China na Marekani wagombania kuutawala au kumiliki Mwezi

China na Marekani wagombania kuutawala au kumiliki Mwezi

mcshonde

Member
Joined
Jul 15, 2022
Posts
66
Reaction score
154
US CHINA.png

Seneta na bosi mstaafu wa Mamlaka ya Marekani ya Usafiri wa Anga (NASA), Bill Nelson, ametoa tahadhari kuwa muda wowote China wanaweza kuumiliki mwezi mzima ukawa mali yao.
"tuko katika mashindano ya kianga, na China watajimilikisha mwezi endapo wakafanikiwa kufika huko kwa kisingizio cha utafiti" amesema bosi huyo.

Wanaanga kutoka China wanategemewa kufika mwezini ndani ya Muongo huu mmoja kulingana na gazeti la The New York Times.

Marekani haitaki China kuwa na eneo la kudumu mwezini..yaani China wakatembee tu mwezini lakini sio kwenda kufanya utafiti...kuanza kuchimba chimba.

Ishu iko siriaz..ripoti kiusalama ya mwezi novemba 2022 kutoka Pentagon kwenda kwa bunge/Congress ilieleza kuwa china wataweka kituo mwezini sawa na kituo cha kijeshi chenya uwezo wa "surveillance" / upelelezi/kuScan au kufuatilia dunia nzima kwa undani zaidi...na wakifanya tu hivyo hakuna atakayeweza kuwazuia.

Source: IJR: Article: NASA Chief Sounds the Alarm - Chinese Moon Base May Soon Be Over our Heads
 
Tofautisha nyumba unayoishi na kugombania mwezi, humo nani ataishi?
Point yangu hapo haikuwa nyumba, bali a long lasting innovation. Unasema hawataishi milele kwahiyo wasijihusishe na uthubutu huo (kuweka makazi mwezini), mambo mengi tunayotumia leo yalianza kama hivyo (uthubutu). Acha wafanye, hata kama hawatatumia wao hayo makazi, watatumia watoto wao na wajukuu na vitukuu. Tunapotaka kufanya jambo lolote la maendeleo, hata kama outcome yake inapatikana baada ya muongo mmoja, tulifanye tu endapo tumeona litakuwa na manufaa. Tusiangalie life span yetu, vinginevyo utakuwa ni ubinafsi, kwakuwa tunajiangalia wenyewe, ndio maana nchi zinaweka mpango mkakati wa miaka hamsini ijayo!
 
China Wana Project nyingine ya Mwezi wa Artificially.

Wanataka wawe na Mwezi wao wapate kuimiliki Dunia.
 
China Wana Project nyingine ya Mwezi wa Artificially.

Wanataka wawe na Mwezi wao wapate kuimiliki Dunia.
Nasikia wameanza project ya kutengeneza jua lao; wanasema hili lililopo linaelekea kuzimika!
 
Point yangu hapo haikuwa nyumba, bali a long lasting innovation. Unasema hawataishi milele kwahiyo wasijihusishe na uthubutu huo (kuweka makazi mwezini), mambo mengi tunayotumia leo yalianza kama hivyo (uthubutu). Acha wafanye, hata kama hawatatumia wao hayo makazi, watatumia watoto wao na wajukuu na vitukuu. Tunapotaka kufanya jambo lolote la maendeleo, hata kama outcome yake inapatikana baada ya muongo mmoja, tulifanye tu endapo tumeona litakuwa na manufaa. Tusiangalie life span yetu, vinginevyo utakuwa ni ubinafsi, kwakuwa tunajiangalia wenyewe, ndio maana nchi zinaweka mpango mkakati wa miaka hamsini ijayo!

Hakuna atakaeweza kuishi mwezini.. Mungu ana makusudio yake kutuumba na kuishi sayari ya dunia yenye oxygen, hewa nzuri, ardhi yenye rutuba, yenye bahari, maziwa na mito..
 
Wao wagombane lakini wajue hup mwezi ni wangu na mimi ndiye mmiliki halali.
 
Wenzetu wanawaza mwezini sisi ndio tumeruhusiwa kufanya mikutano yetu. ..tupo dunia nyingine
 
Back
Top Bottom