China: Rais Xi Jinping asisitiza kuendelea na msimamo mkali dhidi ya dawa za kulevya

China: Rais Xi Jinping asisitiza kuendelea na msimamo mkali dhidi ya dawa za kulevya

CRI Swahili

Member
Joined
Dec 21, 2013
Posts
19
Reaction score
42
Picture1.png


Rais Xi Jinping wa China leo ametoa mwito wa kuendelea kwa juhudi za kupambana na dawa za kulevya. Kwenye ujumbe aliotoa mapema kabla ya maadhimisho ya siku ya kupambana na dawa za kulevya (26 June), Rais Xi amesema msimamo mkali dhidi ya dawa za kulevya ni lazima uendelee, ili kupata maendeleo zaidi kwenye udhibiti wa dawa hizo.

Rais Xi amesema kwa sasa tatizo la dawa za kulevya limefungamana na tatizo hilo nje ya China, na linahusika na uhalifu wa kwenye mtandao wa internet na nje ya mtandao wa internet, na kuhatarisha sana maisha ya watu, afya zao, na utulivu wa kijamii

Akisisitiza msimamo mkali kuhusu tatizo la dawa za kulevya Rais Xi ameziagiza kamati za chama na serikali katika ngazi mbalimbali kuboresha mfumo wa usimamizi kwenye usimamizi wa dawa za kulevya na kuhimiza ushirikiano wa kimataifa katika mapambano dhidi ya dawa za kulevya.

Serikali ya China inatumia mbinu mseto kupambana na dawa za kulevya. Njia hiyo inahusisha kuzuia dawa za kulevya kuingia kwenye mipaka ya China na kushughulikia zile zilizo ndani, kufanya ushirikiano wa kimataifa, kutoa elimu kwa jamii kuhusu madhara ya matumizi ya dawa za kulevya kwa afya, usalama, uchumi na jamii, na kujenga vituo vya kutoa matibabu ya kuwasaidia wenye uraibu wa dawa za kulevya.

Takwimu zilizotolewa mwaka jana na kamisheni ya kupambana na dawa za kulevya zinaonyesha kuwa asilimia 0.18 ya wachina (takribani watu milioni 2.5) wanatumia dawa za kulevya.
 
CHUKUENI HATUA PIA MZUIE NA ULAJI WA PAKA, UMBWA, VYURA , NA POPO NK...
 
DglVNqiUwAAMyLx.jpg

Rais Xi Jinping wa China leo ametoa mwito wa kuendelea kwa juhudi za kupambana na dawa za kulevya. Kwenye ujumbe aliotoa mapema kabla ya maadhimisho ya siku ya kupambana na dawa za kulevya (26 June), Rais Xi amesema msimamo mkali dhidi ya dawa za kulevya ni lazima uendelee, ili kupata maendeleo zaidi kwenye udhibiti wa dawa hizo.

Rais Xi amesema kwa sasa tatizo la dawa za kulevya limefungamana na tatizo hilo nje ya China, na linahusika na uhalifu wa kwenye mtandao wa internet na nje ya mtandao wa internet, na kuhatarisha sana maisha ya watu, afya zao, na utulivu wa kijamii

Akisisitiza msimamo mkali kuhusu tatizo la dawa za kulevya Rais Xi ameziagiza kamati za chama na serikali katika ngazi mbalimbali kuboresha mfumo wa usimamizi kwenye usimamizi wa dawa za kulevya na kuhimiza ushirikiano wa kimataifa katika mapambano dhidi ya dawa za kulevya.

Mkuu wa Kamisheni ya kupambana na dawa za kulevya ya China Bw. Zhao Kezhi, ndio amefikisha ujumbe wa Tais kwenye mkutano wa maadhimisho na kutaka utekelezaji wake uwe na mafanikio. Kwenye mkutano huo mashirika 100 na watu 100 waliotoa mchango mkubwa kwenye mapambano dhidi ya dawa za kulevya walitambuliwa na kupongezwa.

Msimamo mkali wa China kwenye vita dhidi ya dawa za kulevya ni wa muda mrefu. Kutokana na historia ya tangu vita ya kasumba (1839- 1842) China inatambua madhara ya dawa za kulevya kiusalama, kiuchumi na kijamii.

Serikali ya China imekuwa ikichukua hatua mbalimbali za kupambana na dawa hizo ikiwa pamoja na kutumia vyombo vya usalama kuzuia dawa kutoka nje kuingia ndani ya China na kupambana na zile zilizopo ndani ya China, kudhibiti matumizi haramu ya kemikali halali za viwandani kutumika kutengeneza dawa haramu, kutoa elimu kwa umma kuhusu madhara ya matumizi ya dawa za kulevya, na kuwapatia matibabu wale waliokumbwa na uraibu wa dawa za kulevya.

Kutokana na juhudi hizi idadi ya watu wanaotumia dawa za kuleya nchini China imeendelea kupungua. Ripoti iliyotolewa mwezi juni mwaka jana na kamati ya taifa ya kupambana na dawa za kulevya inasema mwaka 2018 ni asilimia 0.18 ya wachina walikuwa wanatumia dawa za kulevya. Idara kuu ya forodha ya China pia ilitoa takwimu ikisema imeshughulikia matukio 604 ya kusafirisha dawa za kulevya na kukamata tani37.5 za dawa za kulevya na kemikali nyingine zinazohusiana na dawa hizo, kiasi ambacho kimeendelea kupungua kwa mwaka wa tatu mfululizo.
 
Haya sasa nyie mnaopanga kupeleka dawa za kulevya China mjipange maana kunyongwa (kula kitanzi) bado kupo palepale.
 
Back
Top Bottom