Chochote kizuri nikimhusisha mama kinakufa

Chochote kizuri nikimhusisha mama kinakufa

KING MIDAS

JF-Expert Member
Joined
Dec 1, 2010
Posts
8,589
Reaction score
16,936
Namshukuru Mungu nimejenga nyumba na nilifanikiwa kwasababu niijenga kwa siri kubwa.

Chochote ninachofanya kizuri au cha kimaendeleo nikimjulisha tu mama kinakufa.

Iwe ni ajira, akinitembelea ofisini kama sijaachishwa kazi bila sababu basi kampuni itafilisika, ili mradi tu niharibikiwe.

Nikajizoazoa nikafungua mgahawa, alipokuja tu, kwa siku nikawa napata mteja mmoja au wawili au hawaji kabisa, nikashindwa ku run business kabisa hadi nikafunga.

Nilikima matikiti, yakaota vizuri sana, nikampeleka shamba kuona jitihada zangu, baada ya siku mbili tu, matikiti yote yakaibwa shambani usiku na hawakuacha hata moja.

Hajawahi kumpenda mtoto wangu hata mmoja, wala mzazi mwenzangu yoyote.

Mimi ni mzaliwa wake wa pili, licha ya kwamba kwa baba yangu ni mzaliwa wa kwanza.

Huyo kaka yangu ni teja, lakini ndio kipenzi chake, kazaliwa mwaka 1976 lakini hadi leo anakaa kwa mama, watoto wake wanasomeshwa shule nzuri.
 
Mwanangu nataka nikwambie Kuna mtu kakutumia Kimavi mama yako kupitia mama yako Mimi Kuna Mbwa mmoja Tena mama yangu mkubwa dada yake kabisa na mama yangu alitaka kufanya ujinga huo Yani Kila akija kunifanyia uchawi namnasa ila anakuwa kaongozana. A mama yangu nawafokea mbaya

Baadae nikaanAza is mama anausika uwezi amini nilimwita mama nikamchana akalia sana nikaamini hajui lolote ila dada yake ni mwanga kweli ila hakuamini kama dada yake ananiloga Sasa changamoto mama mkubwa anaenda kwa ndugu anasema anaona Mimi kama nimerogwa hao ndugu wanachama kama karogwa nenda kamlague weee SI mama yake mkubwa anakaa kimnya.

Yote kwa yote mwamba uchawi upo na watu wanatumia picha na kvuri Cha mama yako maana ni very simpo

Kwa mambo zaidi namwalika ndugu Mshana Jr aje amwage undezi hapa.
 
Pole sana ! Omba kwa ajili ya vita iliyopo ndani yenu kupitia mama Yako mzazi ! Mungu akuongoze zaidi ...akupe maarifa na hekima zaidi jinsi ya kuamuaa na kuhakikisha usimukwaze mama !! AU AKIJA SEHEMU YOYOTE SEMA MANENO HAYA KIMOYO MOYO "Mungu najua wewe unawajua wazuri wangu na wabaya wangu,Na vunja roho ya uharibifu kwa kile chocolate nilichokianzisha kwa jina la Yesu kristo Amen" .... Mkaribishe kwa Tabasamu lote ila Imani iweke kwa Muumba wako !!
 
Hakuna chenye na thamani kama mama, lakini katika hali ya kawaida na isiyo ya kawaida mambo kama haya hutokea ili kuondoa ile thamani ya mama maishani wetu, hio nguvu hasi ilio ndani ya mama dhidi yako unaweza kuiondoa kwa kiroho zaidi kwa kuwaona wale wahusika wa mambo hayo kwa jinsi unavyo amini.

Pole na Mwenyezi Mungu awape heri njema.
 
Mwanangu nataka nikwambie Kuna mtu kakutumia Kimavi mama yako kupitia mama yako Mimi Kuna Mbwa mmoja Tena mama yangu mkubwa dada yake kabisa na mama yangu alitaka kufanya ujinga huo Yani Kila akija kunifanyia uchawi namnasa ila anakuwa kaongozana. A mama yangu nawafokea mbaya

Baadae nikaanAza is mama anausika uwezi amini nilimwita mama nikamchana akalia sana nikaamini hajui lolote ila dada yake ni mwanga kweli ila hakuamini kama dada yake ananiloga Sasa changamoto mama mkubwa anaenda kwa ndugu anasema anaona Mimi kama nimerogwa hao ndugu wanachama kama karogwa nenda kamlague weee SI mama yake mkubwa anakaa kimnya.

Yote kwa yote mwamba uchawi upo na watu wanatumia picha na kvuri Cha mama yako maana ni very simpo

Kwa mambo zaidi namwalika ndugu Mshana Jr aje amwage undezi hapa.
Akija Mshana Jr nitag
 
Namshukuru Mungu nimejenga nyumba na nilifanikiwa kwasababu niijenga kwa siri kubwa.

Chochote ninachofanya kizuri au cha kimaendeleo nikimjulisha tu mama kinakufa.

Iwe ni ajira, akinitembelea ofisini kama sijaachishwa kazi bila sababu basi kampuni itafilisika, ili mradi tu niharibikiwe.

Nikajizoazoa nikafungua mgahawa, alipokuja tu, kwa siku nikawa napata mteja mmoja au wawili au hawaji kabisa, nikashindwa ku run business kabisa hadi nikafunga.

Nilikima matikiti, yakaota vizuri sana, nikampeleka shamba kuona jitihada zangu, baada ya siku mbili tu, matikiti yote yakaibwa shambani usiku na hawakuacha hata moja.

Hajawahi kumpenda mtoto wangu hata mmoja, wala mzazi mwenzangu yoyote.

Mimi ni mzaliwa wake wa pili, licha ya kwaamba kwa baba yangu ni mzaliwa wa kwanza.

Huyo kaka yangu ni teja, lakini ndio kipenzi chake, kazaliwa mwaka 1976 lakini hadi leo anakaa kwa mama, watoto wake wanasomeshwa shule nzuri.
Angalia kijana! Tumia akili na maarifa mengi aliyekujalia muumba wako. Umeshaona hvyo mara kadhaa usiendelee kumshirikisha kwenye mambo yako muhimu.

Na nakuambia usimuamini kabisa, ila mpe heshima kama mama, msaidie kama mama, sali sana,jenga ushirika wa karibu na muumba wako katika kila unalofanya.

NB: Usimuamini yoyote kwenye maisha yako. Ila ishi na watu vizuri
 
Back
Top Bottom