Chapati za mihogo ni chakula kizuri kwa afya pia kwa uchumi

Chapati za mihogo ni chakula kizuri kwa afya pia kwa uchumi

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
57,761
Reaction score
216,011
Gharama za maisha zimepanda sana, sasa hivi kumudu gharama za mkate asubuhi ili uwe kitafunwa cha kifungua kinywa ni wachache wanamudu.

Hawa watoto wetu wengine hawajazoea kula mihogo ya kuchemsha au viazi vya kuchemsha na chai. Kwa kuwabadilishia tu unaweza kufanya hivi.

Chemsha mihogo mpaka iive, iweke kwenye kinu ikiwa bado ya moto uiponde utapata ugali unaovutana. Ugali huu unaweza kulika na mboga yeyote lakini kama lengo lako ni kutengeneza chapati weka ugali kwenye karai au sinia, weka chumvi, mafuta na hamira na uuache uumuke.

Ukisha umuka kata chapati size unayopenda sukuma kwenye kibao na uoke jikoni.

Chapati hizi huweza kuliwa na mchuzi au maharage kama chakula.

1655306122301.png
 
Laiti ungeambatisha na picha ya chapati zilizotengenezwa tayari tuone zinavyofanana...hata hivyo ahsante kwa kushirikisha.
 
Sawa ila hizo picha ni ngano hiyo sio muhogo naoujua mimi..

Si yameandikwa hapo pika wewe sasa uone mizimu unayotoa..😂
 
Asante hukuwa mbinafsi.
hio kitu tumeifanya sana home ila kupikia huo unga wenyewe tu chapati au mandazi ndio sijawai ila huwa tuna utumia Kwa dharula kuongezea kidogo kwenye unga wa ngano wakati wa kuandaa chapati au maandazi pale unga unapokuwa umepungua.
 
hio kitu tumeifanya sana home ila kupikia huo unga wenyewe tu chapati au mandazi ndio sijawai ila huwa tuna utumia Kwa dharula kuongezea kidogo kwenye unga wa ngano wakati wa kuandaa chapati au maandazi pale unga unapokuwa umepungua.
Ukiwa na food processor unabonyeza button tu na kusubiri mihogo ya kichemsha kuchakatwa kuwa ugali.
 
Back
Top Bottom