#COVID19 China: Aliyetoa taarifa za kuibuka kwa Covid-19 aachiwa huru baada ya miaka 3

#COVID19 China: Aliyetoa taarifa za kuibuka kwa Covid-19 aachiwa huru baada ya miaka 3

Suley2019

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2019
Posts
2,203
Reaction score
5,610
1683267769757.png

Picha: Fang Bin
Fang Bin, Mfanyabiashara mdogo kutokea Wuhan, China aliyesambaza taarifa kuhusu mlipuko wa ugonjwa wa Uviko19 kupitia mitandao ya Youtube na WeChat ameachiliwa huru baada ya miaka mitatu.

Fang alipotea mara tu baada ya kushea video na picha zilizoonyesha hali halisi ilivyokuwa katika Mji wa Wuhan, ambacho ndicho kilikuwa kitovu cha Uviko19.

Taarifa zinadai kuwa mwanaume huyo alikamatwa kwa sababu mamlaka husika hazikutaka kutoa taarifa za ukweli kuhusu mlipuko wa Uviko19 ulioleta ‘jinamizi’ kubwa duniani.

Kwa mujibu wa mwanafamilia mmoja, Fang aliachiliwa huru Jumapili iliyopita na hali yake ya kiafya sio nzuri kutokana na matatizo ya kula na kulala yaliyompata alipokuwa kizuizini hivyo kupelekea kupoteza uzito mwingi na kuwa mdhaifu.

Katika moja ya video alizoziposti hospitali za mji wa Wuhan zilionekana zikiwa zimelemewa na wagonjwa pamoja na ndugu zao huku video nyingine ikimuonyesha akihesabu mifuko iliyokuwa imebeba miili ya watu.
 
Chinese Communist Party inaongoza kwa kubinya uhuru wa kupeana habari na kueneza propaganda Duniani.

Hii inaonyesha ni kwa jinsi gani authoritarian government ilivyo sio rafiki kabisa kwenye maisha ya binadamu.

Mwaka jana wakati Dunia imeanza kirecover na kuwa salama kutokana na mlipuko wa Covid 19 nchini China ilikuwa hali ni tofauti kabisa kutokana na Zero covid policy wachina waliendelea kufungiwa ndani na kuwekwa kwenye lockdown badala ya kuwa na mfumo mzuri wa kiafya ikiwemo chanjo n.k
 
China imeficha mambo mengi sana kuhusu Covid

Na ndio nchi iliyofanikiwa kwa kiasi kikubwa kuidhibiti Covid-19.

Ukitazama hata sheria za kuweka karantini watu wanaoingia karantini, wamezilegeza hivi karibuni tu.
 
Back
Top Bottom