Chanjo za watoto wachanga, kwa Afrika tu au Dunia nzima?

Chanjo za watoto wachanga, kwa Afrika tu au Dunia nzima?

Mzizi Mkavu uko wapi? Hebu njoo utupe mwongozo Mkuu.
 
Nadhani ni kama mwezi au miwili imepita sasa kumekuwa na operesheni ya kuchanja watoto..ilikuja kwa kasi sana mpaka wakaweka kambi sehemu zenye watu wengi mfano jengo la kusubiri ferry - K'mboni. Wengi tulijiuliza, why now? walipoona watu hawajitokezi kwa wingi wakaanza operesheni ya nyumba kwa nyumba...kwangu walipita ila nilikuwa nimeacha maagizo wasifunguliwe mlango. Nikaona bora niongee na daktari mmoja maarufu tu...akanijibu kimkato..'USIMPELEKE MTOTO'.

Mungu atusaidie na hawa watoto maana kazi ipo!

kama kweli tunakili vizuri tufanye utafiti wetu kujua kama hizo chanjo zina madhara kwa watoto result zitakazotoka zitatuguide futanye nini sio kulaumu wazungu kwa kila kitu kama hatuna vichwa vya kufikiri na sisi tufanye utafiti pia.
 
Chanjo za watoto zipo hata huku ughaibuni kwa watoto kuanzia anapozaliwa hadi miaka 18. Kuna nyingine ni optional kama flu vaccine na nyingine ni compulsory kama za Polio, Diptheria, Tetanus, Hepatitis A na B ingawa hawakulazimishi iwapo utagoma ila wanakushauri tu kwamba ni muhimu. Na chanjo hizo huchomwa mapajani tu na si kwingineko, na kuna nyingine ni za kunywa. Binafsi sioni tatizo na chanjo hizo maana risk zake ni ndogo kulinganisha na faida.
 
kama kweli tunakili vizuri tufanye utafiti wetu kujua kama hizo chanjo zina madhara kwa watoto result zitakazotoka zitatuguide futanye nini sio kulaumu wazungu kwa kila kitu kama hatuna vichwa vya kufikiri na sisi tufanye utafiti pia.

sasa mkuu, huoni kama uzi huu ni enquiry? huoni kama tunahitaji kupata taarifa kutoka kwa watu mbalimbali? kama huna cha kueleza unasoma, halafu unatoka kimya kimya
 
Chanjo za watoto zipo hata huku ughaibuni kwa watoto kuanzia anapozaliwa hadi miaka 18. Kuna nyingine ni optional kama flu vaccine na nyingine ni compulsory kama za Polio, Diptheria, Tetanus, Hepatitis A na B ingawa hawakulazimishi iwapo utagoma ila wanakushauri tu kwamba ni muhimu. Na chanjo hizo huchomwa mapajani tu na si kwingineko, na kuna nyingine ni za kunywa. Binafsi sioni tatizo na chanjo hizo maana risk zake ni ndogo kulinganisha na faida.

tafadhali tujuze uko wapi, tufahamu utamaduni wa nchi husika if you dont mind
 
Mama taratibu. kwa hiyo tunapokuwa wanaume 10, watano hawana uwezo wa kuzaa? mbona nikiangalia karibu wote hapa ofisini tuna watoto?

Gazeti la mwananchi la majuzi/au juzi(sikumbuki vema) limeandika kwamba nusu ya wanaume nchini wana ugumba....ni utafiti wa daktari bingwa...nadhani ndo nukuu ya bibie FaizaFoxy.
 
Chanjo za watoto zipo hata huku ughaibuni kwa watoto kuanzia anapozaliwa hadi miaka 18. Kuna nyingine ni optional kama flu vaccine na nyingine ni compulsory kama za Polio, Diptheria, Tetanus, Hepatitis A na B ingawa hawakulazimishi iwapo utagoma ila wanakushauri tu kwamba ni muhimu. Na chanjo hizo huchomwa mapajani tu na si kwingineko, na kuna nyingine ni za kunywa. Binafsi sioni tatizo na chanjo hizo maana risk zake ni ndogo kulinganisha na faida.

hivi mkuu, umewahi kujiuliza kwa nini leo nchi kama UJERUMANI hazina watoto na vijana wa kutosha nchi? Umewahi kutafakari kwa nini baadhi ya nchi hutoa zawadi kwa kina mama waliojifungua?
 
Gazeti la mwananchi la majuzi/au juzi(sikumbuki vema) limeandika kwamba nusu ya wanaume nchini wana ugumba....ni utafiti wa daktari bingwa...nadhani ndo nukuu ya bibie FaizaFoxy.

chanzo kimetajwa?
 
..........Chanjo zipo dunia nzima, tena ughaibuni ndio kabisa mtoto toka anazaliwa anachanjwa chanjo, tena kwa wakati mmoja mtoto anaweza pata chanjo 5.
Wenzetu watoto zao hawaumwi umwi kama siye huku kwa sababu ya hizo chanjo. Mtoto kuanza daycare /shule wanahitaji record ya chanjo na kama huna mtoto hapokelewi.

.........Upungufu wa nguvu za kiume msisingizie chanjo, ni vyakula mnavyokula na mapombe hayo, mazoezi hamfanyi, utafikiri hizo nguvu zitatokea wapi?
 
hivi mkuu, umewahi kujiuliza kwa nini leo nchi kama UJERUMANI hazina watoto na vijana wa kutosha nchi? Umewahi kutafakari kwa nini baadhi ya nchi hutoa zawadi kwa kina mama waliojifungua?

Kwa kweli sijawahi kujiuliza. Binafsi naamini chanjo kwa watoto ni muhimu. Wenzetu wamefanikiwa kuelimisha watu wao na asilimia kubwa hutumia chanjo. Kama alivyosema mdau Pretty lazima uonesha kadi ya chanjo ya mtoto kabla hajaandikishwa shule, na uzuri wanakupa pia maelezo ya kila chanjo, madhara yake kama yapo(mengi ni minor kama homa, kutapika kwa siku chache)na lini zlianza kutumika etc. Pia unaweza kuresearch online na ukapata info nyingi tu juu ya hizi chanjo.
 
kama kweli tunakili vizuri tufanye utafiti wetu kujua kama hizo chanjo zina madhara kwa watoto result zitakazotoka zitatuguide futanye nini sio kulaumu wazungu kwa kila kitu kama hatuna vichwa vya kufikiri na sisi tufanye utafiti pia.
Safi mkuu, tutafanya tu utafiti unaosema tena kukuthibitishia hili ni kuwa tutaomba hela toka mfuko wa hisani ya watu wa marekani, kwahiyo tutakuwa tunaandika tumefanya utafiti kwa msaada wa watu wa marekani!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!. Internet connection yangu ipo chini, but nitarudi.
 
Kwa kweli sijawahi kujiuliza. Binafsi naamini chanjo kwa watoto ni muhimu. Wenzetu wamefanikiwa kuelimisha watu wao na asilimia kubwa hutumia chanjo. Kama alivyosema mdau Pretty lazima uonesha kadi ya chanjo ya mtoto kabla hajaandikishwa shule, na uzuri wanakupa pia maelezo ya kila chanjo, madhara yake kama yapo(mengi ni minor kama homa, kutapika kwa siku chache)na lini zlianza kutumika etc. Pia unaweza kuresearch online na ukapata info nyingi tu juu ya hizi chanjo.
hapo kwenye red mkuu. kuhusu ''kuresearch online na ukapata info nyingi'', info nyingine hii hapa: http://articles.mercola.com/sites/articles/archive/2011/11/01/more-parents-waking-up-to-vaccine-dangers.aspx
 
Chanjo za watoto zipo hata huku ughaibuni kwa watoto kuanzia anapozaliwa hadi miaka 18. Kuna nyingine ni optional kama flu vaccine na nyingine ni compulsory kama za Polio, Diptheria, Tetanus, Hepatitis A na B ingawa hawakulazimishi iwapo utagoma ila wanakushauri tu kwamba ni muhimu. Na chanjo hizo huchomwa mapajani tu na si kwingineko, na kuna nyingine ni za kunywa. Binafsi sioni tatizo na chanjo hizo maana risk zake ni ndogo kulinganisha na faida.
Nimefurahi kwakuwa umesema hawakulazimishi, na hili ndilo linalofanya watu tuanze kuhoji. kumbe huko hawalazimishi. Mi nachukia pia tabia ya kusema kupima ukimwi ni hiari wakati huo huo wamama wajawazito wanalazimishwa kupima. Wakitaka twende sawa wasitulazimishe chochote.
 
..........Chanjo zipo dunia nzima, tena ughaibuni ndio kabisa mtoto toka anazaliwa anachanjwa chanjo, tena kwa wakati mmoja mtoto anaweza pata chanjo 5.
Wenzetu watoto zao hawaumwi umwi kama siye huku kwa sababu ya hizo chanjo. Mtoto kuanza daycare /shule wanahitaji record ya chanjo na kama huna mtoto hapokelewi.

.........Upungufu wa nguvu za kiume msisingizie chanjo, ni vyakula mnavyokula na mapombe hayo, mazoezi hamfanyi, utafikiri hizo nguvu zitatokea wapi?

1)''Wenzetu watoto zao hawaumwi umwi kama siye huku kwa sababu ya hizo chanjo.'' waambie waje bongo wamechanjwa hivyo hivyo wang'atwe mbu, waishi bila uhakika wa maji, wale mara moja kwa siku, walale katika nyumba za mbavu za mbwa na ....., wataumwa umwa tu.

2)''Mtoto kuanza daycare /shule wanahitaji record ya chanjo na kama huna mtoto hapokelewi.'' umesoma kuna mchangiaji mmoja anasema alimuuliza daktari wake kuhusu chanjo akaambiwa asimpeleke? wapo madaktari wengi tu wasiokubaliana na hizi silent killers.

3)''.Upungufu wa nguvu za kiume msisingizie chanjo, ni vyakula mnavyokula na mapombe hayo, mazoezi hamfanyi, utafikiri hizo nguvu zitatokea wapi?''.pia hatunywi maji ya kutosha, tunakunywa zaidi soda badala ya maji halisi, tuko bize zaidi na kusaka mahela, tunadanganywa pia kuwa hatuna nguvu za kiume kumbe tunazo pengine watu tu wanataka kuuza dawa zao kupitia ujinga wetu na .........., ​mkuu lazima tuzungumzie nguvu ya mwili kwanza kabla ya nguvu za kiume.
 
.....Hili suala la chanjo naona hapa watu tunapotezana hapa. Hakuna kitu ambacho kiko asilimia 100 salama. lakini mara nyingi binadamu tunaongozwa na kanuni ya kupima faidia dhidi ya hasara. katika chanjo faida ni nyingi kuliko hasara. Hapa tanzania,chanjo za lazima ni BCG (kumkinga mtoto dhidi ya severe forms of TB); DPT-HB (kumkinga mtoto dhidi ya Kifaduro,tetanus, na Polio-na Hepatitis B) na miezi tisa mtot huchanjwa dhidi ya surua(Measles). Wengi wetu tunakumbuka jinsi watoto walivyokuwa wanaugua na kufa na ugonjwa wa Surua(Measle) hadi miaka ya mwanzoni ya tisini. Leo measles Tanzania inaelekea kuwa Historia. Polio (ugonjwa wa kupooza miguu; mojawapo ya causes kubwa ya ulemavu nchini miaka ya nyuma leo ni Historia). Tanzania ni kati ya nci zinazofanya vizuri africa katika kuwafikia watotot wengi na chanjo. Ubishi huu mnaouonyesha hapa wanaufanya huko Nigeria, na leo hii Nigeria ni kati ya nchi chache ambazo bado watoto wanaugua Polio (na hivyo kuwa walemavu). Duniani kote chanjo hizi na nyingine nyingi tu zinatolewa; kwa mfano kwa nchi zilizoendela watumishi wa afya wote(na wanaofanya kazi ya kulea watotot na wazee nk) lazima wapate chanjo dhidi ya Hepatitis B, kitu ambacho hata madaktari TZ wanapigania ili waweze kujikinga dhidi ya ugonjwa huu hatari na unaoambukizwa kwa njia ya damu na majimaji ya mwili kama mate. Marekani (hata watu wazima) wanachanja dhidi ya Flu nadhani kila mwaka.

labda , kwa ufupi sana nieleze chanjo zinafanyaje kazi: Unapochanjwa, unapewa dozi ya vijidudu (kama ni chancho ya surua basi unapata dozi ya measle virus) kwa kiasi ambacho hakitaleta ugonjwa kwa mwili wako bali kitaufanya mfumo wa kinga wa mwili wako kuweka kumbukumbu na kuwa tayari kuukabili ugonjwa wa Surua.

Kuhusu madhara: hakuna dawa isiyo na madhara, hata Panadol ukisoma pale kwenye box kuna side effects.
 
Nimefurahi kwakuwa umesema hawakulazimishi, na hili ndilo linalofanya watu tuanze kuhoji. kumbe huko hawalazimishi. Mi nachukia pia tabia ya kusema kupima ukimwi ni hiari wakati huo huo wamama wajawazito wanalazimishwa kupima. Wakitaka twende sawa wasitulazimishe chochote.

Well, hawakulazimishi in the sense kwamba anakuambia "leo mtoto anatakiwa apate chanjo 1, 2,3 etc, ok? ukikubali lazima usaini documents ambazo wanakuwa wameandika terehe ya chanjo, aina ya chanjo, batch no., chanjo imetengenezwa lini etc.

Niliwahi kuahirisha chanjo moja ya mtoto simply because mume wangu alikuwa na mashaka nayo, daktari hakunilazimisha ila anishauri pros and cons zake na akaniambia "go talk to your husband, but its very important that you protect your child" basi nikaondoka bila kumchanja ila nilikuja kumpeleka baadae akachanjwa.
 
Duniani kote chanjo ni muhimu, tena kwa wenzetu walioendelea ndio usisema, hawakulazimishi isipokuwa mazingira yatakulazimisha
Kwa huku kwetu labda tuhofie kuwa wanaongezea na mambo mengine kwenye hizo chanjo lakini sio kusema chanjo hazifai
Nigeria kuna watu wabishi hawazikubali chanjo eti ni mpango wa kuwamaliza sasa hivi watoto wanakufa na mapolio wanakuwa vilema kwa madegedege nk aibu
 
hakika jf ni shule kwani sikujaliwa hekima ya kuyajua haya. kuanzia leo kwangu no chanjo.

Mkuu for God sake peleka watoto wako wakapate chanjo achana na mawazo ya watu wasio na ushahidi wowote zaidi ya hofu zao.
Kama
Omba mungu mwanao asijepatwa na degedege au sijui kifaduro maana akipona ujue ndio kilema maisha atakuwa mtu wa kubebwa
Talking through experience broda, kwa macho yangu nimeshuhudia
 
me am working hospital huku ughaibuni ... chanjo ni muhimu kwa mtoto mchanga .. plz acheni hizo propaganda .. chanjo zipo dunia nzima...
 
Back
Top Bottom