China yatangaza kupunguza ushuru kwa bidhaa za kigeni kuanzia Januari 2020

China yatangaza kupunguza ushuru kwa bidhaa za kigeni kuanzia Januari 2020

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
China imesema leo kuwa itapunguza ushuru kuanzia Januari mosi kwenye zaidi ya bidhaa 850 za kigeni ikiwemo nyama ya kuhifadhiwa ya nguruwe, madawa ya maradhi ya pumu na baadhi ya vifaa vya teknolojia ili kuchochea maendeleo ya kiuchumi.

Tangazo hilo linafuatia makubaliano ya muda ya kibiashara na Marekani katika vita vya ushuru wa bidhaa ambavyo vimeyayumbisha masoko ya kifedha.

Hatua hiyo inaongeza kwa mfululizo wa mapunguzo ya kodi katika kipindi cha miaka miwili iliyopita ambayo serikali ya China inasema yanalenga kuimarisha usambazaji wa bidhaa mbalimbali na kuhimiza ushindani.

Maafisa wa China wanasema hatua hizo hazipaswi kuchukuliwa kama kusalimu amri kwa shinikizo la Marekani
 
Hiyo ni "Concession", China lazima wafungue zaidi milango ili nao wapokee bidhaa za wengine.

Huwezi kuwageuza wenzako kuwa dampo.
 
Trumpet ni kiboko ya Great China. Uwezi ukawa unauza bidhaa njee alafu utaki wewe kwako walete na bado mpaka aziruhusu Google, Facebook, Twitter na nyenginezo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom