Chimbuko la Uislam na Karen Armstrong

Chimbuko la Uislam na Karen Armstrong

SEHEMU YA VI- SUNNI &. SHIA


A. Sunni.
Jina hili lilitoka na Al Sunna maana yake (wafuasi wa tamaduni i.e mila na desturi za Quran na mafundisho ya Muhamad). Wakati Muhamad amefariki, vigogo walioketi kumteua mrithi walimteua aliyekuwa mfuasi mkubwa wa Muhamad na pia baba wa mke wa pili wa Muhamad aliyeitwa Abu Bakar kuwa ndiye anafaa kuwa mrithi sababu ana elimu kubwa ya uongozi na alikuwa na Busara sana (to me naona ni hoja ya msingi). Waislam wengi waliokubaliana na Uteuzi huu. Hivyo kundi hili likaamini kiongozi wa Kiislam [Caliphate (au Khalifa kwa kiswahili)], anapaswa yule mwenye kufuata na kuzijua Mafundisho ya Muhammad na Quran, kundi hili liliitwa Sunni (wasunni), walikuwa wengi, na hadi leo duniani linahusisha karibu 80+% ya waislam wote duniani.

Nchi nyingi duniani ni Sunni Muslim ( kama nilivyosema hapo juu 80+%). Kwa M.E nchi za Egypt, Jordan, Saudi Arabia, Uturuki na Syria.

B. Shiite/ Shia ( Shiat al Ali - Part/descendants of Ali). -(Washia).

Lakini kapo kakikundi kadogo kalikopinga Abu Bakar kuwa Mrithi wa Muhamad, na kiongozi wa Waislam. Hawa walitaka Ali ibn Talib awe mrithi. Huyu alikuwa ni Binamu wa Muhamad na amemuoa mtoto wa Muhamad aitwaye Fatma. Hivyo wao msimamo wao ni kuwa mrithi alipaswa atoke kwenye damu (ukoo) wa Muhamad mwenyewe-bloodline, kama ilivyokuwa utamaduni wa Kiarabu. Ikumbukwe kuwa Ali, alikuwa ni mmoja wa baraza la vigogo walioshiriki kikao cha kumteua mrithi wa Muhamad kilichompitisha Abu Bakar. Hivyo hawa hawakumtambua Abu Bakar kama Kiongozi wao, hadi mwaka 634, Ali alipokuwa Khalifa baada ya Abu Bakar kufariki. Duniani washia wako kama 10+ %.

Ndani ya M.E Nchi za Iran(90+), Iraq (60+), Bahrain(70+%), Azerbaijan(80%) ndio zenye idadi kubwa zaidi ya washia duniani. Lebanon and Yemen pia takribani nusu ya idadi yao ya watu ni washia. Pia nchi za Saudi Arabia (est 5-10%), Kuwait (abt 36%), Oman(
Lakini pia nao wamegawanyika zaidi. Na migawanyiko hii kwa kiasi kikubwa imetokana na waumini kuwa wafuasi wa wanazuoni fulani fulani wa kiislam (maulamaa) kutoka kwenye madhehebu hayo ya Sunni au Shia

Sunni na Migawanyiko yake:

Hapa licha ya kukubaliana kuwa Khalifa ni lazima atokane na muislam mwenye sifa, lakini hutofautiana kuhusu mafundisho ya sheria za Kiislam. Hapa yapo Makundi Manne, Wahanafi, Wamaliki, Washafii na Wahanbali.
Hawa

[emoji830]Wahanafi.
Hawa ni wafuasi wa mafunzo ya Imamu(mwalimu) Abu Hanifa an-Nu‘man aliyezaliwa Iraq na kuishi Iraq miaka ya 700, mafunzo yake yanafuatwa sana huko Asia ya kati, Afghanistan, Pakistan, maeneo ya Levante (Lebanon, Syria, Iraq, Palestine, and Jordan) India, Bangladesh, Northern Egypt na Turkey, Pia waislam wengi wa Urusi ni wafuasi wahanafi. Pia waislam waliopo nchi za Balkan (slovenia, Croatia, Bosnia and Herzegovina, Serbia, Montenegro, Albania, Macedonia, Greece, Bulgaria and Romania.)

[emoji830]Wamaliki.
Hawa ni wasunni wanaofuata mafundisho ya Imam Malik Bin Anas, aliyekuwa mtu wa Madina miaka ya 700 pia. Mafunzo yameshamiri maeneo ya North Africa, West Africa, the United Arab Emirates, Kuwait, baadhi ya maeneo ya Saudi Arabia na Kaskazini mwa Misri.

[emoji830]Washafii.
Hawa ni wasunni wanaofuata mafunzo ya Imam Muhammad ibn Idris ash-Shafi'i mzaliwa wa Gaza, aliyeishi miaka ya 800. Mafunzo yake ni maarufu Huko Hejaz Saudi Arabia, Mashariki ya Misri, Indonesia, Malaysia, Jordan, Palestine, Singapore, Filipino, Somalia , Thailand, Yemen, Kurdistan, Pia baadhi ya waislam wahindi. Nchini Iraq na Syria pia wako kwa kiasi kikubwa.

[emoji830]Wahanbal
Wasunni hawa, hufuata mafunzo ya Ulamaa, Ahmed Bin Hanbal (Jina lake kamili ni Abū ʿAbdillāh Aḥmad ibn Muḥammad ibn Ḥanbal Ash-Shaybānī, kifupi Ibin Hanbal), aliyeishi karne ya 19 kutoka Iraqi (kumbuka Iraq Wasunni ni wachache). Wafuasi hawa wako zaidi Saudi Arabia, Qatar pia kwa uchache wako Iraq na Syria. Mafunzo ya Hanbal ni ya kiitikadi kali na yana mafungamano na Jihadi.

Note: Pia wafuasi wa Salafi ni hufuata mafunzo ya Hanbal. Salaf ni neno maana yake wahenga/waasisi. Hii ni harakati katika uislam inayopigania mabadiliko huku msisitizo wao ni kurudi kwenye mafunzo na matendo ya wahenga wa kiislam. Vuguvugu hili kimsingi wanaamini kuwa waislam halisi walikuwa kizazi cha kwanza hadi cha tatu cha waislam (kutoka kwa Muhamad 600+ years hadi 900+ yrs) walikuwa ndio waislam sahihi. Wanachokipigania hawa ni maisha ya waislam yawe katika misingi ya Quran na Sunna (Matendo ya Muhamad). Vuguvugu hili lilianzishwa miaka ya 1800 kupambana na influence ya western culture and education. Pia wanaaminika kuwa influenced na wahabia.

Wahabia. Ni vuguvugu la kiislam la Kisuni linalopigania mabadiliko ndani ya Uislam lilioanzishwa Saudi Arabia na Mohamed Ibn Abd al-Wahhab miaka ya 1700. Hawa wanapigania Mafunzo ya kiitikadi kali ya imani kwa Allah na tafsiri ya Quran na Uislam bila kupindisha neno. Wahabia wanaamini Muislam yeyote asiyekuwa na mafungamano au mtazamo huo, basi huyo ni Kaffir (mchafu/aliyelaanika/asiye Muislam) na ni adui wa Uislam. Vuguvugu hili kwa kiasi kikubwa linapata fedha kutoka kwa Serikali ya Saudi Arabia [ili kueneza dini!!!!] Kundi kama ISIS ni wafuasi/sehemu ya Vuguvugu hili.

Washia na Mgawanyo wao:

Hivyo kama tulivyosema hapo juu, Washia wanaamini Khalifa wao wa Kwanza ni Ali bin Talib. Baada ya hapo wakafuata Makhalifa wengine au pia huwaita Maimam (sababu ni walimu wao kiimani).


Washia wako makundi makuu mawili.

i. Imamiyah au Twelvers.
Hawa ni washia wanaoamini kuwa baada ga kifo cha Muhamad, kulifuata Maimam 12 walioongoza Uislam huku imam wa mwisho, Muhamad Al Mahid aliyezaliwa mwaka 870 huko Abissas Empire (Iraq ya Leo) na kupotea akiwa na miaka mi5 atarejea miaka ya baadae akiwa na Nabii Isa (Yesu) na kuwakomboa walimwengu. Wafuasi wa Kikundi hiki wanapatikana Iran, Iraq, Pakistani, Uhindi, Bangladesh, Shamu, Lebanon, Kuwait, Muungano wa Falme za Kiarabu, Bahrain, Uarabuni ya Saudia, Burma, Thailand, Indonesia, Urusi, Tanzania, Kenya, Uganda, Somalia, Zaire, Malagasy, Ungazija, Uingereza, Marekani. Pia chini yao kuna madhehebu Mengine ambayo yanapingana kuhusu idadi ya hao maimamu, wengine wakiwakataa baadhi ya maimamu.

Hawa ndio 12 Imams;

1. Ali bin Abi Talib
2. Hasan bin Ali
3. Husain bin Ali
4. Ali bin Husain
5. Muhammad bin Ali
6. Jaafar bin Muhammad
7. Musa bin Jaafar
8. Ali bin Musa
9. Muhammad bin Ali
10. Ali bin Muhammad
11. Hasan bin Ali
12. Muhammad bin Hasan (aliyetoweka akiwa na miaka 5 na atagemewa kurudi kuwakomboa).

ii. Ismailiya:
Hawa washia wanaamini kuwa Uimamu baada ya Imamu Jaafar Sadiq [huyo watano hapo juu] ulichukuliwa na mwanawe Ismail.

Maismailiya Wamegawanyika tena katika Madhehebu mawili; Aga Khan na Bohora.

Maagha Khani:
Hawa hufahamika zaidi kwa jina la Maismailiya hapa Afrika ya Mashariki na sehemu nyinginezo, ingawa vitabu vya kidini huwaita Nazariya. Wanamwamini Mtukufu Karim Aga Khan IV kuwa ni Imamu wao wa 49.

Mabohora:
Hawa Wanaamini kuwa Imamu wa 21 yu katika Ghaib (haonekani) na yu hai. Kwa wakati huu kiongozi wa jamii yao anaitwa Mufaddal Saifuddin akiishi Bombay, India.
 
Kwa sasa naishia hapa. Ila bado nasoma vitabu vya huyu mama. Hiki cha History of God kimezungumza dini za Uislam, Ukristo na Uyahudi, so naendelea nacho ambapo kinagusa maeneo mengine nje ya Uislam. Baadae nitasoma vitabu vyake viwili ambacho kimoja kimemzungumzia Muhamad na Kingine kimeuelezea Uislam exclusively. So napo nitadonoa mawili matatu nitakayoona yanafaa nitayaweka hapa.
 
Kitabu hicho kinasema ukiona mambo huyelewi uliza vitabu vilivyokuwepo kabla yake yaani injili, zaburi na torati.I injili hasa ya Yohana iko wazi kuhusu uungu wa Yesu. Kwangu Mimi issa bin Mariam ni distorted explanations of Jesus Christ of the Bible. Ni sawa ikiandikwa Hadith ya Nyerere Nigeria inayosema alizaliwa dar, akafia muhimbili. Ila ukija Tanzania utakutana na maandiko yanasema wazi kazaliwa mwitongo na kafia st Thomas UK. Ntawaamini wayahudi zaidi ya Yesu wa uarabuni.
Uislamu unaitambua Injili ya Issa,ambayo hata nyinyi hamna. Hizo Injili za Yohana umezipata wapi ?

Watu wa kitab walio zungumziwa hapo tukiweka katika mizani wewe haupo,sababu haukuwepo kipindi hivyo vitabu wanapewa watu hao wa kitabu.

Lakini umesema Injili ya Yohana,hapo wanazungumziwa waliopewa kitabu Injili ya Issa na Taurati ya Musa. Hakuna Injili ya Yohana,ndiyo maana hata leo hamumjui nani aliandika Injili ya Yohana.
 
Uislam umekuja karne ya ngapi baada ya ukristo?shehe
Kwanza inabidi tujue Ukristo umeletwa na nani ?

Uislamu kwa maana ya imani,upo tangu anaumbwa Adamu,ila kwa sheria alikuja nao Mtume Muhammad.

Nachojua mimi Ukristo ulianza kuwepo kabla ya ujio wa Mtume Muhammad. Hoja yako iko wapi ? Kwamba kisa umetangulia ndiyo Ukristo ni kweli au mafundisho yake ?
 
Kwanza inabidi tujue Ukristo umeletwa na nani ?

Uislamu kwa maana ya imani,upo tangu anaumbwa Adamu,ila kwa sheria alikuja nao Mtume Muhammad.

Nachojua mimi Ukristo ulianza kuwepo kabla ya ujio wa Mtume Muhammad. Hoja yako iko wapi ? Kwamba kisa umetangulia ndiyo Ukristo ni kweli au mafundisho yake ?
Uislam wa Adam ulikuwa vipi?
 
Kama hujui square root ya 2 unaweza kusema kwamba square root ya 2 si 10?

Logical non sequitur.
Kaka bado uko huku gizani ? Hata kuhoji haya mambo huwezi,kuna muda kusoma huwa bora zaidi kwa mambo kama haya kuliko kuchangia. Ona unavyogeuka kituko.
 
Na hata hao Wayahudi wameibadilisha sana Biblia na walivyoiandika awali si inavyotafsiriwa leo, Biblia na Quran ni mkusanyiko wa vitabu vilivyoandikwa na watu wakipambana na mazingira yao, hizi habari za Mungu kuwapo ni za kimapokeo zaidi ya ukweli.

Ukisoma wasomi wa Biblia wanakueleza kwamba inavyotafsiriwa na waumini wengi ni tofauti sana na ukweli wa mambo.

Mfano mzuri ni hiki kitabu cha Profesa James L Kugel aliyekuwa anafundisha masomo ya Biblia Harvard, kachambua vizuri sana jinsi Biblia ilivyobadilishwa sana na tofauti kati ya inavyotafsiriwa na ilivyo kiukweli.


How to Read the Bible​

A Guide to Scripture, Then and Now​

READ AN EXCERPT
Scholars from different fields have joined forces to reexamine every aspect of the Hebrew Bible. Their research, carried out in universities and seminaries in Europe and America, has revolutionized our understanding of almost every chapter and verse. But have they killed the Bible in the process?

In How to Read the Bible, Harvard professor James Kugel leads the reader chapter by chapter through the “quiet revolution” of recent biblical scholarship, showing time and again how radically the interpretations of today’s researchers differ from what people have always thought. The story of Adam and Eve, it turns out, was not originally about the “Fall of Man,” but about the move from a primitive, hunter-gatherer society to a settled, agricultural one. As for the stories of Cain and Abel, Abraham and Sarah, and Jacob and Esau, these narratives were not, at their origin, about individual people at all but, rather, explanations of some feature of Israelite society as it existed centuries after these figures were said to have lived. Dinah was never raped — her story was created by an editor to solve a certain problem in Genesis. In the earliest version of the Exodus story, Moses probably did not divide the Red Sea in half; instead, the Egyptians perished in a storm at sea. Whatever the original Ten Commandments might have been, scholars are quite sure they were different from the ones we have today. What’s more, the people long supposed to have written various books of the Bible were not, in the current consensus, their real authors: David did not write the Psalms, Solomon did not write Proverbs or Ecclesiastes; indeed, there is scarcely a book in the Bible that is not the product of different, anonymous authors and editors working in different periods.

Such findings pose a serious problem for adherents of traditional, Bible-based faiths. Hiding from the discoveries of modern scholars seems dishonest, but accepting them means undermining much of the Bible’s reliability and authority as the word of God. What to do? In his search for a solution, Kugel leads the reader back to a group of ancient biblical interpreters who flourished at the end of the biblical period. Far from naïve, these interpreters consciously set out to depart from the original meaning of the Bible’s various stories, laws, and prophecies — and they, Kugel argues, hold the key to solving the dilemma of reading the Bible today.

How to Read the Bible is, quite simply, the best, most original book about the Bible in decades. It offers an unflinching, insider’s look at the work of today’s scholars, together with a sustained consideration of what the Bible was for most of its history — before the rise of modern scholarship. Readable, clear, often funny but deeply serious in its purpose, this is a book for Christians and Jews, believers and secularists alike. It offers nothing less than a whole new way of thinking about sacred Scripture.



Biography​

James Kugel was the Starr Professor of Hebrew Literature at Harvard University for twenty-one years. He retired from Harvard to become Professor of Bible at Bar Ilan University in Israel, where he also served as chairman of the Department of Bible.

A specialist in the Hebrew Bible and the Dead Sea Scrolls, Kugel is the author of more than eighty research articles and fifteen books, including The Idea of Biblical Poetry, In Potiphar’s House, On Being a Jew, and The Bible As It Was(this last the winner of the Grawemeyer Prize in Religion in 2001). His more recent books include The God of Old, The Ladder of Jacob, How to Read the Bible, awarded the National Jewish Book Award for the best book of 2007, In the Valley of the Shadow, and A Walk Through Jubilees. He is a member of the Society of Biblical Literature, and Editor-in-chief of Jewish Studies: an Internet Journal.
Bible Department
Bar Ilan University
52900 Ramat Gan, Israel
telephone: +9722 672-2197
website: www.jameskugel.com
email: jlk@jameskugel.com
1. Born: August 22, 1945, New York, N.Y. I am married and have four children.
2. Education: Yale University, B.A. (1968)
Harvard University, Junior Fellow (1972-76)
City University of New York, Ph. D. (1978)
3. Areas of interest: Hebrew Bible; history of biblical exegesis; Judaism.
4. Positions held: Andrew Mellon Faculty Fellow, City University (1978-79)
Lecturer, Harvard University (1979-80)
Assistant Professor, Religious Studies and Comparative Literature, Yale University (1980-82); Associate Professor (1982)
Starr Professor of Hebrew Literature, Harvard University (1982-2003)
Professor of Bible, Bar Ilan University (1992-2013)
Professor Emeritus, Bar Ilan University, 2014—
5. Memberships and Offices:
Poetry Editor, Harper’s Magazine (1972-4)
Co-founder and associate editor, Prooftexts: A Journal of Jewish Literary History (1981-2000)
Executive Board, Association for Jewish Studies (1983-84)
Chairman, Department of Near Eastern Languages, Harvard University (1987-91)
Director, Center for Jewish Studies, Harvard University (1996-2001)
Editorial Board, Jewish Studies Quarterly (1993-2003)
Member, American Academy for Jewish Research (1999-2003)
Founder and editor-in-chief, Jewish Studies: an Internet Journal (2002- present)
Director, Institute for the History of the Jewish Bible, Bar Ilan University (2003-10)
Chairman, Department of Bible, Bar-Ilan University (2006-09)
Editorial Board, Themes in Biblical Narrative – Jewish and Christian Traditions (series, Brill Publications, Leiden)
Editorial Board, פרשנות ובקורת (Bar Ilan)
Editorial Board, שנתון המקרא (Jerusalem)
Editorial Board, Biblische Notizen—Neue Folge (Vienna) (2010-present)
Editorial Directorate, מוסד ביאליק מו”ל
Editorial Board, Journal of Ancient Judaism (2011-present)
6. Awards and Prizes: Phi Beta Kappa (1968), Wrexham Prize (1968), Fulbright Graduate Fellowship (1968), Danforth Graduate Fellowship (1968), Woodrow Wilson Fellow (1968), Bryant Dissertation Prize (1977), A. Mellon Fellow (1977), Ingram Merrill Fellow (1978), S. F. Morse Faculty Fellow (1981-82). The Idea of Biblical Poetry was supported by awards from the F. Hilles and A. W. Griswold Funds, and received the book prize of the American Jewish Committee (1982). Research for In Potiphar’s House was sponsored by a grant from the National Endowment for the Humanities (1988-89). The Bible As It Was was supported by awards from the Alan M. Stroock Publication Fund for Jewish Studies and a grant from the Littauer Foundation. It was among five finalists for the National Book Critics Circle Award in the category of General Nonfiction. Traditions of the Bible was honored with a special session at the 1999 Society of Biblical Literature convention. The Bible As It Was and Traditions of the Bible were jointly awarded the $200,000 Grawemeyer Award for the best book in Religion, 2001. How to Read the Bible was awarded the prize for the best book in any category by the National Jewish Book Awards, 2007. It was chosen as one of the New York Times “Best Books of 2007, All Categories.” Outside the Bible, coedited with Louis Feldman and Lawrence Schiffman, was just awarded the National Jewish Book Award for Scholarship, 2014.
vipi kuhusu wanao sema Qur'an ilishushwa moja kwa moja . Nini maoni yako kuhusu hili?
 
Kaka bado uko huku gizani ? Hata kuhoji haya mambo huwezi,kuna muda kusoma huwa bora zaidi kwa mambo kama haya kuliko kuchangia. Ona unavyogeuka kituko.
Inawezekana mimi ni kituko.

Lakini, wewe kusema mimi ni kituko bila kuonesha kituko kipo wapi, kipo vipi, kwa nini ni kituko, na ili kisiwe kituko inabidi iweje, wewe umekuwa kituko zaidi yangu.

Siwezi hata kubishana nawe.

Kwa sababu hujajenga hoja.

Umekebehi tu.

Kwa kebehi tupu.

Kumpinga mtu aliyejenga hoja kwa kutumia hesabu na mantiki.

Sasa hapo kati yangu na wewe nani kituko?
 
Swali, kwanini Mungu alipomuumba Adam hakumpa Muongozo hadi ipite miaka takribani 5,000 ndipo Muongozo huu uitwao Uislam utoke?
Muongozo alio pewa Adamu ulimtosheleza na wanawe. Lakini zama za Adamu muongozo ulikuwa unatoka moja kwa moja tu,anapewa maelekezo,fanya hivi acha hiki.

Ndiyo maana ukisoma katika habari za mitume,utaona ya kuwa Nuhu ndiyo alikiwa mtume wa kwanza,na hii ni baada ya watu kuanza kufanya ushirikina.

Lakini jambo lingine ambalo ni jipya kwangu ni kuwa hii idadi ya makadirio ya miaka 5000,umeijuaje ?
 
Ilishushwa kutoka wapi?

Maana inawezekana kuwa ilishushwa kutoka vichwani mwa watu.Hilo siwezi kupinga.
ilishushwa kutoka mbinguni kuja duniani kwa Prophet Muhammad Peace Be Upon Him kupitia malaika Gabriel. Malaika Gabriel alikuwa anamsomea Prophet Muhammad aya za Qur'aan tukufu na kumuamuru kwenda kuziandika. Jambo hili lilifanyika mara kwa mara katika vipindi tofauti tofauti. Mwisho wa siku mkusanyiko wa hizo aya ndio ukatengeneza kitu kinaitwa Qur'aan.
 
ilishushwa kutoka mbinguni kuja duniani kwa Prophet Muhammad Peace Be Upon Him kupitia malaika Gabriel. Malaika Gabriel alikuwa anamsomea Prophet Muhammad aya za Qur'aan tukufu na kumuamuru kwenda kuziandika. Jambo hili lilifanyika mara kwa mara katika vipindi tofauti tofauti. Mwisho wa siku mkusanyiko wa hizo aya ndio ukatengeneza kitu kinaitwa Qur'aan.
Unaweza kuthibitisha kimantiki kwamba hiyo mbingu ipo kweli na huyo Malaika yupo au aliwahi kuwepo?

Na kwamba hizi habari si hadithi za mapokeo tu?
 
Inawezekana mimi ni kituko.

Lakini, wewe kusema mimi ni kituko bila kuonesha kituko kipo wapi, kipo vipi, kwa nini ni kituko, na ili kisiwe kituko inabidi iweje, wewe umekuwa kituko zaidi yangu.

Siwezi hata kubishana nawe.

Kwa sababu hujajenga hoja.

Umekebehi tu.

Kwa kebehi tupu.

Kumpinga mtu aliyejenga hoja kwa kutumia hesabu na mantiki.

Sasa hapo kati yangu na wewe nani kituko?
Hili ndiyo tatizo la kuandika mambo bila kusoma ulicho kiandika,rejea ulicho kiandika.

Ulicho andika si uhalisia kisha unakuja kujengea hoja kwa uhalisia. Hii logic ya wapi ? Sasa nashangaa pia kuona unataka uonyeshwe ujinga wako ambao uko wazi zaidi. Ulichotaka nimekifanya,sasa uje kusema sijaonyeonyesha.
 
Hili ndiyo tatizo la kuandika mambo bila kusoma ulicho kiandika,rejea ulicho kiandika.

Ulicho andika si uhalisia kisha unakuja kujengea hoja kwa uhalisia. Hii logic ya wapi ? Sasa nashangaa pia kuona unataka uonyeshwe ujinga wako ambao uko wazi zaidi. Ulichotaka nimekifanya,sasa uje kusema sijaonyeonyesha.
Nilichokiandika kipi? wapi? si uhalisia vipi? uhalisia ni nini? unaupimaje kuwa huu uhalisia na si kitu unachofikiri tu kuwa ni uhalisia?

Your intellectual laziness is directly proportional to your false sense of superiority.
 
Back
Top Bottom