Changamoto wakutanazo wakinamama waokotao nguo zilizotupwa Dampo na kwenda kuziuza masokoni

Changamoto wakutanazo wakinamama waokotao nguo zilizotupwa Dampo na kwenda kuziuza masokoni

Bushmamy

JF-Expert Member
Joined
Aug 18, 2019
Posts
9,140
Reaction score
15,963
Wafanyabiashara wanaokota nguo jalalani na kwenda kuziuza tena masokoni wametaja baadhi ya changamoto ambazo hukutana Nazo huko majalalani.

Maiti za watoto wachanga walioviringishwa kwenye nguo ni kawaida sana kukutana nazo,
Wa mama hao wamesema kuwa mara nyingi hukutana na maiti za watoto wachanga na haswa walionyongwa mara baada tu ya kuzaliwa na maiti nyingine ni zile zilizotolewa tumboni kabla ya wakati yani (arbotion) na baada ya kukutana nazo hupiga simu polisi na kuja kuchukua maiti hizo kwa ajili ya upelelezi.

Changamoto nyingine ni pamoja na nguo nyingine kuwa zimejaa kila aina ya uchafu wa chakula na damu na hivo Kufua kwa shida kwani hawatumii hata gloves Bali Mikono mitupu.

Wakati mwingine fangasi za mikononi wakati wa Kufukutokana na kuwa nguo hizo huwa na kila aina ya uchafu unaonekana na usionekana

Wafanyabiashara hao wamesema pamoja na changamoto mbalimbali wanazokutana nazo lakini biashara hiyo inalipa kwa kuwa wateja wao hawajui ya kuwa nguo hizo zimeokotwa jalalani hivyo kuzichangamkia kwa urahisi kwa kuwa huwauzia bei rahisi.
20240830_145630.jpg
20240719_142646.jpg
 
Allah anatulinda na mengi waja wake, yaan nguo imemsababishia yeye fangasi kwa kufua tu je yule anaeenda kuivaa?
 
Back
Top Bottom