Chenge ashikiliwa polisi kwa ajali ya gari iliyosababisha vifo

Chenge ashikiliwa polisi kwa ajali ya gari iliyosababisha vifo

Wakuu niulize kitu kimoja.. Hizi Bajaj huwa haziko registered?.. ina maana mtu akikimbia hawezi kutafutwa kwa njia yoyote kupitia vitambulisho vya mmliki wa Bajaj hiyo!...
Hakika nadhani sasa tuna kila sababu ya kuwa na vitambulisho maanake madereva wote siku hizi wakiua wanatoka mkuku tu na hawapatikani tena..Tukumbuke kifo cha Salome Mbatia..

Mkuu, bajaji zinasajiliwa na hii inayohusika na ajali hii ni yenye namba T736 AXE ambayo inamilikiwa na Zuwena Feith. Polisi wamemtaka Zuwena ajisalimishe ili asaidie polisi hasa kuhusu dereva aliyetoroka baada ya ajali.

But who knows labda dereva ameambiwa akimbie au alikufa na wameficha ili kesi iwe rahisi kwa mheshimiwa. Kwa spidi waliyokuwa nayo wote wawili, siyo rahisi kwa dereva wa bajaji kutoka mzima na kuweza kukimbia.
 
Understably perhaps the JF Mob wants to crucify Chenge lakini in this matter.. jamaa haguswi kwakweli... Anakosa la kutokuwa na insuarance lakini dereva wa bajaj kutoweka imempa jamaa nafasi nzuri yakuonekana msafi... And to be honest Bajaj pale maisha hua zina jichomeka barabarani so atakama Chenge alikuwa kawaka wmanzo mwisho.... bajaj hazina safety features nothin.. mimi personally sipandi..lol and never will..its just dangerous..

Unajua ishu sio ku-crucify Chenge; Sheria za barabarani si anazijua, inawezekana ni kawaida yake kuendesha gari kwa speed kubwa huku akiwa amelewa. Kunywa pombe na kuendesha gari ni kusa tayari kwa sababu unahatarisha usalama wako na wa wengine. sasa hapa kisichoeleweka ni kitu gani???
 
Ha! So unafikiri hilo ni tatizo kwa Chenge! Like I said hii ni minor inconvenience kwake.

Mkuu hapa hatufuati majina kama angekuwa na hizo pesa si angekuwa na Valid Insurance
Kwa kifupi kulipia bima kumemshinda vinginevyo kama unataka kumtukana mimi simo
Najua utasema Mzembe au Mpumbavu waka sheria anazijua kinyume nyume
(Ikiwa insurance tuu tatizo jee kulipa libel compensation itakuwaje ? )
 
Apo naona unakwenda kasi mbona karatasi inaonyesha kuwa bima itamalizika mwezi wa nne ,(22/04/09 ) ,angalia vizuri kuna ,Type Toyota,Hilux ,engene namba ,Chasis number ,Colour Silver ,body type pickup,hiyo ndio karatasi ya Bima.

Sasa kama unataka nikusomee na hilo la kati la idara ya Bima ambalo limehusisha na Zanzibar act 1953 sema, usione soo.

Kuna tofauti ya bima na road license
 
Kuna tofauti ya bima na road license
Nipe tofauti haraka maana naona tunababaishana ,mimi nasema gari iliyokuwa akiendesha ilikuwa na bima ambayo inamalizika tarehe 22/04/09 ,sasa nifahamishe road license ni kitu gani maana sijawahi kukisikia.Maana sijajua umezungumza kitu gani ?
 
Nipe tofauti haraka maana naona tunababaishana ,mimi nasema gari iliyokuwa akiendesha ilikuwa na bima ambayo inamalizika tarehe 22/04/09 ,sasa nifahamishe road license ni kitu gani maana sijawahi kukisikia.Maana sijajua umezungumza kitu gani ?

Ukiangalia vema kuna vibandiko (stickers 3) hapo kwenye windscreen
Ya kwanza ya square ni Road Licence ambayo ndo ina expire 22/4
Inayofuata ni insurance amabyo inaonyesha imekwisha expire tangia 6/6/2007
Ya chini kabisa ni sticker ya usalama barabarani
una jingine?
 
Nipe tofauti haraka maana naona tunababaishana ,mimi nasema gari iliyokuwa akiendesha ilikuwa na bima ambayo inamalizika tarehe 22/04/09 ,sasa nifahamishe road license ni kitu gani maana sijawahi kukisikia.Maana sijajua umezungumza kitu gani ?

Kazi kweli,Road Licence ni ile inayolipiwa kila mwaka TRA na insurance ni bima,vitu viwili tafauti.Huyu driver wa bajaj hajakimbia wala kupewa kitu apotee kwa kuwa kungekuwa na uwezekano wa habari hii kujulikana baadae mi nahisi atakuwa kanyamazishwa 'kenya style' na sitashangaa maiti kupatikana msituni baada ya muda.
 
Kazi kweli,Road Licence ni ile inayolipiwa kila mwaka TRA na insurance ni bima,vitu viwili tafauti.Huyu driver wa bajaj hajakimbia wala kupewa kitu apotee kwa kuwa kungekuwa na uwezekano wa habari hii kujulikana baadae mi nahisi atakuwa kanyamazishwa 'kenya style' na sitashangaa maiti kupatikana msituni baada ya muda.

Asafali umetumia lugha nyepesi zaidi kumuelimisha Mwiba. Thanx
 
Bado hamjanieleza tofauti yake kabsaa naona mna matatizo ya hukumu, Sasa Chenge aliendesha gari isiyokuwa na Bima au isiyokuwa na road licence,hilo ni suali ?Pengine mtaniambia panajieleza lakini nyinyi mnasemaje ?

kuna mtu kazidi kufahamisha kuwa road licence ni ile inayolipiwa kila mwaka ,sasa hajamalizia na Bima ni ipi ,mbali ya yote kwa upande wangu nizionavyo kwa mlivyozieleza zote zitakuwa ni bima ,lakini kwa mlivyoeleza ,nionavyo Bima haswa huwa ile ambayo inaonyesha kabila ya gari,aina ya gari kama ni basi au bajaji ,rangi ya gari,engene namba ya gari au Chasisi number ikiwa gari haina chasis nafikiri inawekwa engene namba,nguvu ya gari ,mahali ilikotengezwa ,nambari ya gari,kama gari ni ya binafsi,shirika au serikali,shirika liliyoidhamini gari ,muda ambao kwa gari kongwe huwa ni mwaka,aidha aina ya bima wenyewe kama ni first party au third part,kwa nchi zilizoendelea hawabandiki tena makaratasi ukutani wanakupa kipande chenye maalumati yote hayo sawa na ukurasa wa mwanzo wa pasi zetu za kusafiria .

Sasa kile kipande cha kati nafikiri ni ruhusa fulani ambayo pengine gari hiyo iliruhusiwa kwenda na kurudi Zanzibar kwa mwaka mmoja ,inakuwaje panakuwa na Zanzibar pale na halafu iwe Bima,wacheni kubambikiza.
 
Bado hamjanieleza tofauti yake kabsaa naona mna matatizo ya hukumu, Sasa Chenge aliendesha gari isiyokuwa na Bima au isiyokuwa na road licence,hilo ni suali ?Pengine mtaniambia panajieleza lakini nyinyi mnasemaje ?

kuna mtu kazidi kufahamisha kuwa road licence ni ile inayolipiwa kila mwaka ,sasa hajamalizia na Bima ni ipi ,mbali ya yote kwa upande wangu nizionavyo kwa mlivyozieleza zote zitakuwa ni bima ,lakini kwa mlivyoeleza ,nionavyo Bima haswa huwa ile ambayo inaonyesha kabila ya gari,aina ya gari kama ni basi au bajaji ,rangi ya gari,engene namba ya gari au Chasisi number ikiwa gari haina chasis nafikiri inawekwa engene namba,nguvu ya gari ,mahali ilikotengezwa ,nambari ya gari,kama gari ni ya binafsi,shirika au serikali,shirika liliyoidhamini gari ,muda ambao kwa gari kongwe huwa ni mwaka,aidha aina ya bima wenyewe kama ni first party au third part,kwa nchi zilizoendelea hawabandiki tena makaratasi ukutani wanakupa kipande chenye maalumati yote hayo sawa na ukurasa wa mwanzo wa pasi zetu za kusafiria .

Sasa kile kipande cha kati nafikiri ni ruhusa fulani ambayo pengine gari hiyo iliruhusiwa kwenda na kurudi Zanzibar kwa mwaka mmoja ,inakuwaje panakuwa na Zanzibar pale na halafu iwe Bima,wacheni kubambikiza.

hiyo ya ruhusa ya kwenda na kurudi zanzibar imenichekesha sana.

hivi hao waliogongwa na kufa wangekuwa watoto wake kamanda kova chenge angekuwa nje sasa?
 
But who knows labda dereva... alikufa... Kwa spidi waliyokuwa nayo wote wawili, siyo rahisi kwa dereva wa bajaji kutoka mzima na kuweza kukimbia.

Hata mimi wasiwasi huo umenijia. Ukiangalia impact ya ajali (kutokasna na gari la chenge linavyoonekana, ni vigumu kuamini kuwa abiria, waliokuwa wamekaa nyuma walikufa na dereva akaondoka, tena na nguvu za kukimbia
 
Bado hamjanieleza tofauti yake kabsaa naona mna matatizo ya hukumu, Sasa Chenge aliendesha gari isiyokuwa na Bima au isiyokuwa na road licence,hilo ni suali ?Pengine mtaniambia panajieleza lakini nyinyi mnasemaje ?

kuna mtu kazidi kufahamisha kuwa road licence ni ile inayolipiwa kila mwaka ,sasa hajamalizia na Bima ni ipi ,mbali ya yote kwa upande wangu nizionavyo kwa mlivyozieleza zote zitakuwa ni bima ,lakini kwa mlivyoeleza ,nionavyo Bima haswa huwa ile ambayo inaonyesha kabila ya gari,aina ya gari kama ni basi au bajaji ,rangi ya gari,engene namba ya gari au Chasisi number ikiwa gari haina chasis nafikiri inawekwa engene namba,nguvu ya gari ,mahali ilikotengezwa ,nambari ya gari,kama gari ni ya binafsi,shirika au serikali,shirika liliyoidhamini gari ,muda ambao kwa gari kongwe huwa ni mwaka,aidha aina ya bima wenyewe kama ni first party au third part,kwa nchi zilizoendelea hawabandiki tena makaratasi ukutani wanakupa kipande chenye maalumati yote hayo sawa na ukurasa wa mwanzo wa pasi zetu za kusafiria .

Sasa kile kipande cha kati nafikiri ni ruhusa fulani ambayo pengine gari hiyo iliruhusiwa kwenda na kurudi Zanzibar kwa mwaka mmoja ,inakuwaje panakuwa na Zanzibar pale na halafu iwe Bima,wacheni kubambikiza.

Mwiba wewe ni mbishi by nature. OK wewe unamiliki gari aina gani. Unaweza ukakuta tunajadiliana na mtu ambaye gari kwao mpaka ende mbunge ndo wanaliona.
Taka usitake huo ndo ukweli kuwa bima imekwisha! Full stooooooooooooooooop. Nenda ka grocery ka hapo jirani kapate kasoda kale ka mia 2 labda akili inaweza kufanya kazi kidogo. Pia ikielekea hapo grocery ukikuta gari lolote imepark hapo chungulia hapo kwenye kioo cha mbele ukirudi utatwambia umeona nini. C U baadaye
 
Saasa kutokana na maelezo yako nimekuuliza suali unipe tofauti, Road licenze inamalisikia mwaka mmoja ,na bima nayo je ,umetoka mkuku na makelele kibao.
Hapa lazima munipe maana ,sio mnapotosha ukweli ,ile ya kati sio bima ,pale mmevamia na mpiga picha ameenda ngowe na kupandisha watu mkenge. 😀

Au niwawekee sawa yale maandishi ya kati ili mjue kuwa Mheshimiwa gari yake ilikuwa na bima iliyo hai.Msione soo ?
 
Last edited:
mwizi ni mwizi na hatosheki....
hata insurance huna....
halafu kwa confidence zote unasema ulikua speed kati ya 80 -100 kmph kwenye maeneo ya makazi ya watu. hiyo ni speed kubwa sana kwenye maeneo ya watu.

huyu jamaa hana akili nina shindwa kueluewa hivyo vyeti vyake alivipataje
1. mara ya kwanza alivyoulizwa swali akajibu vijisenti
2. leo anatuambia alikua speed 80 -100 kwa confidence jamani huyu kweli ni
mwanasheria, ndio maana mikataba mingi ilikua mibovu chini yake
 
Naona mmekwama na mnafikiria mlivyopandishwa mkenge ,tatizo la gari sio kuwa halina bima bali tatizo gari haikusajiliwa,kwa maana hiyo gari haina kumbukumbu serikalini ,tokea iliposajiliwa mwaka 2006 na kumalizia 2007 .lakini inaonyesha alikuwa akiikatia Bima ,hapo hana kosa wakati yeye ni mtu mkubwa serikalini ,tunaweza kusema alikuwa halipi TRA ila akilipa Bima ,kwa ufupi akikwepa kodi na hakuna wa kumkamata ,hivyo utaona anarudia kule kule kwenye kutumia wazifa wake kukwepesha kodi. Take care ile ya kati ni Consignment Date 07/06/2006 hadi 06/06/2007 ada ya kulipa TRA ,sio Bima wandugu msikurupuke tu mtaumbuka baadae.natumai kuna watu wameshaliona hilo.Sijui wenye magazeti wanaoweka chambo kuuza magazeti yao.Nyie mliosema BIMA hivi TRA inashugulika na Bima ?

tabu wengine hapa wanakurupuka tu na kulaani kuwa hana ishuwarezi ,hata sijui kama wanafahamu maana yake ,basi watu wanasema na wao wanasema ,mtafungwa !
 
Naona tatizo ni dereva wa Bajaj yupo wapi ? Je alimalizwa kwa risasi ,pengine walikuwa wanafukuzana tokea walikotoka ,huwezi kujua !
 
Chenge alikuwa anatembea na huyo dada mmoja nini?
Ajali Dar: Chenge adaiwa kujuana na mmoja wa marehemu (Gazeti la Mwananchi)

Frederick Katulanda,Mwanza
SAKATA la ajali ya gari la Andrew Chenge ambalo limesababisha vifo vya wanawake wawili, limeingia katika sura mpya baada ya ndugu wa wasichana hao kudai kuwa Chenge alikuwa akimfahamu mmoja wa marehemu.


Chenge ambaye alikuwa Waziri na Mwanasheria mkuu wa zamani wa serikali, aliingia matatani baada ya gari alilokuwa akiendesha kugonga "bajaji" usiku wa kuamkia juzi na kuua wanawake wawili ambao ni Beatrice Costantine ambaye ni mfanyabiashara wa Mwanza na mmiliki wa saluni ya kike na Vicky George Makanya.

牋?p> Wakizungumza kwa nyakati tofauti jijini Mwanza baadhi ya ndugu waliohojiwa na Mwananchi Jumapili akiwamo mama mzazi wa Vicky, walisema wanafahamu Chenge kuwa alikuwa akimjua ndugu yao Vicky.


Akizungumza na Mama wa marehemu Vicky, Nazifa Kambi nyumbani kwao Iloganzala ambako kuna matanga alisema amesikitishwa na taarifa za upotoshaji zilizoeleza kuwa mwanae na rafiki yake walikuwa wakienda Zanzibar kwa ajili ya kufunga ndoa jambo ambalo alilipinga na kueleza kuwa alikuwa akija Mwanza baada ya kutoka Zanzibar ambako walikwenda kununua vifaa vya saluni ya mwenzake.


牋牋牋牋?揂jali hii inanipa mashaka makubwa kutokana na kupokea taarifa za kupotosha za kufunga ndoa," alisema.


Alisema pia amepata taarifa kutoka kwa wafanyakazi wenzake kuwa Chenge walikuwa wakifahamiana na Vicky na kwamba kila mara alipokuwa akifika Mwanza Hotel alikuwa akimtaka kumhudumia vinywaji yeye.


牋牋牋Nazifa alisema marehemu Vicky ambaye alikuwa mfanyakazi wa Mwanza Hotel katika kitengo cha King Casino ambayo kwa sasa inajulikana kama The Stone, hata yeye mwenyewe aliwahi kumsikia mwanaye kuhusu mbunge huyo kumtaka atoke nyumbani kwenda kumhudumia siku ambayo hakuwa kazini.


Ameiomba serikali kufanya uchunguzi wa kina kuhusu ajali hiyo ili kupata nini kilichosababisha ajali hiyo.


Kwa upande wa msemaji wa familia ya Beatrice, kaka wa marehemu, Andrew Costantine akiwa Kiseke kwenye matanga alisema wanachofahamu wao ni kuwa dada yake amepatwa ajali akiwa njiani kurejea hotelini walikofikia ya JVL Hotel iliyopo Mwananyamala wakati wakitoka Oysterbay kwa ajili ya kuchukua mizigo yao tayari kwa kuondoka Dar es Salaam kwenda Mwanza.


Andrew alieleza kuwa tayari marehemu na rafiki yake walikuwa wamekwisha kutoka Zanzibar ambako walikwenda kununua bidhaa na vifaa vya saluni ya kike ambavyo vimekutwa hotelini walikokuwa wamefikia.


Alisema marehemu hakuwa amekwenda kufunga ndoa Zanzibar kwa vile alikuwa na mume wake ambaye ni mzungu raia wa Marekani na kwamba mpaka anafikwa na mauti mme wake alikuwa nje ya nchi.


Alisema habari zilizotolewa na baadhi ya vyombo vya habari kuwa walikuwa wakienda kufunga ndoa siyo za kweli.


揥akati wakiondoka alimuaga rafiki yake Khadija Hassani ambaye ndiye alimuachia nyumba yake na wakati akiwa Zanzibar alimtumia fedha kwa ajili ya kuwalipia ada ya shule watoto, sasa mambo mengine hakuna anayejua tunaomba uvumulivu msiba uishe,?alieleza.


Alisema mpaka sasa Chenge ameahidi kusaidia familia kusafirisha miili ya marehemu hao, lakini bado hawajapokea lolote kutoka kwake na wanaendelea kumsubiria wakati polisi wakikamilisha taratibu za uchunguzi huku na wao wakijipanga kusafirisha miili ya ndugu zao.


Msiba hii imeacha simanzi Jijini Mwanza na kuwa gumzo kubwa huku ukizua minog抩no ya hapa na pale na baadhi ya wakazi wa jiji la Mwanza wengine wakishangazwa na tukio hilo na jinsi jeshi la polisi lilivyounda tume kushughulikia ajali hiyo tofauti na ajali nyingine.


Marehemu hao waliondoka Jijini Mwanza Machi 24, mwaka huu kwa safari ya kibiashara Dar es salaam na baadaye Zanzibar na walikuwa wakitarajiwa kureja Ijumaa Machi 27, Beatrice ameacha watoto wanne ambao wanasoma shule tofauti za bweni na mwenzake Vicky ameacha mtoto mmoja mwenye umri wa miaka mitano.


Hata hivyo, juhudi za kumpata Chege kwa simu jana hazikuzaa matunda jana.
 
TWIST AND TURNS at every corner,what more will come out.sasa chenge anamjua marehemu mmojawapo-conspiracy or what,the press in tanzania must be having a field day
 
mmm...i think il agree with some people here that the middle sticker is the insurance tag ..and it expired in 07...that sticker has nothing to do with TRA...hence the words "commission of insurance tanzania" ...act of 1953 blah blah...
Kwenye Sticker ya insurance kuna
Veh No.
Make....Model...Color....
Commencement date (not consignment date)
Expiry date..06/06/2007
signature ya commissioner
then some numebr (policy i think
 
Back
Top Bottom