Chanzo cha kuendelea kwa Umasikini na Ujinga ni CCM

Chanzo cha kuendelea kwa Umasikini na Ujinga ni CCM

Umaskini wetu ambao mahala kwingine umetopea, ujinga tulionao unaosababisha maradhi kwa watanzania wengi chanzo chake ni CCM.

Siku CCM ikiondoka madarakani, Umaskini utapungua, ujinga utakuwa kwa watu wachache na maradhi yatadhibitiwa.
Hebu fafanua kidogo mkuu huo umaskini utaondokaje Kwa kuondoka ccm?
 
Tatizo ni tabia za waafrika.

Hata hao vyama vya upinzani nao wanashikana uchawi kufuja fedha za ruzuku nk
 
Siku ukikua na kukomaa kiakili na kimawazo ndio siku utakomboka kutoka kwenye umasikini na ujinga. Nasikitika kusema kwamba kwa mawazo kama yako ambaye in kijana bado kama taifa tuna safari ndefu, kama vijana wana mawazo ya kuletewa samaki badala ya kujifunza kuvua, ni nini hatima ya taifa letu kwa kuendelea kuamini vijana in tqifa LA Leo na kesho?
 
Acha upotoshaji wako hapa ,, Tangia tupate Uhuru serikali ya CCM imekuwa ikipambana na maadui ujinga maradhi na umaskini kwa Kasi ya mshale, mfano katika kupambana na umaskini serikali ya CCM imeweka mazingira wezeshi kwa kila mtu kuweza kunufaika na fursa mbalimbali zinazopatikana hapa nchini, serikali imejitahidi kutumia Rasilimali zetu katika kuboresha huduma za kijamii na Miundombinu ambayo imemsaidia mtanzania katika kujikwamua kiuchumi, mfano kwa Sasa mkulima anaouwezo wa kusafirisha mazao yake Hadi sokoni kwa urahisi kabisa

Lakini pia usambazaji wa umeme Hadi vijijini umefungua fursa nyingi za kiuchumi na kusaidia vijana na makundi mengine kuweza kujiajiri kwa urahisi na hivyo kujipatia kipato na kuondokana na umaskini kwa mtu mmoja mmoja,

Katika kilimo pia ambayo Ni secta tegemezi kwa watu wengi serikali imekuwa ikiongeza bajeti mwaka Hadi mwaka mpaka Sasa kufikia billioni Mia Tisa na point, Hali hii imesaidia kuongeza uzalishaji na kupunguza umaskini kwa kaya nyingi hapa nchini, hii Ni pamoja na kuhakikisha mkulima anapata soko la uhakika, lakini pia serikali imekuwa ikitoa Ruzuku kila inapowezekana Kama ilivyofanya kipindi hiki kwa kutoa Ruzuku ya billion Mia moja hamsini na kupelekea kushuka kwa Bei ya mbolea sokoni

Katika Elimu nako juhudi za serikali zimekuwa kubwa Sana ikiwa Ni ongezeko la uandikishaji wa wanafunzi shule za msingi ,kuongeza ujenzi wa madarasa na shule mpya ili kuendana na ongezeko la wanafunzi, vyuo vya Kati na hata vya Elimu ya juu navyo vimeongezwa na serikali, hivyo kutoa fursa kwa vijana wengi kupata Elimu bila shida yoyote, hapa pia serikali imeondoa vikwazo vya kupata Elimu hata kwa wanafunzi wanaotoka familia maskini kwa serikali kufuta ada kuanzia shule za msingi Hadi sekondari, lakini pia serikali imekuwa ikiongeza bajeti ya Elimu ili vijana wengi wapate fursa ya Elimu ya juu

Katika Afya pia serikali imejenga zahanati kwa kila Kijiji na pia vituo mbalimbali vya Afya vimejengwa maeneo mengi hapa nchini ikiwemo 234 vilivyo jengwa hapa majuzi tu, hii imepunguza vifo vya mama na mtoto, lakini pia watanzania wengi Sasa wanapata huduma karibu kabisa na maeneo yao, huduma mbalimbali za kibingwa zimekuwa zikitolewa katika hospitali zetu za Kanda na Taifa ambapo awali wagonjwa walikuwa wanalazimika kwenda nchi za nje na wale wakipato Cha chini walikuwa wanaishia kupoteza maisha,

Mambo iliyoyafanya serikali ya CCM ni mengi Wala siwezi kumaliza kuyaelezea hapa, kikubwa nakushauri tu kuwa nenda kawaambie chadema wenzio kuwa watu wanasema ni aibu kwa chadema kukaa miaka yote na kupokea mamilioni kwa mamilioni Kama Ruzuku lakini mmeshindwa kujenga hata ofisi za makao makuu na kuishia kuzitafuna zote na kulewea mapombe tu, watu pia wanauliza pesa mlizochangisha majuzi za join the chain zipo wapi? Mbona kimya au nazo mmepeleka kwenye pombe?

Mwisho Ni kuwa watanzania Wana Imani na matumaini makubwa Sana na serikali ya CCM chini ya mh Rais wetu mpendwa mama Samia suluhu Hassani, na kwamba hawana habari Wala mpango wa kuwaunga upinzani uliyojichokea na kukosa ajenda na Sera za kueleweka, wanasema wameshawapuuza kwa Sasa na kuwaacha na ubabaishaji wenu
 
Siku ukikua na kukomaa kiakili na kimawazo ndio siku utakomboka kutoka kwenye umasikini na ujinga. Nasikitika kusema kwamba kwa mawazo kama yako ambaye in kijana bado kama taifa tuna safari ndefu, kama vijana wana mawazo ya kuletewa samaki badala ya kujifunza kuvua, ni nini hatima ya taifa letu kwa kuendelea kuamini vijana in tqifa LA Leo na kesho?
Nadhani mleta mada ana point ila kashindwa kuiwaslisha na kuitetea. Jana niliona hapa makinda akiwaasa vijana wajiajiri wasitegemee kuajiriwa. Mdau akahoji je mwanao(fulani) amejiajiri? Sikuona jibu, na nadhani makinda huwa anapita humu. Ccm ni kanga.
 
Nadhani mleta mada ana point ila kashindwa kuiwaslisha na kuitetea. Jana niliona hapa makinda akiwaasa vijana wajiajiri wasitegemee kuajiriwa. Mdau akahoji je mwanao(fulani) amejiajiri? Sikuona jibu, na nadhani makinda huwa anapita humu. Ccm ni kanga.
Hoja imewasilishwa kikamilifu.Asiyeielewa ni kwa kuwa uwezo wake wa kuielewa ni mdogo.

Yeye anazungumzia kufundishwa kuvua badala ya kupewa samaki, lakini kwenye hii hoja anaonesha anataka kupewa samaki badala ya kuvua.
 
Back
Top Bottom