Chato yatangazwa kuwa kitovu cha Utalii Kanda ya Ziwa

Dodoma imebuma sasa mwendo ni Chato,hata hivyo sijaelewa mantiki ya kuweka kila kitu Chato.Hasa wakati miradi ya kujenga Mji mkuu Dodoma,Bwawa la Nyerere, SGR,Daraja la Busisi,bado haijakamilika.
Bado Chato ina wakazi wachache mno kuweka shughuli za kiserikali za kikanda hapo.
Je kwanini tusijenge viwanda vya kufua chuma huko Liganga vitakavyotuwezesha kujitosheleza kupata chuma ya kutosha kufungua viwanda vingi vya mazao ya chuma?
Kwa mwendo huu kilichobakia Chato ni kuunganishwa reli ya SGR kutokea Isaka kwenda Rwanda na Uganda.
 
Kitovu cha utalii ni mji Wa MUGUMU wilayani Serengeti mkoani Mara mana ni rahisi sana kwa mtalii kufika huko kujionea maajabu ya dunia.
Ngoja raisi atoke Mara. Haiwezekani mbuga kubwa iwe Mara afu mugumu pawe pa kifala hivi.
Jk alitaka uwanja Wa ndege mkubwa ujengwe Mugumu na watu walilipwa wakahama.
Yani haya Tanapa HQ Mara mana ndo kuna mojawapo wa kivutio kikubwa duniani na kinajulikana
 
TZ kuna maeneo yamepiga hatua za maendelea kutokana na sababua za kihistoria e.g. wakoloni waleweka makazi yao huku, n.k. Haya maeneo kwa vile yana mwanga wa maendeleo yataendelea kujikongoja kwenda mbele. Ole wa maeneo ambayo yako nyuma na hayajapata kiongozi "jasiri" wa kuhamishia kila kitu huko, hawa wataenedlea kuhesabu nyota.
 
Baada ya kuitangaza Serengeti mkoani mara yenye mbuga kubwa Zaidi Africa ambayo imewahi kuwa among the seven wonders of the world Leo Chato
 
Aisee......Chato kuna kivutio gani cha maana mpaka iwe Kitovu? Ivi Serengeti si ipo lake zone? Kwamba Chato kuna vivutio zaidi ya Serengeti.........???
 
The young bird does not crow until it hears the old ones.

N.B Same thing happen to dogs and SAME THING HAPPEN TO HUMANS.
 
No impact whatsoever! TBC ndio jukwaa lao la kuvutia watalii wa nje!

Waziri wa utalii aliyekuwa ana hit right target ni Nyalandu. Afadhali yeye tulikuwa tunamwona kwenye vyombo vikubwa vya nje akiongelea vivutio vya Tanzania!

Hawa wengine bora hata wabakie kuuza vivutio vya Tanzania kwa WASANII WA TANZANIA. Uko nje awachelewi kusema njooni Tanzania kuna maji safi.. What an embarrassment!!
 
safi sana naamia huko nami niambulie kigogo

kanda ya ziwa oyeeeeeeeeeee yees maguuu oyeeeeeeee
 
Chato ni bab kubwa, yaani unaambiwa hospitali ya Chato Ina hadhi ya juu kuliko Bugando.
Fafanua vizuri, hadhi kuliko Bugando unamaanisha majengo, madaktari wa chato NI mahiri kuliko wa Bugando, vifaa tiba ni vya kisasa zaidi ya Bugando na Wana uwezo wa kutibu maradhi ambayo Bugando hawawezi au una maanisha kitu gani hasa inaizidi Bugando ili tuweze kwenda huko chato badala ya Bugando.
 
Duwa la kuku Hilo, badala ya kuchangia mjadala upendekeze Cha kufanya ili haya maupendeleo yasiendelee wananchi tukuelewe wewe unakuja na utani.
 
Yaani siamini nachokisoma, sijui tulilogwa na nani, mtu mzima na akili zake anasema kuna utalii wa maji! Mbona yapo dunia nzima?

Huyo alietuloga sasa hivi amekaa mahali anatucheka kweli.
Mmerogwa na Mbowe na kweli anawacheka akiwaambia muandamane mnakimbilia kwenye keyboard.
 
Utalii wa upendeleo ukanda na ubaguzi wa kikabila au sio ?
 
Hapa bongo wenye PHd wengi ni kama plain paper tena wamejazana kwenye ofsi za umma wanakula bure pesa za umma wakati output zao ni almost zero.
 
Siyo Mara kwenye Serengeti?
unashindwa kuwa muelewa.sawa serenget,ni kivutio pekee dunian.ila unafikir mtalii huwa mda wote anaangalia wanyama?

anaposema wazir kafikia uamuzi kama huo based on criteria/vigezo.
familia za kitalii huja makund makund au mtu mmoja mmoja kulingana na bajeti ya muhusika,sio muda wote kuangalia masimba tuu,atataka na kufanya vingine,
kuna ziwa ambalo tyari uwepo wake ni kivutio tosha cha utalii wa Majini kwa kuanzia beach tourism,uvuaji samak wa watalii, safari za boat,.Pili kuna kisiwa cha Rubondo,hiki pekee ni kivutio tosha,pale ukifanyika uwekezaji kuanzia bandari ya Chato ambapo kungewekwa boti za kisasa na uwekezaji ukifqnyika ina maana kila wiki makund kwa makund ya watalii kwa kuanzia wa ndan watakua wanatembelea Rubondo,saa nyibgine watu wanakod boti kufanyq utalii wa kuvua sangara kwa kutumia ndoano maalum,ukija kwenye wanyama nao wapo sasa kwa nini kusipewe kipaumbelee??
utalii sio wamyama tuuuu,kuna utalii wa vyakula,utalii wa utamduni utalii wa kila kitu.ni wkaat sasa wa wizara husika kupainua kuwapa watalii machaguo .mlaji anachagua wap aensde ima kaskazain au kanda ya ziwa akaone utalii mchanganyiko. sekta ya utalii usiitizame katika angle ya wanyama tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…