China yaripoti visa vipya vya corona 62 na vifo 2

China yaripoti visa vipya vya corona 62 na vifo 2

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
Mamlaka ya afya nchini China imethibitisha visa vipya 62 vya maambukizi ya virusi vinavyosababisha ugonjwa hatari wa Covid-19, ambapo janga hilo lilizuka mwezi Desemba mwaka jana.

Siku moja kabla watu 32 waliambukizwa virusi vya Corona, kwamujibu wa mamlaka ya afya.

Vifo viwili vya nyongeza vinavyohusiana na COVID-19 vimeripotiwa, Tume ya kitaifa ya afya imesema katika mkutano wake la kila siku na waandishi wa habari.

Kulingana na ripoti ya tume hiyo, visa 81,802 vya maambukizi na vifo 3,333 vimeripotiwa nchini China Bara tangu kuzuka kwa janga hilo.

Wakati huo huo rais Donald Trump amelishukia shirika la afya duniani WHO na kulilaumu kwa kuegemea upande wa China.Trump amesema asasi hiyo ya kimataifa ilishirikiana na China kuficha ukweli kuhusu ugonjwa hatari wa Covid-1.

Rais wa Marekani Trump ametishia kulikatia fedha shirika la afya Duniani WHO kwa sababu amesema shirika hilo halikutilia maanani kwa namna ilivyopasa hatari ya maambukizi ya virusi vya corona
 
Mamlaka ya afya nchini China imethibitisha visa vipya 62 vya maambukizi ya virusi vinavyosababisha ugonjwa hatari wa Covid-19, ambapo janga hilo lilizuka mwezi Desemba mwaka jana.

Siku moja kabla watu 32 waliambukizwa virusi vya Corona, kwamujibu wa mamlaka ya afya.

Vifo viwili vya nyongeza vinavyohusiana na COVID-19 vimeripotiwa, Tume ya kitaifa ya afya imesema katika mkutano wake la kila siku na waandishi wa habari.

Kulingana na ripoti ya tume hiyo, visa 81,802 vya maambukizi na vifo 3,333 vimeripotiwa nchini China Bara tangu kuzuka kwa janga hilo.

Wakati huo huo rais Donald Trump amelishukia shirika la afya duniani WHO na kulilaumu kwa kuegemea upande wa China.Trump amesema asasi hiyo ya kimataifa ilishirikiana na China kuficha ukweli kuhusu ugonjwa hatari wa Covid-1.

Rais wa Marekani Trump ametishia kulikatia fedha shirika la afya Duniani WHO kwa sababu amesema shirika hilo halikutilia maanani kwa namna ilivyopasa hatari ya maambukizi ya virusi vya corona
China wameanza kuona aibu ya kusema uongo wa vifo chini mwao......sasa wameanza kutangaza, case mpya wakati jana walisema hawaja pokea mgonjwa hata mmoja mji huwani....... waongo wakubwa hao wa China wametuletea gonjwa kukolificha mda mlefu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Visa - cases

Bado sijaelewa it means case kwa kiswahili ni kisa...?

Tuache showcase, briefcase au case kama case, kwa nini iwe kisa baada ya kesi japokuwa hata kesi pia inakuwa haina mantiki pia kwa tafsiri ya case kuipeleka mpaka kwenye tafsiri ya kisa.
 
Bado sijaelewa it means case kwa kiswahili ni kisa...?

Tuache showcase, briefcase au case kama case, kwa nini iwe kisa baada ya kesi japokuwa hata kesi pia inakuwa haina mantiki pia kwa tafsiri ya case kuipeleka mpaka kwenye tafsiri ya kisa.
Neno moja linaweza kuwa na maana zaidi ya moja.

"Case" inaweza kumaanisha kisa cha tendo fulani na vile vile ikamaanisha kisa kinachosababisha mtu kwenda mahakamani. Mahakamani huko wanafanya rejesha ya kisa cha matendo yaliyotokea nyuma.
 
Neno moja linaweza kuwa na maana zaidi ya moja.

"Case" inaweza kumaanisha kisa cha tendo fulani na vile vile ikamaanisha kisa kinachosababisha mtu kwenda mahakamani. Mahakamani huko wanafanya rejesha ya kisa cha matendo yaliyotokea nyuma.

Japo nimekuwa mgumu kuelewa ila acha tu nijaribu kukuelewa kiongozi.

Nakushkuru sana kwa msaada wako na muda wako pia.

Thanks.
 
China wameanza kuona aibu ya kusema uongo wa vifo chini mwao......sasa wameanza kutangaza, case mpya wakati jana walisema hawaja pokea mgonjwa hata mmoja mji huwani....... waongo wakubwa hao wa China wametuletea gonjwa kukolificha mda mlefu

Sent using Jamii Forums mobile app
Exactly huwez danganya watu milele, utawadanganya kwa mda
 
Back
Top Bottom