Chinese Contractor

Chinese Contractor

Invisible

JF Admin
Joined
Feb 26, 2006
Posts
16,286
Reaction score
8,380
Dear Seh

The steel roof and framework she is already constructed.

Pleese send us the foundation plans and the drawings before the big wind she comes.

Regards from Sipho,

Site Supervisor.


(Notice the wordings huh... 🙂 )

NOW SEE WHAT'S ALL ABOUT!

i361_Indian.jpg
 
HII NDIO TANZANIA ZAIDI YA UIJUAVYO!
no professional ethics at all!
 
We robot wewe acha masihara wewe.
hahahahahahahaha
kaaaaz kweli kweli
 
Duu Nimecheka si utani.Hiyo construction si mchezo!
 
the chinese are taking over our continent.they are destroying our environment with their substandard ,fake or cloned machendise as well as also strangling our local economic enterprises[jua kali sector].it is a good idea to start sensitizing people around us so that it will not be too late when we realize that we have been dancing with the devil.
 
Tusiwalaumu hawa wachina ,makosa ni yetu wenyewe! Jakaya aliahidi watanzania ajira lakini cha kushangaza vijana wakichina wamekuja na kuchukua ajira za;- Kuchomelea magari, fundi uashi, kuuza karanga na maua wakati vijana wetu wanashinda vijiweni. Mimi najiuliza hivi serikali yetu haioni mambo yote haya? Pengine wanangoja waunde kikosi kazi au tume ya kutafuta nani amewaruhusu vijana wakichina kuuza mitumba kariakoo!!Hii ni aibu kwa serikali; someone is sleeping on his/her job!!
 
It is a wake up call to start strengthening our position in the construction industries. Tanzania kama sio made in China basi itakuwa made in India mana ndio wanapeta zaidi kwenye local construction projects karibu zote.
 
i myself and i like chinesse... ur money buys the quality...and everybody atapata the same product but different quality...sasa mnapowalaumu kuwa hawafai ni juu ya nini?Uchumi gani unaokufa kwa wachina kuuza vitu vibovu na kwa bei rahisi??
 
Invisible,

Ulipoweka hiyo picha uliandika kama JOKE. Ila hukujua kuwa jamaa wanafanya kweli. Kwenye ujenzi wa majengo marefu, ni muhimu sana kuweka msingi imara wa jengo maana ukifanya mchezo, basi jengo laweza kuturn na kupinda mhimili wake wa 90 degree na kuwa kama yale majengo ya chuo cha biashara Dodoma (ila yale yaliengwa yaonekane hivyo) na au hayo majengo huanguka kabisa. Ndiyo maana ni muhimu sana kuweka au msingi mrefu sana kwenda chini au kujenga kwa kutumia piles foundations ambazo hupigiliwa chini na nyundo kubwaa (nafikiri BoT waliweka misingi hiyo kwani miaka ya 80 mwishoni kulikuwa na makelele sanaa pale kwao). Katika shule zote duniani, mfano wa uzembe au kutokujua huwa wanachukulia jengo la PIZZA TOWER (http://www.aroundtheplanet.org/wp-content/uploads/2008/04/pisa.jpg) ambalo ukiliona tu unaona hilo tatizo kwani jengo limepinda si kawaida.

pisa.jpg


Wachina kama vile hiyo mifano haitoshi, wameamua na wao watengeneze yao ila sema wao haikusimama, ikapitiliza na kuanguka. Jengo kwa bahati nzuri liliuwa mtu mmoja tu. Naweka link na picha kwa wasiotaka kwenda kusoma zaidi.

Man Killed in Building Collapse
 

Attachments

  • China building.jpg
    China building.jpg
    32.4 KB · Views: 59
  • China building 1.jpg
    China building 1.jpg
    26.5 KB · Views: 51
  • China building 2.jpg
    China building 2.jpg
    37.5 KB · Views: 49
Mkuu;
Tuslaumu wachina, je vijana wa kitanzania ukiwapa kazi watafanya kweli?.Lazima tujiulize kwanza, je vijana tuna nidhamu ya kazi?.Make katika sehemu ya kazi nilizopitia nimekuwa na vijana wengi sana, lakini kufika kazini ni saa tatu au saa nne eti shida ya usafiri.Nimekuwa sehemu nyingi nimeona haya mambo.
Watoto wa kike ndo usiseme kabisa anafika saa tatu na anataka aondoke saa nane kurudi nyumbani
Mkuu tunaharibu wenyewe, tuslaumu mtu yeyote.
Tunaitaji kuwa na nidhamu yakazi, ebu tuchukulie mfano,nenda sekita za serikali ambazo wanafika na kuweka sahihi kwenye kitabu na kuondoka, ni wangapi wanakuja wamelewa kazini.Nenda muhimbili pale wanaita first track,utakuta foreni ya watu wanasubiri kulipia malipo ili wakapate hudumu, mhudumu mwenyewe bila kujali anapiga simu na kuzunguka kwenye kiti akifurahia watu walivyopanga foreni na bila kujali mtu gani anaumwa.Nenda pale aridhi makao makuu, kuna bango limeandikwa kwamba anayeitaji huduma aje kuanzia saa tatu asubuhi.Huduma na panctuality kwenye kazi sisi watanzania ni ZEROOOOO!, upo mkuu.
Mwisho nakukalibisha ufanye kazi kwenye makampuni ya wazungu uone panctuality na nidhamu ya kazi ilivyo.
 
Last edited:
Mkuu;
Tuslaumu wachina, je vijana wa kitanzania ukiwapa kazi watafanya kweli?.Lazima tujiulize kwanza, je vijana tuna nidhamu ya kazi?.Make katika sehemu ya kazi nilizopitia nimekuwa na vijana wengi sana, lakini kufika kazini ni saa tatu au saa nne eti shida ya usafiri.Nimekuwa sehemu nyingi nimeona haya mambo.
Watoto wa kike ndo usiseme kabisa anafika saa tatu na anataka aondoke saa nane kurudi nyumbani
Mkuu tunaharibu wenyewe, tuslaumu mtu yeyote.
Tunaitaji kuwa na nidhamu yakazi, ebu tuchukulie mfano,nenda sekita za serikali ambazo wanafika na kuweka sahihi kwenye kitabu na kuondoka, ni wangapi wanakuja wamelewa kazini.Nenda muhimbili pale wanaita first track,utakuta foreni ya watu wanasubiri kulipia malipo ili wakapate hudumu, mhudumu mwenyewe bila kujali anapiga simu na kuzunguka kwenye kiti akifurahia watu walivyopanga foreni na bila kujali mtu gani anaumwa.Nenda pale aridhi makao makuu, kuna bango limeandikwa kwamba anayeitaji huduma aje kuanzia saa tatu asubuhi.Huduma na panctuality kwenye kazi sisi watanzania ni ZEROOOOO!, upo mkuu.
Mwisho nakukalibisha ufanye kazi kwenye makampuni ya wazungu uone panctuality na nidhamu ya kazi ilivyo.

Mkuu,
I agree with you kwamba vijana wengi hawana nidhamu ya kazi. Yuko rafiki yangu ambaye ni raia wa kigeni yeye na wenzake wameamua kuajiri wafanyakazi wa nyumbani kutoka nchi moja ya jirani kwa sababu tu anasema wafanyakazi wa kitanzania si wachapakazi na wanavisingizio katika kila wanaposhindwa kutimiza wajibu wa kazi zao. Anasema haoni haja ya kuendelea kuvumilia upuuzi ilhali kuna watu wengine wanaoweza kufanya kazi hiyo kwa ufanisi mkubwa bila ya matatizo.
Suala la wachina kkuchukua nafasi za kazi zetu au kufanya biashara hili niliwahi kulizungumzia huko nyuma, endapo utawaondoa wachina pale Kariakoo basi ujitayarishe kuwapokea watanzania kadhaa wanaoishi China na kufanya biashara, vile vile kwa kuwa China ndiyo itakayokuwa taifa kubwa kiuchumi basi Tanzania ijitayarishe kusimama kivyake-vyake.
 
Hii ndiyo Tanzania ya Lowassa.

Kwani hii imetokea TAnzania???? BTW sio suala la usanii au kushangaaa kwa jinsi teknologia inavyoendelea hii inawezekana kabisa, hujawahi kusikia nchi iliyosogeza magorofa kilomita kadhaa???????
 
Kwani hii imetokea TAnzania???? BTW sio suala la usanii au kushangaaa kwa jinsi teknologia inavyoendelea hii inawezekana kabisa, hujawahi kusikia nchi iliyosogeza magorofa kilomita kadhaa???????

Wee Kandambili,

Comedown. Kama ungelifikiri mara mbili ungelijua nilikuwa ninamaana gani. Hapa nilikuwa nalinganisha SIASA za Lowassa za kufanya mambo bila maandalizi mazuri (Msingi). Kafungua mashule kibao ya secondary bila kuandaa waalimu na vitendea kazi kwenye shule hizo. Matokeo shule nzima ya secondary ina mwalimu mmoja au wawili. Huo ni mfano mmoja tu.

Juu ya kusogeza majengo nalifahamu hilo. Pembeni mwa Sony Center, Potsdamer Platz, Berlin's kuna ki-CAFE kimoja kimeunganishwa na hilo Center. Part ya hilo jengo ni jengo la zamani na part wameifanyia matengenezo na kuna picha ya sehemu hiyo ilivyokuwa zamani. Hilo ni mfano wa majengo ambayo yalisogezwa kutoka yalipokuwa mwanzo.
Sijui kama hii kitu umeiona au unasikia tu. Kusogeza ghorofa kwanza inategemea na urefu. Kighorofa kifupi au jengo la kawaida ni rahisi ila jengo refu si rahisi. Hapa nina maaanisha jengo refu Height and length kwani kuna kesi ya uzito, na kuna kesi ya kulisafirisha jengo bila kuharibu structure bonds (internal) ya jengo hilo. Hivyo hii kitu huhitaji uchimbe, uweke msingi imara sana wa reli, utandike reli chini ya jengo, ulinyenyue jengo lote na kuliweka kwenye tray na hiyo tray iwe chini ya reli na ndipo safari ianze....... Sijui kama unaona gharama za muda, umeme na very expensive machines za kufanya kitu hiki. USA wanajenga nyumba zao kwa mbao na inakuwa rahisi kulibeba jengo zimazima kwani ni light structures na ni flexible kwenye joints zake.

Ujenzi wa Wachina ni wa kizembe zembe. Majengo mengi imara kwa sasa wanashirikiana na Wahandisi wa kutoka kona zote duniani. Wakifanya wao ndiyo inakuwa kama kwenye hilo ghorofa lililoanguka au hiyo picha kaweka Invisible. Kwenye ghorofa ukiangalia sana ule udongo, kama sikosei utakuwa ni SILT/CLAY. Udongo huo kama wee umesoma Soil Mechanics, ukishapata maji inafahamika huwa unaweza kufanya maajabu gani. Kwa kuangalia ubichi wa udongo, nafikiri huo ndiyo ulilisukuma jengo na jengo likaenda zimazima.

BTW: Inasemekana jengo limeanguka na ndani ni zima kabisaa. Ni kama mtu alilinyenyua na kulilaza. Hapa wadau wanasema "hongera nyingi kwa wajenzi na Structure Engineers" waliofanya kazi kwenye jengo hilo. Mtu pekee aliyechezea kazi ni Mhandisi aliyedesign hizo Piles Foundations kwani ndiye alifanya uzembe au kama si yeye basi ni watu waliofanya Soil Analysis na kutoa Wrong data juu ya udongo wa hapo.
 
Mkuu;
Tuslaumu wachina, je vijana wa kitanzania ukiwapa kazi watafanya kweli?.Lazima tujiulize kwanza, je vijana tuna nidhamu ya kazi?.Make katika sehemu ya kazi nilizopitia nimekuwa na vijana wengi sana, lakini kufika kazini ni saa tatu au saa nne eti shida ya usafiri.Nimekuwa sehemu nyingi nimeona haya mambo.
Watoto wa kike ndo usiseme kabisa anafika saa tatu na anataka aondoke saa nane kurudi nyumbani

Rombwene,

Hapa naona umechanganya somo. Hapa wakulaumiwa ni Maboss tu na Wahandisi kwa ujumla walioshughulika na msingi wa jengo. Hapa kosa si kuchelewa kazini au kuwahi. Wangeweza kufika hata saa sita mchana kazini ila kama wangelijenga msingi imara (zaidi soma ujumbe wangu wa juu) basi hili ghorofa lisingelianguka.

Juu ya Watz nikuambie ukweli. Watanzania wanapenda sana ku-try. Ukiwabana hasahasa watawahi, amini usiamini. Akikudanganya mara ya kwanza ukakubali basi ataendelea siku zote.

Nilishawahi kuona wafanyakazi wa Interchick pale Dar walikuwa wameambiwa kuwa ikifika saa mbili asubuni hujaingia getini, basi wee siku hiyo hukufuka kazini kabisaaa....... Mhhh, mie nilikuwa nafanya kazi pale kwa muda na ninaishi Ilala, ilikuwa kivumbi. Ilibidi niamke shehe akiita Salaa (saa 10:30 alfajiri). Mie na mshikaji tulioga, tukapata breackfast na kuondoka kwenda Kariakoo. Basi la kwanza kwenda Tegeta (Mbele kwa mbele kwenu Tegeta) ilikuwa lazima tuliwahi vinginevyo ni kuwa umechelewa. Amini usiamini tulikuwa tunawahi kila siku.

Watanzania nilishasema siku nyingi, si wavivu ila inabidi uwaSISITIZE wajibu wao kwa nguvu kidogo au vitisho.... Kama una kampuni, weka pale Boss mpya na aje na siasa ya kuandika mtu kafika kazini saa ngapi. Wataanza kuwahi wakiona wengine wameenda na maji.
 
Back
Top Bottom