watu wengi wana matatizo ya meno, wa tz tuna tabia ya kupiga mswaki asubuhi kabla ya breakfast halafu baasi mpaka kesho tena. tabia mbaya sana hii!
matokeo yake tunaondoka asubuhi na vinywa vichafu, tunashinda kutwa nzima na vinywa vichafu, tunalala na vinywa vichafu....tunalala na mabaki ya ugali, nyama choma, pombe etc mdomoni usiku mzima tukiamka asubuhi si harufu hiyo ..bakteria tayari wamesha fanya kazi yao....
meno inatakiwa yasafishwe kwanza usiku kabla ya kulala ili ukiamka unasukutua tu unapata chai halafu unaingia bafuni tena unapiga mswaki vizuri unaondoka home na kinywa safi kabisa.