BUMIJA
JF-Expert Member
- Oct 19, 2011
- 5,950
- 11,295
Nimekua nafanya mahojiano na wanaosomea na waliopo katika ualimu kuhusu kada hii.Leo ukazuka mjadala wengi wanadai kua wanasomea ualimu mana kwao ni masikini wapate ajira haraka,wengine wanadai tumejipachika kwa muda masters ntasomea kitu kingine.Hakuna alioyesema ana wito au ameridhika kua Mwalimu.Waalimu wengi hatujaridhika na kazi tunayofanya au kusomea.Na hili ni tatizo mana hatutakubalika kama hatujikubali.Wengi tunajifanya ni kazi ya mda na ni kua hatufundishi kwa moyo mmoja.Tubadilike waalimu na tujipende na watoto watafaulu.