A
Anonymous
Guest
Utoaji huduma kwa jamii unatakiwa kuwa rafiki ili kufikia malengo yaliyowekwa kwa manufaa ya TAIFA letu.
Mimi kama mchangiaji wa NHIF kuna changamoto nimeziona katika ofisi za NHIF (Chache kama sio zote).
1. Utashi mdogo kwa baadhi ya watoa huduma.
Mteja anapohitaji kujisajili/kuendelea na huduma katika utoaji wa maelekezo watoa huduma hukinzana katika viambatisho. Uliyemkuta juzi atakupatia maelekezo tofauti na uliyemkuta jana. Kwani ofisi hazina miongozo ili mtoa huduma awe anapiga chabo kama kichwa hakiko vizuri?
Mteja anajaza fomu anaziwasilisha anapatiwa ankara ya malipo analipia halafu viambatisho vikimfikia mtoa huduma mwingine zinaonekana hazijakamilika.
Kwanini muidhinishe malipo wakati viambata havijakamilika?
2. Lugha mbovu ya mawasiliano
Mara zote tunaamini mtoa huduma wa Sekta husika anakuwa na uelewa wa jambo analolitolea huduma, hivyo kutakiwa kutoa maelezo kwa lugha stahiki isiyo na mihemko.
Cha kushangaza imekuwa tofauti kwa watoa huduma wetu, wanaongea kama wamekurupushwa na mihemko juu.
3. Urejeshaji wa kadi za bima
Hapa ni kwa uongozi wa Shirika, mnatakiwa kuiga kama wafanyavyo benki katika urejeshaji wa kadi zilizopotea/kuharibika.
Tuko Ulimwengu wa digitali, kwanini kujaza jaza mikaratasi maofisini wakati taarifa za mwanachama zinaonekana kwenye mfumo?
Kama kadi imepotea ama kuharibika ina maana mwanachama alipatiwa kadi kwa kutimiza vigezo vyote, iweje muanze kurundika sijui vyeti vya kuzaliwa, taarifa ya upotevu. Yote hayo ya kazi gani? Kwanini kusiwe na Taarifa ya upotevu tu ili mhakiki taarifa za mteja wenu kupitia namba ya uchangiaji?
Haya yamebainika tawi la ILALA, bila shaka yatakuwa yanafanyika karibu ofisi zote.
Ni KERO kubwa kwa watumia huduma. Mjirekebishe.
Mimi kama mchangiaji wa NHIF kuna changamoto nimeziona katika ofisi za NHIF (Chache kama sio zote).
1. Utashi mdogo kwa baadhi ya watoa huduma.
Mteja anapohitaji kujisajili/kuendelea na huduma katika utoaji wa maelekezo watoa huduma hukinzana katika viambatisho. Uliyemkuta juzi atakupatia maelekezo tofauti na uliyemkuta jana. Kwani ofisi hazina miongozo ili mtoa huduma awe anapiga chabo kama kichwa hakiko vizuri?
Mteja anajaza fomu anaziwasilisha anapatiwa ankara ya malipo analipia halafu viambatisho vikimfikia mtoa huduma mwingine zinaonekana hazijakamilika.
Kwanini muidhinishe malipo wakati viambata havijakamilika?
2. Lugha mbovu ya mawasiliano
Mara zote tunaamini mtoa huduma wa Sekta husika anakuwa na uelewa wa jambo analolitolea huduma, hivyo kutakiwa kutoa maelezo kwa lugha stahiki isiyo na mihemko.
Cha kushangaza imekuwa tofauti kwa watoa huduma wetu, wanaongea kama wamekurupushwa na mihemko juu.
3. Urejeshaji wa kadi za bima
Hapa ni kwa uongozi wa Shirika, mnatakiwa kuiga kama wafanyavyo benki katika urejeshaji wa kadi zilizopotea/kuharibika.
Tuko Ulimwengu wa digitali, kwanini kujaza jaza mikaratasi maofisini wakati taarifa za mwanachama zinaonekana kwenye mfumo?
Kama kadi imepotea ama kuharibika ina maana mwanachama alipatiwa kadi kwa kutimiza vigezo vyote, iweje muanze kurundika sijui vyeti vya kuzaliwa, taarifa ya upotevu. Yote hayo ya kazi gani? Kwanini kusiwe na Taarifa ya upotevu tu ili mhakiki taarifa za mteja wenu kupitia namba ya uchangiaji?
Haya yamebainika tawi la ILALA, bila shaka yatakuwa yanafanyika karibu ofisi zote.
Ni KERO kubwa kwa watumia huduma. Mjirekebishe.