Change is possible

Change is possible

Shayu

Platinum Member
Joined
May 24, 2011
Posts
608
Reaction score
1,655
Katika Taifa hili naamini kabisa kuna watu bora ambao wanauwezo wa kubadili mwelekeo wa Taifa hili kama wakipewa nafasi.

Wanaoamini katika Taifa hili na uwezo wake wa kufika mbali ikiwa jitihada mahsusi zitawekwa ili watu wa Taifa hili watoke hapa tulipo. Katika maisha yangu yote nimeendelea kuamini toka nilipopata akili zangu katika uwezo wa Taifa hili kukua na kutoka hapa tulipo. Kwanini tusifanikiwe kama tukiamua kwa dhati kuleta mageuzi katika nchi yetu? Mabadiliko yanawezekana ni maamuzi yetu tu ya dhati.

Kama Taifa kamwe hatutakuwa na furaha kama hatutawekeza juhudi zetu kuleta mageuzi katika Taifa hili.

Tutakuwa na furaha kama tukiwa na mipango ya pamoja kisha kuwekeza fikra na nguvu zetu kufanikisha mipango hiyo. Taifa hili ni Taifa la watu wasiokuwa na furaha kwasababu kama Taifa hatujafanikiwa kitu chochote kikubwa cha kujivunia. Ni muhimu kuwekeza juhudi zetu ili kuandika historia katika dunia. Na hili hatutafanikiwa kama hatutakuwa wamoja kama Taifa. Ni muhimu kutambua hili, tuna kitu cha kukijenga kama watu tunaoishi pamoja. Kitu hicho ni nchi yetu. Tukiijenga nchi yetu vizuri tutajivunia. Lakini hatutaweza kuijenga vyema nchi hii pasipo kwanza kujenga mahusiano yetu.

Kama tutapendana sisi wenyewe kwa wenyewe tutakuwa na nafasi kubwa ya kulijenga Taifa hili. Ni lazima tulipende Taifa hili ama sivyo hatutakuwa na nguvu ya kulijenga. Kwahiyo lazima tuelewe hapa ni sehemu pekee ambako tunaweza kupaita nyumbani. Kwahiyo ni lazima juhudi mahsusi zifanyike kuwaleta watu pamoja ili tulijenge Taifa hili kwa pamoja.

Najua kuna matatizo ya corrupt leaders ambao ndio chanzo cha mgawanyiko uliopo. Lazima tuwaambie ukweli. Kwamba wana haribu mwelekeo wa Taifa hili na future yake. Lazima waelewe wao wamekuwa viongozi kwa lengo moja tu, kuleta umoja wa watu wa Taifa hili na kulitoa Taifa hili kutoka hapa lilipo. Lazima wajue cheo ni dhamana na wana majukumu ya dhati ya kulijenga hili Taifa na sio kinyume chake. Roho ya uzalendo ya watu wetu imepotea sababu yao. Ni lazima wajue historia itawahukumu. Watazania wana kiu ya kusonga mbele kama Taifa na hili halitowezekana kama tusipokuwa wamoja. Taifa limekosa uongozi wenye maono na hili ni Tatizo kubwa sana ambalo naliona. Naona msambaratiko katika familia, katika dini na katika ukabila. Hivi vitu vyote vinahitaji kuunganishwa na kuwa kitu kimoja. Ili tujenge Taifa imara. Wajibu wa mtu kwa familia yake, kwa jamii yake na kwa Taifa lake. Sisi sote tuko pamoja katika ujenzi wa Taifa hili. Kama ni nyumba tunatakiwa tuinyanyue pamoja na kuiezeka pamoja.

Tukifikiria au tukiwa na fikra ya kwamba uongozi ni sehemu ya kupatia mali au kutajirikia tutakuwa hatulipendi Taifa hili na baadae yetu itakuwa matatani. Muono huo ambao uko akilini mwa viongozi wengi ni hatari kwa uhuru na mustakabali wa watu wa Tanzania. Uongozi sio sehemu ya kutafutia ufahari au sifa. Uongozi ni kitu kingine kabisa na unahitaji mtu mwenye maono na mwenye busara kwakuwa unahusiana na uhuru na maisha ya watu, una husiana na haki za watu. Ukiwa na Taifa la viongozi wa namna hiyo nchi haitokalika na haki haito tamalaki. Taifa huunganishwa kwa haki. Order na harmony katika Taifa italetwa na haki tu.

Tutakuwa na Taifa lenye watu ambao watakuwa wanagombania kama fisi Mali ya Taifa, tutakuwa na vurugu na fujo na maskini hawatopata chochote, tukiwa na viongozi walifuata mali katika siasa haki itatendekaje? Tunahitaji kiongozi atakaye tufikisha salama katika safari yetu. Kiongozi huyo sio mwingine bali ni mwenye busara na maono.

Msidhani DRC imelaaniwa na Tanzania itaendelee kubarikiwa ikiwa Viongozi wetu wataendelea kuabudu mali. Hatua ya kwanza ya serikali yeyote kuwa ya kiimla ni pale inapoanza kuwa ya kifisadi na yenye tamaa ya mali. Ni lazima itagandamiza watu wake. Kubadilisha mawazo kutoka kutumikia watu kuja kujilimbikizia mali ni hatua ya kwanza ya ugandamizaji dhidi ya raia. Wananchi wana haki ya kulinda uhuru wao dhidi ya serikali yeyote ya kidhalimu ambayo haizingatii maslahi ya umma. Kwahiyo kundi dogo litahodhi utajiri na kujikusanyia mamlaka na kudhani ya kwamba wana haki ya kutawala wengine, uongozi utakuwa wa kuridhishana. Kutakuwa na maskini wengi mno na matajiri wachache.

Watanzania ni lazima wafikirie upya uhuru wao ambao kwasasa unaonekana uko mashakani au umewekwa reheni na kikundi kidogo cha watu kilicho hodhi utajiri mkubwa usio halali, kundi hilo ni la viongozi. Watanzania wana haki juu ya bunge, mahakama na serikali. Ambavyo vyote vinaonekana viko corrupt. Na imani ya wananchi juu ya vyombo hivyo ni ndogo. Raia wowote wale popote pale duniani wana haki ya kuiondoa serikali yeyote iie isiyo kidhi matarajio yao na matumaini yao ya kujenga jamii huru na yenye matumaini. Watu wa Taifa hili wana hamu ya maendeleo lakini wanazuiwa na rushwa na viongozi waliokosa dira na will power ya kulinyanyua Taifa hili kutoka hapa lilipo.

Nchi hii kamwe haitojengwa kwa propaganda na uongo bali itajengwa kwa haki na ukweli. Nchi hii haitojengwa kwa porojo bali kwa juhudi za dhati za watu wake kujiletea maendeleo yao wenyewe. Ni ukweli usiopingika kuna upuuzi mwingi unaendelea katika Taifa hili ambao hauvumliki kwa mtu ambaye ana hamu ya kuliona Taifa hili likinyanyuka. Vijana wa Taifa hili wanahitaji kuona Taifa hili likiendelea. Hatutuwezi kuendelea na viongozi waliopo. Lazima uje wito mpya katika Taifa hili wa uongozi na uadilifu. Vijana wa Taifa hili lazima wajengwe upya kulipenda Taifa lao ni wao tu wenye uwezo wa kulinyanyua Taifa hili kutoka hapa lilipo. Vijana wa Taifa hili wanahitaji heshima kwa Taifa lao. Hatuwezi kuendelea kujenga Taifa hili kwa porojo. Lazima tulijenge Taifa hili kwa akili na ukweli. Raia wana haki ya kuambiwa ukweli kuhusu nchi yao.

Ni lazima tujenge msingi mpya wa Taifa hili na tusonge mbele. Hatutaweza kama hatutakuwa wamoja katika akili na roho. Hatutaweza kama hatutajenga uaminifu na kuheshimiana miongoni mwetu.

Kila wakati nimekuwa nikiamini hatua ya kwanza kwa Taifa lolote kupiga hatua ki maendeleo ni kwa raia wao kulipenda Taifa lao. Ni lazima tulipende Taifa letu. Ni lazima tuzalishe watu wetu bora ambao watetembea kifua mbele duniani kote. Hili lazima litokee na hii ndio itakuwa furaha yetu. Sisi kama Taifa ni lazima tukue. Kuna chaguzi mbili tu. Tukubali na kutia juhudi kufanikisha ndoto yetu ya kwamba tuna uwezo wa kuwa Taifa kubwa kama tukijipanga na kutia juhudi au tusiamini na tubaki hapa tulipo kwenye udhaifu wetu? ''This need bold decision and courage'' but we must move forward like trained Army. We must move forward. We have the power to move this Nation forward. Hatuwezi kuendelea kuwa watu wanaotafuta kwenda kupata mali kwenye uongozi. Tunahitaji viongozi watakao lisongesha Taifa hili. Those who will uplift the spirit of the ''Nation''. We must have our core '' beliefs'' . Tuna viongozi ambao they lead us no where. Watu wa taifa hili wanahitaji muongozo na dira. Wanahitaji jua la asubuhi liwamulikie na matumaini yawajae mioyoni mwao. Tumaini ambalo litajenga Taifa hili. Tunahiaji viongozi wanaoamini kwamba Taifa hili lazima lisonge mbali kwa damu na kwa jasho. Tukiwa wamoja nothing shall be impossible to us. Tunahitaji kongozi atakayeanzisha movement hii. Kiongozi mkweli na mzalendo.

We must build spirit of love and admiration toward this country. Our children must love this NATION. We have ability to grow and to become greater kuna msemo ambao tunauzungumza sana; ''Hata mbuyu ulianza kama mchicha'' . There is the truth on this. Kama tukiamua leo kwa dhati kabisa za nafsi zetu kulijenga Taifa hili nani atatuzuia kuwa Taifa kubwa? Ni juhudi zetu tu na umoja wetu na uaminifu katika kulijenga TAIFA hili. Taifa lolote litakuwa huru pale litakapo jitambua na watu wake watakapojitambua, ni lazima tujitambue sasa.

Those who are educated must initiate change and growth.

Ni lazima tujenge watoto wetu katika utaifa na katika uzalendo. Ni lazima waamini katika Utanzania.'Tutakapo badilisha mawazo ya watu kutoka katika ubinafsi kuja kwenye utaifa ni hatua ya kwanza ya maendeleo.

We need honest leaders who speaks from their hearts, who are ready to sacrifice everything for the Nation growth.We need a leader who will move our cause forward. We must set a Nation dream and handover that dream in each generation. I want you to believe this; our country can grow and become a great Nation on the earth. If we want to move this country forward we must forget ourselves and focus on building this country.

CHANGE IS POSSIBLE.
 
Serikali yeyote duniani hutengeneza nchi na raia wanaofanana na asili ya serikali yenyewe. Serikali isiyo na nidhamu itatengeneza raia wasio na nidhamu. Na kinyume chake ni sahihi.

Kwahiyo tabia ya nchi inategemea sana tabia za viongozi wake. Ni ukweli usiopingika huwezi kutoa usichokuwa nacho..Serikali isiyo kuwa na nidhamu haiwezi kuleta utaratibu katika nchi...

Baadae ya taifa hili itategemea sana busara ya watu wake kuchagua viongozi wenye nidhamu na busara ya kutosha ya kulitoa taifa hili hapa lilipo. Kwakuweka akilini kwamba watu wanaowachagua watajenga taswira ya nchi kulingana na tabia zilizo ndani yao..Kiongozi asiyetenda haki hawezi kuleta haki katika nchi ni ujinga kutegemea haki kutoka katika kiongozi asiyezingatia misingi ya haki.

Kama tukikumbatia uongo na kuwachukua viongozi tunaowajua kabisa sio waadilifu kwasababu ya kuhongwa au sababu ya kutokuwa makini kwetu kuchagua watu wenye maadili mazuri ubaya hautaweza kutoka mlangoni kwetu.

Kwahiyo matatizo tuliyonayo ni mengi na tunahitaji kubadili taswira ya nchi yetu pamoja na mwelekeo wa siasa zetu , mwelekeo tulionao kwa sasa si sahihi na wala sio wenye kuzaa matunda kwa taifa letu. Siasa zetu mbovu ndizo zimetufikisha hapo tulipo na hali inaonyesha kuwa tunaelekea pabaya zaidi kama hatutabadili mwelekeo wetu wa fikra. Sitachoka kuelezea kuhusu ubinafsi ambao ni tatizo tulilonalo kwa sasa; linalo tuzuia kusonga mbele kama taifa.

Watu wanaingia kwenye siasa sio kwa manufaa ya taifa hili, sababu ya ubinafsi wao. Na taifa kwa sasa limegawanyika kila mtu anajiangalia yeye hatuwezi kwenda na fikra za namna hii tukalinyanyua taifa hili. Ni lazima tubadilike, katika mtazamo huu wa ubinafsi hatutaweza kupendana, hatutaweza kuwa na wajibu wa pamoja katika ujenzi wa taifa hili.

Vijana lazima watambue ya kwamba katika siasa sio sehemu ya kutokea, tusichezee uongozi una madhara makubwa kwa jamii kama hatutakuwa na watu makini kwenye siasa, baadae yetu kama taifa itakuwa gizani. Tusipokuwa na viongozi wazuri haki haitokuwepo na kama haki haitopatikana, taifa litakuwa na mgawanyiko. Ni lazima tuwe na viongozi wanaowajibika kwa watu.

My dear brothers:Human beings need guidance: those who have knowledge and understanding must lead others. The prudent Must be presidents and rulers and nation will get direction and great prosperity.

Kwenye uongozi sio sehemu ya kutafutia sifa bali ni sehemu ya kuongoza watu na kufanya maamuzi sahihi yatakayosaidia watu. '' Wote sisi ni lazima tuwe msaada kwa taifa hili na sio kulibomoa'' Ni lazima tuzae matunda kwa taifa hili na tulijaze taifa hili kwa mema, tubadili mtazamo wetu na tutabadili taifa hili. We must do good...and our nation will be healed..

Wote mlio katika siasa katika vyama vyote tuache ubinafsi, Tuelekeze akili zetu katika kujenga taifa hili na sio kubomoana na kubomoa taifa hili. Ni lazima tukumbuke sisi ni wamoja na mwisho wetu ni mmoja. Ni lazima tuwe wamoja na tuache huu mgawanyiko hautusaidii, kama unatafuta uongozi kwasababu ya faida za kibinafsi hufai.

Tunahitaji watu watakaoleta matunda katika taifa letu na bunge litakalo reflect ''Nobility and courage'' Kujitolea huku kwa taifa pasipo ubinafsi ili kuona taifa hili likiendelea pamoja na watu wake is the most noblest job for any great man. Let us embrace this truth'' Nguvu ya kubadilisha taifa hili iko mikononi mwetu, iko kwenye viganja vyetu tuna hii nguvu. Kitu tunachohitajika tu ni kubadilika, kubadili fikra zetu. Nina matumaini haya ndani kabisa ya moyo wangu; tunaweza kulinyanyua taifa hili, tuna uwezo huo, tuna uwezo wa kulinyanyua taifa hili likapendeza zaidi ya mataifa mengi na likatuletea heshima yetu na watoto wetu wakafurahia kuitwa watanzania, badala ya kufurahia mataifa mengine.

Sisi sio taifa la kugeza mataifa mengine, tuna uwezo wa kujenga taifa letu wenyewe na watu wetu wakawa na mtazamo na sura ya kipekee kwa mataifa. Tunahitaji kuweka program mpya katika fikra na mioyo ya watu wetu ili kuleta mtazamo mpya na chanya kwa watu wetu juu ya utaifa. Bila hivyo hatutaweza kulipeleka taifa hili mbele. Tunahitaji kujenga kuridhika kwa watu wetu kwa taifa lao ili kurudisha amani katika taifa na mwelekeo wa pamoja wa kujenga taifa hili. Utaifa hujengwa katika akili na mioyo ya watu na huimarishwa na haki na ubomolewa katika akili na mioyo ya watu watu wasipozingatia kutendeana haki. This Bond of unity and love among our citizens we must build. As the nation we are in great confusion: We need light and we need direction. Trust disapear. we are no longer binded by Nationhood but by our selfishness. There is no Hope anymore! No future!

Tumetawanyika na hatuna nguvu ya pamoja ya kujenga taifa. Ni lazima turudishe imani kwa taifa hili; Taifa hili ni kama mtoto asiye na baba, ni kama mtoto wa mtaani asiye na mwelekeo; ni lazima sasa tujenge nidhamu na mweleko wa taifa hili na watu wake. Hisia hii ya upendo miongoni mwetu na kwa taifa letu ni lazima ijengwe. Wote wanaoleta mgawanyiko kwaajili ya faida binafsi ni lazima tupambane nao ili kulinda taifa hili lisigawanywe.

Baadae ya taifa hili na kizazi kijacho iko mikononi mwetu, tunawajibu wa kujenga nidhamu ya watoto na vijana wetu ili wawe wenye kuwajibika na kulipenda taifa lao. Kwasababu bila nidhamu hii ambayo ni muhimu sana taifa hili haliwezi kusonga mbele. Ni lazima tuondoe ubinafsi wetu na wote tujielekeze kwa pamoja kujenga taifa hili. Tuna matatizo mengi ambayo yanahitaji nguvu ya pamoja na busara kuyatatua.

Katika mtazamo huu; ambao tutaacha ubinafsi tutaendelea kwa haraka zaidi. Ni lazima tuwe na kiu ya kutaka kuendelea kwa pamoja kama taifa. Kama tukiendelea kwa pamoja kama taifa tutakuwa na furaha ya pamoja na kila mtu atalithamani taifa hili. Hatuwezi kujenga taifa la matajiri wachache na maskini wengi. Hatuwezi kuendelea kuwasahau maskini wa taifa hili khalafu tukajenga taifa bora. Ni lazima tujenge uzalendo na wajibu kuanzia kizazi hili. Wote ni lazima tujue tunawajibika kwa taifa hili. Kuanguka au kunyanyuka kwa taifa hili kuko katika mikono ya kila mmoja wetu.

Kwahiyo Chadema na Ccm na vyama vingine ni lazima wabadilishe fikra zao na wajue umoja wa nchi hii ni muhimu kuliko ubinafsi. Nawaomba wote wabadilishe mwelekeo wa mawazo yao. Fikra zetu iwe kujenga jamii bora sio kuleta mgawanyiko katika taifa ambao hauna faida kwetu. Ili kujenga taifa hili ni lazima tulijenge katika fikra sahihi na katika ukweli na uwajibikaji. Ni lazima tuwe na dhamira ya dhati ya kulijenga taifa hili. Kutaka sifa binafsi hakutasaidia taifa hili. Lakini pili wapime watu wanaowapa nafasi ya kugombea uongozi katika vyama vyao kama watakuwa ni wenye manufaa kwa taifa. Taswira ya taifa letu itategemea sana viongozi tulionao. Viongozi ndio wanao mould taifa according to their virtues. Taifa lenye viongozi waovu litatengeneza jamii na taifa lenye maovu. Kwahiyo ni lazima tubadilike tuache kuingia kwenye siasa ili tujijenge kibiashara. ''Administration of justice must be our primary aim as the nation without it we can not prosper''

Kwahiyo tunahitaji mwelekeo kutoka katika confusion iliyopo, tunahitaji dira. Ili kizazi chetu kijacho kisikose dira. Sisi vijana tuliopo tulitegemea kupata dira hii kutoka kwa wazee wetu lakini haina budi kuitafuta sasa na kuilazimisha kuwepo ili kuokoa taifa hili na vizazi vingi vijavyo, ni lazima tufikiri zaidi ya uwepo wetu. Ni muhimu kutofikiri kwa kizazi hiki tu bali tutengeneze future ya kizazi chetu kijacho ni lazima tuitayarishe sasa. Naamini watu wa taifa hili wako tayari kutayarisha baadae ya watoto wao wenyewe waliozaliwa na watakaokuja vizazi vingine vijavyo. Naamini kila mmoja wetu yuko tayari kufanya kazi kuona taifa hili likiendelea.

Naamini nyinyi nyote mnalipenda taifa hili. Naamini nyinyi nyote mnanhitaji mabadiliko. Mabadiliko sio kuondoa serikali moja na kuingiza nyingine kisha mazoea na taratibu kuwa zile zile, ni lazima tuvunje gamba la yai. All we need is total transformation of our hearts and minds. Kutoka katika kiza mwangaza lazima utokee. Nina matumaini makubwa na baadae ya taifa hili kama tutabadili fikra zetu. Kama tuta shape siasa zetu ili ziwe zenye tija kwa taifa letu.

Na mambo yote haya ya msingi yanahitaji nidhamu na kujitolea ili kuona misingi imara ya taifa hili ikijengwa na heshima ya taifa hili ikirudi. Ni Lazima tubadili siasa zetu tusipo badili maendeleo kwetu itakuwa ni ndoto. Ni lazima tujenge siasa zenye kuwajibika na za watu waliokomaa wanaojua nini wanajenga.

Ni lazima tufanye installation kwenye akili za watu wetu na kuweka new programs kwenye akili na mioyo ya watu wetu ambazo zitakuwa na manufaa kwa ujenzi wa taifa hili. Ni lazima tuondoe virusi wote na tulete fikra mpya.

Mwelekeo wa mawazo yetu wa sasa hauna matunda. Lazima taifa hili lijiamini, lazima taifa hili liwe na busara, lazima taifa hili liji tambue. We must be most noblest people on the earth and this; is within our reach.. we can shape our behaviour.

Ni lazima tujenge tabia ambazo zitakuwa na manufaa katika ujenzi wa taifa hili ili kizazi cha vijana wa taifa hili wafurahie utaifa wao. Ni lazima turudishe akili zetu katika utaifa. Huku ndiko kujitambua ama sivyo tutakuwa taifa la watu wasiojitambua wao ni kina nani. We must be pioneers kwa kizazi kijacho. Ili kizazi kijacho kifurahie matunda ya juhudi zetu pamoja na maarifa yetu.

Najua wewe sasa hivi unayesoma hii makala uko tayari kuona taifa hili likiendelea, uko tayari kujitolea..UKO TAYARI kuona taifa hili likiwa moja na likiwa huru kutoka katika rushwa na ufisadi , kwa kubadili tabia yako utabadili taifa. Na wote tuseme no kwa rushwa na ufisadi ili tujenge jamii bora na watu bora katika ulimwengu. Wote tukatae viongozi waovu na wala rushwa ili tujenge taifa kwa pamoja.


CHANGE IS POSSIBLE!


Now faith is being sure of what we hope for and certain of what we do not see. This is what the ancients were commended for. By faith we understand that the universe was formed at God's command, so that what is seen was not made out of what was visible.

Hebrew 11
 
Change is Possible, and to be precise CHANGE IS INEVITABLE.

Change th woman and you have changed the whole family.

Change the Head Of State, and you have changed the entire Nation.
 
Ni lazima tujenge watoto wetu katika utaifa na katika uzalendo. Ni lazima waamini katika Utanzania.'Tutakapo badilisha mawazo ya watu kutoka katika ubinafsi kuja kwenye utaifa ni hatua ya kwanza ya maendeleo.


Mkuu
nimeyapenda sana maneno yako kama nilivoyarudia hapo juu, tunawakati mgumu kwa kuwa na watanzania wachache kutumia elimu na uelewa wao vibaya kwa kupotosha jamii kila kukicha na hapa ndipo tunapokuwa taifa la wajinga na wapumbavu na itatuchukuwa muda mrefu kubadili watu wa aina hiyo kutoka katika ubinafsi, propaganda chafu, uchoyo na ulafi- kuingia kwenye uzalendo wa kweli.
 
Ni lazima tujenge watoto wetu katika utaifa na katika uzalendo. Ni lazima waamini katika Utanzania.'Tutakapo badilisha mawazo ya watu kutoka katika ubinafsi kuja kwenye utaifa ni hatua ya kwanza ya
maendeleo.



Mkuu
nimeyapenda sana maneno yako kama nilivoyarudia hapo juu, tunawakati mgumu kwa kuwa na watanzania wachache kutumia elimu na uelewa wao vibaya kwa kupotosha jamii kila kukicha na hapa ndipo tunapokuwa taifa la wajinga na wapumbavu na itatuchukuwa muda mrefu kubadili watu wa aina hiyo kutoka katika ubinafsi, propaganda chafu, uchoyo na ulafi- kuingia kwenye uzalendo wa kweli.

Nashukuru sana na nimefurahi kuona na wewe unaliona tatizo lilipo. Moyo wangu na roho yangu iwe nawe ni ukweli usiopingika tunahitaji mabadiliko ya nafsi.
 
Nashukuru sana na nimefurahi kuona na wewe unaliona tatizo lilipo. Moyo wangu na roho yangu iwe nawe ni ukweli usiopingika tunahitaji mabadiliko ya nafsi.

HAKIKA! Tunahitaji mapinduzi ya NAFSI ZETU! Maana Adui wa kwanza wake mtu ni NAFSI YAKE MWENYEWE! Humo ndimo maamuzi hufanywa, Je, uishi HULKA ZAKO ama MANTIKI YA MAISHA! Nafsi zetu zimekiuka MANTIKI, na kuamua kuishi HULKA mama wa MATAMANIO mbeleko ya KUPIGANIA UKUU-MIMI KWANZA mama wa UBINAFSI rafiki wa rushwa, mauaji, fitna, ufisadi, umamluki, ukoloni, n.k na kila aina ya uozo ndani ya jamii, kwa kifupi ni "UBEPARI"

Piga kelele, zunguka, tafakari, fanya upembuzi wa kila aina, jibu utakalopata juu ya matatizo yetu ni kutokuwa na misingi imara ya kusimamia mahusiano yaliyopo baina ya mtu na mtu/watu na baina ya watu na mazingira yao! Unapopata balanced relationship kati ya hayo, ndiyo tuiitayo "MANTIKI" - "UTU" haipo sasa kwani NAFSI ZETU ZIMEGEUKIA HULKA ZETU, hivyo hatuna budi kuzifanyia MAPINDUZI MAKUBWA! Mabadiliko ni jambo rahisi sana, ila ukiwa na IMANI THABITI. Nani anayo? Kamwe USIIACHE IKAPOTEA!

Cheza nafsi yako leo, na mifupa yako italowanishwa na maji ya mito ya machozi ya furaha kutoka machoni mwa wajukuu wetu kesho! That's more than LOVE!

Mungu wetu yu tayari kutupigania vitani!
Anaita sasa!
 
JingalaFalsafa

Tuko pamoja mkubwa wangu ni mawazo yetu tu ndio yatakayoweza kubadili jamii hii lakini kwanza ni lazima tuamini kile tunachokisimamia na kukihubiri ni sahihi na chenye faida KWa UMMA WOTE.

And though the philosopher may live remote from business, the genius of philosophy, if carefully cultivated by several, must gradually diffuse itself throughout the whole society, and bestow a similar correctness on every art and calling. (David Hume, 1737)
 
Change is Possible, and to be precise CHANGE IS INEVITABLE.

Change th woman and you have changed the whole family.

Change the Head Of State, and you have changed the entire Nation.

Sio kila wakati ukibadilisha kiongozi wa nchi utaleta mabadiliko chanya kwa Taifa.
 
Mada yako ndugu Shayu inaonekana kuongelea mambo ya jumla mno kama vile mhubiri wa kulitakia jema taifa letu. Nakubaliana na mengi ambayo umeongelea kwa jumla jumla ikiwemo jambo la upendo ambalo husaidia kutukutanisha na kuondoa tofauti kadhaa amazo zinaweza kuendeleza hali ya kutoelewana na kuziba nyufa ambazo hazisaidii kujenga taifa bali kulidumaza.

Ningetazamia ungajaribu kutujengea ufafanuzi wa kina ni mambo yapi ambayo ni muhimu katika kuleta mabadiliko katika jamii na njia za utekelezaji waji.
 
Mada yako ndugu Shayu inaonekana kuongelea mambo ya jumla mno kama vile mhubiri wa kulitakia jema taifa letu. Nakubaliana na mengi ambayo umeongelea kwa jumla jumla ikiwemo jambo la upendo ambalo husaidia kutukutanisha na kuondoa tofauti kadhaa amazo zinaweza kuendeleza hali ya kutoelewana na kuziba nyufa ambazo hazisaidii kujenga taifa bali kulidumaza.

Ningetazamia ungajaribu kutujengea ufafanuzi wa kina ni mambo yapi ambayo ni muhimu katika kuleta mabadiliko katika jamii na njia za utekelezaji waji.



Sidhani kama umenielewa vizuri kile nilichoandika. Kama wewe ni mfuatiliaji mzuri wa mada zangu utajua kile ninachopigania. Kitu chochote kile lazima kianzie na msingi na ili Taifa hili liendelee ni lazima msingi wa mahusiano yetu kama watu wa Taifa hili uwe imara. Ni lazima tuwe wamoja. Nahubiri kuhusu mabadiliko ya fikra. Sio kwamba sijui masuala ya uchumi najua. Lakini natambua kwanza ili Taifa hili liendelee kuna baadhi ya mambo ambayo ni ya kimsingi lazima yazingatiwe. Pengine wewe ungeniambia mambo yapi ambayo unaodhani nilipaswa kuongelea sijaongelea. Kama ni masuala ya elimu nimeishawahi kuongalea na kuwahi kusema bila Elimu iliyobora mabadiliko katika Taifa hili itakuwa ni ndoto na nikawahi kusema elimu lazima iwe na lengo la kunufaisha jamii na sio mtu binafsi.


Ninaweza kuongea pia kuhusu aina gani ya elimu ambayo inapaswa kutolewa ili kukomboa Taifa hili lakini kila kitu kina wakati wake. Kwasasa nimeamua kuandika nilichoandika. Sijafahamu kilichokutatiza ni nini?

Mimi nafikiri tubadilike. Na hata aina ya siasa tunazofanya tuzibadilishe ili ziwe zenye manufaa kwa jamii na zinazojenga. Taifa hili halitoweza kuendelea kama tutaendekeza utoto na tamaa. Elewa kwamba mawazo yetu ndiyo yanayojenga Taifa hili. Je mawazo yetu ni bora kiasi gani kuwezesha ujenzi wa Taifa hili? Je tunaweza kujenga Taifa hili kama hatuaminiani? Tunahitaji kubadilisha mawazo yetu sasa na kufikiria upya kuhusu Taifa hili tukifahamu baadae yetu iko mikononi mwetu. Najua itachukua muda sana kubadilisha mioyo migumu ya watu wa Taifa hili kuwaleta katika uzalendo lakini kwangu mimi hii ni kazi yenye heshima na tunu kubwa, kuona watu wa Taifa hili ni wa moja na wenye dhamira ya dhati ya maendeleo yao.
 
Sidhani kama umenielewa vizuri kile nilichoandika. Kama wewe ni mfuatiliaji mzuri wa mada zangu utajua kile ninachopigania. Kitu chochote kile lazima kianzie na msingi na ili Taifa hili liendelee ni lazima msingi wa mahusiano yetu kama watu wa Taifa hili uwe imara. Ni lazima tuwe wamoja. Nahubiri kuhusu mabadiliko ya fikra. Sio kwamba sijui masuala ya uchumi najua. Lakini natambua kwanza ili Taifa hili liendelee kuna baadhi ya mambo ambayo ni ya kimsingi lazima yazingatiwe. Pengine wewe ungeniambia mambo yapi ambayo unaodhani nilipaswa kuongelea sijaongelea. Kama ni masuala ya elimu nimeishawahi kuongalea na kuwahi kusema bila Elimu iliyobora mabadiliko katika Taifa hili itakuwa ni ndoto na nikawahi kusema elimu lazima iwe na lengo la kunufaisha jamii na sio mtu binafsi.


Ninaweza kuongea pia kuhusu aina gani ya elimu ambayo inapaswa kutolewa ili kukomboa Taifa hili lakini kila kitu kina wakati wake. Kwasasa nimeamua kuandika nilichoandika. Sijafahamu kilichokutatiza ni nini?

Mimi nafikiri tubadilike. Na hata aina ya siasa tunazofanya tuzibadilishe ili ziwe zenye manufaa kwa jamii na zinazojenga. Taifa hili halitoweza kuendelea kama tutaendekeza utoto na tamaa. Elewa kwamba mawazo yetu ndiyo yanayojenga Taifa hili. Je mawazo yetu ni bora kiasi gani kuwezesha ujenzi wa Taifa hili? Je tunaweza kujenga Taifa hili kama hatuaminiani? Tunahitaji kubadilisha mawazo yetu sasa na kufikiria upya kuhusu Taifa hili tukifahamu baadae yetu iko mikononi mwetu. Najua itachukua muda sana kubadilisha mioyo migumu ya watu wa Taifa hili kuwaleta katika uzalendo lakini kwangu mimi hii ni kazi yenye heshima na tunu kubwa, kuona watu wa Taifa hili ni wa moja na wenye dhamira ya dhati ya maendeleo yao.
Hatuko mbali, tupo pamoja, ninachokuomba ni hiki, jaribu kuleta mambo kadhaa ambayo tunatakiwa kubadilika, maana kuleta tu neno mabadiliko au kubadilika ni la jumla mno, ila kama elaboration ya kubadilika ndiyo inayohitajika tufanye nini ili tubadilike.

Mfano Katibu Mkuu wa CCM Kinana amewaagiza viongozi wa CCM kuachana na uheshimiwa bali wakubali undugu ili wateremke kutoka pale juu walipo ili kuwafikia wananchi. Maana yake ameona gape iliopo kati ya wananchi na viongozi ambazo wamejipandisha ngazi kuwa waheshimiwa inawawia vigumu hata kusahihiswa kwa vile mheshimiwa hasahihiswi ila akiacha uheshimwa na kujiona ndugu kati ya ndugu kuna kusahihisha kindugu na wanaweza kufikwia na kila ndugu. Hii ni moja ya mambo ambayo yanahitaji kubadilika. Je, wewe katika mtazamo wako unataka tubadilike katika mambo yapi?
 
Hatuko mbali, tupo pamoja, ninachokuomba ni hiki, jaribu kuleta mambo kadhaa ambayo tunatakiwa kubadilika, maana kuleta tu neno mabadiliko au kubadilika ni la jumla mno, ila kama elaboration ya kubadilika ndiyo inayohitajika tufanye nini ili tubadilike.

Mfano Katibu Mkuu wa CCM Kinana amewaagiza viongozi wa CCM kuachana na uheshimiwa bali wakubali undugu ili wateremke kutoka pale juu walipo ili kuwafikia wananchi. Maana yake ameona gape iliopo kati ya wananchi na viongozi ambazo wamejipandisha ngazi kuwa waheshimiwa inawawia vigumu hata kusahihiswa kwa vile mheshimiwa hasahihiswi ila akiacha uheshimwa na kujiona ndugu kati ya ndugu kuna kusahihisha kindugu na wanaweza kufikwia na kila ndugu. Hii ni moja ya mambo ambayo yanahitaji kubadilika. Je, wewe katika mtazamo wako unataka tubadilike katika mambo yapi?



Umesoma kweli niliyoandika? Chukua muda usome nadhani kila kitu kinaeleweka nimejaribu kuweka katika lugha nyepesi. Ondoa fikra za kukosoa akilini mwako ndio utanielewa vizuri. Kama kuchangia tuchangie kwa kuelimishana.

Ukiwaelimisha watu kulipenda Taifa lao watakuwa na will na affection ya kulitumikia nami naamini kabisa hiyo ni hatua moja kubwa kuelekea kwenye maandeleo. Hatutaweza kulijenga Taifa hili kama hatutalipenda na kama hatutakuwa wamoja. Mambo mengine kama ya Elimu yetu iwaje ni mambo ya mipango na hii inahitaji umoja. Tutawezaje kukaa meza moja na kupanga mipango ya future ya watoto wetu na Taifa kama hatupendani na sio wamoja? Tutakuwa na mwelekeo kama Taifa kama tutakuwa wamoja. Sikiliza rafiki yangu wewe pia una sehemu Ya ujenzi kwa Taifa hili. Kama ukiwaelimisha watu umuhimu wa Utaifa na uzalendo. Kama ukiwaelimisha watu umuhimu wa kuchagua viongozi watenda haki na wenye busara na maono ambao wanaweza kuliongoza vyema Taifa hili. Lengo langu na maono yangu ni kujenga Taifa la haki, kujenga Taifa la la raia wanaojitambua wao ni kina nani na wanawajibu gani kwa Taifa lao. Nilisema na nitaendelea kusema Taifa hili ni lazima tulijenge kwa ukweli. Msingi wa kwanza kuunda Taifa lolote imara ni mahusiano ya watu wake ambao baadae wataunganishwa na nia ya pamoja ya kuleta maendeleo yao wenyewe. Tutalinyanyua Taifa hili kama tutakuwa watu wenye nia moja na waaminifu kwa Taifa.
 
Umesoma kweli niliyoandika? Chukua muda usome nadhani kila kitu kinaeleweka nimejaribu kuweka katika lugha nyepesi. Ondoa fikra za kukosoa akilini mwako ndio utanielewa vizuri. Kama kuchangia tuchangie kwa kuelimishana.

Ukiwaelimisha watu kulipenda Taifa lao watakuwa na will na affection ya kulitumikia nami naamini kabisa hiyo ni hatua moja kubwa kuelekea kwenye maandeleo. Hatutaweza kulijenga Taifa hili kama hatutalipenda na kama hatutakuwa wamoja. Mambo mengine kama ya Elimu yetu iwaje ni mambo ya mipango na hii inahitaji umoja. Tutawezaje kukaa meza moja na kupanga mipango ya future ya watoto wetu na Taifa kama hatupendani na sio wamoja? Tutakuwa na mwelekeo kama Taifa kama tutakuwa wamoja. Sikiliza rafiki yangu wewe pia una sehemu Ya ujenzi kwa Taifa hili. Kama ukiwaelimisha watu umuhimu wa Utaifa na uzalendo. Kama ukiwaelimisha watu umuhimu wa kuchagua viongozi watenda haki na wenye busara na maono ambao wanaweza kuliongoza vyema Taifa hili. Lengo langu na maono yangu ni kujenga Taifa la haki, kujenga Taifa la la raia wanaojitambua wao ni kina nani na wanawajibu gani kwa Taifa lao. Nilisema na nitaendelea kusema Taifa hili ni lazima tulijenge kwa ukweli. Msingi wa kwanza kuunda Taifa lolote imara ni mahusiano ya watu wake ambao baadae wataunganishwa na nia ya pamoja ya kuleta maendeleo yao wenyewe. Tutalinyanyua Taifa hili kama tutakuwa watu wenye nia moja na waaminifu kwa Taifa.

Mambo yapi ambayo hayaleti umoja wa kitaifa? Je, kwa mtazamo wako taifa hili halina mahusiano baina wananchi na kama ndivyo ni kwa namna ipi?

Wiki hii Kamati ya kuratibu maoni ya katiba ilipokuwa katika jiji la Dar es Salaam, kuna baadhi ya wachangiaji waliotaka katika katiba mpya vyama vya siasa visiruhusiwe kuwa na sare za chama cha kisiasa, ila tuwe na ishara ya namna moja inayoonyesha utaifa kama bendera ya taifa. Vyama viuze tu sera tu kwa sababu:
  • sare zinagawa wananchi na kuweka matabaka ambayo yanadhoofisha mshikamano na umoja wa kitaifa,
  • kuleta uhasama baina wa wafuasi wa vyama vya siasa hata kusababisha mauaji ya raia,
  • sare hizo hufanywa na vyama husika kama moja ya rushwa kwa wapiga kura.
Hilo ni jambo ambalo limepambanuliwa vizuri na kueleweka nami nimepiga filimbi kutangaza. Hii ya kusema tu mshikamano wa kitaifa bila kutoa ufafanuzi na mapendekezo nini na namna gani tufanya itakuwa sawa na kucheze mpira danadana pila kufunga goli.
 
Mambo yapi ambayo hayaleti umoja wa kitaifa? Je, kwa mtazamo wako taifa hili halina mahusiano baina wananchi na kama ndivyo ni kwa namna ipi?

Wiki hii Kamati ya kuratibu maoni ya katiba ilipokuwa katika jiji la Dar es Salaam, kuna baadhi ya wachangiaji waliotaka katika katiba mpya vyama vya siasa visiruhusiwe kuwa na sare za chama cha kisiasa, ila tuwe na ishara ya namna moja inayoonyesha utaifa kama bendera ya taifa. Vyama viuze tu sera tu kwa sababu:
  • sare zinagawa wananchi na kuweka matabaka ambayo yanadhoofisha mshikamano na umoja wa kitaifa,
  • kuleta uhasama baina wa wafuasi wa vyama vya siasa hata kusababisha mauaji ya raia,
  • sare hizo hufanywa na vyama husika kama moja ya rushwa kwa wapiga kura.
Hilo ni jambo ambalo limepambanuliwa vizuri na kueleweka nami nimepiga filimbi kutangaza. Hii ya kusema tu mshikamano wa kitaifa bila kutoa ufafanuzi na mapendekezo nini na namna gani tufanya itakuwa sawa na kucheze mpira danadana pila kufunga goli.

Hayo uliyoandika una uhakika ndiyo yanayoligawa Taifa hili? Ni kwa vipi sare za chama zika ligawa Taifa? Taifa hil linagawa una ufisadi, ulafi, ubinafsi na uroho wa baadhi ya watu. Hayo uliyoongelea hayawezi kulisaidia Taifa.
 
Hayo uliyoandika una uhakika ndiyo yanayoligawa Taifa hili? Ni kwa vipi sare za chama zika ligawa Taifa? Taifa hil linagawa una ufisadi, ulafi, ubinafsi na uroho wa baadhi ya watu. Hayo uliyoongelea hayawezi kulisaidia Taifa.
Yes, moja ya mambo makubwa yanayotugawa watanzania na kutuweka kimakundi badala ya kitaifa. Imefikia hata mtu kukutwa umevaa sare ya chama fulani kuonekana eneo ambalo si la wapenzi basi ni nongwa ya kuzomewa hadi mtu kukimbia.

Imetokea wengine hata kupopolewa kwa mawe kwa sababu ya sare za siasa. Lakini kama tungebaki na casual cloth ingesaidia kupunguza tension ya kuonekana kwa wazi makundi ndani ya jamii ila watu wale wale wanapata itikadi toka vyama tofauti na kuchagua mtu wanayemtaka.
 
Tuwatambue wale watu ambao ni viongozi miongoni mwetu. Tuache hii re-cycling ya viongozi wale wale ambao hawawezi kufanya kazi. Ni kwamba,viongozi wa sasa,they have kept house new breed of leadership has been groomed. Now they must step aside.
 
Kama alivyosema mtoa mada ndani ya post ya kwanza, ili kuleta mabadiliko sahihi ni lazima tujenge MAHUSIANO YETU UPYA! Hapo ni wazi kwamba tunatakiwa kufanyia mageuzi FIKRA zetu kwanza kabla ya kufanya chochote!

*MAHUSIANO yetu ya leo hayaruhusu mabadiliko kwetu, yaani jinsi TUNAVYOCHUKULIANA sisi kwa sisi kwanza! Mwanaafrika wa Tanzanzani leo hii anamchukulia mtanzania mwenzake kama DARAJA la kujikweza binafsi, ndio maana leo wanatuingza kwenye mikataba mibovu kwa kujifikiria binafsi, nitapigania kukufanya daraja la ukuu wangu nawe pia utapigania kunifanya daraja ili ujikweze, hapo ni lazima TUKINZANE! TUNAKINZANA wakati wote tunajenga nyumba moja(Tanzania). Ukifunga fito mimi nitafungua, nawe vivyo hvyo kwangu! UMOJA na MSHIKAMANO umekufa, UTENGANO NI UDHAIFU! Hata ukija na mikakati mizuri kiasi gani ya kuinua uchumi, kama hakuna UMOJA ni UPUMBAVU sawa na kutwanga maji kwenye kinu!

*Pia tutathimini MAHUSIANO yetu juu ya mali zetu wenyewe jinsi gani TUNACHUKULIA MALI ZETU, embu kwa mifano midogo tu tufikirie mahusiano yetu juu ya mali zetu, leo watu wako radhi kuchimba kokoto barabarani, wanang'oa viti viwanjani, wanachoma moto misitu, n.k hzo ndio FIKRA zetu vichwani mwetu! Ni upumbavu kuja na mikakati ya kujenga barabara na viwanja vingi zaidi pasi kufikiria kwanza kiaje FIKRA za watu hao zitabadilikaje wathamini mali zao.

*Leo watu hawana HARI ya kufanya kazi, kilichomo FIKRANI "NIKIAJIRIWA TU NIPIGANIE JINSI GANI KWANZA NITAIIBIA KAMPUNI AU SERIKALI, wakati waajiri nao wanawaza jinsi gani watawanyonya wafanyakazi wao" hapo ni Ndoto za mchana kutumaini maendeleo! KOMBOA FIKRA ZAO KWANZA, WATAMBUE WAJIBU WAO KWA JAMII NDIO JAMBO LA KWANZA! Na hiyo ndio HAKI! Ni upumbavu kuhangaikia kujenga viwanda vingi na kuajiri wafanyakaz wengi wakati FIKRA ZAO MFU!

*Leo kila aingiaye madarakani anawaza jinsi gani atajinufaisha kwanza, badala jinsi gani atalitumikia taifa. FIKRA MFU! Tutabadilisha uongozi kila leo, lakini kama hatujapigania kufuta fikra hzo vichwani mwetu ni UPUNGUANI kuota maendeleo!

Ndio maana nakubaliana na mkuu Shayu anaposema, "I can see the future bright if we change our mind"

Wanasiasa wetu leo wameng'ang'ania takwimu na data za kukandiana wakidai ni wakombozi wetu, wakati FIKRA zetu ndio kikwazo cha kwanza cha maendeleo yetu!

TUNAHITAJI IMANI MPYA FIKRANI MWETU! Imani itakayofanya TUFIKIRIANE KWANZA, TUHESHIMIANE NA KUJALIANA KWANZA. Imani itakayotufanya TUPENDANE-TUWE WAZALENDO! Imani mpya kujenga MAAZIMIO MAPYA ya uchumi, siasa na utamaduni!

MAMBO SIO RAHISI, TUUMIZE VICHWA. Ni kwa namna gani tutaweza kubadili FIKRA ZETU kutoka UFU na kuwa HAI kwa maendeleo yetu!

Nguvu yetu ni UMOJA na KUTHUBUTU, TUNAWEZA.

Mungu wetu yu hai tayari kutushindia vitani.

Anaita sasa!
 
JingalaFalsafa

Sina cha kuongezea ndugu yangu umenijibia yote yaliyokuwemo nafsini mwangu kwa ufasaha mkubwa. Nafikiria umeweka sawa hoja yangu katika ukamilifu wake. Hakika Fikra zako ni sahihi katika hili.
 
Last edited by a moderator:
Tuwatambue wale watu ambao ni viongozi miongoni mwetu. Tuache hii re-cycling ya viongozi wale wale ambao hawawezi kufanya kazi. Ni kwamba,viongozi wa sasa,they have kept house new breed of leadership has been groomed. Now they must step aside.

Nakubaliana na wewe bwana Andrew. Tunahitaji mwelekeo mpya kama Taifa na viongozi wapya wenye maono tofauti juu ya Taifa hili.
 
Back
Top Bottom