Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 21,967
- 32,074
Chato ya kwanza ni kitabu kipya kinachoeleza historia ya kijiji cha Chato Tanzania.
Chato ya pili ni jina la movie iliyochezwa mwaka wa 1972 muigizaji akiwa Charles Bronson.
Kitabu cha Chato kama ingekuwa movie ingekuwa na waigizaji wakubwa wa sifa.
Halikadhalika ingekuwa movie ya kuvutia na kusisimua sana khasa ukizingatia kuwa "script writers" ni waandishi watatu mashuhuri sana katika tasnia ya uandishi wa magazeti.
Kitabu kina kasi kubwa. Ni kitabu cha mkasa mmoja kwenda mwingine.
Mikasi ikifatana na maelezo ya wahusika wakuu.
Ingekuwa movie tungesema ina "dialogue," ya kuvutia.
Ukianza ukurasa wa kwanza hukifungi na kukiweka chini hadi umegonga tamati.
Movie Chato's Land wachambuzi wa senema wanasema haina, "dialogue," yaani mazungumzo ni kidogo sana.
Matukio ya unyama na ubabe wa Sheriff na kundi lake la askari Wamarekani wanaomtafuta Apache jina lake Chato aliyemuua Shariff umechukua nafasi ya mazungumzo.
Mambo haya mawili ndiyo yaliyonipelekea kurudi nyuma kuangalia upya senema niliyoiona miaka 50 iliyopita Empire Cinema na kutaka kujua kama kuna kipi naweza kufananisha kati ya kisa cha Chato ya Tanzania ya leo karne ya 21 na kwao Chato, Apache Muhindi Mwekundu aliyethubutu kumuua Sheriff katika mji wake.
Walioshuhudia ugomvi ule walisema kuwa Sheriff ndiye aliyemchokoza Chato kisa kaingia kwenye "salon" ya Watu Weupe ilhali yeye kwa upande wa mama ni Red Indian mtu dhalili hana hadhi kunywa whisky pamoja na Wazungu lau kama baba yake ni Mweupe.
Kaingia mahali si pake.
Lakini Chato akivaa nguo kama Mmarekani yeyote yule na akijihisi hivyo.
Sheriff yeye kachukizwa na kule kujifaragua huko.
Hapo ndipo ugomvi ulipoanza na kuishia kwenye kuchomoleana bastola.
Sheriff akisimama kwenye dhana kuwa pale ni kwake ana madaraka ya utawala.
Hiki ndicho kilichomponza.
Kalamu na akili ya binadamu kuna wakati vinakutana na kuhadithia hadithi moja katika miaka iliyopishana sana.
Chato huyu wa Marekani ya karne ya 19 hata kwa mbali hakupata kuwaza kuwa mkasa wake utakuja siku moja kufananishwa na kijiji chenye jina lake Afrika.
Chato ya pili ni jina la movie iliyochezwa mwaka wa 1972 muigizaji akiwa Charles Bronson.
Kitabu cha Chato kama ingekuwa movie ingekuwa na waigizaji wakubwa wa sifa.
Halikadhalika ingekuwa movie ya kuvutia na kusisimua sana khasa ukizingatia kuwa "script writers" ni waandishi watatu mashuhuri sana katika tasnia ya uandishi wa magazeti.
Kitabu kina kasi kubwa. Ni kitabu cha mkasa mmoja kwenda mwingine.
Mikasi ikifatana na maelezo ya wahusika wakuu.
Ingekuwa movie tungesema ina "dialogue," ya kuvutia.
Ukianza ukurasa wa kwanza hukifungi na kukiweka chini hadi umegonga tamati.
Movie Chato's Land wachambuzi wa senema wanasema haina, "dialogue," yaani mazungumzo ni kidogo sana.
Matukio ya unyama na ubabe wa Sheriff na kundi lake la askari Wamarekani wanaomtafuta Apache jina lake Chato aliyemuua Shariff umechukua nafasi ya mazungumzo.
Mambo haya mawili ndiyo yaliyonipelekea kurudi nyuma kuangalia upya senema niliyoiona miaka 50 iliyopita Empire Cinema na kutaka kujua kama kuna kipi naweza kufananisha kati ya kisa cha Chato ya Tanzania ya leo karne ya 21 na kwao Chato, Apache Muhindi Mwekundu aliyethubutu kumuua Sheriff katika mji wake.
Walioshuhudia ugomvi ule walisema kuwa Sheriff ndiye aliyemchokoza Chato kisa kaingia kwenye "salon" ya Watu Weupe ilhali yeye kwa upande wa mama ni Red Indian mtu dhalili hana hadhi kunywa whisky pamoja na Wazungu lau kama baba yake ni Mweupe.
Kaingia mahali si pake.
Lakini Chato akivaa nguo kama Mmarekani yeyote yule na akijihisi hivyo.
Sheriff yeye kachukizwa na kule kujifaragua huko.
Hapo ndipo ugomvi ulipoanza na kuishia kwenye kuchomoleana bastola.
Sheriff akisimama kwenye dhana kuwa pale ni kwake ana madaraka ya utawala.
Hiki ndicho kilichomponza.
Kalamu na akili ya binadamu kuna wakati vinakutana na kuhadithia hadithi moja katika miaka iliyopishana sana.
Chato huyu wa Marekani ya karne ya 19 hata kwa mbali hakupata kuwaza kuwa mkasa wake utakuja siku moja kufananishwa na kijiji chenye jina lake Afrika.