Chibu, Kiba na timu za mashabiki

Chibu, Kiba na timu za mashabiki

clinician

JF-Expert Member
Joined
Mar 5, 2014
Posts
2,098
Reaction score
4,926
Tukio la tuzo za kili limeshapita,lakini vumbi lake bado linatimka,na chafya zinazidi kuongezeka.Kama inavyokuwa miaka yote lawama zimeendelea kuwepo,kunyosheana vidole,vijembe,kujigamba n.k kupo pale pale.

Midahalo imekuwa mingi sana lakini huu wa Ali kiba kuchukua tuzo nyingi umekolezwa zaidi.Umekolezwa kwa sababu ya uwepo wa timu mbili zinazokinzana kwa sasa,timu kiba na timu Diamond.Makala yangu imelenga kuchokonoa jipu hili.

Kuna watu wanao amini kuwa Ali kiba alistahili kuchukua tuzo alizopata na wengine wanahoji kwanini diamond apate tuzo chache licha ya viashiria vingi vya kufanya vizuri zaidi kitaifa na kimataifa.

Kwa mtazamo wangu Ali Kiba alistahili kuchukua tuzo alizopata kutokana na vigezo vifuatavyo;

Kwanza kabisa Ali kiba alistahili kushinda kwa kuwa aliingia kwenye category zile na yeyote aliyeingia kwenye category husika ana haki ya kushinda tuzo husika.Kama kulikuwa na room ya kulalamikia ushindi wa Ali kiba katika category yeyote basi malalamiko hayo yangeanzia wakati jina lake limeingizwa kwenye category.

Pili,Ali kiba alifanya kampeni ya kuomba kura na alipata marafiki wengi wenye ushawishi waliojitokeza kumuombea kura kwa mashabiki mfano Wema Sepetu,Jokate,Abdu kiba na wengineo.

Tatu,Ali kiba ni mwanamuziki wa muda mrefu,anajua kuimba,ana sauti nzuri na fundi wa kuandika nyimbo hivyo siona shaka kwa mtu wa hulka hiyo kutunukiwa tuzo nyingi ambazo hata 'msanii 20%' alizipata miaka michache nyuma.

Diamond siyo mwanamuziki mbaya,wala kukosa tuzo hakumaanishi kuwa diamond ni mbovu kuliko kiba,ikumbukwe kwamba hizi tuzo hutolewa kwa wasanii waliofanya vizuri katika mwaka husika hivyo kama mashabiki wameona kuwa kwa mwaka uliopita Ali kiba ndio amefanya vizuri kupitia wimbo wake wa Mwana basi maamuzi yao yaheshimiwe na tusubiri mchakato mwaka ujao.

Diamond hakujihusisha sana na upigaji kampeni hivyo kwa tuzo mbili alizopata bado ni ishara kuwa anapendwa na kukubalika na mashabiki.

Kufanya vizuri kimataifa hakumpi Diamond guarantee ya kuchukua tuzo za ndani kwa kuwa mbali na sifa nyingine nyingi alizokuwa nazo Diamond Video zake nzuri ndio zimemfanya apae kimataifa, Watanzania watam-judge Diamond kwa kuangalia zadi ya video anazotoa.

Diamond ni mwanamuziki mkubwa kwa sasa barani Afrika,anafanya vizuri na kuiwakilisha Tanzania nje ya nchi hastahili kubezwa,kuchukiwa,kushushwa wala kufanyiwa fitina na mtanzania wa "timu" yeyote.

Ali kiba ana potential ya kuja kuwa mwanauziki mkubwa,mkubwa kuliko anavyoweza kujitathmini,ushindani uliojitokeza baina yake na diamond unaonekana kumwamsha kifikra,lakini bado hajafanya yote aliyotakiwa kuyafanya,naamini[kama anajielewa] akitiririsha yote yaliyokuwa kwenye locker lake tutakuwa tunaongelea balaa lingine.
 
Kila siku watu hawahawa tu, sisi mashabiki ndo tunasababisha yote haya
 
Hata ben poll anasauti nzur hata barnaba mtunzi mzuri sana tu hapa ni swala la mashabiki na kupiga kura tu ndilo linalotufautisha kumbuka kupata tuzo nyingi sio lazima uwe mkali kupita wengine na kupata tuzo chache sio kuwa ni mbovu kupita wengine na ukikosa tuzo sio kuwa hujui unakumbuka ya Kendrick
lamar...!?hapo ni kama issue ya ronaldo na messi...😆
 
Hata ben poll anasauti nzur hata barnaba mtunzi mzuri sana tu hapa ni swala la mashabiki na kupiga kura tu ndilo linalotufautisha kumbuka kupata tuzo nyingi sio lazima uwe mkali kupita wengine na kupata tuzo chache sio kuwa ni mbovu kupita wengine na ukikosa tuzo sio kuwa hujui unakumbuka ya Kendrick
lamar...!?hapo ni kama issue ya ronaldo na messi...��
ni kweli mkuu
 
Wewe mchezo unaochezwa haufahamu na hauujui,kuna kundi kubwa sana lisilopenda kuona DIAMOND anasonga mbele ila ukiwa nje ya mchezo utaona ya kiba na DIAMOND tu
 
itafika kipindi tutahitaji kuwa na vyote viwili ,lkn hatutakuwanavyo tena .Na vile tutakavyokuwa navyo havitajitokeza kwa sbb vitabezwa na wachache ,watanzania tunatia huruma sana , kama hatujijui tulipo ,sijui tunaelea sijui tunazama hata hatujui, tupo tupo , mpaka nakumbuka kauli ya Mchungaji mbunge Peter Msigwa , tumebeba vichwa vikubwa akili ndogo , hatujui tuendako wala tulikotoka .Kiba ,Diamond wote ni watanzania wote ni wanamuziki wa tanzania na wengine wote niwambie tu hz timu zinawamaliza so soon macho mnayo masikio mnayo .Naipenda nchi yangu na wanamuziki wote mnaopiga mziki mzuri Tz na nje Tz.
 
kila mtu atachambua mwisho wa siku ni nani anafanya kazi kwa bidii nani anajipahisha nani anajiingizia pesa ndefu etc kila mtu na lwake

Cha muhimu sasa katika wanamuziki wetu wa TZ ni kujivunia hawa wanaopeperusha bendera yetu MTV Africa na ni
Diamond Platnumz anawania tuzo 3 na Vanessa 1 kuwapigia kura bila kuchoka

ingia katika link hii


http://mama.mtv.com/voting/

View attachment 262268
 
Uzi upo clear sana na mkuu umenena vyema kabisa na "TRUTH NOTED" ila kabla hata hatujafika mbali kuna watu wameshaanza kuleta UTEAM FULANI HIVI...kwani ukikocomment bila kubase kwenye uteam wenu mtapungukiwa nin?..lakini mtu ana comment moja kwa moja kwa msanii fulani na hii ndiyo sababu ata malumbano yasiyo ya msingi hayotokuja kuuisha humu celeb.forum maana hakuna asiyefahamu kuwa diamond ana hit africa,na pia tayari kingkiba ameshaanza kufungua locker lake la mazagazaga...so I hope soon naye ata GO TO THE TOP!!!!!!
 
Uzi upo clear sana na mkuu umenena vyema kabisa na "TRUTH NOTED" ila kabla hata hatujafika mbali kuna watu wameshaanza kuleta UTEAM FULANI HIVI...kwani ukikocomment bila kubase kwenye uteam wenu mtapungukiwa nin?..lakini mtu ana comment moja kwa moja kwa msanii fulani na hii ndiyo sababu ata malumbano yasiyo ya msingi hayotokuja kuuisha humu celeb.forum maana hakuna asiyefahamu kuwa diamond ana hit africa,na pia tayari kingkiba ameshaanza kufungua locker lake la mazagazaga...so I hope soon naye ata GO TO THE TOP!!!!!!
Well said mkuu
 
kila mtu atachambua mwisho wa siku ni nani anafanya kazi kwa bidii nani anajipahisha nani anajiingizia pesa ndefu etc kila mtu na lwake

Cha muhimu sasa katika wanamuziki wetu wa TZ ni kujivunia hawa wanaopeperusha bendera yetu MTV Africa na ni
Diamond Platnumz anawania tuzo 3 na Vanessa 1 kuwapigia kura bila kuchoka

ingia katika link hii


MAMA 2015

View attachment 262268
sawa mkuu let us vote for our countrymen,#vanesa and diamond
 
itafika kipindi tutahitaji kuwa na vyote viwili ,lkn hatutakuwanavyo tena .Na vile tutakavyokuwa navyo havitajitokeza kwa sbb vitabezwa na wachache ,watanzania tunatia huruma sana , kama hatujijui tulipo ,sijui tunaelea sijui tunazama hata hatujui, tupo tupo , mpaka nakumbuka kauli ya Mchungaji mbunge Peter Msigwa , tumebeba vichwa vikubwa akili ndogo , hatujui tuendako wala tulikotoka .Kiba ,Diamond wote ni watanzania wote ni wanamuziki wa tanzania na wengine wote niwambie tu hz timu zinawamaliza so soon macho mnayo masikio mnayo .Naipenda nchi yangu na wanamuziki wote mnaopiga mziki mzuri Tz na nje Tz.
Ni kweli mkuu,hakuna haja ya kuwakubali wote ila sio lazima mmoja ashushwe,ni busara zaidi kama tutakuwa na wasanii wengi wenye mafanikio zaidi ya kiba na diamond
 
Wewe mchezo unaochezwa haufahamu na hauujui,kuna kundi kubwa sana lisilopenda kuona DIAMOND anasonga mbele ila ukiwa nje ya mchezo utaona ya kiba na DIAMOND tu
inawezekana ni kweli kuna kundi lisipenda diamond afanikiwe lakini hakuna ushahidi wa malalamiko hayo...hatuwezi kujenga hoja kwa malalamiko yasiyo na ushahidi
 
Back
Top Bottom