China-US TechWar: Pentagon wakiri ni vigumu kuachana na huduma za Huawei kikamili

China-US TechWar: Pentagon wakiri ni vigumu kuachana na huduma za Huawei kikamili

Xi Jinping

JF-Expert Member
Joined
Jun 14, 2023
Posts
3,651
Reaction score
11,548
Mwaka 2019 serikali ya Marekani chini ya aliyekuwa raisi wakati huo Donald Trump, iliweka sheria ya kutotumia huduma na vifaa vya Huawei katika idara nyeti za usalama wa taifa hilo.

Sababu kuu ilikuwa ni kwamba usalama wa taifa hilo ulikuwa hatarini, ikidai kuwa China inaitumia kampuni ya Huawei kama chombo cha kijasusi.

Pentagon ambayo ni idara kuu ya usalama ya Marekani, ilipewa kazi hiyo ya kuhakikisha kuwa idara zote za kiusalama, huduma za kijeshi, kambi za jeshi la Marekani zilizo ndani na nje ya Marekani, maafisa wa usalama na ulinzi wa Marekani hawatumii huduma na vifaa vya Huawei.

Ikiwa inakaribia miaka 5 tangu Pentagon wapewe kazi hiyo, imeonekama hawajatimiza ipaswavyo jukumu hilo walilopewa na bunge la Marekani.


Ni changamoto gani zimefanya Pentagon ishindwe? Changamoto kuu 6 walizokumbana nazo Pentagon:
  • Huawei ni kampuni kubwa ya teknolojia ya mawasiliano ambayo huduma zake zinatawala kwa 40% katika soko la dunia. Hivyo imekuwa vigumu sana kwa nchi washirika zenye kambi za jeshi la Marekani kuachana na Huawei from the scratch.
"Kuna sehemu fulani za ulimwengu ambapo huwezi kabisa kuikimbia Huawei."
–Brennan Grinon (the Former U.S Defense Dept official)

  • Pentagon bado inafanya kazi na defense contractors ambao wanatumia components na huduma za kampuni ya Huawei.

  • Bado wataalamu wa masuala ya kijeshi, ulinzi na usalama wa Marekani wanatumia Huawei networks kwenye shughuli zao muhimu sehemu mbalimbali duniani.

  • Mpango huu unagharamiwa kifedha na serikali ya Marekani. Lakini mpaka sasa fedha zinazotolewa hazikidhi mahitaji. Kwa mujibu wa ripoti za vyombo vya habari vya Marekani, miaka minne baada ya Bunge la Congress kuamuru watoa huduma za mawasiliano na mtandao wa nchini humo kuondoa vifaa vya simu na intaneti kutoka kwa makampuni ya China, bado kuna vifaa vingi vya Huawei na ZTE ambavyo havijabadilishwa. Hawawezi kukamilisha kuondolewa kwa vifaa vya Huawei na ZTE kutokana na upungufu wa fedha wa dola bilioni 3.

  • Mpaka sasa Marekani haijapata mbadala kamili atakayechukua nafasi ya Huawei kutoa huduma na vifaa kwa gharama nafuu. Hii imepelekea mataifa ambayo ni washirika wa Marekani kujiondoa kwenye mpango huu. Nchi kama UAE imekataa ombi la Marekani la kuachana na huduma za Huawei katika idara zake nyeti ambazo zina ushirika na Marekani. Nchi za Saudi Arabia na Latin America pia hazijaunga mkono.

  • Pentagon inaamini kwamba ikiwa vikwazo vyote vilivyoainishwa kuhusiana na Huawei vitatimizwa, kutavuruga pia uwezo wa Pentagon wa kununua kiasi kikubwa cha vifaa vya matibabu, dawa, nguo na aina nyingine za usaidizi wa vifaa jeshi linategemea.
"Sheria hii ya bunge ilikuwa na nia nzuri sana, lakini hatukujua utekelezaji na matokeo ya kile ingemaanisha ingekuwa vigumu, mimi binafsi nadhani hilo haikufikiriwa kabisa."
–Brennan Grinon (Former Defense Dept official)


Katika miezi 3 ya mwanzo ya mwaka 2024 (Jan-Mar), kampuni ya Huawei imepata ongezeko la faida la 564% katika biashara zake. Hili limekuwa pigo kubwa sana kwa Marekani kwa sababu imeenda kinyume kabisa na matarajio yake ilipoiwekea vikwazo kampuni hiyo.

Huawei is growing stronger and less vulnerable.


Je, unafikiri Trump akichaguliwa kuwa raisi wa Marekani atakuja kufanikiwa kukimaliza kiporo alichokiacha ambacho Biden kimemshinda pia?


CREDIT: Bloomberg
 
China ina umri wa miaka 5000, Marekani ina umri wa miaka 400

Wachina wana uzoefu wa muda mreeeefu wa struggles za kibinadamu kuliko hao wazungu , ndiyo maana China haibabaiki

Kitakachoiangusha China ni uonevu wake tu dhidi ya waislamu wa Xinjiang. Ikiweza kurekebisha hilo doa inaweza kupanda na kuwa Taifa la kuaminika duniani kama taifa kiongozi.
 
Kitakachoiangusha China ni uonevu wake tu dhidi ya waislamu wa Xinjiang. Ikiweza kurekebisha hilo doa inaweza kupanda na kuwa Taifa la kuaminika duniani kama taifa kiongozi
Ni media za Magharibi tu ndio huwa wanasema hivyo ili kuiharibia sifa China kwenye jamii ya kimataifa ila kihalisi hakuna uonevu wowote ndani ya Xinjiang
 
Ni juzi tu hapo wawakilishi kutoka Uturuki walienda Xinjiang kuona kama kweli kuna uonevu wamejionea hakuna watu wanaishi vizuri tu
Volkswagen-FAW wana joint venture ya kiwanda Xinjiang

Baada ya kusikia Marekani inalaumu VW-FAW inatumia slave labor wafanyakazi ikabidi Wajerumani wa Volkswagen kuwatuma wawakulishi wao wakachunguze

Hawakuona utumikishaji wowote, Marekani wakaumbuka
 
China ina umri wa miaka 5000, Marekani ina umri wa miaka 400

Wachina wana uzoefu wa muda mreeeefu wa struggles za kibinadamu kuliko hao wazungu , ndiyo maana China haibabaiki

Kitakachoiangusha China ni uonevu wake tu dhidi ya waislamu wa Xinjiang. Ikiweza kurekebisha hilo doa inaweza kupanda na kuwa Taifa la kuaminika duniani kama taifa kiongozi.
Kama ni miaka misri ina miaka mingi sana kuipita china tena imeipita kwa mbali sana na still ipo hapo ilipo. Hivyo umri wa taifa kwenye maendeleo sio hoja.
Iran, Ugiriki, Irak ni kati ya mataifa yenye miaka mingi na yalitisha duniani leo hii yapo hoi kiuchumi
 
Volkswagen-FAW wana joinf venture ya kiwanda Xinjiang

Baada ya kusikia Marekani inalaumu VW-FAW wanasema kuwa wafanyakazi wanatumikishwa, ikabidia Wajerumani wa Volkswagen kuwatuma wawakulishi wao wakachunguze

Hawakuona utumikishaji wowote, Marekani wakaumbuka
Yeah hii niliisikia pia

Ona life la Xinjiang
20240706_214407.jpg
20231120_093237.jpg
20231120_093056.jpg
20231120_093234.jpg
 
Iran, Ugiriki, Irak ni kati ya mataifa yenye miaka mingi na yalitisha duniani leo hii yapo hoi kiuchumi
Kwa hiyo inawezekana siku Marekani ikashuka kama hizo dola nyingine zilizokuwa kubwa duniani miaka hiyo?
 
Kwa uchumi gani uliopo? Eurozone ambayo wana zero growth economy?

Huku industrial output za mataifa makubwa ya Ulaya zikishuka
Stay tuned hivi unaijua former rome empire lakini? unajua ilikuwa na nchi zipi? Unajua nguvu iliyokuwa nayo? Sasa ndo inaenda kurudi tena upya.
Najua we kichwa yako imejaa china china tu huwezi elewa ninachoandika hapa.
 
Moto uliowashwa na China hakuna wa kuuzima kwa sasa
China yupi huyo wa vitu feki, ambaye anapambana real estate industry isimfie huyo ambaye anapambana banks zake zisicollapse?
Huyo china wa mikopo kausha damu?
 
Stay tuned hivi unaijua former rome empire lakini? unajua ilikuwa na nchi zipi? Unajua nguvu iliyokuwa nayo? Sasa ndo inaenda kurudi tena upya.
Najua we kichwa yako imejaa china china tu huwezi elewa ninachoandika hapa.
Naijua Rome empire vizuri sana. Unafikiri ni kwa nini ilianguka?

Ilikuwa superpower kabla ya US kuchukua kijiti

Na ilikuja kuwa superpower baada ya Greece empire kufall

Hizi zote zilikuwa superpowers kabla ya Marekani, ukitaka njoo tuzidiscuss moja baada ya nyingine

1. Egypt Kingdom
2. Assyria
3. Babylon Empire
4. Iranian/Persian Empire
5. Greece Empire
6. Roman Empire

7. Marekani
 
China yupi huyo wa vitu feki, ambaye anapambana real estate industry isimfie huyo ambaye anapambana banks zake zisicollapse?
Huyo china wa mikopo kausha damu?
Unaandika kwa mihemko sana ni banks zipi za China zinataka kucollapse?

20240706_223342.jpg
 
Naijua Rome empire vizuri sana. Unafikiri ni kwa nini ilianguka?

Ilikuwa superpower kabla ya US kuchukua kijiti na ilipanda kuwa superpower baada ya Greece empire kufall
Unajua kwa nini kuna EU? Ushawahi sikia sikia au hata kusoma kuhusu kurudi tena kwa hiyo rumi? Sasa hiyo Rome Empire inarudi soon. Na ndo itakuwa inadrive dunia nzima kiuchumi na itatoa kiongozi atakayetawala dunia nzima hiyo china yako unayoipigia debe humu JF yenyewe nayo itakuwa chini ya hiyo new rome empire. Najua huelewi namaanisha hivi hiyo china yako hiyo itatawaliwa kutokea rumi mpya na itatii vizuri tu najua bado huelewi na hutoelewa.
 
Back
Top Bottom