China ina mpango wa kuichukua Taiwan kama Urusi inavyotaka kuichukua Ukraine?

China ina mpango wa kuichukua Taiwan kama Urusi inavyotaka kuichukua Ukraine?

FRANCIS DA DON

JF-Expert Member
Joined
Sep 4, 2013
Posts
38,920
Reaction score
44,970
Jana nilikuwa na mazungumzo na mchina mmoja juu ya mgogoro unaondelea baina ya Urusi na Yukrein.

Kubwa kabisa nilimuuliza, ni kwanini uChina haitaki kumchukulia hatua kali Urusi ili kuonyesha kupinga anachokifanya Yukrein ambacho ni kitendo haramu cha uvamizi?

Akajibu kwamba anachofanya Putin ni sahihi kwa sababu intelijensia ya Uchina na Urusi imeonyesha kwamba Marekani ina mpango wa kurudisha tena silaha za nyuklia nchini Yukrein ambayo kabla ya kuvunjika kwa umoja wa Kisovieti , ilikuwa ni sehemu ya Urusi. Mpango huu unaenda sambamba na kuijumuisha Yukrein katika umoja wa kujihami wa nchi za Ulaya (NATO) ambapo baada ya kujiunga nayo, NATO ambayo kiranja wake asiye rasmi ni Marekani, ina kuwa na uwezo sasa wa kuingiza silaha za aina mbalimbali katika himaya za nchi mwanachama aliyejiunga kwa madhumuni ya kuimarisha ulinzi wa kujihami, silaha za nyuklia zikiwa mojawapo.

Akasema, kitendo hicho kinamuogopesha sana hasimu mkuu wa Marekani tangu kipindi cha vita baridi iliyodumu kwa miongo kadhaa baada ya vita kuu ya pili ya dunia, naye si mwingine bali ni Urusi, ambapo inakuwa ni kama adui yake ameleta silaha za nyuklia uwani kwake, kitu ambacho Putin hawezi kukubali kamwe. Anasema, tangu 2008 , Urusi imekuwa ikiipa Yukrein maonyo makali sana juu ya mpango wake huo wa kutaka kujiunga na NATO, lakini nguvu kubwa waliyonayo mabeberu ikiwemo misaada na marupurupu mengine mengi yaliifanya Yukrein imgeuzie kisogo Urusi na kuegemea upande wa mabeberu, na hivi karibuni lile vuguvugu la kujiunga na NATO ndio lilipamba moto sana.

Sasa kwa mujibu wa NATO, ni kwamba ukaigusa nchi yeyote ile ambayo ni mwanachama wake, hiyo ni sawa na kuivamia ulaya yote, maana yake ni kwamba nchi zote za ulaya na wanachama wa NATO, Marekani ikiwemo, watajibu mapigo kwa haraka na kwa uhakika, mercilessly!!, ndio maana Urusi hathubutu hata kurusha jiwe kwenda Poland ambayo ni mwanachama. Sasa ili kuepusha vita kuu ya tatu ya Dunia, Putin akaamua kuiwahi Yukrein kabla haijajiunga na NATO, maana angejiunga tu, ndio ingekuwa mwisho wa mchezo, asingeweza hata kurusha mkuki achilia mbali kombora kwenda Yukrein. So in essence, huu ni mwendelezo wa ‘Proxy wars’ baina ya Urusi na Marekani kama ile ya Syria, Vietnam nk; ni vita ambazo mabeberu wanapigana kwa remote control, ila wanaokufa ni raia wa nchi zingine, wao kazi yao ni kutoa misaada ya silaha tu ili muendelee kupigana, hata ISIS walipewa silaha za kutosha tu ili kumg’oa Bashar Al-Assad, lakini kwakuwa Urusi nayo ilikuwa ikimpa sapoti ya silaha na kifedha Assad, basi hadi leo wamegonga mwamba.

Akaniambia hata Taiwan ilikuwa sehemu ya Uchina, na katika hili vuguvugu la sasa, kuna hamu na mnyevuo mkubwa ndani serikali ya Uchina, kutaka kuikwapua Taiwan ili kuirudisha chini ya himaya ya Uchina, na mipango yote imefikia hatua nzuri sana...

Pia akasema kwa dunia ya sasa, vita kubwa zaidi ni vita ya ki-propaganda, ambapo mabeberu wa magharibi wameshika mpini na Urusi imeshika makali, maana mitandao mikubwa ya kijamii yote imeshikwa na mabeberu hayo, ikiwemo Facebook, Instagram, Youtube, twitter, google NK, ambapo ukadiriki tu kutoa mtazamo kama huu juu ya mgogoro huu, basi moja kwa moja utapoteza akaunti yako, hata sattelite TV nyingi zipo mikononi mwa mabeberu, na mwanzo mwisho wanatapika propaganda za kibeberu tu...

===============================
 
Hii dunia ngumu sana.
Mwenye kisu kikali anakata nyama kubwa atakavyo
 
 
Hizo silaha za nyuklia ambazo US anataka kuziweka Ukraine Zinafanya kazi zikiwa ndani ya ardhi ya UKRAINE tu ila ukiziweka Poland ama kwingineko hazifanyi kazi ndiyo maana US analazimisha Ukraine aingie NATO?

Nauliza hivyo kwasababu, ikiwa Lengo la US ni kuweka silaha za nyuklia mlangoni mwa Urusi why asiweke Poland ambae tayari ni mwanachama?.

MNATUVURUGA SANA BHANA!!
 
Hizo silaha za nyuklia ambazo US anataka kuziweka Ukraine Zinafanya kazi zikiwa ndani ya ardhi ya UKRAINE tu ila ukiziweka Poland ama kwingineko hazifanyi kazi ndiyo maana US analazimisha Ukraine aingie NATO?

Nauliza hivyo kwasababu, ikiwa Lengo la US ni kuweka silaha za nyuklia mlangoni mwa Urusi why asiweke Poland ambae tayari ni mwanachama?.

MNATUVURUGA SANA BHANA!!
Ukraine ipo karibu zaidi, ndio maana mtu akitoka Ukraine anaelekea magharibi kwenda Poland
 
Hizo silaha za nyuklia ambazo US anataka kuziweka Ukraine Zinafanya kazi zikiwa ndani ya ardhi ya UKRAINE tu ila ukiziweka Poland ama kwingineko hazifanyi kazi ndiyo maana US analazimisha Ukraine aingie NATO?

Nauliza hivyo kwasababu, ikiwa Lengo la US ni kuweka silaha za nyuklia mlangoni mwa Urusi why asiweke Poland ambae tayari ni mwanachama?.

MNATUVURUGA SANA BHANA!!
MNATUVURUGA SANA BHANA!!

Kama huyo alivyotohoa/alivyotafsiri kutoka vyombo/wachambuzi wa kimataifa na kujifanya magwiji wa habari za kimataifa kwa kuziweka hapa jamvini au??

Unavurugwa na nini Sheikh wangu!!
 
MNATUVURUGA SANA BHANA!!

Kama huyo alivyotohoa/alivyotafsiri kutoka vyombo/wachambuzi wa kimataifa na kujifanya magwiji wa habari za kimataifa kwa kuziweka hapa jamvini au??

Unavurugwa na nini Sheikh wangu!!
Ujasoma andishi lake, mimi nimelisoma ndiyo maana nimeweka hoja kinzani.
Wewe ambae hujasoma bandiko lake badala yake umekwenda moja kwa moja kunikot bila kusoma bandiko lake kwanza ndiyo maana UNAHISI alichokiandika jamaa amekitoa kwenye vyombo/wachambuzi wakati yeye hajasema kuwa bandiko lake ni kwa mujibu wa chombo iki ama kile ama wachambuzi hawa na wale ndiyo wanasema hivi.unamsingizia jamaa kitu ambacho hajakisema.
Yeye kasema kamuuliza Mchina, si kila Mchina ni mchambuzi.
Let say chanzo cha andiko lake ni hivyo ulivyovitaja ila ilo haliondoi uhalali wa swali langu Chief.
 
Hizo silaha za nyuklia ambazo US anataka kuziweka Ukraine Zinafanya kazi zikiwa ndani ya ardhi ya UKRAINE tu ila ukiziweka Poland ama kwingineko hazifanyi kazi ndiyo maana US analazimisha Ukraine aingie NATO?

Nauliza hivyo kwasababu, ikiwa Lengo la US ni kuweka silaha za nyuklia mlangoni mwa Urusi why asiweke Poland ambae tayari ni mwanachama?.

MNATUVURUGA SANA BHANA!!
Unajivuruga mwenyewe. Mimi nikikuletea kisu nikitege kwenye mbavu zako kila ukiamka unanikuta nimekushikia kisu mbavuni, utaona ni sawa?
 
Ajaribu ili akutane na vikwazo na mudahuu warusi wanatakiwa kutoka ulaya woooote warudi kwao hilo dogo makubwa mengine mmeyasikia
 
Ujasoma andishi lake, mimi nimelisoma ndiyo maana nimeweka hoja kinzani.
Wewe ambae hujasoma bandiko lake badala yake umekwenda moja kwa moja kunikot bila kusoma bandiko lake kwanza ndiyo maana UNAHISI alichokiandika jamaa amekitoa kwenye vyombo/wachambuzi wakati yeye hajasema kuwa bandiko lake ni kwa mujibu wa chombo iki ama kile ama wachambuzi hawa na wale ndiyo wanasema hivi.unamsingizia jamaa kitu ambacho hajakisema.
Yeye kasema kamuuliza Mchina, si kila Mchina ni mchambuzi.
Let say chanzo cha andiko lake ni hivyo ulivyovitaja ila ilo haliondoi uhalali wa swali langu Chief.
Umeshinda Sheikh, ingawa hujanielewa nilimaanisha nini. Akili kubwa tu ndio wangeelewa nililenga nini.

Sheikh wangu tulia, soma tena halafu urudi, utakuwa umepata kitu!!.
 
Umeshinda Sheikh, ingawa hujanielewa nilimaanisha nini. Akili kubwa tu ndio wangeelewa nililenga nini.

Sheikh wangu tulia, soma tena halafu urudi, utakuwa umepata kitu!!.

So, akili kubwa ndiyo wanaona kila Mchina atakae ongelea habari ya Ukraine ni mchambuzi?.

Na ikitokea mtu baki akikataa kuwa si kila Mchina anae ongelea vita ya Ukraine ni mchambuzi ni akili Ndogo?
Sawa,subiri akili kubwa watakuja
 
Jana nilikuwa na mazungumzo na mchina mmoja juu ya mgogoro unaondelea baina ya Urusi na Yukrein.

Kubwa kabisa nilimuuliza, ni kwanini uChina haitaki kumchukulia hatua kali Urusi ili kuonyesha kupinga anachokifanya Yukrein ambacho ni kitendo haramu cha uvamizi?

Akajibu kwamba anachofanya Putin ni sahihi kwa sababu intelijensia ya Uchina na Urusi imeonyesha kwamba Marekani ina mpango wa kurudisha tena silaha za nyuklia nchini Yukrein ambayo kabla ya kuvunjika kwa umoja wa Kisovieti , ilikuwa ni sehemu ya Urusi. Mpango huu unaenda sambamba na kuijumuisha Yukrein katika umoja wa kujihami wa nchi za Ulaya (NATO) ambapo baada ya kujiunga nayo, NATO ambayo kiranja wake asiye rasmi ni Marekani, ina kuwa na uwezo sasa wa kuingiza silaha za aina mbalimbali katika himaya za nchi mwanachama aliyejiunga kwa madhumuni ya kuimarisha ulinzi wa kujihami, silaha za nyuklia zikiwa mojawapo.

Akasema, kitendo hicho kinamuogopesha sana hasimu mkuu wa Marekani tangu kipindi cha vita baridi iliyodumu kwa miongo kadhaa baada ya vita kuu ya pili ya dunia, naye si mwingine bali ni Urusi, ambapo inakuwa ni kama adui yake ameleta silaha za nyuklia uwani kwake, kitu ambacho Putin hawezi kukubali kamwe. Anasema, tangu 2008 , Urusi imekuwa ikiipa Yukrein maonyo makali sana juu ya mpango wake huo wa kutaka kujiunga na NATO, lakini nguvu kubwa waliyonayo mabeberu ikiwemo misaada na marupurupu mengine mengi yaliifanya Yukrein imgeuzie kisogo Urusi na kuegemea upande wa mabeberu, na hivi karibuni lile vuguvugu la kujiunga na NATO ndio lilipamba moto sana.

Sasa kwa mujibu wa NATO, ni kwamba ukaigusa nchi yeyote ile ambayo ni mwanachama wake, hiyo ni sawa na kuivamia ulaya yote, maana yake ni kwamba nchi zote za ulaya na wanachama wa NATO, Marekani ikiwemo, watajibu mapigo kwa haraka na kwa uhakika, mercilessly!!, ndio maana Urusi hathubutu hata kurusha jiwe kwenda Poland ambayo ni mwanachama. Sasa ili kuepusha vita kuu ya tatu ya Dunia, Putin akaamua kuiwahi Yukrein kabla haijajiunga na NATO, maana angejiunga tu, ndio ingekuwa mwisho wa mchezo, asingeweza hata kurusha mkuki achilia mbali kombora kwenda Yukrein. So in essence, huu ni mwendelezo wa ‘Proxy wars’ baina ya Urusi na Marekani kama ile ya Syria, Vietnam nk; ni vita ambazo mabeberu wanapigana kwa remote control, ila wanaokufa ni raia wa nchi zingine, wao kazi yao ni kutoa misaada ya silaha tu ili muendelee kupigana, hata ISIS walipewa silaha za kutosha tu ili kumg’oa Bashar Al-Assad, lakini kwakuwa Urusi nayo ilikuwa ikimpa sapoti ya silaha na kifedha Assad, basi hadi leo wamegonga mwamba.

Akaniambia hata Taiwan ilikuwa sehemu ya Uchina, na katika hili vuguvugu la sasa, kuna hamu na mnyevuo mkubwa ndani serikali ya Uchina, kutaka kuikwapua Taiwan ili kuirudisha chini ya himaya ya Uchina, na mipango yote imefikia hatua nzuri sana...

Pia akasema kwa dunia ya sasa, vita kubwa zaidi ni vita ya ki-propaganda, ambapo mabeberu wa magharibi wameshika mpini na Urusi imeshika makali, maana mitandao mikubwa ya kijamii yote imeshikwa na mabeberu hayo, ikiwemo Facebook, Instagram, Youtube, twitter, google NK, ambapo ukadiriki tu kutoa mtazamo kama huu juu ya mgogoro huu, basi moja kwa moja utapoteza akaunti yako, hata sattelite TV nyingi zipo mikononi mwa mabeberu, na mwanzo mwisho wanatapika propaganda za kibeberu tu...

===============================
Kutokana na hasara aliyoipata Russia kwenye Uvamizi wa Ukraine Licha ya lengo kutokamilika,Basi ni wazi kuwa China hatajaribu kuichukua Taiwan kijeshi,hiyo Option alikuwa nayo,lakini MATOKEO ya Vita vya Ukraine yamemvunja Moyo na kuifuta hiyo Option.

Kama Urusi angeiteka Kiev ndani ya 24 Hrs bila hata vifo 100 vya Raia na Kuweka Rais Kibaraka Basi ni wazi China naye angefuata nyayo hizohizo kuichukua Taiwan kimabavu. Lakini mpaka Sasa Imebuma.
 
Back
Top Bottom