Chato pajengwe Chuo Kikuu cha Afya kama MUHAS

Chato pajengwe Chuo Kikuu cha Afya kama MUHAS

Wanabodi salaam.

sitokei kanda ya ziwa na wala sipapigii debe Chato nyumbani kwa Mzee JPM, ila naleta mada hii kwa maslahi mapana ya Taifa letu.

Pale Chato pamejengwa Hospitali kubwa ya Rufaa ya Kanda, ina majengo mazuri sana na nina Imani hata vitendea kazi pia, lakini nna mashaka bado idadi ya wagonjwa ni ndogo hata ukilinganisha na ya pale Bugando, wengi wamepiga kelele kuwa Mzee JPM alivutia kwao, sawa but ni Tanzania moja hii.

Nashauri ili kuipa hii hospital ubize na kuweza kufanya kazi kwa viwango kama ulivyo ukubwa wake pale Chato pajengwe Chuo kikuu cha Afya kama ilivyo MUHAS.

Chuo kiitwe tu Chato University of Health and Allied Sciences (CUHAS), tukifanya hivi maana yake wanafunzi wa CUHAS wataitumia hii hospital ktk mafunzo yao kama ilivyo wa MUHAS wanavyoitumia MNH. hii itasaidia sio tu kutibu watu wengi pale lakini pia kuongeza fursa kwa watanzania wanaotaka kusomea kada za Afya kwa kuongeza wigo mpana wa vyuo lakini pia kutaongezeka Ajira.

Nawasilisha, aone Rais Samia Suluhu ili aone namna.
MATAGA ndio mmebaki wachache,mnaendelea kupoteana
 
Mwanzo wa chato kupotea kwenye ramani za kisiasa na kipaumbele...
 
Mtoa mada nakuunga mkono unaona mbali sana.
Huyu dictator uchwara alikuwa anatumia sijui matope kufiri
Hakuna sehemu amechoma mabilioni kijinga kama kwenye hiyo hospital,. sijui yale majengo watafanyia nini asee
 
Kwa kweli kuna haja ya kutafuta matumizi bora ya miundo mbinu kama hiyo kuliko kuiacha ikiharibika bure, kama kutumika kama hospitali ya rufaa inapwaya! Raslimali za umma nyingi zimetumika pale, kwa kukurupuka au la lakini tusiziache zikapotea bure!
Mkuu na hiyo ndo hoja yangu haswaa, kuwa tumeshawekeza pale tusipaache tukapoteza fedha bure, so ni bora kuongeza ubunifu ili pawena manufaa zaidi mtambuka
 
Mtoa mada nakuunga mkono unaona mbali sana.
Huyu dictator uchwara alikuwa anatumia sijui matope kufiri
Hakuna sehemu amechoma mabilioni kijinga kama kwenye hiyo hospital,. sijui yale majengo watafanyia nini asee
ndo mana nashauri kuboresha zaidi ili pasijifie bure Mkuu
 
Kwanza kuhitimu katika chuo kama hicho, itakuwa ni kubeba laana fulani katika maisha yako.
 
Duh, kwa hiyo Geita Gold ikipanda daraja ikachezee Chato wilayani iache mkoani. Hauko serious ndugu yangu.
hata ule uwanja wa kisasa wa mpira uharakishwe geita gold wanapanda ligi kuu wanahitaji uwanja wa kisasa atleast watu 50,000
 
Wanabodi salaam.

sitokei kanda ya ziwa na wala sipapigii debe Chato nyumbani kwa Mzee JPM, ila naleta mada hii kwa maslahi mapana ya Taifa letu.

Pale Chato pamejengwa Hospitali kubwa ya Rufaa ya Kanda, ina majengo mazuri sana na nina Imani hata vitendea kazi pia, lakini nna mashaka bado idadi ya wagonjwa ni ndogo hata ukilinganisha na ya pale Bugando, wengi wamepiga kelele kuwa Mzee JPM alivutia kwao, sawa but ni Tanzania moja hii.

Nashauri ili kuipa hii hospital ubize na kuweza kufanya kazi kwa viwango kama ulivyo ukubwa wake pale Chato pajengwe Chuo kikuu cha Afya kama ilivyo MUHAS.

Chuo kiitwe tu Chato University of Health and Allied Sciences (CUHAS), tukifanya hivi maana yake wanafunzi wa CUHAS wataitumia hii hospital ktk mafunzo yao kama ilivyo wa MUHAS wanavyoitumia MNH. hii itasaidia sio tu kutibu watu wengi pale lakini pia kuongeza fursa kwa watanzania wanaotaka kusomea kada za Afya kwa kuongeza wigo mpana wa vyuo lakini pia kutaongezeka Ajira.

Nawasilisha, aone Rais Samia Suluhu ili aone namna.
Wewe unachokonoa tu ,maana huo ndo ulikua mpango wa mwendazake kuunganisha Muhimbili na udsm kada ya afya main campus kua chato, mwendazake alikua mbinafsi haijawai tokea, kidogo tu angeamisha na bunge
 
Back
Top Bottom