Cheo cha Floor Manager kinapuuzwa bila sababu

Cheo cha Floor Manager kinapuuzwa bila sababu

Andrew123

JF-Expert Member
Joined
Jun 2, 2012
Posts
8,358
Reaction score
10,976
Ma-floor manager harusini hatutambuliki kisheria, why?

Kazi zetu zinaonekana na mambo yanakwenda kama yalivyopangwa, wageni waalikwa wanakula, wanakunywa, Ulinzi wa Magari fresh.

NB: hicho cheo kitajwe kwenye katiba Mpya
 
Umenikumbusha mbalii

Haya mambo ya sherehe za harusi sitaki tena kujihusisha...

Nilifunzwa enzi zetu shughuli ikowa ya kwenu wale ndugu wa karibu ndo mnaishika sherehe na siku ya shughuli nyie hamshereheki bali mnakuwa wima na macho kuangalia wageni wanapata huduma zote mlizoandaa ukumbini.

Na ndo maana ya vunja kamati, ile sasa sio kila aliyekuwa anakuja kwenye vikao ndo aje kwenye vunja kamati, hapana watakuwa wale ndugu wa karibu waliokuwa wima sherehe nzima kuanzia kupokea wageni, hadi kusafirisha wale waliozima ukumbini na kuhakikisha zawadi zimefika salama kwa maharusi.

Maana ssiku ya sherehe pamoja na kuwa mtakuwa mmependeza ila inawezekana kabisa mkaishia kunywa soda moja au maji moja na saa ingine hata chakula msile.
Busy busy, ila siku ya vunja kamati sasa weeeh hapo ndo mnapiga ulabu na nyama na vyuku kama vyotee.

Miaka kadhaa nyuma ndugu (mabinamu) wakanishirikisha kwenye sherehe kama ndugu wa karibu, aiseeh nikauvaa uhusika nilipiga makitaimu mule ukumbini sina hamu. Nilijitoa hata mziki sikucheza mwisho wa shughuli nikawa hoiii kwa uchovu, sasa hao mabinamu waliniboa.....harusi ya mdogo wao, wao wakaingiza marafiki zao ukumbini naa kukaa kwenye meza kutaka kuhudumiwa.... walikunywa wakalewa hakuna hata ushirikiano kwwnyw kusimamia shughuli....
Nilichukia,nikasema wacha nifanye wajibu wangu ila... hawanioni tenaaa kwenye sherehe zao.

Ndugu mkishikana na mkaelewana hamhitaji floor manager. Kila mtu akae sekta yake na awajibike..

Eeeh sijui nani anifunze kufupisha habari.... nashindwaa....😑
 
Floor Manager in Swahili (Meneja wa Sakafu)


Wapi mnatambulika kisheria?

Floor Manager ni kama Malaya muuza uchi pale River Side!,Kaeni kwa kutulia!
 
Ma-floor manager harusini hatutambuliki kisheria, why?

Kazi zetu zinaonekana na mambo yanakwenda kama yalivyopangwa, wageni waalikwa wanakula, wanakunywa, Ulinzi wa Magari fresh.

NB: hicho cheo kitajwe kwenye katiba Mpya
Katiba mpya ni sasa. Kwa huku ccm wanaweza anzisha mchakato ili utambulike rasmi na wao watafune Kodi utakayotozwa.

Sent from my moto g 5G (2022) using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom