China ni mwenzi wa dhati wa Afrika, asema msomi wa Kenya Dkt. Wafula

China ni mwenzi wa dhati wa Afrika, asema msomi wa Kenya Dkt. Wafula

ldleo

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2010
Posts
1,116
Reaction score
1,121
IMG-1533 (1).jpg

Mwaka huu Chama cha Kikomunisti cha China, CPC, kinatimiza miaka 100 tangu kuanzishwa.

Mtaalamu wa masuala ya China ambaye pia ni Mhadhiri wa Siasa ya Jamii.

katika Chuo Kikuu cha Kenyatta nchini Kenya, Dkt. Otiato Wafula anasema China chini ya usimamizi wa chama cha kikomunisti cha China imezisaidia Nchi nyingi za Afrika Katika utekelezaji wa miradi mikubwa ya miundombinu.

Dk Wafula anasema China ni mwenzi na rafiki wa dhati wa Afrika.

Aidha anasema kuwa Nchi za Afrika zinafaa kuiga sera ya ujamaa ya China na kujifunza utamaduni wa China ili kufikia maendeleo makubwa zaidi.
 
Wale wakenya wenye akili wa dizaini za akina Ngugi hawapo tena , imebakia Kenya iliyojaa wababaishaji na wahuni kama akina Sonko. Kwa anayejua sifa ya mikopo ya China na namna ya ulipaji wake hawezi kusema vile.
 
View attachment 1772617
Mwaka huu Chama cha Kikomunisti cha China, CPC, kinatimiza miaka 100 tangu kuanzishwa.

Mtaalamu wa masuala ya China ambaye pia ni Mhadhiri wa Siasa ya Jamii.

katika Chuo Kikuu cha Kenyatta nchini Kenya, Dkt. Otiato Wafula anasema China chini ya usimamizi wa chama cha kikomunisti cha China imezisaidia Nchi nyingi za Afrika Katika utekelezaji wa miradi mikubwa ya miundombinu.

Dk Wafula anasema China ni mwenzi na rafiki wa dhati wa Afrika.

Aidha anasema kuwa Nchi za Afrika zinafaa kuiga sera ya ujamaa ya China na kujifunza utamaduni wa China ili kufikia maendeleo makubwa zaidi.
Huyu nae akili hana ,tunajifunza uzeeni hizi sio dhama tena zakujifunza maswala ya China au marekani ,tujikite katika Uhuru na kufanya kazi..msomi gani huyu anapingana na nyerere wetu ,RAIA ndo centre ya maendeleo anataka tumuige China yenye serikali ndo centre ya maendeleo......
 
Naiona Zambia ya pili.
Sooner or later.
Huyo msomi Ni mchumia Tumbo .
Ova
 
Huyu nae akili hana ,tunajifunza uzeeni hizi sio dhama tena zakujifunza maswala ya China au marekani ,tujikite katika Uhuru na kufanya kazi..msomi gani huyu anapingana na nyerere wetu ,RAIA ndo centre ya maendeleo anataka tumuige China yenye serikali ndo centre ya maendeleo......
Nyerere alifanya Tanzania ikawa masikini wa kutupwa. Nyerere aliwarudisha nyuma sana kimaendeleo na kiuchumi. Sasa unatoa wapi ubavu wa kuidharau Communist party of China wakati CCM yenu imeshindwa na kazi? Afadhali Wachina wanapata maendeleo ya kiuchumi licha ya wao kukosa uhuru wa kujieleza. Nyinyi mumekosa uhuru wa kujieleza na pia mumekosa maendeleo ya kiuchumi.
 
MK254 Nairobian Tony254
Njooni huku. Mnatakiwa kubadili sera muingie kwenye ujamaa ili mle mema ya nchi 🤣

Tukithubutu ujinga wa ujamaa nitaihama nchi, ujamaa hulemaza akili watu wanakua controlled namna ya kufikiri na kuishi, rais akisema hakuna corona wote chali mnakubali bila hata mmoja kuhoji.
Hehehe hapana yaani no freaking no.....
 
Tukithubutu ujinga wa ujamaa nitaihama nchi, ujamaa hulemaza akili watu wanakua controlled namna ya kufikiri na kuishi, rais akisema hakuna corona wote chali mnakubali bila hata mmoja kuhoji.
Hehehe hapana yaani no freaking no.....
Unamkana purofesa kabisa? Msomi huyu ujue🤣🤣🤣
 
Nyerere alifanya Tanzania ikawa masikini wa kutupwa. Nyerere aliwarudisha nyuma sana kimaendeleo na kiuchumi. Sasa unatoa wapi ubavu wa kuidharau Communist party of China wakati CCM yenu imeshindwa na kazi? Afadhali Wachina wanapata maendeleo ya kiuchumi licha ya wao kukosa uhuru wa kujieleza. Nyinyi mumekosa uhuru wa kujieleza na pia mumekosa maendeleo ya kiuchumi.
Mimi nimezungumzia wazo ,MTU hadi anang'atuka aliona jambo gumu...sisi tushakua wazee ucomunist hautufai ,kinachotufaa kua na sheria zuri ,tufanye kazi kwabidii na uongozi safi(Democratic not otherwise
 
Don't worry Africa China is around,si mwenzi mwema kwani kuna vitu anavyovitaka,anaweza kutoa misaada lakini mwisho wa siku yeye pia atataka aweze kupata faaida kubwaa kuliko ile aliyetoa ,nikimnukuu Dambisa Moyo mwanaharakati wa kike toka Zambia alisema foriegn aid is dead aid ,akimaanisha kuwa ni irrelevant na not functioning in developing countries,tujitegee ni jambo zuri ,ukienda kama zambia unakuta nchi ya kigeni ishaingia katika vyombo vya usalama unakuta polisi mchina,haifai
 
Back
Top Bottom