Charles Hilary ateuliwa kuwa Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu - Zanzibar

Amefaa kuliko Dr. Ayubu Rioba?
Hongera Sana tena sana kwa Charles Hilaray.
Hakika anastahiki kuwa Mkurugenzi wa mawasiliano Ikulu ZNZ.

ni Mwanahabari Nguli, mweledi asiye na majivuno wala roho mbaya.

Watanzania wote tunamtakia kila la heri ktk majukumu yake mapya.
Amefaa kuliko Dr. Ayubu Rioba?
 
Nitamiss sana kwny Habari UTV!
Ivona Kamunthu atam-misi zaidi yako.

Tayari Baruan Muhuza (Muha) amerithi kigoda cha Charles.

Wajumbe waliomtenda Hillary kwenye kinyang'anyiro 2020 sasa macho juu. Ukiziba riziki ya mtu kwa kufunga mlango isiingie itabomoa dirisha na kuingia. Riziki ya Charles Hillary imebomoa dirisha.

Taswira zote kwa hisani ya google.


Charles Hillary aliyechinjiliwa mbali na wajumbe kwenye kinyang'anyiro 2020. (Mimi ni BWANA Mungu wako nitakuketisha pamoja na Wafalme)


Kada wa chama aliyekuwa kwenye nafasi ya Itikadi na Uenezi Taifa na mmoja wa walioshiriki vikao vya uteuzi wa majina ya wagombea kwenye kinyang'anyiro cha 2020. Vikao hivi vilikuwa na uwezo wa kumvuta hata mgombea aliyekataliwa na wajumbe na akasimamishwa kugombea. (1Kor.1:20 Yuko wapi mwenye hekima? Yuko wapi mwandishi? Yuko wapi bingwa wa mjadala wa nyakati hizi? Je, Mungu hakufanya hekima ya ulimwengu huu kuwa ni ujinga? ) pia (Mungu Hutumia Vitu Vinyonge Ili Kuvipinga Na Kuviaibisha Vyenye Nguvu; Hutumia Vitu Vipumbavu Ili Kuviaibisha Vyenye Hekima) Mungu amemtumia Charles Hillary!


Mojawapo ya vikao vya juu vya chama vifanyavyo maamuzi yakiwemo yale ya kinyang'anyiro.

Charles Hillary naamini huo ni mwanzo tu, utastaafu kama ama Katibu Mkuu wa wizara, RC au Mkurugenzi Mkuu wa taasisi.
 
Alkua analipwa shilingi ngapi? Sababu waswahili wanasema mbongo mpe picha tu stori nzima anatunga
Milioni Kumi kwenda juu,chanzo jamaa yangu Yuko pale mtangazaji.charles alikua mkurugenzi wa radio.habari kwenye TV alikua anasoma tu.
 
Inasemekana baba yake alikuwa rafiki na Rais Karume( Mkubwa). Maji hufuata mkondo, kama baba Yako anaurafiki na walima nyanya basi nawe utakuja kuwa mkulima wa myanya badae. Tuwaombe wazee wawe wanajiatach kwa marafiki wa maama
 
Machalanga si juzi tu hapa. Charles Hilary alianzia RTD ya kina Deborah Mwenda
 
Kwani jamaa ni Tiss?
Kama alikuwa mtoto wa Polisi unategemea nini mkuu? Ikulu hateuliwi mtu ambaye siyo wa system. Najiongeza kwamba hata DW huenda alikuwa anafanyakazi ya nusanusa, hii dunia kubwa hii.
Milioni Kumi kwenda juu,chanzo jamaa yangu Yuko pale mtangazaji.charles alikua mkurugenzi wa radio.habari kwenye TV alikua anasoma tu.
Mkuu, kwani Azam wana kituo cha redio pia?
 
Inasemekana baba yake alikuwa rafiki na Rais Karume( Mkubwa). Maji hufuata mkondo, kama baba Yako anaurafiki na walima nyanya basi nawe utakuja kuwa mkulima wa myanya badae. Tuwaombe wazee wawe wanajiatach kwa marafiki wa maama

Anza wewe kujiatach na watu wa maana kwa ajili yako na watoto wako.
 
Natamani 2025 tumpe Mh. Dr Hussein Mwinyi Bara kwa miaka 10.
Mkuu Zogwale,

Lakini duru zinasema Dr. Mwinyi ni Dr. Magufuli per se (replica) kwa SMZ (groomsman of the bridegroom) hivyo ukimtamani Dr. Mwinyi ni sawa na kumtamani Dr. Magufuli maana hapana tofauti kati ya Myahudi na Myunani.

Aidha, ikumbukwe hapo awali Dr. Magufuli alikuwa na ndoto za kuibadili Znz kbs kimaendeleo, ndoto ambazo amemrithisha Dr. Mwinyi ambaye sasa anaipeleka Znz viwango vingine kbs katika historia ya mapinduzi ya visiwa hivyo vya karafuu, mwani na vanila.

Inaaminika kwamba ifikapo 2025 chini ya Dr. Mwinyi, Wazanzibari watajikuta wanakosoa majira na nyakati kwamba ili Znz isingechelewa kimaendeleo Dr. Mwinyi alitakiwa kuwa rais baada ya Abeid Karume na siyo kipindi hiki.


Taswira kwa hisani ya google.
 
Marin Hassan Marini toka ARIDHIO.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…