambaye kwa kiasi kikubwa bado anahitaji ukaribu na mama yake.

Nimeshuhudia ndoa ya Jirani yangu ikiyumba baada ya mtoto wa miaka takribani miwili na nusu au mitatu Kuletwa nyumbani na mkewe kwani wamekaa wastani wa miezi 3 bila ya mtoto huyo kuwepo.

Tatizo ninaloliona ni utundu wa huyo mtoto ambao wakati mwingine unasababishwa na kudekezwa na mama yake.

Mfano siku moja aliiburuza chini Iphone ya baba yake mlezi, akafokewa na baba huyo, Jambo hilo lilisababisha mama akasirike kwa madai kuwa baba hampendi mtoto.

Je changamoto gani nyingine za kuoa mwanamke mwenye mtoto mdogo?
Kuoa mwanamke mwenye mtoto ni sawa umeoa mke wa mtu.
Kumbuka ipo siku baba wa mtoto atamtaka mtoto wake je? mamaye akimpeleka mtoto kwa babaye nin kitatokea huko?

#Ushauri!
Lakin pia wanaume tupunguze kuwazalisha wanawake na kuwaacha, Kama unahisi mwanamke huyo huna malengo naye usi date nae.
 
Vile wanaume wakipenda wanawaprotect wake zao
Hakuna anayeweza kumuolea mwanaume mwenzie mke wake labda huyo mwenye mke awe ameamua kuipoteza nafasi yake mwenyewe
Mwanamke akizalishwa na kuachwa hajajiongeza...ila ukweli ni kwamba anapendwa ndo maana kazalishwa.

Afu mwanamke akishazaa hana nguvu tena kwa bwana alomzalisha....hata akiolewa na askofu bado atampelekea tu baby baba
 
Unaacha kuoa mwanamke mbichi hajazaa unaenda oa single mother kweli aisee huo ni udhaifu sababu wao ni easy to access

Achana single mother waoane na single father
 
Exactly hili hua nawaeleza watu kwamba hapo ni sawa na wanaume wawili mnaendeshwa na mwanamke mmoja yaani kwako atake pesa na kule atataka pesa sasa ni either aliyemuoa ahudumie na mtoto au akuachie mtoto umlee mwenyewe na utimize majukumu yote ukiwa nae.
Kweli binadam tunatofautiana,
Yani wakati mimi nawaza kuoa demu mwenye bikra jamaa mmoja yeye anawaza kuoa demu aliyekambwa hadi kuzaa hahahah
 
Mwanamke akizalishwa na kuachwa hajajiongeza...ila ukweli ni kwamba anapendwa ndo maana kazalishwa.

Afu mwanamke akishazaa hana nguvu tena kwa bwana alomzalisha....hata akiolewa na askofu bado atampelekea tu baby baba


Sio wanawake wote wenye watoto wamezalishwa wakaacha kilambimkwidu

Wengine wameamua kukaa pembeni baada ya kuona yule aliyeshirikiana nae kupata mtoto sio mume sahihi

Hujawahi kutana na wanawake wanadai talaka na waume zao hawako tayari kwa hilo?

Hujawahi kutana na situation ambayo mahakama inabidi isimame talaka itolewe ili kuokoa maisha ya mwanandoa?

Btw kuvunjika kwa ndoa sio kitu kizuri wala cha kupendeza ila ndoa hatarishi ni hatari zaidi ya talaka

Hayo mengine ya baby baba ni maoni yako wewe binafsi
 
Teenagers ndiyo wenye kiburi cha kusema sioi/siishi na mwanamke asiye na mtoto, kwakua wana uhakika wa kupata mwanamke chuchu konzi ambaye bado hajazaa.

Wanaume wenye umri kuanzia miaka 35+, ni nadra kupata mwanamke hajazaa, kwakua wanawake saizi yao wanakua wameshazaa.

Hizi kauli za sioi mwanamke aliyezaa, ni za vijana wa umri mdogo, watu wazima oeni tu mwanamke aliyezaa, hakuna namna

Ukikuta Mwanamke kazaa jambo la msingi ni kuongeza wako mmoja kisha unaendelea na ratiba zingine hakuna kujenga kwenye kiwanja cha mgogoro
 
Back
Top Bottom