China vs Japan

Mbona mkuu umepigia mahesabu kidananda sana!?
Kwa mahesabu hayo hufai kuwa mwanauchumi.
Piga mahesabu idadi ya watu wa China na Japan.
China per capita yake inaonekana ndogo kwasababu ya idadi yake ya watu kuwa ni kubwa.
Je Hilo umelitizama??

Pia umetizama GROSS NATIONAL INCOME ya China!??
China ana GNI kubwa kuliko ya Japan.
Utasemaje China Ni Cha mtoto Kwa Japan!??
Hizo hesabu zako ni za kiuchumi wa wapi ulizopiga mkuu?
 
Kwa urahisi wa maisha yako Hapa kuliko China, China bado kuna vijiji wanatumia jembe la mkono, hata wachina wengi wanakimbilia Ulaya.
Wachina kutumia majembe ya mkono haimaanishi hakuna technological advancement.
Ni kazi ndogo ndogo tu za Nikon ndio zinawafanya watumie majembe.
Pia katizame behind poverty line ya China Kesha urudi hapa ndio uongee.
Utagundua wanaokimbia China na idadi wanaobaki ni sawa na tone la mvua baharini.
 
Per capita Yao ni kubwa kwasababu ya idadi yao ya raia Ni ndogo.
Embu chukulia nao China wangekua na population kama ya Japan halafu igawe GDP Yao Kwa idadi ya watu.
Per capita ya China ingekua Mara 4+ ya Japan.
Sasa per Capital inamaana gani ukifanya hivyo?
 
Sasa per Capital inamaana gani ukifanya hivyo?
Per capita maana yake ni kuchukua pato la nchi gawanya kwa idadi ya raia.
Sasa kama nchi yenu raia wachache lazima per capita itasomeka kubwa.
 
Mimi kiutafutaji ningechagua Japan.
Kwasababu nina ushuhuda wa ndugu waliokanyaga China na Japan kwa ujumla.
Inasemekana Japan fursa za kazi ni nyingi kama tu za China.
Ila Japan unaweza ukafanya kazi kiuhuru zaidi kama mtu mweusi kuliko China.
China kuna biasness fulani kwenye rangi na manyanyaso madogo madogo yanakuondolea comfortability.
Pia Mjapan kukupa fursa kubwa zaidi ya kutoka kimaisha ni rahisi kuliko Mchina.
Mchina huwa anapenda uendelee kuwa mtumishi wake siku zote.
Cha mwisho mshahara wa Japan ni mzuri kuliko wa China na ni rahisi na kuna uwezekano wa kuomba uraia Japan lakini China ni impossible.
 
Japo mimi maamuma wa uchumi..

Ila najua per capital income hua iko relevant kwa maeneo yenye idadi ya watu inayokaribiana...
 
Ningechagua China, kwasababu ni rahisi kufanya kazi yoyote hata bodaboda na pia ni sehemu ambayo Kwa mtu mvivu kama Mimi ni rahisi kuishi.

Kwa upande wa Japan, nisingeweza maana Kwa takwimu za kiduni Japani ndio Nchi ambayo raia wake wanafanya kazi masaa mengi zaidi mpaka hupelekea stress wengi wao hujiua.
 
China kupata kazi mtu mweusi ni ngumu sana ila wanawaamini watu weusi wa Amerika tu.
Ukiwa Master hapo China ukiwa mweusi utaambulia kufundisha shule ya chekechea au uende huko kijijini ukafundishe.
 
Nchi yenu haieleweli huku eti unachagua ipi inatusaidia nini sasa
 
kipimo sahihi cha uchumi ni PPP na sio GDP, hii GDP inadanganya sana, haitoi uhalisia wa tofauti ya gharama za maisha!
 
Per capita Yao ni kubwa kwasababu ya idadi yao ya raia Ni ndogo.
Embu chukulia nao China wangekua na population kama ya Japan halafu igawe GDP Yao Kwa idadi ya watu.
Per capita ya China ingekua Mara 4+ ya Japan.
Ukipinguza idadi ya watu China basi na uchumi usingekuwa 18.5 trillion tena. Uchumi ungeshuka mara dufu.
Japan ina watu wachache kuliko China na bado uchumi wao ni 4.4 trillion USD. We huogopi?
Japan ni nchi tajiri kuliko China
 
Ukipinguza idadi ya watu China basi na uchumi usingekuwa 18.5 trillion tena. Uchumi ungeshuka mara dufu.
Japan ina watu wachache kuliko China na bado uchumi wao ni 4.4 trillion USD. We huogopi?
Japan ni nchi tajiri kuliko China
Watu zaidi ya miln 120 sio watu wachache.
Hao watu wanapunguzwa China tu ila Japan hawapunguzwi ?
 
Watu zaidi ya miln 120 sio watu wachache.
Hao watu wanapunguzwa China tu ila Japan hawapunguzwi ?
Linganisha population ya Japan na uchumi wao. Fanya hivyo hivyo kwa China
Utaelewa ninachosema
 
Obviously Japan!
 
Nini unachosema ?
Japan ni nchi tajiri kuliko China
China ina uchumi mkubwa kuliko Japan ila ukilinganisha na population yao maana yake serikali ina kazi kubwa ya kugawa resources zake kila kona ya China ili kufit population. Kwa upande mwingine Japan hizo trillion 4.4 ni nyingi kuliko population yao.

Mfano kama familia tatu (watu 15) zikiunganisha utajiri wao ukawa milioni 50, halafu kuna familia moja 1 (watu 5) yenyewe ina TSh milioni 30. Obviously hiyo familia 1 ni tajiri kuliko hizo familia tatu kwa sababu licha ya kutofikia familia 3 kwa pesa, hii familia moja ina watu wachache wa kuhudumia kuliko familia 3 zilizoungana. Familia hii moja inaweza kuhakikisha kuwa wote wanakula vizuri kuliko hizo familia 3

Ndio kama China na Japan sasa. Kuna sababu inayofanya uone China kuna restaurant, hotels au malls nyingi za bei rahisi kuliko Japan licha ya China kuwa na uchumi mkubwa zaidi. Hii maana yake ni kwamba bado kuna Wachina wengi ambao wana uwezo mdogo wa ku afford expensive life, ingawa malls za kitajiri zipo China pia, wakati Japan malls nyingi ni expensive na kupata hizo za bei ya chini ni nadra sana kwa sababu per capita income ya Japan ni kubwa.

Kutokana na population kuwa kubwa China, bado wana safari ndefu kufikia maisha ya Japan sasahivi.

Mpaka kufikia sasa kwa data za Human Development Index, kwenye nchi zinazoongoza kwa kuwa na maisha bora duniani Japan ni ya 24 wakati China ni ya 75


Ni kama ukijiuliza kwa nini Luxembourg ndio nchi tajiri zaidi duniani wakati USA ndio ina uchumi mkubwa kuliko nchi zote. Ni kwa sababu per capita income ndio inarahisisha kujua nchi ipi ni tajiri zaidi.

Canada ni nchi tajiri kuliko India. Lakini India ina uchumi mkubwa kuliko Canada. Kwa nini?
Hapo pia ndio inaturudisha kwenye fact. Japan ni nchi tajiri kuliko China. Ila China ina uchumi mkubwa kuliko Japan? Jibu ni ler capita income
Tunalinganisha pato la nchi yako na population ya nchi yako
 
Japan GDP per capita $33,834
Macau GDP per capita $78,962
Hong-Kong GDP per capita $50,889
Taiwan GDP per capita $33,234

Unaelewa maana ya nchi tajiri kweli ?
 
Japan GDP per capita $33,834
Macau GDP per capita $78,962
Hong-Kong GDP per capita $50,889
Taiwan GDP per capita $33,234

Unaelewa maana ya nchi tajiri kweli ?
Usikasirike mkuu, mbona comment yangu haikuwa na povu?
Taiwan GDP ni $33234
Halafu hizo nyingine unazotaja sio nchi. Japan ni nchi, hapa tunafananisha na China, sio miji ya China.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…