Chenge ashikiliwa polisi kwa ajali ya gari iliyosababisha vifo

"Changa la macho!Kwa kitendo cha ajari na kuua watu na kujisalimisha polisi kisheria sawa lakini kama ajali na mtu kama change kutiwa ndani wakati uchunguzi unaendelea ili ni changa la macho kwani tukio lake tofauti na la Ditto ambae alimpiga mtu risasi.Ingeniingia kichwani kama Change angelijisalimisha katika vyombo vya sheria kwa tuhuma za rushwa na ufisadi.Tunafahamu ya kua serikali ya Uingereza imekamilisha uchunguzi wake na kuwataja wahusika.Hapa serikali badala ya kuchukua hatua na kumkamata mtu huyu kwa makosa ya ufisadi na kumkabidhi katika vyombo vya sheria wanaanza kuzusha makosa mengine ili kutupoteza na kutusahaulisha makosa makubwa yanayomkabili Mzee wa visenti sasa gumzo wanataka kulihamishia katika ajali.Sitashangaa kama hiyo ajali imepangwa au hakuwepo kabisa hilo ni changa la macho.MUNGU IBARIKI TANZANIA.'

***********************

ADVOCATE JASHA: Umenena. huyu mtu asipotiwa mbaroni kwa ufisadi wa radar atatumalizia wananchi wetu kwa kuwaua pole pole. Ni bora akasweka ndani haraka sana
 
Jamani naomba msaada hivi hiyo gari iligonga Bajaj tu au baada ya hapo iligonga kitu kingine kwani hiyo gari ya Mzee wa visenti ilivyolivyobondeka nashindwa kuamini kwamba kwa kuigonga Bajaj ingelibondeka kiasi hicho.Hilo ni changa la macho jama anataka kuyahamishi macho na mawazo yetu katika ajali na kutusahaulisha swala la rada ambpo serikali ya Uingereza imekamilisha uchunguzi na huyu Bwana anatajwa katika sakata la rada.Cha kusikitisha kwa kuafuatitilia mjadala unavyoendelea nagundua kwamba wengi tumeisha pigwa chenga ya mwili au tumefungwa goli la kisigino.Naombeni tulitizame swala hili kwa mtizamo mwingine na sio SUBSTITUTION ya sakata la rushwa na ufisadi{Rada}MUNGU IBARIKI TANZANIA
 
halafu hiyo Bajaj inaonekana iligongwa kwa mbele ,watu habari inaonesha wamepotosha ukweli ,kwa jinzi picha cinavyoonekana ni kuwa hii ilikuwa face to face.
Ndugu umeiangalia vizuri hiyo picha ya bajaj? Mbona vyuma vyake vimeelekea mbele ikimaanisha msukumo ulitokea nyuma? Kama ni face to cace, kwa vyuma vya bajaji wala sura yake isingeonekana hata taa ya mbele isingebaki
 
Hivi zile picha kule kwenye ile link ni za leo?? Yaani kaua watanzania aliokwishawaibia then anacheka huku anapunga mikono kana kwamba kaua ndezi....😡😡
 

Hivi zile picha ...Yaani kaua watanzania aliokwishawaibia then anacheka huku anapunga mikono kana kwamba kaua ndezi....😡😡

Si afadhali Chenge anajulikana moyo wake mkavu hana huruma, mimi hao maafande wanaojichekesha ndio hata sielewi kilicho funny kuhusu ajali ni nini yani.

Halafu hatufundishwi toka utoto kuwa ajali ni noma, usalama barabarani ni muhimu, watoto wanaachiwa waje kupiga chabo katikati ya scene of an accident, katoto kamoja kakilimwa na truck hapo sijui itakuwaje.
 
We were made to believe that this man is a 'night mover' a behavior known to be a permanent sticker.
Should we connect this remorseless behavior with the practice?

The useless men in power!
 
Si afadhali Chenge anajulikana moyo wake mkavu hana huruma, mimi hao maafande wanaojichekesha ndio hata sielewi kilicho funny kuhusu ajali ni nini yani.


Labda wanashangilia wamepata camera moment...
 
Hata barara zenyewe zimekalia kusababisha ajali,hivi taa za barabarani zilikuwa zikiwaka ,halafu hiyo Bajaj inaonekana iligongwa kwa mbele ,watu habari inaonesha wamepotosha ukweliwa jinzi picha cinavyoonekana ni kuwa hii ilikuwa face to face.
abu


Shekhe,
Ebu chondechonde usiaangalia kiarabu vile yaani kuanzia kulia kwenda kushoto. Kusingekuwa na picha hizo tungekuelewa. Iweje igongwe kwa mbele halafu iharibike nyuma?
 
Dah izo picha zinawaonyesha watoto ,kwa kweli Tz ni shida ndio mnaona wenyewe hapo ,sisi tunayajua maana tupo katikati ya jiji,si mnawaona hao watoto hata nywele hawana ,nywele zinakataa kuota kwa ziki ,hawana lishe bora.Ndio maana yake.Hakuoti kitu.

je ingekuwa watoto wa tandika sijui wangekuwa na hali gani, siju ungesemaje
 
nasikia ajali ilipotokea mh alifuatwa na gari ingine kupelekwa hm, na polisi wawili waliletwa na taxi kuja kulinda gari yake mpaka ilipochukuliwa na breakdown, kumbe aliwapa taarifa nao wakamwambia mh. kapumzike tunashughulikia, kwahiyo system ilijuwa na wakapanga iweje, ik mwenyewe amesema alikuwa akidrive kati ya 80-100 km,si tayari ameshavunja sheria? lakini tuiache system ifanye kazi kama inavyofanya.
 

Perfect observation. Ukiunganisha na analysis ya Moelexe53 hapo juu kila kitu kinajieleza wazi. Kama anasema alikuwa anaenda mwendo wa kati ya 80 km na 100 km ina maana yeye ndiye alikuwa anajaribu kuovertake. Bajaj sana sana ikienda maximum speed haiwezi kuzidi 50km/hr. Na kama mwendo wake ndio huo na Vijisenti alikuwa speed hiyo no wonder aliigonga bajaj. Reckless driving at its best period.
 
kumbe watu walimuona na kusema chenge chenge (statement yake)
ndio maana akarudi polisi na kama watu wasingemuona asingerudi polisi
lazima alirudi nyumbani akawasiliana na polisi na wakubwa usika halafu ndio wakamwambia aende wao wa take business
cha kushangaza tyre ipo flat alirudije nyumbani?
kama alirudi nyumbani na gari inamaanisha na zile damu na nyama zinazoning'inia (sio kafara hii)
 
Hiyo barabara ya hapo mjini watu mnaendesha speed ya 80 to 100 km/h? Kweli ndio maana mnaua watu. Hiyo barabara haitakiwi kuzidi 60km/h.
 

Yaani vijisenti vyote hivyo alivyonavyo hata insurance inamshinda kulipa au wakuu mnamsingizia kuhusu hizo pesa Jersey
 
yule aliyempiga kofi Mzee Ruhsa alisamehewa na mzee ruhusa lakini Jamhuri ilipress charge, sasa na mzee wa vijisenti ameendesha gari bila ya bima na akiwa na kilaji sijuwi sheria za bongo zinasemaje? sheria zipo mbili ya kabachodi na wazee na ya pili ya walalahoi
 
Chenge kapata ajali kagonga bajaj watu wawili wamekufa papo hapo.
Hilo ni tatizo la kwanza.

Tatizo la pili.

Dar tunatumia usafiri wa Bajaj. Je usafiri huu ni salama?
 

Unataka kufanananisha ulimwengu wa kwanza na ulimwengu wa tatu ???wapi na wapi tena ulimwengu wenyewe wa tatu ni TANZANIA.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…