Chombezo: Bao tatu za mgeni!

Chombezo: Bao tatu za mgeni!

Lukas atakuwa anaugua tezi dume au yupo HIV positive huko mjini.
 
8yi
Chombezo………….BAO TATU ZA MGENI!

Sehemu ya 3[emoji1665]

Nilishafanya mitihani mingi hasa ya shule nikamaliza,sikujua kama ntakuja kukutana na mtihani mwingine kama huu!
Nilijiuliza nitawezaje kulala chumba kimoja na binti mrembo kaa yule nma nisiwaze kumgusa!
Baada ya kumwambia vile kuwa nimeambiwa nilale naye mle ndani,yule binti alinikaribisha ndani huku akionyesha kutokuwa na wasiwasi wowote jambo lililozidi kunitia wasiwasiw!
Yule binti alitandika chini kisha akataka mi nilale kwenye kile kitanda cha chuma chenye kigodoro cha pamba!
“Hapana wewe lala hapo juu mi ntalala chini!”
“hapana kaka wewe lala kitandani tu,wewe ni mgeni!”
Tulibishana sana ila sikukubali kulala kitandani,mwisho yule binti ambaye nilisikia yule mzee anamuita Regina akakubali kulala kitandani!
Nililala pale chini baridi lilikuwa kali kiasi cha kushawishi kumkumbatia yule dada tupeane joto!Ila nilipowaza kauli ya yule mzee kuwa nisifanye naye chochote nilituliza nyege zangu!
“Huku kutafutana ubaya tu,huyu mzee ananitafutia sababu tu aniroge anipeleke Gamboshi huyu!Anawezaje kumlaza Simba kwenye banda la swala?Ila hanipati kudadeki!”
Nilijisemea japo hisia zilikuwa kali,shetani alikuwa kazini anafanya kazi yake,usingizi ulikuwa mgumu sana siku ile!

Sijui nililala sangapi nilikuja kushtuka asubuhi jogoo anawika,nilifumbua macho nikaangalia kitandani sikumuona yule binti,nikajua tu alishaamka zamani,mabinti wa kijijini huamka mapema siyo kama wale wa mjini wanaokesha whatsap na insta!
Nilikurupuka nikajinyoosha,kwa mbali nilihisi mbavu zinauma sababu ya kulala chini,ila nilishukuru sababu nililala ndani kuliko kulala nje,halafu sehemu yenyewe ni Sumbawanga sasa!
Nilitoka nje nikamkuta yule mzee amewasha moto halafu amekaa pembeni yake,nilisogea pale sababu kulikuwa na baridi sana!
Nilichukua kigoda nikakaa pembeni ya yule mzee ambaye niligundua kwenye ule moto alikuwa anachoma viazi vitamu!
“Karibu kijana!”
“Ahsante sana shkamoo mzee wangu!”
“Marahaba kijana!”
Bado nilikuwa sijiamini amini,nilikuwa nawaza itakuwaje yule mzee akisema nimefanaya mapenzi na binti yake?
Ukimya ulitawala kati yetu muda huo yule mzee akatoa kiazi kimoja kwenye ule moto akanipatia!
Nilikipokea nikakiweka chini maana kilikuwa cha moto hatari,sijui hata yule mzee aliwezaje kukishika!
Muda huo yule binti alikuja akiwa amebeba maji,nikajua tu anatoka kisimani,nilipata muda sasa wa kumuona vizuri mrembo yule!
Dah!nilijisifu sana kuushinda mtihani ule,moyoni nilikiri nimekuwa sasa maana siyo kwa mtihani ule duh!
Nilipogeuza shingo kumuangalia yule mzee,nilikuta ananiangalia nikainama chini kwa aibu maana kaniona nilivyokuwa namtathimini binti yake!
“Hahahahahahah kijana!”
Alicheka yule mzee nisijue anacheka nini?nilikuwa mtu wa mashaka mashaka tu bado sikujiamini kabisa!
“Hongera kijana wewe ni mwanaume,uanaume siyo kufungua zipu tu hata ukijifunza kuifunga ni uanaume tena uanaume wa kweli!”
“Unamaanisha nini mzee wangu?”
“Namaanisha usiwe kama mbwa kila mgeni unambwekea tu ukiamni ni mtu mbaya!unaonekana utakuwa mgeni wa tofauti kuliko wageni wengine,kwa ajili yako naweza kuwaza kukishauri kijiji changu kianze kupokea wageni tena!”
“Wageni!!!!”
Niliuliza kwa mshangao cha ajabu yule mzee akaondoka zake huku anacheka,nilianza kuwaza namna nilivyopokelewa na wanakijiji wa pale,nilipounganisha na maneno ya yule mzee nilishindwa kuelewa,nikabaki na maswali mengi kichwani!
“WAGENI WANA NINI KWENYE HIKI KIJIJI?”
Licha ya kilichonileta nilitamani pia nifanye uchunguzi nijue kuna siri gani ya kile kijiji na wageni!
Yule binti alimaliza kuchota maji akachemsha uji na viazi tukanywa,muda ule yule mzee hakuwepo,alikuwa ameshaondoka zake!
Nilianza utafiti wangu kwa ajili ya kitabu changu kwa kumuuliza mambo mbali mbali yule binti ambaye alinipa ushirikiano wa kutosha kabisa!
Baada ya kumuuliza maswali yangu karibu yote ndipo nikaamua kumuuliza hili duku duku langu kuhusu wageni!
“Hivi Regina!”
“Rabeka!”
“Kuna kitu nataka nikuulize!”
“Kitu gani kaka halafu hujaniambia unaitwa nani?”
“Naitwa Jack Mambo!”
“Mmh aya unataka uniulize nini?”
“Oooh!nataka kujua kuna nini kwenye hiki kijiji mpaka wageni hawapokelewi vizuri?”
Swali lile lilimfanya Regina ainame chini na uso wake ukabadilika,ghafla akainuka akaacha kula na kuondoka!
Nilibaki njia panda yule mzee kasikia wageni kainuka akaondoka,Regina naye hataki kusema chochote,kuna nini katika kijiji hiki?wageni walikosea wapi?
JE NINI WAGENI WALIKOSEA WAPI HAPA KIJIJINI?USIKOSEEE
88v z@v h,
 
Chombezo………….BAO TATU ZA MGENI!
Mtunzi……………….Jack Mambo
Whtsp………………..0752761388
Call…………………….0716352102
Umri…………………..18+

Sehemu ya 51

Shauku ilikuwa kubwa sana kwa wanakijiji,kuna waliobakiwa wake zao pia binti zao!kijiji kilikuwa na hasira sana!
Mzee Mtata alisimama kabla hajamleta hadharani alitaka kutoa onyo kwa wanakijiji wale ambo walionyesha hasira za waziwazi!
“Jamani mnataka nimtoee?”
“Ndiyooooo!”,waliitikia kwa pamoja!
“Mnata mumuone mchumba wenuuuu?”,alitania lakini hapo wanakijiji walikaa kimya!
“Hahahahahhaha!natania jamani!sasa nisikilizeni namtoa hadharani anayesumbua kijiji hiki,lakini chonde msimguse wala kumpiga,atakayemgusa ajue atakuwa anatembelewa kila siku na huyu mgeni awe mwanaume au mwanamke!”
Mzee Mtata ilibidi awatishe maana walikuwa na hasira za wazi wazi kabisa,baada ya kusikia vile wanakijiji waliogopa sana!
“Jamani tumeelewanaaaa!”
“Ndiyooooo!”
“Hamtamgusaaaaa?”
“Ndiyooooo!”
“Shauri yake atakayemgusa sitamtibia!”
Baada ya kutoa vitisho Mzee Mtata alichora duara kubwa kwa majivu kisha akaweka dawa zake akachukua kibuyu chake akaweka maji mdomoni na kuanza kuyapuliza juu!
Alipomaliza alianza kuuita ule mzimu ambao ghafla ulitokea kwenye lile duara huku unatetemeka na kuzunguka ndani ya ile duara!
Wanakijiji walipigwa na butwaa,kilikuwa kiumbe kinachotisha sana,wanawake waliokuwa wamehisi kufanya mapenzi na kile kiumbe walipatwa kichefuchefu wengine hadi wakatapika!
“Mmemuona eeh,ndiyo huyuuu!sasa namrudisha alipotoka hamtamuona tena kijijini,mimi ndiyo mzee Mtataaa!”,alisema huku anajipiga kifuani!
“OYOOOOOOOOOHH!”,wanakijiji walipiga kelele kumshangilia mzee huyu waliyemuona kama mkombozi wao,bila kujua kuwa ndiye mkandarasi wa kila kitu!
Lukas pekee ndiye alikuwa anaujua mchezo ule,alijua ni maigizo tu hakuna chochote pale,pembeni yake alikuwa na Selina
Alimshika mkono Selina akatoka naye pembeni,Selina alimshangaa Lukas kwa kumtoa pale uwanjani!
“Unanipeleka wapi?”,alihoji Selina!
“Nyumbani!”
Hakuwa na jinsi binti yule waliondoka mpaka nyumbani,moja kwa moja akaingia naye kwenye kijumba chake,Selina ilikuwa ni mara yake ya kwanza kuingia mle ndani!
Lukas hakuwa na subira alianza kumpapasa Selina ambaye si muda alilegea na muda mfupi baadaye wakawa watupu tayari kwa kuvunja chaga!
********

Huku kwa mzee Mtata alifanya manyanga yake na mwisho akaufanya ule mzimu ukapotea mbele za macho ya watu!
Ni yeye pekee alijua ulipoenda,wanakijiji walimshangilia na kumpa zawadi mbali mbali huku viongozi wakimkabidhi ng’ombe zake kumi pamoja na mbuzi wake watano!
Ilikuwa ni sherehe kubwa kumuondoa aliyewanyima amani kijijini,waliamini sasa watalala kwa amani!
Mzee Mtata alipomaliza kazi yake aliondoka na kurejea kwake,wake zake walimpokea kishujaa na kumsifia kwa kufanikiwa kuudhibiti mzimu!
Mzee Mtata hakuwa na hofu na ngvu zake kupungua,alijua kila kitu kiko sawa bila kujua dawa yake ambayo iebeba nusu ya nguvu zake imetupwa,na kadri anacvyotumia nguvu alizonanzo sasa zinazidi kupungua!
*********
Lukas na Selina walienda mzunguko mmoja tu wakatulia,hawakuwa na muda sababu muda wowote ule wengine wangerudi kutoka uwanjani!
“Selina mi nataka kuondoka hapa kijijini!”
Kauli ya Lukas ilimshtua sana Selina ambaye alijikuta anaacha kuvaa nguo zake kwanza amsikilize!
“Unasema!!!!?”
“Naondoka!”
“Unaenda wapi?”
“Narudi zangu mjini
“Lukasiiiii!”
Selina aliachia alichokuwa kakishika mikono akaitupia kichwani akiwa haamini alichokisika,alikaa kitandani machozi yalikuwa yanamtoka!
“Sasa unaniacha na nani jamani?”
“Naondoka na wewe!”
“Lukasiiiiiii!”
Alishtuka Selina hakujua Lukas anaondoka naye kivipi?na wataondokaje na nani atawaruhusu?kichwani yalipita maswali mengi!
“Hutaki?”
“Siyo sitaki Lukas,tunaondokaje na nani ataturuhusu!”
“Hatuhitaji ruhusa ya mtu!”
“Lukasiiiii!unamaanisha tutoroke?”
JE NINI KITAENDELEA?SELINA ATAKUBALI ?NA VIPI MZIMU UMEONDOKA?

Chombezo………….BAO TATU ZA MGENI!
Mtunzi……………….Jack Mambo
Whtsp………………..0752761388
Call…………………….0716352102
Umri…………………..18+

Sehemu ya 52

Kila mzazi ana kipenzi chake kati ya wanae wote,atawapenda wote lakini yupo mmoja mzani utaelemea kwake!
Mzee Jomo alikuwa na mapenzi mazito juu ya binti yake wa mwisho ambaye ni Selina,na Lukas naye kajikuta kafanya mapenzi na familia nzima ila kwa Selina ndipo kaweka kituo!patamu hapo!
Selina ilimuwia ngumu kukubaliana na maneno ya Lukas,hakutaka kuamini kwamba ni yeye anataka kutoroka na mwanaume!
“Lukas mi siwezi!”
“Selina utaishi kijijini mpaka lini?mi mjini nina maisha mazuri,utakuwa mkewangu acha huku unanishea na dada yako Suzy!”
“Lukas mi naogopaaa!”,alisema Selina huku akilia!
“Usilie Selina mi nimekupenda na niko tayari kufanya kila kitu kwa ajili yako,tafadhali naomba ukubali kuondoka na mimi!”
Baada ya kubembeleza sana mwisho alikubali kishingo upande kuondoka na Lukas mjini,Lukas alifurahi sana akamuahidi baada ya siku mbili kila kitu kingekuwa tayari!
Baada ya kuachana na Selina alianza kufanya mpango wa nauli,hakuwa na njia nyingine zaidi ya kuuza ng’ombe za mzee Jomo!
Alitafuta mteja wa ng’ombe akampata dalali ambaye alimpa dili,kesho yake akiwa machungani dalali alikuja na mteja akawauzia ng’ombe wawili wakubwa ambao thamani yao ilikuwa zaidi hata ya milioni,lakini aliuza kwa laki tano tu!
Ilikuwa ni ngumu kujua ng’ombe wamepungua sababu zilikuwa ni nyingi sana,akawa tayari amepata nauli ya kwenda mjini!
Baada ya kuirudisha mifugo nyumbani alipumzika akapewa chakula akawa anakula,wakati anakula alishangaa kumuona mzee Jomo anakuja na begi lake!
Alipatwa na mshangao mkubwa sana akashindwa hata kula kabisa,hofu na wasiwasi vilimtawala!
“Babaaaaaaaaa!”,wanae walimpokea kwa furaha kubawa!
Mzee Jomo akaingia nyumbani kwake,akiamini kila kitu kiko sawaa hakujua alimkabidhi fisi bucha,na fisi kaitumia vizuri nafasi ile!
“Lukas!”,alimuita Lukas!
“Naam mzee shikamoo pole na safari!”
“Marahaba!vipi umeenda machungani?”
“Ndo nimefika si muda mrefu napoza njaa hapa karibu!”
“Safi sana!”
Mzee Jomo aliingia ndani na kumuacha Lukas anakula,kwa upande wake Lukas alikuwa na hofu kubwa sana!
Mambo aliyoyafanya yalimfanya ajishtukia na kushindwa kabisa kumtazama mzee Jomo machoni!
Wanasema mwizi akimuona askari huwa anajistukia hata kama askari ana mambo yake tu,anaweza kujikuta anakimbia tu!
Alipopata tu upenyo wa kuongea na Selina alimvutia pembeni akamuambia suala la kuondoka!
“Tunaondoka kesho!”
“Lukas!huoni ni hatari baba karudi!”
“Hatuwezi vuruga ratiba yetu!”
“Lukas tusubiri baba aondoke!”
“Hatuna muda kama huondoki sawa mi kesho hutoniona,kama unaondoka ujue unaamka usiku saa tisa utanikuta nakusubiri!”
Lukas aliondoka na kumuacha Selina kasimama akiwa njia panda,hakujua afanyaje?abaki na ndugu zake au akubali kuondoka na mgeni huyu ambaye ndiye aliyemuingiza kwenye ulimwengu wa mapenzi!

Familia ya mzee Jomo ilikuwa na furaha sana siku ile,kawaida akirudi na zawadi kibao kutoka mjini,aliwapa zawadi zao wakafurahi sana!
Hakumsahau Lukas,alimletea suruali na shati jipya kabisa,hakujua kuwa anayemthamini katembea na familia nzima na kama haitoshi anataka kutoroka na mwanaye kipenzi Selina!
Usiku uliingia wakatawanyika Lukas akaingia kwenye makazi yake,alikuwa na mawazo sana kuhusu Selina!
“Itakuwaje hasipotoka,dah ila itabidi niondoke niliyoyafanya hapa yanatisha,huyu mzee ataniua!”
Usingizi ulimchukua akalala,lakini alikuja kushtuka akipapaswa usiku wa manane,alipoamka alimkuta Zahara ndiyo kamvamia usiku ule!
“Wewe unafanya nini?”,aliuliza Lukas kwa mshangao!
“Unajua nachotaka Lukas acha kujichetua,unataka Zubeda akufaidi peke yake,hujanipa siku nyingi nimeijia utamu wangu!”
“Zahara mi leo sijiskii utakuja kesho!”
“Yani kati ya vitu sitaki kuviskia ni huo upuuzi wako,ukitaka niondoke nipe hutaki nalala hapa Zubeda anikute mpaka asubuhi!”
“We unamuwaza Zubeda tu hujui kwamba mzee Jomo karudi”
“Afadhali tena akiona huyo atanipeleka kwa baba halafu baba atanileta unioe!”
“Unasemaje?”
Lukas alijua kabisa Zahara atamharibia mipango yake ya kuondoka!
JE LUKAS ATAFANYA NINI?ATAFANIKIWA KUONDOKA?

Chombezo………….BAO TATU ZA MGENI!
Mtunzi……………….Jack Mambo
Whtsp………………..0752761388
Call…………………….0716352102
Umri…………………..18+

Sehemu ya 53

Ulikuwa mtihani mkubwa sana kwa Lukas,kwake siku hiyo muda ulikuwa ni kitu muhimu kuliko vyote!
Zahara hakutaka kuelewa kabisa somo siku ile,alichotaka ni penzi la Lukas!licha ya kumkatalia sana lakini hakuelewa somo!
“Lukas we ongea vyote ila penzi utanipa ndiyo niondoke hapa!”
“Lakini nime…!”
Kabla hajamalizia kusema Zahara alimvamia na kuitoa bakora nje,Lukas hakuwa na namna,alichokifanya alimuacha Zahara afanye anachotaka!
“Zahara mi naumwa nakupa bao moja tu hapa kesho uje tutafanya vizuri!”
“Hayo ndiyo mambo sasa siyo nitoke usiku wote huu nirudi bila bao,huo ni ushamba!”
Lukas aliamua kufanya mapenzi na Zahara ili aondoke,alichokifanya ni kutumia staili zilizomchosha haraka Zahara!
Baada ya Zahara kuvunja dafu tatu tu alianza kuomba po!Lukas alipomaliza bao moja tu Zahara akavaa nguo zake!
“Nitarudi kesho umalizie bao zangu!”
Lukas hakuongea neno alimuacha Zahara akiondoka zake,aliona haukuwa muda wa kulala tena,alivaa zile nguo mpya alizoletewa na Mzee Jomo tayari kwa safari!
Kabla hata hajatoka nje alisikia sauti inamuita nje akajua pengine ni Zahara amerudi tena,akaisikiliza tena kwa makini!
“Lukas!Lukaas!”
Hakuamini alipotoka na kumkuta kipenzi chake Selina,ilikuwa bado kidogo tu amfumanie ila bahati ilikuwa upande wake,ni kama shetani alimlinda siku zote.
Kwa furaha ya kumuona Selina alimkumbatia kwa nguvu sana,hakuamini kama kweli Selina ameamua kuacha familia yake na kuongozana naye mjini!
“Selina siamini!”
“Nakupenda Lukas nimekubali kuiacha famili yangu sababu yako!”
“Naahidi nitakupenda daima mpenzi wangu!”
“Tuondoke Lukas baba huwa anatoka nje usiku!”
Hawakuwa na cha kubeba hata Selina alitoka na nguo alizovaa tu,safari ilianza huku Selina akiongoza njia!
Bahati nzuri walipata gari lililokuwa linapeleka mahindi mjini,wakapanda na kuendelea na safari walifika mjini na siku hiyo hiyo wakapata basi la alfajiri la kwenda Dar!
MGENI AKAWA KAONDOKA KIJIJINI!!
********
Mzee Mtata mambo yalikuwa si mambo tena,baada ya kufanikiwa kuwaaaminisha wanakijiji kuwa ameurudisha ule mzimu ulikotoka,alianza kuona mambo yanamwendea kombo!
Ile dawa yake ambayo mkewe mkubwa aliitupa ilimletea matatizo,sababu ilikuwa ni moja ya nguvu yake kubwa ya uchawi!
Ilikuwa inailinda misukule yake na pia iliwafanya hata maadui zake waogope kuingia kwenye ngome yake!
Kumbe siku ile baada ya kuutoa ule mzimu mbele za watu aliupeleka kilingeni kwake akiamini usiku unaofuata ataurudisha kaburini!
Kweli usiku uliingia mzee Mtata akafunga safari mpaka makaburini akafanya manyanga yake kaburi likafunguka na jeneza likatoka kama kawaida!
Tatizo likaja kwenye ule mzimu,aliuita uje lakini haukutokea,hali ile ilimchanganya sana Mzee Mtata!
Alijaribu mara kadhaa lakini hali bado ilikuwa ileile,mzimu haukutokea kabisa alipotaka kulirudisha lile kaburi kwenye hali yake liligoma pia kujifunga!
Mtata alichanganyikiwa kabisa kijasho kilimtoka,kila alichokifanya kaburi lilimzomea tu,muda ulizidi kwenda mpaka kukakaribia kukucha!
Hakuwa na namna alirudi nyumbani kwake na kuliacha kaburi lile wazi,moja kwa moja aliingia kilingeni alipongalia kwenye misukule yake aliuona ule mzimu umekaa umetulia hauna habari!
Aliuangalia kwan hasira lakini hakuwa na cha kuufanya maana ule ni mzimu siyo msukule wake!Alitoka nje kwa hasira akaanza kujiuliza imekuwaje hali ile inatokea?
Baada ya kuwaza sana aliingia ndani kwa mkewe mkubwa akachukua jembe Chiku akabaki kumshangaa!
“Mume wangu wapi na majembe usiku?”
Chiku hakujibiwa kitu,Mtata alitoka moja kwa moja mpaka alipofukia dawa yake ambayo ndiyo inabeba asilimia nyingi ya uchawi wake!
Alifika akachimba lakini kwa jinsi alivyokuwa anachimba aligundua mahari pale pamefukuliwa siku si nyingi,ardhi yake ilikuwa rahisi sana kuchimbika!
Alijipa moyo akaendelea kuchimba lakini hakuona kitu,hakutaka kuamini kuwa dawa yake haipo alichimba shimo refu sana lakini hakuona kitu!
Mtata alichanganyikiwa kabisa hakuamini kama dawa yake haipo,ile peke yake ndiyo ingemuwezesha kuurudisha mzimu kaburini!
Alijiuliza pengine labda alikosea sehemu siyo ile,kila akivuta hisia akili inamrudisha pale pale!
“Hapana ni hapa hapa,sasa imeenda wapi?oooh Maskini ntaadhilika hapa kijijini!”
Mzee mtata alirudi kilingeni akiwa na mawazo,usingizi haukuja alitamani kukuche awaite wake zake na kuwahoji juu ya wapi dawa yake ilipo!
Alikuwa na wasiwasi sana na mkewe mkubwa Chiku,sababu ndiyo msiri wake mkubwa na ndiye peke yake anayejua siri ya dawa ile ya mzee Mtata!
JE NINI KITAENDELEA?MZEE MTATA ATAFANYAJE AKIJUA CHIKU AMEITUPA ILE DAWA?


Chombezo………….BAO TATU ZA MGENI!
Mtunzi……………….Jack Mambo
Whtsp………………..0752761388
Call…………………….0716352102
Umri…………………..18+

Sehemu ya 54

Siku ile Mzee Mtata aliamka mapema akachukua kiti chake na kukaa nje karibu na jikoni kabisa akiwasubiri wake zake waamke!
Kwa alipokaa alikuwa anaona kila mlango wa nyumba za wake zake,katika hali ya kushangaza alimuona mkewe mdogo Vero akitoka mbio mbio ndani na kuanza kutapika kisha akarudi ndani bila kujua mumewe kamuona!
Hali ile ilimshangaza sana mzee Mtata kwa akili ya kikubwa alijua kabisa ile itakuwa mimba tu jambo ambalo hakutaka kuliamini sababu anajua kabisa hana uwezo wa kumpa mimba mwanamke yoyote duniani!
Akiwa kwenye hali ya kujiuliza alishangaa kuona mkewe mwingine ambaye ni Lolenza naye anatoka mbio akatapika na kurudi ndani!
“Hii ni nini?”,alijiuliza Mtata!
Hatimaye wake zake walitoka nje na kushangaa kumkuta mzee yule nje kakaa,mzee Mtata alimuita Chiku!
“Abee mumewangu”
“Naomba waite wenzako wote hapa nina kikao na nyinyi!”
“Sa..sawa mume wangu!”
Sauti ya Mtata ilimtia hofu sana Chiku,hakuongea kama kawaida alionekana ni mtu mwenye hasira sana!
Wake zake walikusanyika kwa pamoja wakakaa kumsikiliza ana nini cha kusema,alionekana amejaa sumu haswa!
“Nauliza hivi nani alichimba dawa yangu pale uwanjani,na aliipeleka wapi?”
Chiku alishtuka sana kusikia vile sababu ni yeye aliitupa ili wapate uhuru wa kufanya mapenzi na Lukas,sababu ile ilikuwa kama inampa machale mume wao!
“Chiku najua ni wewe peke yako unajua niliweka pale ile dawa nambie umeipeleka wapi?”
“Mi..mi…si..si..sjiui mume..!”
“Nyamazaaaa sitaki kusikia upumbavu hapa,nisubirini nije!”
Mzee mtata aliondoka akiwa na hasira akaingia kilingeni kwake,haikujulikana alifuata nini?Huku wake zake wakaanza kutupiana karata!
“Jamani mi simo,Chiku ndiyo uliitupa!”,alisema Vero!
“Hajitoi mtu hapa zilikuwa ni nyege zenu hakuna mtu kujitoa hapa!”,alisema Chiku!
Hakuna aliyejua Mzee Mtata kafuata nini ndani,walikaa kusubiri mpaka alipotoka alikuwa amebeba kinu!
“MUNGU WANGUU!”,Chiku alishtuka baada ya kuona kile kinu sababu alijua maana yake ni nini?
“Nini mbona unashtuka ni nini kwani?”
“Kinu cha kiapo kile tumekwishaaa!”
Mzee Mtata alirudi akiwa na kinu chake akakishusha chini,akamimina maji ndani ya kinu akachanganya na dawa kisha akaongea maneno yake!
Wakati anafanya yake alishangaa sana kumuona mkewe mwingine ambaye ni Tausi akiwa kashika ndimu analamaba muda wote!
Alimezea mate jambo lile akaendelea na jambo lake,alipomaliza kusema maneno yake alikaa huku chungu kikiwa katikati yao!
“Chiku nadhani unajua maana ya hiki kinu,kwa nyie wengine labda niwaambie tu kuwa hiki ni kinu cha kiapo,nitakuuliza kitu unatakiwa useme ukweli,ukitia mikono yako ndani ya hiki chungu kama umedanganya unakauka na kufa hapa hapa!”
“Nadhani mmenielewa,Vero simama ya juu!”
Mzee Mtata alimuamrisha mke wake mdogo asimame akafanya ivyo huku anatetemeka kwa hofu!
“Nadhani umenielewa ukweli wako ndiyo utakuweka hai aya nakuuliza je una mimba?”
Aliuliza swali ambalo lilikuwa nje kabisa na mada aliyokuwa ameianzisha,walibaki wameduwaa,hakuana aliyetegemea swali lile kabisa!
“Nijibu nina mambo mengi ya kufanya,una mimba!”
“Ndiyo!”
“Siyo mimba yangu si ndiyo?”
“Ni..ni…yako mume…!”
“Weka mikono humo usipoteze muda!”
Hapo ndipo palikuwa pagumu,Vero hakutaka kuweka mikono mzee Mtata akamuamsha mkewe Lolenza akasimama!
“Una mimba?”
“Ndiyo mume wangu”
“Kama ni yangu weka mikono kwenye kinu msiniletee mambo ya mzee Nyage na diamond hapa!”
Lole naye alishindwa kuweka mikono akaambiwa akae,akaamshwa Tausi naye alikuwa na mimba lakini hakutia mikono kwenye kinu!
Mpaka hapo ni wazi alijua kuwa wake zake wote wana mimba na siyo mimba zake,sababu hata yeye anajua hana uwezo wa kuzalisha!
Ilifika zamu ya Chiku ambaye aliulizwa swali tofauti na wenzake,Chiku alitetemeka kwan hofu!
“Nambie dawa yangu umeitupa wapi?kama hujaitupa tia mikono kwenye kinu!”
“Mume wangu na…nasema!”
“Ndiyo useme sasa!”
“Nili,,niliitupa!”
“Unasemaje wewe!!!”
ITAKUWAJE MZEE MTATA ATAFANYAJE?

Chombezo………….BAO TATU ZA MGENI!
Mtunzi……………….Jack Mambo
Whtsp………………..0752761388
Call…………………….0716352102
Umri…………………..18+

Sehemu ya 55

Mzee Mtata alihisi mapigo ya moyo wake yanaenda mbio sana,kijasho kilimtoka jazba na hasira zilimkaba!
“Umeitupia wapi!!!!?”
“Mtoni!”
“Hivi unajua umenimaliza?dah ivi iviiiii daaah!”
Mtata alikosa neno la kusema,alipatwa na kigugumizi,bora ingekuwa imetupwa hata vichakani angesema wakaitafute ila siyo mtoni!
Wake zake wote walikuwa wanamwaga machozi,lilikuwa ni jambo la aibu kwao kusimama mbele ya mume wake na kusema wana mimba lakini siyo zake!
“Kwanini uliitupa?ilikukera nini?”
Chiku hakusema kitu alilia kwa sauti mpaka kwikwi ikamshika,hakuweza kujibu swali la mumewe!
“Sema kabla sijakugeuza nyau hapaaa!’,alifoka akijua njia pekee ya kumpata mwanamke ni kumtia hofu!
“N..nananananasema babaanguaa nasema!”
Chiku kwa hofu alianza kueleza yote mwanzo mpaka mwisho jinsi ilivyokuwa hakuacha hata punje,na mwisho akamtaja Lukas!
“Lukasiiii!!!!”
Alisimama mzee Mtata akiwa haamini kabisa kama kijana aliyeamua kumtibu bure bila malipo na kumpa kinga dhidi ya uchawi wa aina yoyote ndiye aliyewajaza mimba wake zake!
Tiba ya Lukas ndiyo inamfanya saivi mzimu anamsumbua hataki kurudi kaburini,huku mkewe akiwa ametupa nguvu zake mtoni!
“Unamaanisha Lukas ndiyo kawapa mimba hawa !”
“Siyo hao tu na mimi pia nina mimba!”,alijibu Chiku!
“Niniiiiiiii!
Mtata alianguka presha ilipanda akapoteza fahamu na katika kuanguka kwake aliangukia kile kinu cha kiapo yale maji yakamwagikia miguuni,wake zake wakaanza kulaumiana!
“Unaona sasa tatizo umesema kila kitu!”
“Mlitaka nife acheni ujinga njooni tumbebe tumuingize ndani!’
Walimbeba mume wao wakamuingiza ndani akiwa hajitambui kabisa,hali ya mzee Mtata ilikuwa mbaya sana,kwa vile Chiku anajua baadhi ya amadawa akaanza kumtibia!tatizo alimwagikiwa na maji yale miguuni miguu yake ikapooza!

*********

Mzee Jomo aliamka akiwa hana hili wala lile ,alizunguka nyumba yake akapita zizini huku anapiga miluzi,mkononi kashika mswaki waake wa mti!
Alizunguka na kuridhika na mazingira ya nyumba yake,ndipo akafikiria kwenda kumuamsha Lukas maana alimuahidi kumfundisha baadhi ya madawa!
Taratibu akazipiga hatua zake mpaka kwenye kijumba ambacho Lukas amekuwa akiegesha mbavu zake tangu amkaribishe kijijini!
Alifika akagonga sana mlango akimuita Lukas lakini ukimya ulimpa mashaka sana,hakukuwa na muitikio ndipo akaamua kuingia ndani,alishangaa kukuta kitanda kikiwa kitupu!
“Huyu kijana kashakuwa mwenyeji sasa”
Alijisemea mzee Jomokisha akaendelea na mambo yake,hakuwa na wasiwasi aliaminikama ametoka basi hatokuwa mbali!
Suzy alishtuka baada ya kuamka na kumkosa Selina kitandani,kama kuna watu walikuwa wavivu kuamka mapema ni Selina,alijiuliza inakuwaje leo aamke mapema kiukweli alistaajabu sana!
Aliamua kupotezea akiamini pengine mdogo wake kaamua kubadilika,maana walishapiga kelele mpaka wakachoka!
Aliamka akamkuta baba yake nje akamsalimia kisha akaendelea na shughuli zake kama kawaida,ila kadri muda ulivyozidi kwenda ndivyo wasiwasi ulimjaa!

Mama Zubeda kama kawaida aliingia zizini kukamua maziwa,lakini kuna kitu kilimshangaza siku ile,alijisikia kichefuchefu sana akiwa anakamua maziwa hadi akatapika!
Ilibidi amuite Zubeda aje akamue yeye akashindwa kabisa kuendelea,hali ile ilimshangaza sana mzee Jomo ila akachukulia pengine ni homa za kawaida!
Selina ndiye alikuwa binti anayempenda kuliko mabinti zake wote,alimjua binti yake ni mvivu sana kuamka,hivyo alipoona mabinti zake wote wapo nje ila yeye hajaonekana akajua tu atakuwa amelala!
Alivumilia sana mwisho uvumilivu ukamshinda na muda ule hata Lukas naye alikuwa hajaonekana bado!
“Suzy ebhu kaniamshie huyo Selina analalaje mpaka saivi amekua sasa!”
Kauli ile ilimfanya Suzy aanze kuwaza upya ni wapi mdogo wake alipo,alimsogelea baba yake karibu!
“We sinimekwambia ukamwamshe mdogo wako?”
“Baba misijui hata nisemeje?”
“Usemeje ndiyonini?”
“Baba mimi nimeamka sijamkuta Selina kitandani?”
Mzee alisimama kichwa kilimzunguka,alijiuliza binti yake atakuwa ameenda wapi?Haraka akaiita familia yake yote!
“Nambieni Selina yuko wapi na kaanza lini hii tabia?”
“Mume wangu kwa kweli nayaona haya ni mageni kwa wengine naweza kukubali ila siyo kwa Selina hata mi sielewi!”
“Hayo siyo majibu nayotaka kusikia,nataka kusikia mnaniambia Selina alipo!”
“Baba labda kwa mgeni!”,Suzy alijikuta karopoka!
“Nini?umesema nini wewe?unamaanisha Lukas huyu au mwingine?”
Mzee Jomo kijasho kilimtoka akaanza kuunganisha matukio,Suzy alichafua hali ya hewa!

JE NINI KITAENDELEA?ZUBEDA ATAFANYAJE AKIGUNDUA LUKAS KAONDOKA NA MDOGO WAKE?


Chombezo………….BAO TATU ZA MGENI!
Mtunzi……………….Jack Mambo
Whtsp………………..0752761388
Call…………………….0716352102
Umri…………………..18+

Sehemu ya 56

Haliya hewa ilichafuka,Suzy aliyaibua yaliyojificha na kumfanya Mzee Jomo asimame akiwa amefura kwa hasira!
Suzy baada ya kuona daliliya kutokumuona mdogo wake alijua moja kwa moja atakuwa kwa Lukas,na ukizingatia kuwa jana yake aliwaona waliondoka uwanjani kabla hata shughuliya kuutoa mzimu haijaisha!
“Naomba uniambie kila kitu,unajua nini kuhusu Selina na Lukas?”
“Baba mi niliwafumania siku moja kwenye zizi wanafanya mambo ya ajabu,nikamkanya Selina akasema hatorudia lakini jana tulikuwa kwenye shughuli uwanjani kule,ila waliondoka kabla haijaisha,nikawafutailia wakaingia humo kwa Lukas!”
“Kwanini hukumwambia mamayako?”
“Baba nilitaka nikuambie asubuhi!”
“Baba Suzy muongo Lukas ni mchumba wangu,nilikuwa nakusubiri tu urudi nikuambie?”
“Paaaaa”
Mzee Jomo alishindwa kuvumilia alimtandika kofi zito Zubeda akaangukia pembeni akaanza kulia!
“Mama Zubedaaaa hivi ndivyo unavyolea mabinti zako?”
Mama Zubeda alikuwa analia na mengi,aliwaza mpaka hapo ameshea penzi na binti zake wawili Zubeda na Selina!
“Baba unanipiga bure tu Lukas ni mchumba wangu nampenda!”
“Nyamaza kenge wewe!”,alifoka mzee Jomo akaelekea kwenye kijumba cha Lukas akafanya ukaguzi akagundua Lukas katoka na kavaa nguo alizomletea jana!
Alitoka akiwa na hasira isiyoelezeka alizunguka kama chizi,Selina ni binti ambaye alikuja na neema mapema tu,mpaka hapo alikuwa anategemea mwanae ataolewa na tajiri mkubwa mjini,ambaye alishaonyesha nia ya kumtaka binti yake!
Walishaongea na kukubaliana kabisa ilikuwa mahari tu itoke japo hilo suala hakuwa amemshirikisha hata mkewe!
“Nawaambia kama Lukas kaondoka na Selina na nyie mnaondoka hapa!”
“Baba Zubeda kwani hayupo ndani!”
“Unauliza makofi polisi,watoto mpaka wanapelekwa mazizini eti wapo wanaishi na mama!”
Kilio cha mama Zubeda alilia akiwaza mpaka hapo ana mimba na Lukas kakimbia na mwanaye!
Mzee mtata alichukua baiskeli yake akawahi mpaka katikati ya kijiji huko akaiweka baiskeli kwa mtu akapata gari mpaka Sumbwanga mjini!
Aliangaza huku na kule lakinihakuambulia kitu ni wazi alikuwa amechelewa sana,mgeni kaondoka na mwenyeji wake,kamchukua kampeleka mjini!
Alichoka akatafuta sehemu akakaa kwanza akiwa hana hamu na Lukas,Lukas kampokonya dhahabu yake!
“Lukas nakuua,utakauka kama mti,utateketea kama mkaa,nitakufanya majivu!”,alisema kwa hasira mzee Jomo kisha akaanza safari ya kurudi kijijini!

Huku kila mtu alibaki ana sikitikia moyoni hakuna aliyekuwa nauwezo wakumwambia mwenzake,kila mtu alibaki na aibu yake!
Mama Zubeda alikuwa chumbani akiwaza mengi,kitendo cha kushea bakora na binti zake ilikuwa ni aibu kubwa sana kwake,kibaya zaidi Lukas hakumuacha hivi hivi kamuacha na ujauzito ambao anajua kabisa si wa mumewe!
“Lukas mbona hufananii na matendo yako,ivi kweli we ni wa kunichanganya na binti zangu!”,machozi yaliuosha uso wake siku ile!

Suzy licha ya kusema yale mbele ya baba yake kwa kuona wivu ila moyo ulimuuma sana,hasa alipogundua kuwa licha ya Lukas kufanya mapenzi na yeye na Selina pia alikuwa anatoka na Zubeda!
Aliumia kwa upande mwingine alitamani Selina angemshirikisha katika safari ile wakalifaidi wote penzi tamu la lukas!
“Lukas ivi wewe ni binadamu au mnyama?”,alijisemea akiwa haamini !

Kwa Zubeda yeye kilikuwa ni kilio tu kwa kwenda mbele,kati wanawake waliowahi kumpenda Lukas kupitiliza ni Zubeda,lakini ndiyo ivyo tena moyo Lukas ulikuwa kwa Selina!
Johari yeye hakuumia sana ila alikuwa anajicheka tu! Mpakawakati huo alikuwa hajui kabisa alilalaje na Lukas!
“Huyu kaka jamani au mchawi,yani nikamfuata nikavua nguo mwenyewe mmmmh!hapana hii siyo kawaida!”
Siku hiyo hakuna kazi iliyofanyika,hata chakula hakikulika kabisa,kila mtu alikuwa na majonzi yake!
Mifugo ililia zizini hakukuwa na mchungaji,kama walishindwa kujilisha wao wangewezaje kuwalisha wengine?
Mzee Jomo alirudi akiwa mpole tayari alijua kapoteza,alijuta kumkaribisha Lukas nyumbani kwake,kibaya zaidi hajui anaishi wapi?alimpokea kama msaada tu!
Aliikuta nyumba imekuwa kama imepatwa na msiba,tabasamu lilienda likizo kwa muda na haikujuikana litarudi lini!alitamani kujilaumu lakini hakuona alikosea wapi,anachoamini yeye alitenda wema kama binadamu wengine!
Akatamani kumlaumu mkewe lakini akakumbuka ile siku anampokea yule mgeni muharibifu mkewe alimzuia kabisa,yeye akalazimisha!
“Umeumia Lukas hii ni Sumbawanga,pole sana kijana!”

Siku ile ilipita kesho yake asubuhi na mapema mzee Jomo akapanda baiskeli mpaka kwa swahiba wake wa muda mrefu,naye si mwingine ni mzee Mtata!
Aliuamini uwezo wa Mzee Mtata alijua kwake ni jambo dogo sana,kiufupi alitaka kumfanyia Lukas michezo ya kiswahili ikibidi awe hata kipofu kabisa!
Alifika salama kwa Mzee Mtata lakini alichokutana nacho kilimkatisha tamaa,Mtata alikuwa hoi kitandani anaumwa hawezi kutembea!
“Mzee mwenzangu mbona kitandani?”,aliuliza mzee Jomo!
“Acha tu mzee mwenzangu,ninaumwa umwa ila niko sawa!”
“Kuna kazi nataka unifanyie utaweza kweli?”
“Kazi gani tena?”
Mzee Jomo hakumficha kitu alieleza kila kitu jinsi alivyompokea Lukas na mwisho kaondoka binti yake Selina!
“Umesema Lukas kaondoka na binti yako?”
“Ndiyo!”,mzee Mtata presha ilipanda ghafla hadi Mzee Jomo akashangaa!
“Mzee mwenzangu,mzee mwenzangu vipi tena?”
JE NINI KINAENDELEA?MZEE JOMO AKIJUA KUWA LUKAS KAWATIA MIMBA WAKE WA MGANGA WOTE ITAKUWAJE?

Chombezo………….BAO TATU ZA MGENI!
Mtunzi……………….Jack Mambo
Whtsp………………..0752761388
Call…………………….0716352102
Umri…………………..18+

Sehemu ya 57

Mzee Mtata hakuwa yule katili wa kuogopwa tena,alikuwa mdogo kama pilitoni,aliposikia jina la Lukas,hasira ilipanda na presha ikawa juu!
Machozi yalibisha hodi na hata kabla hajayaruhusu yalitoka kwa wingi,Mzee Jomo alimshangaa sana Mzee mwenzie,amemzoea ni mtu mwenye kiburi na majivuno,hakuwahi kufikiria kwamba kuna siku atatokwa na machozi mbele yake!
“Mzee mwenzangu nini tatizo!”
“Acha tu mzee mwenzangu!”
Bila kuficha kitu japo alijihisi aibu lakini aliamua kumueleza kila kitu mzee Jomo,jinsi alivyomkamata na kumleta kwake!Alieleza mengi sana kuhusu Lukas!
“Mzee Mtata kwa hiyo unamaanisha Lukas kawapa mimba wake zako wote?”
“Ndiyo!”
“Dah!hiki kitoto kumbe kishetani hivi!”
“Nakushauri mzee mwenzangu kaipime familia yako yote,yule kijana sidhani kama ametembea na binti zako wawili tu mpime hadi mkeo!”
“Mkewanguuu hapana hapo nakataaa!”
Mzee Mtata alimueleza jinsi mke wake alikuwa anakuja kwake akisema Lukas ni mdogo wake,kwahiyo ana wasiwasi pia na mkewe!
“Kama kamgusa mkewangu namuua namuua mende yule!”
“Humuwezi!”
“Unasema?”,aliuliza Mzee Joma kwa mshangao!
“Nasema humuwezi na hicho ndicho kinachoniuma mimi,yule kijana nilimuamini sana,kwa upendo niliokuwa nao kwake nilimpa kinga kali sana ambayo hata mimi nikitaka kumfanyia ubaya siwezi,muache tu!”
“Haiwezekeni nasema haiwezekani!”,aliondoka kwa hasira mzee Jomo na kumuacha Mtata anamuita bila mafanikio!

Alirudi kwake akachukua ndimu tatu akazikata kisha akachanaganya na madawa aliyoyajua yeye,alipomaliza aliita familia yake yote!
“Huyo mpuuzi kawatia mimba wake wa mzee Mtata wote,navyoongea na nyinyi hapa Mzee Mtata yuko hoi kitandani!”
“Siyo kweli baba siyo kweli Lukas wanamsi…!”
“Kimyaaa!mwanaizaya wewe!”
Zubeda alijaribu kumtetea Lukas lakini baba yake alimnyamazisha!
“Sasa nisikilizeni hapa,ninawapima mimba!”
Mama Zubeda alishtuka sana,kauli ya mume wake ilimfanya apate hofu kubwa sana,aliamua kujitetea mbele ya mume wake!
“Sasa baba Zubeda kwanini usiwapime watoto mimi mambo yao yananihusu nini?”
“Tena unyamaze Mtata kaniambia kila kitu!naomba mchukue ndimu hizo kila mtu alambe!”
Alisema lakini hakuna aliyeshika ndimu kila mtu alibaki kukodoa macho,mzee Jomo akasimama!
“Msinitanie kila mtu achukue ndimu hapo!”
Kwa hofu wote walichukua ndimu wakiwa wanatetemeka baada ya kulamba wakakaa kusubiri,ile ni dawa ambayo imechanganywa ili kama mtu ana mimba akilamba atahisi kichefuchefu na kutapika!
Johari ndiye alikuwa wa kwanza kutapika wote wakamshangaa,mzee Jomo alijiuliza ina maana na Johari ametembea na Lukas!
Wakati anajiuliza swali lile Suzy naye ngoma ikatiki akarudisha chenji wote wakashangaa ,maana yeye anasema aliwafumania Lukas na Selina!
“Wewe si ulisema umewafumania?”
Kabla hajajibu kitu alishangaa kumuona mkewe anarudisha chenji kumaanisha na yeye naye kitu kimetiki!
“Mamaaaaaaaaaaaaaaa!na wewe!”,binti zake waliuliza kwa mshangao!
Mzee Mtata aliingia ndani akatokana panga akasimama akiwaangalia,wote walikuwa wanatetemeka!
Ajabu Zubeda hakuwa na mimba alisubiliwa lakini hakukuwa na matokeo yoyote,jambo lile llimuuma sana akabaki kulia tu!
Mzee Jomo aliwauliza na wote walikiri kuwa mimba ni za Lukas,alitetemeka kwa hasira alihisi kujutia sana!
“LUKASIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIII!!!!”
Alipiga kelele kubwa akiwa haamini kama Lukas ndiye kanmfanyia unyama ule,akiwa katika sintofahamu ghafla alikuja mgeni akiwa ameongozana na binti yake!
Hakuwa mwingine alikuwa ni mama Zahara na Zahara,alipofika tu hakuuliza moja kwa moja akauliza!
“Yuko wapi huyo klidume aliyemtia mimba binti yangui?”
“Kuna nini?”,aliuliza Mzee Jomo!
“Kuna kijana anaishi hapa anaitwa Lukas kamtia mimba binti yangu!”
Kauli ile ilimfanya Zubeda aanguke na kupoteza fahamu,shughuli ikawa imeishia pale!Mzee Jomo hakuwa na namna japo moyoni alisema atamfanya kitu kibaya Lukas!
Siku ile ilipita lakini kesho yake asubuhi walipoamka hawakumkuta Zubeda ,alikuwa ameacha ujumbe kuwa anaenda mjini kumtafuta Lukas!
“Lukas!Lukas!Lukas!”,alilia Mzee Jomo familia yake iligawanyika,mpaka hapo kapoteza binti zake wawili!
JE NINI KITAENDELEA?


Chombezo………….BAO TATU ZA MGENI!
Mtunzi……………….Jack Mambo
Whtsp………………..0752761388
Call…………………….0716352102
Umri…………………..18+

Sehemu ya 58

Kijiji kiliingia gharika,ule mzimu uliokamatwa na Mzee Mtata na kuwahakikishia kuwa hautorudi,ulirudi kwa kasi sasa ukawa unabaka watu mpaka mchana!
Mzimu ule ulikuja na nguvu kubwa sana,safari hii hii ulikuwa unabaka na kupotea,wanakijiji waliogopa hata kutembea hasa mabinti na wanawake!
Siyo ivyo tu misukule nayo ilionekana mara kwa mara ikikatiza mitaani,walionekana hata watu waliosadikika kufa zamani ambo kumbe walikuwa wamechukuliwa na mzee Mtata!
Kucha zao zilikuwa ndefu na nywele zao pia,kiufupi walikuwa wanatisha sana,hawakuwa wakiongea wengine walikuwa wamekatwa ulimi na wengine walikuwa wana ndimi ila zilikuwa nzito kuongea!
Viongozi walifunga safari mpaka kwa mzee Mtata hili wakamuulize imekuwaje mzimu umerudi na kingine ile misukule imetokea wapi?
Walipofika walishangaa kukuta mazingira ya nyumba yakiwa yamebadilika kila kitu kilikuwa ovyo ovyo tu,ng’ombe walikuwa wamekufa na mbuzi pia,wake wa mzee Mtata hawakuonekana!
Inasemekana walikimbia baada ya kuona misukule imetoka na inaanza kufanya fujo,ule mzimu pia ulianza kuwabaka hata wao!
Mazingira ya nyumba yaliwatisha viongozi lakini walijikaza wakaingia kilingeni ambako hawakuamini walimkuta mzee Mtata kafariki siku nyingi mpaka kaoza,pembeni yake ulikuwaa umekaa ule mzimu ila ulipowaona ukapotea!
Viongozi walitoka mbio baada ya kuona tukio lile,hawakuwa na namna mdaiwa wao alikuwa amekufa!
Hata ng’ombe walizompa walizikuta zimekufa zote na mbuzi,ilibidi wakakae upya kutafakari hatima ya kijiji chao ambacho sasa kila kona ni misukule na ule mzimu ulishika kasi!
Baada ya kutafakari sana walimtafuta mganga nguli kutoka kijiji cha jirani ili aje awasaidie kufanya ile kazi arudishe amani kijijini!
Alikuja nguli kutoka kijiji cha jirani ambaye alipofika tu aliitisha kikao cha wanakijiji wote wakakusanyika!
Alifanya manyanga yake mwisho akaamrisha aitwe mtu anayeitwa mzee Jomo,watu walishangaa sana!
Mzee Jomo alikuwa nyumbani na mawazo yake akafuatwa na sungusungu wa kijiji na kupelekwa mpaka kwenye ule umati!
Hakuwa anajua chochote kuhusu wito ule alibaki kushangaa,Mganga alipomuona tu alisema!
“Matatizo yote yameanzia kwa huyu mzee!”
Wanakijiji walishangaa sana na kubaki kuulizana imekuwaje mzee Jomo anahusikaje na mzimu ule,hata mzee Jomo alibaki kushangaa tu!
“Najua mnashangaa ila huyu mzee kuna mgeni alimkaribisha kwake,mzee uongo kweli?”
Kidogo sasa mzee Jomo akaanza kuelewa alitingisha kichwa kuashiria ni kweli alimkaribisha mgeni ,japo mpaka hapo hajui mgeni yule anahusikaje na ule mzimu!
Alipewa nafasi aelezee kilichotokea mpaka akamakaribisha mgeni nyumbani kwake,alisimama kwa masikitiko makubwa sana!
Kwanza aliwataka radhi wanakijiji kisha akahadithia jinsi alivyokutana na mgeni yule na kumpa hifadhi nyumbani kwake!
Alielezea yote kila kitu mpaka alivyotoroka na mwanaye na kuacha amewatia mimba binti zake wawili,ila hakumtaja mkewe!
Bila kuficha alieleza pia kuwa mgeni aliwatia mimba wake wote wa mzee Mtata hadi kupelekea akapata presha iliyomlaza kitandani na kuuchukua uhai wake!
Wanakijiji walishika kichwa walitamani sana kumjua huyo mgeni shujaa aliyeingia kwa mzee Mtata na kuwajaza mimba wake zake wote!
Waliona ni mtu wa ajabu sana,baada ya kumaliza kuongea aliomba radhi tena huku analia machozi,aliumia kuona kumbe mgeni ndiye amesababisha mambo ya mizimu kuja kijijini!
Mganga alisimama na kuanza kuelezea chanzo sasa rasmi kilichopelekea mzee Mtata autoe mzimu kaburini!
Wanakijiji walishangaa kusikia kuwa mgeni alilala kaburini siku tatu ili aweze kurudi mjini,ila mganga alisema pia mzee Mtata alipoteza nguvu nyingi kumpatia kinga mgeni yule ambayo amekufa akijutia mapa leo!
Kila kilichoongewa kilikuwa kama ndoto au filamu fulani iliyoigizwa na waigizaji mahiri sana duniani!
Baada ya hapo yule mganga alifanya manyanga yake na kuutoa hadharani ule mzimu,wanakijiji walitaka kuushambulia lakini akawazuia!
Baada ya hapo akaongozana na wanakijiji mpaka makaburini huko akafika mpaka kaburini ulipotoka!
Walishangaa kukuta kaburi liko wazi na jeneza liko wazi juu likiwa limechakaa sababu ni la zamani sana!
Mganga alifanya yake mzimu ukakubali kuingia kwenye jeneza na kisha akaurudisha kaburini,kanuri likafukiwa,wanakijiji ili kuhakikisha hautokuja tena kutokea waliufukia kwa mawe na kokoto nyingi sana!
Amani ikarejea kijijini tena mganga yule aliiondoa misukule haikuonekana kabisa amani ilirejea kama zamani!
Ndipo hapo likatolewa tamko kubwa kuhusu wageni kuingia ndani ya kijiji hiko,na hapo ndipo chuki dhidi ya wageni ilianzishwa rasmi!
Wageni hawakukaribishwa tena vizuri katika kijiji kile,ukipata mgeni unaenda kumtambulisha kwa mjumbe kwanza na unaulizwa anakaa siku ngapi?
JE NINI KITAENDELEA?USIKOSEEEE!


Chombezo………….BAO TATU ZA MGENI!
Mtunzi……………….Jack Mambo
Whtsp………………..0752761388
Call…………………….0716352102
Umri…………………..18+

Sehemu ya 59

Mzee Jomo alianza kuhangaika huku na kule akitafuta dawa ya kumfanyia ubaya Lukas,lakini kila alipoenda aliambiwa haiwezekani na wengine wakamtapeli tu!
Aliuza mpaka ng;ombe zake akasafiri mpaka Nigeria lakini hakuambulia kitu,kinga aliyoweka mzee Mtata ilikuwa kiboko!
Hatimaye mkewe alijifungua na binti zake wakajifungua pia,watoto ambao ukiwaona unasema huyu ni Lukas mtupu!
Hali ile ilimchefua zaidi mzee yule ambaye aliongeza juhudi za kutaka kumfanyia ubaya Lukas ambaye zote ziligonga mwamba!
Mzee Jomo hakula kwa amani,alikonda kwa mawazo na huzuni,miaka ikakatika watoto wakawa wanakuwa na kibaya walichukua sura ya baba yao mtupu!
Mawazo hayakumuacha salama Mzee Mtata alifariki miaka mitano baadae, na kumuacha mkewe akiwa analea familia!
Wake wa mzee Mtata waliondoka na kwenda kuishi kijiji cha jirani,ambako wengine walishaolewa huku kila mtu akiwa na chata ya Lukas!
Miaka kumi sasa imepita siyo Lukas,Selina wala Zubeda walioonekana kijijini,hakuna aliyewaona wala kupata tetesi za wapi walipo!
Historia ya mgeni ikawa imeishia hapo,mgeni alikuja mwenyewe kaondoka na watu wawili,hakuja na mtoto lakini kaacha watoto!
Mgeni kamuua shujaa wa kijiji hiki aliyeogopwa mpaka na sisimizi,mgeni kamuua mzee Jomo kabla hata ya siku zake!
Mgeni kafufua mizimu,mgeni kaleta mizimu mgeni kaleta taharuki,ni nani atampenda mgeni tena katika kijiji hiki?Nani atamkaribisha mtu hasiyemjua tena katika kijiji hiki?nani?nani atamuamini tena mgeni katika kijiji hiki!Hakuna hakuna hakuna!
MGENI ALISHUSHA THAMANI YA WAGENI KATIKA KIJIJI CHETU,VIJIJI VINGINE WANAFURAHI WAKIPATA WAGENI LAKINI HAPA MGENI ANATOA KUMBUKUMBU MBOVU SANA ILIYOWAHI KUTOKEA!

**************


“EFUUUUUUUUUUUUHHHHHHH!”
Nilishusha pumzi ndefu sana,hakika ilikuwa ni simulizi yenye kusisimua na kusikitisha sana,hata mimi nilikubali kwa namna ile ni haki wageni tuchukiwe!
“Ndiyo hivyo kaka!”
“Aiseeh poleni sana!”
“Tulishapoa ila ndo ivyo hatupendi wageni!”
“Kwahiyo na mimi unanichukia?”
“Kidogo maana umeonyesha utofauti!”
“lakini hujaniambia mwanzo kabisa ulisema ulimpoteza dada yako kisa mgeni!”
“Zahara alikuwa dada yangu,alifariki akijifungua yeye pamoja na mtoto!”
“Dah pole sana!”
Wakati tukiwa pale tunajadili walipita watoto watatu wanacheza ndipo Regina akanishtua!
“Eeeh unamuona yule mtoto?”
“Ndiyo!”
“Sasa yule mtoto wa Johari yule aliyekuwa anamchukia mgeni basi unaambiwa ndo kaizaa kopi yake yani ukimuona huyo wanasema ni sawa na Lukas kabisa kwa wanaomjua!”
“Ebhu muite!”
“Unataka ufanyeje?”
“We muite tu!”
Regina alimuita yule mtoto alipofika akatusalimia kisha nikachukua simu yangu nikampiga picha kama tatu hivi!
“Sasa mbona umempiga picha?”
“Aaah nimependa tu!”

Kiukweli nilikuwa sina sababu ya kubaki kijijini sababu nilikuwa nimemaliza utafiti wangu kwa asilimia zote,mbali na utafiti wangu lakini pia mbali na utafiti nilipata story nzuri ambayo nina uhakika itapendwa sana na wengi!
Niliomba nipelekwe kwa mama Zubeda wakafanya ivyo,haikuwa rahisi lakini kutokana na kwamba niliwaambia nataka niwasaidie kuwatafuta binti zao yaani Selina na Zubeda walikubali nikaongea nao kisha nikawapiga picha ya pamoja na picha moja moja!
Niliaga nikaondoka kijijini huku Regina akionekana kuhuzunika sana,hata mzee wake aliumia akinisihi nibaki lakini sikukubali!
Niliondoka nikiwaahidi kuwa nitarudi na Selina,Zubeda na pia nitamleta Lukas aje aombe msamaha kwa kijiji ili wageni tupokelewe tena kijijini!
Nilipanda gari asubuhi na mapema na kuanza safari ya kurejea Dar,safari yangu ilitawaliwa na tabasamu pana kwa kupata simulizi nzuri!
Lakini kichwani nilitamani kuyajua maisha ya Lukas baada ya kurudi mjini,je ni kweli wabaya wake walimsamehe au mzee Mtata alimuingiza choo cha kike!
Nilifika nikapumzika wiki nzima kisha nikachukua ile picha ya yule mtoto wa Lukas nikaitoa kisha nikamtafuta mchoraji hodari na maarufu sana kwa jina la Masoud Kipanya!
“Mdogo wangu mambo vipi?”
“Safi kaka shikamoo!”
“Ahh unaniona mzee,nilishakukataza kunizeesha nambie vipi hatuonani?”
“Kaka Masoud nina shida!”
“Ipi tena!”
“Nina picha hapa”,nilimpa ile picha akaiangalia kisha nikamuambia!”
“Kaka nataka iyo picha unichoree lakini huyo mtoto akiwa mtu mzima,yani uvute taswira huyo dogo akiwa mtu mzima atafananaje najua unaelewa cha kufanya we mzoefu!’
Nilimuelezea Masoud kwanini naitaka ile picha akakubali kunifanyia,baada ya wiki moja aliniita na kunikabidhi picha tatu zikiwa tofauti nyingine zina ndevu nyingine hazina!
Nilizichukua zile picha nikarudi nyumbani nikazihifadhi,nilitamani sana kumpata Lukas ili anipe stori yake na Selina mjini!
Bado namtafuta na hakika nikimpata nawaahidi nitawaletea simulizi nyingine ya Lukas kama season ya pili ya hadithi hii!
Bado nina shauku ya kumjua Lukas kiundani,nataka nimjue aliishije baada ya kutoka kijijini?

Nawashukuru sana kwa kuwa pamoja unaweza kutoa maoni yako kuhusu simulizi hii,mwisho wa hadithi hii ni mwanzo wa hadithi nyingine!TUTEGEMEE SEASON TWO KAMA NIKIMPATA NDUGU YETU LUKAS!


MWISHOOOOOOOOO**********
JACK MAMBO THE KING OF STORIES****

Me ni mvivu sana kusoma hadithi ila hii imenifanya nianze kusoma hadithi zako zoote na nyinginezo Hongera sana Mwandishi
 
Chombezo………….BAO TATU ZA MGENI!
Mtunzi……………….Jack Mambo
Whtsp………………..0752761388
Call…………………….0716352102
Umri…………………..18+

Sehemu ya 51

Shauku ilikuwa kubwa sana kwa wanakijiji,kuna waliobakiwa wake zao pia binti zao!kijiji kilikuwa na hasira sana!
Mzee Mtata alisimama kabla hajamleta hadharani alitaka kutoa onyo kwa wanakijiji wale ambo walionyesha hasira za waziwazi!
“Jamani mnataka nimtoee?”
“Ndiyooooo!”,waliitikia kwa pamoja!
“Mnata mumuone mchumba wenuuuu?”,alitania lakini hapo wanakijiji walikaa kimya!
“Hahahahahhaha!natania jamani!sasa nisikilizeni namtoa hadharani anayesumbua kijiji hiki,lakini chonde msimguse wala kumpiga,atakayemgusa ajue atakuwa anatembelewa kila siku na huyu mgeni awe mwanaume au mwanamke!”
Mzee Mtata ilibidi awatishe maana walikuwa na hasira za wazi wazi kabisa,baada ya kusikia vile wanakijiji waliogopa sana!
“Jamani tumeelewanaaaa!”
“Ndiyooooo!”
“Hamtamgusaaaaa?”
“Ndiyooooo!”
“Shauri yake atakayemgusa sitamtibia!”
Baada ya kutoa vitisho Mzee Mtata alichora duara kubwa kwa majivu kisha akaweka dawa zake akachukua kibuyu chake akaweka maji mdomoni na kuanza kuyapuliza juu!
Alipomaliza alianza kuuita ule mzimu ambao ghafla ulitokea kwenye lile duara huku unatetemeka na kuzunguka ndani ya ile duara!
Wanakijiji walipigwa na butwaa,kilikuwa kiumbe kinachotisha sana,wanawake waliokuwa wamehisi kufanya mapenzi na kile kiumbe walipatwa kichefuchefu wengine hadi wakatapika!
“Mmemuona eeh,ndiyo huyuuu!sasa namrudisha alipotoka hamtamuona tena kijijini,mimi ndiyo mzee Mtataaa!”,alisema huku anajipiga kifuani!
“OYOOOOOOOOOHH!”,wanakijiji walipiga kelele kumshangilia mzee huyu waliyemuona kama mkombozi wao,bila kujua kuwa ndiye mkandarasi wa kila kitu!
Lukas pekee ndiye alikuwa anaujua mchezo ule,alijua ni maigizo tu hakuna chochote pale,pembeni yake alikuwa na Selina
Alimshika mkono Selina akatoka naye pembeni,Selina alimshangaa Lukas kwa kumtoa pale uwanjani!
“Unanipeleka wapi?”,alihoji Selina!
“Nyumbani!”
Hakuwa na jinsi binti yule waliondoka mpaka nyumbani,moja kwa moja akaingia naye kwenye kijumba chake,Selina ilikuwa ni mara yake ya kwanza kuingia mle ndani!
Lukas hakuwa na subira alianza kumpapasa Selina ambaye si muda alilegea na muda mfupi baadaye wakawa watupu tayari kwa kuvunja chaga!
********

Huku kwa mzee Mtata alifanya manyanga yake na mwisho akaufanya ule mzimu ukapotea mbele za macho ya watu!
Ni yeye pekee alijua ulipoenda,wanakijiji walimshangilia na kumpa zawadi mbali mbali huku viongozi wakimkabidhi ng’ombe zake kumi pamoja na mbuzi wake watano!
Ilikuwa ni sherehe kubwa kumuondoa aliyewanyima amani kijijini,waliamini sasa watalala kwa amani!
Mzee Mtata alipomaliza kazi yake aliondoka na kurejea kwake,wake zake walimpokea kishujaa na kumsifia kwa kufanikiwa kuudhibiti mzimu!
Mzee Mtata hakuwa na hofu na ngvu zake kupungua,alijua kila kitu kiko sawa bila kujua dawa yake ambayo iebeba nusu ya nguvu zake imetupwa,na kadri anacvyotumia nguvu alizonanzo sasa zinazidi kupungua!
*********
Lukas na Selina walienda mzunguko mmoja tu wakatulia,hawakuwa na muda sababu muda wowote ule wengine wangerudi kutoka uwanjani!
“Selina mi nataka kuondoka hapa kijijini!”
Kauli ya Lukas ilimshtua sana Selina ambaye alijikuta anaacha kuvaa nguo zake kwanza amsikilize!
“Unasema!!!!?”
“Naondoka!”
“Unaenda wapi?”
“Narudi zangu mjini
“Lukasiiiii!”
Selina aliachia alichokuwa kakishika mikono akaitupia kichwani akiwa haamini alichokisika,alikaa kitandani machozi yalikuwa yanamtoka!
“Sasa unaniacha na nani jamani?”
“Naondoka na wewe!”
“Lukasiiiiiii!”
Alishtuka Selina hakujua Lukas anaondoka naye kivipi?na wataondokaje na nani atawaruhusu?kichwani yalipita maswali mengi!
“Hutaki?”
“Siyo sitaki Lukas,tunaondokaje na nani ataturuhusu!”
“Hatuhitaji ruhusa ya mtu!”
“Lukasiiiii!unamaanisha tutoroke?”
JE NINI KITAENDELEA?SELINA ATAKUBALI ?NA VIPI MZIMU UMEONDOKA?

Chombezo………….BAO TATU ZA MGENI!
Mtunzi……………….Jack Mambo
Whtsp………………..0752761388
Call…………………….0716352102
Umri…………………..18+

Sehemu ya 52

Kila mzazi ana kipenzi chake kati ya wanae wote,atawapenda wote lakini yupo mmoja mzani utaelemea kwake!
Mzee Jomo alikuwa na mapenzi mazito juu ya binti yake wa mwisho ambaye ni Selina,na Lukas naye kajikuta kafanya mapenzi na familia nzima ila kwa Selina ndipo kaweka kituo!patamu hapo!
Selina ilimuwia ngumu kukubaliana na maneno ya Lukas,hakutaka kuamini kwamba ni yeye anataka kutoroka na mwanaume!
“Lukas mi siwezi!”
“Selina utaishi kijijini mpaka lini?mi mjini nina maisha mazuri,utakuwa mkewangu acha huku unanishea na dada yako Suzy!”
“Lukas mi naogopaaa!”,alisema Selina huku akilia!
“Usilie Selina mi nimekupenda na niko tayari kufanya kila kitu kwa ajili yako,tafadhali naomba ukubali kuondoka na mimi!”
Baada ya kubembeleza sana mwisho alikubali kishingo upande kuondoka na Lukas mjini,Lukas alifurahi sana akamuahidi baada ya siku mbili kila kitu kingekuwa tayari!
Baada ya kuachana na Selina alianza kufanya mpango wa nauli,hakuwa na njia nyingine zaidi ya kuuza ng’ombe za mzee Jomo!
Alitafuta mteja wa ng’ombe akampata dalali ambaye alimpa dili,kesho yake akiwa machungani dalali alikuja na mteja akawauzia ng’ombe wawili wakubwa ambao thamani yao ilikuwa zaidi hata ya milioni,lakini aliuza kwa laki tano tu!
Ilikuwa ni ngumu kujua ng’ombe wamepungua sababu zilikuwa ni nyingi sana,akawa tayari amepata nauli ya kwenda mjini!
Baada ya kuirudisha mifugo nyumbani alipumzika akapewa chakula akawa anakula,wakati anakula alishangaa kumuona mzee Jomo anakuja na begi lake!
Alipatwa na mshangao mkubwa sana akashindwa hata kula kabisa,hofu na wasiwasi vilimtawala!
“Babaaaaaaaaa!”,wanae walimpokea kwa furaha kubawa!
Mzee Jomo akaingia nyumbani kwake,akiamini kila kitu kiko sawaa hakujua alimkabidhi fisi bucha,na fisi kaitumia vizuri nafasi ile!
“Lukas!”,alimuita Lukas!
“Naam mzee shikamoo pole na safari!”
“Marahaba!vipi umeenda machungani?”
“Ndo nimefika si muda mrefu napoza njaa hapa karibu!”
“Safi sana!”
Mzee Jomo aliingia ndani na kumuacha Lukas anakula,kwa upande wake Lukas alikuwa na hofu kubwa sana!
Mambo aliyoyafanya yalimfanya ajishtukia na kushindwa kabisa kumtazama mzee Jomo machoni!
Wanasema mwizi akimuona askari huwa anajistukia hata kama askari ana mambo yake tu,anaweza kujikuta anakimbia tu!
Alipopata tu upenyo wa kuongea na Selina alimvutia pembeni akamuambia suala la kuondoka!
“Tunaondoka kesho!”
“Lukas!huoni ni hatari baba karudi!”
“Hatuwezi vuruga ratiba yetu!”
“Lukas tusubiri baba aondoke!”
“Hatuna muda kama huondoki sawa mi kesho hutoniona,kama unaondoka ujue unaamka usiku saa tisa utanikuta nakusubiri!”
Lukas aliondoka na kumuacha Selina kasimama akiwa njia panda,hakujua afanyaje?abaki na ndugu zake au akubali kuondoka na mgeni huyu ambaye ndiye aliyemuingiza kwenye ulimwengu wa mapenzi!

Familia ya mzee Jomo ilikuwa na furaha sana siku ile,kawaida akirudi na zawadi kibao kutoka mjini,aliwapa zawadi zao wakafurahi sana!
Hakumsahau Lukas,alimletea suruali na shati jipya kabisa,hakujua kuwa anayemthamini katembea na familia nzima na kama haitoshi anataka kutoroka na mwanaye kipenzi Selina!
Usiku uliingia wakatawanyika Lukas akaingia kwenye makazi yake,alikuwa na mawazo sana kuhusu Selina!
“Itakuwaje hasipotoka,dah ila itabidi niondoke niliyoyafanya hapa yanatisha,huyu mzee ataniua!”
Usingizi ulimchukua akalala,lakini alikuja kushtuka akipapaswa usiku wa manane,alipoamka alimkuta Zahara ndiyo kamvamia usiku ule!
“Wewe unafanya nini?”,aliuliza Lukas kwa mshangao!
“Unajua nachotaka Lukas acha kujichetua,unataka Zubeda akufaidi peke yake,hujanipa siku nyingi nimeijia utamu wangu!”
“Zahara mi leo sijiskii utakuja kesho!”
“Yani kati ya vitu sitaki kuviskia ni huo upuuzi wako,ukitaka niondoke nipe hutaki nalala hapa Zubeda anikute mpaka asubuhi!”
“We unamuwaza Zubeda tu hujui kwamba mzee Jomo karudi”
“Afadhali tena akiona huyo atanipeleka kwa baba halafu baba atanileta unioe!”
“Unasemaje?”
Lukas alijua kabisa Zahara atamharibia mipango yake ya kuondoka!
JE LUKAS ATAFANYA NINI?ATAFANIKIWA KUONDOKA?

Chombezo………….BAO TATU ZA MGENI!
Mtunzi……………….Jack Mambo
Whtsp………………..0752761388
Call…………………….0716352102
Umri…………………..18+

Sehemu ya 53

Ulikuwa mtihani mkubwa sana kwa Lukas,kwake siku hiyo muda ulikuwa ni kitu muhimu kuliko vyote!
Zahara hakutaka kuelewa kabisa somo siku ile,alichotaka ni penzi la Lukas!licha ya kumkatalia sana lakini hakuelewa somo!
“Lukas we ongea vyote ila penzi utanipa ndiyo niondoke hapa!”
“Lakini nime…!”
Kabla hajamalizia kusema Zahara alimvamia na kuitoa bakora nje,Lukas hakuwa na namna,alichokifanya alimuacha Zahara afanye anachotaka!
“Zahara mi naumwa nakupa bao moja tu hapa kesho uje tutafanya vizuri!”
“Hayo ndiyo mambo sasa siyo nitoke usiku wote huu nirudi bila bao,huo ni ushamba!”
Lukas aliamua kufanya mapenzi na Zahara ili aondoke,alichokifanya ni kutumia staili zilizomchosha haraka Zahara!
Baada ya Zahara kuvunja dafu tatu tu alianza kuomba po!Lukas alipomaliza bao moja tu Zahara akavaa nguo zake!
“Nitarudi kesho umalizie bao zangu!”
Lukas hakuongea neno alimuacha Zahara akiondoka zake,aliona haukuwa muda wa kulala tena,alivaa zile nguo mpya alizoletewa na Mzee Jomo tayari kwa safari!
Kabla hata hajatoka nje alisikia sauti inamuita nje akajua pengine ni Zahara amerudi tena,akaisikiliza tena kwa makini!
“Lukas!Lukaas!”
Hakuamini alipotoka na kumkuta kipenzi chake Selina,ilikuwa bado kidogo tu amfumanie ila bahati ilikuwa upande wake,ni kama shetani alimlinda siku zote.
Kwa furaha ya kumuona Selina alimkumbatia kwa nguvu sana,hakuamini kama kweli Selina ameamua kuacha familia yake na kuongozana naye mjini!
“Selina siamini!”
“Nakupenda Lukas nimekubali kuiacha famili yangu sababu yako!”
“Naahidi nitakupenda daima mpenzi wangu!”
“Tuondoke Lukas baba huwa anatoka nje usiku!”
Hawakuwa na cha kubeba hata Selina alitoka na nguo alizovaa tu,safari ilianza huku Selina akiongoza njia!
Bahati nzuri walipata gari lililokuwa linapeleka mahindi mjini,wakapanda na kuendelea na safari walifika mjini na siku hiyo hiyo wakapata basi la alfajiri la kwenda Dar!
MGENI AKAWA KAONDOKA KIJIJINI!!
********
Mzee Mtata mambo yalikuwa si mambo tena,baada ya kufanikiwa kuwaaaminisha wanakijiji kuwa ameurudisha ule mzimu ulikotoka,alianza kuona mambo yanamwendea kombo!
Ile dawa yake ambayo mkewe mkubwa aliitupa ilimletea matatizo,sababu ilikuwa ni moja ya nguvu yake kubwa ya uchawi!
Ilikuwa inailinda misukule yake na pia iliwafanya hata maadui zake waogope kuingia kwenye ngome yake!
Kumbe siku ile baada ya kuutoa ule mzimu mbele za watu aliupeleka kilingeni kwake akiamini usiku unaofuata ataurudisha kaburini!
Kweli usiku uliingia mzee Mtata akafunga safari mpaka makaburini akafanya manyanga yake kaburi likafunguka na jeneza likatoka kama kawaida!
Tatizo likaja kwenye ule mzimu,aliuita uje lakini haukutokea,hali ile ilimchanganya sana Mzee Mtata!
Alijaribu mara kadhaa lakini hali bado ilikuwa ileile,mzimu haukutokea kabisa alipotaka kulirudisha lile kaburi kwenye hali yake liligoma pia kujifunga!
Mtata alichanganyikiwa kabisa kijasho kilimtoka,kila alichokifanya kaburi lilimzomea tu,muda ulizidi kwenda mpaka kukakaribia kukucha!
Hakuwa na namna alirudi nyumbani kwake na kuliacha kaburi lile wazi,moja kwa moja aliingia kilingeni alipongalia kwenye misukule yake aliuona ule mzimu umekaa umetulia hauna habari!
Aliuangalia kwan hasira lakini hakuwa na cha kuufanya maana ule ni mzimu siyo msukule wake!Alitoka nje kwa hasira akaanza kujiuliza imekuwaje hali ile inatokea?
Baada ya kuwaza sana aliingia ndani kwa mkewe mkubwa akachukua jembe Chiku akabaki kumshangaa!
“Mume wangu wapi na majembe usiku?”
Chiku hakujibiwa kitu,Mtata alitoka moja kwa moja mpaka alipofukia dawa yake ambayo ndiyo inabeba asilimia nyingi ya uchawi wake!
Alifika akachimba lakini kwa jinsi alivyokuwa anachimba aligundua mahari pale pamefukuliwa siku si nyingi,ardhi yake ilikuwa rahisi sana kuchimbika!
Alijipa moyo akaendelea kuchimba lakini hakuona kitu,hakutaka kuamini kuwa dawa yake haipo alichimba shimo refu sana lakini hakuona kitu!
Mtata alichanganyikiwa kabisa hakuamini kama dawa yake haipo,ile peke yake ndiyo ingemuwezesha kuurudisha mzimu kaburini!
Alijiuliza pengine labda alikosea sehemu siyo ile,kila akivuta hisia akili inamrudisha pale pale!
“Hapana ni hapa hapa,sasa imeenda wapi?oooh Maskini ntaadhilika hapa kijijini!”
Mzee mtata alirudi kilingeni akiwa na mawazo,usingizi haukuja alitamani kukuche awaite wake zake na kuwahoji juu ya wapi dawa yake ilipo!
Alikuwa na wasiwasi sana na mkewe mkubwa Chiku,sababu ndiyo msiri wake mkubwa na ndiye peke yake anayejua siri ya dawa ile ya mzee Mtata!
JE NINI KITAENDELEA?MZEE MTATA ATAFANYAJE AKIJUA CHIKU AMEITUPA ILE DAWA?


Chombezo………….BAO TATU ZA MGENI!
Mtunzi……………….Jack Mambo
Whtsp………………..0752761388
Call…………………….0716352102
Umri…………………..18+

Sehemu ya 54

Siku ile Mzee Mtata aliamka mapema akachukua kiti chake na kukaa nje karibu na jikoni kabisa akiwasubiri wake zake waamke!
Kwa alipokaa alikuwa anaona kila mlango wa nyumba za wake zake,katika hali ya kushangaza alimuona mkewe mdogo Vero akitoka mbio mbio ndani na kuanza kutapika kisha akarudi ndani bila kujua mumewe kamuona!
Hali ile ilimshangaza sana mzee Mtata kwa akili ya kikubwa alijua kabisa ile itakuwa mimba tu jambo ambalo hakutaka kuliamini sababu anajua kabisa hana uwezo wa kumpa mimba mwanamke yoyote duniani!
Akiwa kwenye hali ya kujiuliza alishangaa kuona mkewe mwingine ambaye ni Lolenza naye anatoka mbio akatapika na kurudi ndani!
“Hii ni nini?”,alijiuliza Mtata!
Hatimaye wake zake walitoka nje na kushangaa kumkuta mzee yule nje kakaa,mzee Mtata alimuita Chiku!
“Abee mumewangu”
“Naomba waite wenzako wote hapa nina kikao na nyinyi!”
“Sa..sawa mume wangu!”
Sauti ya Mtata ilimtia hofu sana Chiku,hakuongea kama kawaida alionekana ni mtu mwenye hasira sana!
Wake zake walikusanyika kwa pamoja wakakaa kumsikiliza ana nini cha kusema,alionekana amejaa sumu haswa!
“Nauliza hivi nani alichimba dawa yangu pale uwanjani,na aliipeleka wapi?”
Chiku alishtuka sana kusikia vile sababu ni yeye aliitupa ili wapate uhuru wa kufanya mapenzi na Lukas,sababu ile ilikuwa kama inampa machale mume wao!
“Chiku najua ni wewe peke yako unajua niliweka pale ile dawa nambie umeipeleka wapi?”
“Mi..mi…si..si..sjiui mume..!”
“Nyamazaaaa sitaki kusikia upumbavu hapa,nisubirini nije!”
Mzee mtata aliondoka akiwa na hasira akaingia kilingeni kwake,haikujulikana alifuata nini?Huku wake zake wakaanza kutupiana karata!
“Jamani mi simo,Chiku ndiyo uliitupa!”,alisema Vero!
“Hajitoi mtu hapa zilikuwa ni nyege zenu hakuna mtu kujitoa hapa!”,alisema Chiku!
Hakuna aliyejua Mzee Mtata kafuata nini ndani,walikaa kusubiri mpaka alipotoka alikuwa amebeba kinu!
“MUNGU WANGUU!”,Chiku alishtuka baada ya kuona kile kinu sababu alijua maana yake ni nini?
“Nini mbona unashtuka ni nini kwani?”
“Kinu cha kiapo kile tumekwishaaa!”
Mzee Mtata alirudi akiwa na kinu chake akakishusha chini,akamimina maji ndani ya kinu akachanganya na dawa kisha akaongea maneno yake!
Wakati anafanya yake alishangaa sana kumuona mkewe mwingine ambaye ni Tausi akiwa kashika ndimu analamaba muda wote!
Alimezea mate jambo lile akaendelea na jambo lake,alipomaliza kusema maneno yake alikaa huku chungu kikiwa katikati yao!
“Chiku nadhani unajua maana ya hiki kinu,kwa nyie wengine labda niwaambie tu kuwa hiki ni kinu cha kiapo,nitakuuliza kitu unatakiwa useme ukweli,ukitia mikono yako ndani ya hiki chungu kama umedanganya unakauka na kufa hapa hapa!”
“Nadhani mmenielewa,Vero simama ya juu!”
Mzee Mtata alimuamrisha mke wake mdogo asimame akafanya ivyo huku anatetemeka kwa hofu!
“Nadhani umenielewa ukweli wako ndiyo utakuweka hai aya nakuuliza je una mimba?”
Aliuliza swali ambalo lilikuwa nje kabisa na mada aliyokuwa ameianzisha,walibaki wameduwaa,hakuana aliyetegemea swali lile kabisa!
“Nijibu nina mambo mengi ya kufanya,una mimba!”
“Ndiyo!”
“Siyo mimba yangu si ndiyo?”
“Ni..ni…yako mume…!”
“Weka mikono humo usipoteze muda!”
Hapo ndipo palikuwa pagumu,Vero hakutaka kuweka mikono mzee Mtata akamuamsha mkewe Lolenza akasimama!
“Una mimba?”
“Ndiyo mume wangu”
“Kama ni yangu weka mikono kwenye kinu msiniletee mambo ya mzee Nyage na diamond hapa!”
Lole naye alishindwa kuweka mikono akaambiwa akae,akaamshwa Tausi naye alikuwa na mimba lakini hakutia mikono kwenye kinu!
Mpaka hapo ni wazi alijua kuwa wake zake wote wana mimba na siyo mimba zake,sababu hata yeye anajua hana uwezo wa kuzalisha!
Ilifika zamu ya Chiku ambaye aliulizwa swali tofauti na wenzake,Chiku alitetemeka kwan hofu!
“Nambie dawa yangu umeitupa wapi?kama hujaitupa tia mikono kwenye kinu!”
“Mume wangu na…nasema!”
“Ndiyo useme sasa!”
“Nili,,niliitupa!”
“Unasemaje wewe!!!”
ITAKUWAJE MZEE MTATA ATAFANYAJE?

Chombezo………….BAO TATU ZA MGENI!
Mtunzi……………….Jack Mambo
Whtsp………………..0752761388
Call…………………….0716352102
Umri…………………..18+

Sehemu ya 55

Mzee Mtata alihisi mapigo ya moyo wake yanaenda mbio sana,kijasho kilimtoka jazba na hasira zilimkaba!
“Umeitupia wapi!!!!?”
“Mtoni!”
“Hivi unajua umenimaliza?dah ivi iviiiii daaah!”
Mtata alikosa neno la kusema,alipatwa na kigugumizi,bora ingekuwa imetupwa hata vichakani angesema wakaitafute ila siyo mtoni!
Wake zake wote walikuwa wanamwaga machozi,lilikuwa ni jambo la aibu kwao kusimama mbele ya mume wake na kusema wana mimba lakini siyo zake!
“Kwanini uliitupa?ilikukera nini?”
Chiku hakusema kitu alilia kwa sauti mpaka kwikwi ikamshika,hakuweza kujibu swali la mumewe!
“Sema kabla sijakugeuza nyau hapaaa!’,alifoka akijua njia pekee ya kumpata mwanamke ni kumtia hofu!
“N..nananananasema babaanguaa nasema!”
Chiku kwa hofu alianza kueleza yote mwanzo mpaka mwisho jinsi ilivyokuwa hakuacha hata punje,na mwisho akamtaja Lukas!
“Lukasiiii!!!!”
Alisimama mzee Mtata akiwa haamini kabisa kama kijana aliyeamua kumtibu bure bila malipo na kumpa kinga dhidi ya uchawi wa aina yoyote ndiye aliyewajaza mimba wake zake!
Tiba ya Lukas ndiyo inamfanya saivi mzimu anamsumbua hataki kurudi kaburini,huku mkewe akiwa ametupa nguvu zake mtoni!
“Unamaanisha Lukas ndiyo kawapa mimba hawa !”
“Siyo hao tu na mimi pia nina mimba!”,alijibu Chiku!
“Niniiiiiiii!
Mtata alianguka presha ilipanda akapoteza fahamu na katika kuanguka kwake aliangukia kile kinu cha kiapo yale maji yakamwagikia miguuni,wake zake wakaanza kulaumiana!
“Unaona sasa tatizo umesema kila kitu!”
“Mlitaka nife acheni ujinga njooni tumbebe tumuingize ndani!’
Walimbeba mume wao wakamuingiza ndani akiwa hajitambui kabisa,hali ya mzee Mtata ilikuwa mbaya sana,kwa vile Chiku anajua baadhi ya amadawa akaanza kumtibia!tatizo alimwagikiwa na maji yale miguuni miguu yake ikapooza!

*********

Mzee Jomo aliamka akiwa hana hili wala lile ,alizunguka nyumba yake akapita zizini huku anapiga miluzi,mkononi kashika mswaki waake wa mti!
Alizunguka na kuridhika na mazingira ya nyumba yake,ndipo akafikiria kwenda kumuamsha Lukas maana alimuahidi kumfundisha baadhi ya madawa!
Taratibu akazipiga hatua zake mpaka kwenye kijumba ambacho Lukas amekuwa akiegesha mbavu zake tangu amkaribishe kijijini!
Alifika akagonga sana mlango akimuita Lukas lakini ukimya ulimpa mashaka sana,hakukuwa na muitikio ndipo akaamua kuingia ndani,alishangaa kukuta kitanda kikiwa kitupu!
“Huyu kijana kashakuwa mwenyeji sasa”
Alijisemea mzee Jomokisha akaendelea na mambo yake,hakuwa na wasiwasi aliaminikama ametoka basi hatokuwa mbali!
Suzy alishtuka baada ya kuamka na kumkosa Selina kitandani,kama kuna watu walikuwa wavivu kuamka mapema ni Selina,alijiuliza inakuwaje leo aamke mapema kiukweli alistaajabu sana!
Aliamua kupotezea akiamini pengine mdogo wake kaamua kubadilika,maana walishapiga kelele mpaka wakachoka!
Aliamka akamkuta baba yake nje akamsalimia kisha akaendelea na shughuli zake kama kawaida,ila kadri muda ulivyozidi kwenda ndivyo wasiwasi ulimjaa!

Mama Zubeda kama kawaida aliingia zizini kukamua maziwa,lakini kuna kitu kilimshangaza siku ile,alijisikia kichefuchefu sana akiwa anakamua maziwa hadi akatapika!
Ilibidi amuite Zubeda aje akamue yeye akashindwa kabisa kuendelea,hali ile ilimshangaza sana mzee Jomo ila akachukulia pengine ni homa za kawaida!
Selina ndiye alikuwa binti anayempenda kuliko mabinti zake wote,alimjua binti yake ni mvivu sana kuamka,hivyo alipoona mabinti zake wote wapo nje ila yeye hajaonekana akajua tu atakuwa amelala!
Alivumilia sana mwisho uvumilivu ukamshinda na muda ule hata Lukas naye alikuwa hajaonekana bado!
“Suzy ebhu kaniamshie huyo Selina analalaje mpaka saivi amekua sasa!”
Kauli ile ilimfanya Suzy aanze kuwaza upya ni wapi mdogo wake alipo,alimsogelea baba yake karibu!
“We sinimekwambia ukamwamshe mdogo wako?”
“Baba misijui hata nisemeje?”
“Usemeje ndiyonini?”
“Baba mimi nimeamka sijamkuta Selina kitandani?”
Mzee alisimama kichwa kilimzunguka,alijiuliza binti yake atakuwa ameenda wapi?Haraka akaiita familia yake yote!
“Nambieni Selina yuko wapi na kaanza lini hii tabia?”
“Mume wangu kwa kweli nayaona haya ni mageni kwa wengine naweza kukubali ila siyo kwa Selina hata mi sielewi!”
“Hayo siyo majibu nayotaka kusikia,nataka kusikia mnaniambia Selina alipo!”
“Baba labda kwa mgeni!”,Suzy alijikuta karopoka!
“Nini?umesema nini wewe?unamaanisha Lukas huyu au mwingine?”
Mzee Jomo kijasho kilimtoka akaanza kuunganisha matukio,Suzy alichafua hali ya hewa!

JE NINI KITAENDELEA?ZUBEDA ATAFANYAJE AKIGUNDUA LUKAS KAONDOKA NA MDOGO WAKE?


Chombezo………….BAO TATU ZA MGENI!
Mtunzi……………….Jack Mambo
Whtsp………………..0752761388
Call…………………….0716352102
Umri…………………..18+

Sehemu ya 56

Haliya hewa ilichafuka,Suzy aliyaibua yaliyojificha na kumfanya Mzee Jomo asimame akiwa amefura kwa hasira!
Suzy baada ya kuona daliliya kutokumuona mdogo wake alijua moja kwa moja atakuwa kwa Lukas,na ukizingatia kuwa jana yake aliwaona waliondoka uwanjani kabla hata shughuliya kuutoa mzimu haijaisha!
“Naomba uniambie kila kitu,unajua nini kuhusu Selina na Lukas?”
“Baba mi niliwafumania siku moja kwenye zizi wanafanya mambo ya ajabu,nikamkanya Selina akasema hatorudia lakini jana tulikuwa kwenye shughuli uwanjani kule,ila waliondoka kabla haijaisha,nikawafutailia wakaingia humo kwa Lukas!”
“Kwanini hukumwambia mamayako?”
“Baba nilitaka nikuambie asubuhi!”
“Baba Suzy muongo Lukas ni mchumba wangu,nilikuwa nakusubiri tu urudi nikuambie?”
“Paaaaa”
Mzee Jomo alishindwa kuvumilia alimtandika kofi zito Zubeda akaangukia pembeni akaanza kulia!
“Mama Zubedaaaa hivi ndivyo unavyolea mabinti zako?”
Mama Zubeda alikuwa analia na mengi,aliwaza mpaka hapo ameshea penzi na binti zake wawili Zubeda na Selina!
“Baba unanipiga bure tu Lukas ni mchumba wangu nampenda!”
“Nyamaza kenge wewe!”,alifoka mzee Jomo akaelekea kwenye kijumba cha Lukas akafanya ukaguzi akagundua Lukas katoka na kavaa nguo alizomletea jana!
Alitoka akiwa na hasira isiyoelezeka alizunguka kama chizi,Selina ni binti ambaye alikuja na neema mapema tu,mpaka hapo alikuwa anategemea mwanae ataolewa na tajiri mkubwa mjini,ambaye alishaonyesha nia ya kumtaka binti yake!
Walishaongea na kukubaliana kabisa ilikuwa mahari tu itoke japo hilo suala hakuwa amemshirikisha hata mkewe!
“Nawaambia kama Lukas kaondoka na Selina na nyie mnaondoka hapa!”
“Baba Zubeda kwani hayupo ndani!”
“Unauliza makofi polisi,watoto mpaka wanapelekwa mazizini eti wapo wanaishi na mama!”
Kilio cha mama Zubeda alilia akiwaza mpaka hapo ana mimba na Lukas kakimbia na mwanaye!
Mzee mtata alichukua baiskeli yake akawahi mpaka katikati ya kijiji huko akaiweka baiskeli kwa mtu akapata gari mpaka Sumbwanga mjini!
Aliangaza huku na kule lakinihakuambulia kitu ni wazi alikuwa amechelewa sana,mgeni kaondoka na mwenyeji wake,kamchukua kampeleka mjini!
Alichoka akatafuta sehemu akakaa kwanza akiwa hana hamu na Lukas,Lukas kampokonya dhahabu yake!
“Lukas nakuua,utakauka kama mti,utateketea kama mkaa,nitakufanya majivu!”,alisema kwa hasira mzee Jomo kisha akaanza safari ya kurudi kijijini!

Huku kila mtu alibaki ana sikitikia moyoni hakuna aliyekuwa nauwezo wakumwambia mwenzake,kila mtu alibaki na aibu yake!
Mama Zubeda alikuwa chumbani akiwaza mengi,kitendo cha kushea bakora na binti zake ilikuwa ni aibu kubwa sana kwake,kibaya zaidi Lukas hakumuacha hivi hivi kamuacha na ujauzito ambao anajua kabisa si wa mumewe!
“Lukas mbona hufananii na matendo yako,ivi kweli we ni wa kunichanganya na binti zangu!”,machozi yaliuosha uso wake siku ile!

Suzy licha ya kusema yale mbele ya baba yake kwa kuona wivu ila moyo ulimuuma sana,hasa alipogundua kuwa licha ya Lukas kufanya mapenzi na yeye na Selina pia alikuwa anatoka na Zubeda!
Aliumia kwa upande mwingine alitamani Selina angemshirikisha katika safari ile wakalifaidi wote penzi tamu la lukas!
“Lukas ivi wewe ni binadamu au mnyama?”,alijisemea akiwa haamini !

Kwa Zubeda yeye kilikuwa ni kilio tu kwa kwenda mbele,kati wanawake waliowahi kumpenda Lukas kupitiliza ni Zubeda,lakini ndiyo ivyo tena moyo Lukas ulikuwa kwa Selina!
Johari yeye hakuumia sana ila alikuwa anajicheka tu! Mpakawakati huo alikuwa hajui kabisa alilalaje na Lukas!
“Huyu kaka jamani au mchawi,yani nikamfuata nikavua nguo mwenyewe mmmmh!hapana hii siyo kawaida!”
Siku hiyo hakuna kazi iliyofanyika,hata chakula hakikulika kabisa,kila mtu alikuwa na majonzi yake!
Mifugo ililia zizini hakukuwa na mchungaji,kama walishindwa kujilisha wao wangewezaje kuwalisha wengine?
Mzee Jomo alirudi akiwa mpole tayari alijua kapoteza,alijuta kumkaribisha Lukas nyumbani kwake,kibaya zaidi hajui anaishi wapi?alimpokea kama msaada tu!
Aliikuta nyumba imekuwa kama imepatwa na msiba,tabasamu lilienda likizo kwa muda na haikujuikana litarudi lini!alitamani kujilaumu lakini hakuona alikosea wapi,anachoamini yeye alitenda wema kama binadamu wengine!
Akatamani kumlaumu mkewe lakini akakumbuka ile siku anampokea yule mgeni muharibifu mkewe alimzuia kabisa,yeye akalazimisha!
“Umeumia Lukas hii ni Sumbawanga,pole sana kijana!”

Siku ile ilipita kesho yake asubuhi na mapema mzee Jomo akapanda baiskeli mpaka kwa swahiba wake wa muda mrefu,naye si mwingine ni mzee Mtata!
Aliuamini uwezo wa Mzee Mtata alijua kwake ni jambo dogo sana,kiufupi alitaka kumfanyia Lukas michezo ya kiswahili ikibidi awe hata kipofu kabisa!
Alifika salama kwa Mzee Mtata lakini alichokutana nacho kilimkatisha tamaa,Mtata alikuwa hoi kitandani anaumwa hawezi kutembea!
“Mzee mwenzangu mbona kitandani?”,aliuliza mzee Jomo!
“Acha tu mzee mwenzangu,ninaumwa umwa ila niko sawa!”
“Kuna kazi nataka unifanyie utaweza kweli?”
“Kazi gani tena?”
Mzee Jomo hakumficha kitu alieleza kila kitu jinsi alivyompokea Lukas na mwisho kaondoka binti yake Selina!
“Umesema Lukas kaondoka na binti yako?”
“Ndiyo!”,mzee Mtata presha ilipanda ghafla hadi Mzee Jomo akashangaa!
“Mzee mwenzangu,mzee mwenzangu vipi tena?”
JE NINI KINAENDELEA?MZEE JOMO AKIJUA KUWA LUKAS KAWATIA MIMBA WAKE WA MGANGA WOTE ITAKUWAJE?

Chombezo………….BAO TATU ZA MGENI!
Mtunzi……………….Jack Mambo
Whtsp………………..0752761388
Call…………………….0716352102
Umri…………………..18+

Sehemu ya 57

Mzee Mtata hakuwa yule katili wa kuogopwa tena,alikuwa mdogo kama pilitoni,aliposikia jina la Lukas,hasira ilipanda na presha ikawa juu!
Machozi yalibisha hodi na hata kabla hajayaruhusu yalitoka kwa wingi,Mzee Jomo alimshangaa sana Mzee mwenzie,amemzoea ni mtu mwenye kiburi na majivuno,hakuwahi kufikiria kwamba kuna siku atatokwa na machozi mbele yake!
“Mzee mwenzangu nini tatizo!”
“Acha tu mzee mwenzangu!”
Bila kuficha kitu japo alijihisi aibu lakini aliamua kumueleza kila kitu mzee Jomo,jinsi alivyomkamata na kumleta kwake!Alieleza mengi sana kuhusu Lukas!
“Mzee Mtata kwa hiyo unamaanisha Lukas kawapa mimba wake zako wote?”
“Ndiyo!”
“Dah!hiki kitoto kumbe kishetani hivi!”
“Nakushauri mzee mwenzangu kaipime familia yako yote,yule kijana sidhani kama ametembea na binti zako wawili tu mpime hadi mkeo!”
“Mkewanguuu hapana hapo nakataaa!”
Mzee Mtata alimueleza jinsi mke wake alikuwa anakuja kwake akisema Lukas ni mdogo wake,kwahiyo ana wasiwasi pia na mkewe!
“Kama kamgusa mkewangu namuua namuua mende yule!”
“Humuwezi!”
“Unasema?”,aliuliza Mzee Joma kwa mshangao!
“Nasema humuwezi na hicho ndicho kinachoniuma mimi,yule kijana nilimuamini sana,kwa upendo niliokuwa nao kwake nilimpa kinga kali sana ambayo hata mimi nikitaka kumfanyia ubaya siwezi,muache tu!”
“Haiwezekeni nasema haiwezekani!”,aliondoka kwa hasira mzee Jomo na kumuacha Mtata anamuita bila mafanikio!

Alirudi kwake akachukua ndimu tatu akazikata kisha akachanaganya na madawa aliyoyajua yeye,alipomaliza aliita familia yake yote!
“Huyo mpuuzi kawatia mimba wake wa mzee Mtata wote,navyoongea na nyinyi hapa Mzee Mtata yuko hoi kitandani!”
“Siyo kweli baba siyo kweli Lukas wanamsi…!”
“Kimyaaa!mwanaizaya wewe!”
Zubeda alijaribu kumtetea Lukas lakini baba yake alimnyamazisha!
“Sasa nisikilizeni hapa,ninawapima mimba!”
Mama Zubeda alishtuka sana,kauli ya mume wake ilimfanya apate hofu kubwa sana,aliamua kujitetea mbele ya mume wake!
“Sasa baba Zubeda kwanini usiwapime watoto mimi mambo yao yananihusu nini?”
“Tena unyamaze Mtata kaniambia kila kitu!naomba mchukue ndimu hizo kila mtu alambe!”
Alisema lakini hakuna aliyeshika ndimu kila mtu alibaki kukodoa macho,mzee Jomo akasimama!
“Msinitanie kila mtu achukue ndimu hapo!”
Kwa hofu wote walichukua ndimu wakiwa wanatetemeka baada ya kulamba wakakaa kusubiri,ile ni dawa ambayo imechanganywa ili kama mtu ana mimba akilamba atahisi kichefuchefu na kutapika!
Johari ndiye alikuwa wa kwanza kutapika wote wakamshangaa,mzee Jomo alijiuliza ina maana na Johari ametembea na Lukas!
Wakati anajiuliza swali lile Suzy naye ngoma ikatiki akarudisha chenji wote wakashangaa ,maana yeye anasema aliwafumania Lukas na Selina!
“Wewe si ulisema umewafumania?”
Kabla hajajibu kitu alishangaa kumuona mkewe anarudisha chenji kumaanisha na yeye naye kitu kimetiki!
“Mamaaaaaaaaaaaaaaa!na wewe!”,binti zake waliuliza kwa mshangao!
Mzee Mtata aliingia ndani akatokana panga akasimama akiwaangalia,wote walikuwa wanatetemeka!
Ajabu Zubeda hakuwa na mimba alisubiliwa lakini hakukuwa na matokeo yoyote,jambo lile llimuuma sana akabaki kulia tu!
Mzee Jomo aliwauliza na wote walikiri kuwa mimba ni za Lukas,alitetemeka kwa hasira alihisi kujutia sana!
“LUKASIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIIII!!!!”
Alipiga kelele kubwa akiwa haamini kama Lukas ndiye kanmfanyia unyama ule,akiwa katika sintofahamu ghafla alikuja mgeni akiwa ameongozana na binti yake!
Hakuwa mwingine alikuwa ni mama Zahara na Zahara,alipofika tu hakuuliza moja kwa moja akauliza!
“Yuko wapi huyo klidume aliyemtia mimba binti yangui?”
“Kuna nini?”,aliuliza Mzee Jomo!
“Kuna kijana anaishi hapa anaitwa Lukas kamtia mimba binti yangu!”
Kauli ile ilimfanya Zubeda aanguke na kupoteza fahamu,shughuli ikawa imeishia pale!Mzee Jomo hakuwa na namna japo moyoni alisema atamfanya kitu kibaya Lukas!
Siku ile ilipita lakini kesho yake asubuhi walipoamka hawakumkuta Zubeda ,alikuwa ameacha ujumbe kuwa anaenda mjini kumtafuta Lukas!
“Lukas!Lukas!Lukas!”,alilia Mzee Jomo familia yake iligawanyika,mpaka hapo kapoteza binti zake wawili!
JE NINI KITAENDELEA?


Chombezo………….BAO TATU ZA MGENI!
Mtunzi……………….Jack Mambo
Whtsp………………..0752761388
Call…………………….0716352102
Umri…………………..18+

Sehemu ya 58

Kijiji kiliingia gharika,ule mzimu uliokamatwa na Mzee Mtata na kuwahakikishia kuwa hautorudi,ulirudi kwa kasi sasa ukawa unabaka watu mpaka mchana!
Mzimu ule ulikuja na nguvu kubwa sana,safari hii hii ulikuwa unabaka na kupotea,wanakijiji waliogopa hata kutembea hasa mabinti na wanawake!
Siyo ivyo tu misukule nayo ilionekana mara kwa mara ikikatiza mitaani,walionekana hata watu waliosadikika kufa zamani ambo kumbe walikuwa wamechukuliwa na mzee Mtata!
Kucha zao zilikuwa ndefu na nywele zao pia,kiufupi walikuwa wanatisha sana,hawakuwa wakiongea wengine walikuwa wamekatwa ulimi na wengine walikuwa wana ndimi ila zilikuwa nzito kuongea!
Viongozi walifunga safari mpaka kwa mzee Mtata hili wakamuulize imekuwaje mzimu umerudi na kingine ile misukule imetokea wapi?
Walipofika walishangaa kukuta mazingira ya nyumba yakiwa yamebadilika kila kitu kilikuwa ovyo ovyo tu,ng’ombe walikuwa wamekufa na mbuzi pia,wake wa mzee Mtata hawakuonekana!
Inasemekana walikimbia baada ya kuona misukule imetoka na inaanza kufanya fujo,ule mzimu pia ulianza kuwabaka hata wao!
Mazingira ya nyumba yaliwatisha viongozi lakini walijikaza wakaingia kilingeni ambako hawakuamini walimkuta mzee Mtata kafariki siku nyingi mpaka kaoza,pembeni yake ulikuwaa umekaa ule mzimu ila ulipowaona ukapotea!
Viongozi walitoka mbio baada ya kuona tukio lile,hawakuwa na namna mdaiwa wao alikuwa amekufa!
Hata ng’ombe walizompa walizikuta zimekufa zote na mbuzi,ilibidi wakakae upya kutafakari hatima ya kijiji chao ambacho sasa kila kona ni misukule na ule mzimu ulishika kasi!
Baada ya kutafakari sana walimtafuta mganga nguli kutoka kijiji cha jirani ili aje awasaidie kufanya ile kazi arudishe amani kijijini!
Alikuja nguli kutoka kijiji cha jirani ambaye alipofika tu aliitisha kikao cha wanakijiji wote wakakusanyika!
Alifanya manyanga yake mwisho akaamrisha aitwe mtu anayeitwa mzee Jomo,watu walishangaa sana!
Mzee Jomo alikuwa nyumbani na mawazo yake akafuatwa na sungusungu wa kijiji na kupelekwa mpaka kwenye ule umati!
Hakuwa anajua chochote kuhusu wito ule alibaki kushangaa,Mganga alipomuona tu alisema!
“Matatizo yote yameanzia kwa huyu mzee!”
Wanakijiji walishangaa sana na kubaki kuulizana imekuwaje mzee Jomo anahusikaje na mzimu ule,hata mzee Jomo alibaki kushangaa tu!
“Najua mnashangaa ila huyu mzee kuna mgeni alimkaribisha kwake,mzee uongo kweli?”
Kidogo sasa mzee Jomo akaanza kuelewa alitingisha kichwa kuashiria ni kweli alimkaribisha mgeni ,japo mpaka hapo hajui mgeni yule anahusikaje na ule mzimu!
Alipewa nafasi aelezee kilichotokea mpaka akamakaribisha mgeni nyumbani kwake,alisimama kwa masikitiko makubwa sana!
Kwanza aliwataka radhi wanakijiji kisha akahadithia jinsi alivyokutana na mgeni yule na kumpa hifadhi nyumbani kwake!
Alielezea yote kila kitu mpaka alivyotoroka na mwanaye na kuacha amewatia mimba binti zake wawili,ila hakumtaja mkewe!
Bila kuficha alieleza pia kuwa mgeni aliwatia mimba wake wote wa mzee Mtata hadi kupelekea akapata presha iliyomlaza kitandani na kuuchukua uhai wake!
Wanakijiji walishika kichwa walitamani sana kumjua huyo mgeni shujaa aliyeingia kwa mzee Mtata na kuwajaza mimba wake zake wote!
Waliona ni mtu wa ajabu sana,baada ya kumaliza kuongea aliomba radhi tena huku analia machozi,aliumia kuona kumbe mgeni ndiye amesababisha mambo ya mizimu kuja kijijini!
Mganga alisimama na kuanza kuelezea chanzo sasa rasmi kilichopelekea mzee Mtata autoe mzimu kaburini!
Wanakijiji walishangaa kusikia kuwa mgeni alilala kaburini siku tatu ili aweze kurudi mjini,ila mganga alisema pia mzee Mtata alipoteza nguvu nyingi kumpatia kinga mgeni yule ambayo amekufa akijutia mapa leo!
Kila kilichoongewa kilikuwa kama ndoto au filamu fulani iliyoigizwa na waigizaji mahiri sana duniani!
Baada ya hapo yule mganga alifanya manyanga yake na kuutoa hadharani ule mzimu,wanakijiji walitaka kuushambulia lakini akawazuia!
Baada ya hapo akaongozana na wanakijiji mpaka makaburini huko akafika mpaka kaburini ulipotoka!
Walishangaa kukuta kaburi liko wazi na jeneza liko wazi juu likiwa limechakaa sababu ni la zamani sana!
Mganga alifanya yake mzimu ukakubali kuingia kwenye jeneza na kisha akaurudisha kaburini,kanuri likafukiwa,wanakijiji ili kuhakikisha hautokuja tena kutokea waliufukia kwa mawe na kokoto nyingi sana!
Amani ikarejea kijijini tena mganga yule aliiondoa misukule haikuonekana kabisa amani ilirejea kama zamani!
Ndipo hapo likatolewa tamko kubwa kuhusu wageni kuingia ndani ya kijiji hiko,na hapo ndipo chuki dhidi ya wageni ilianzishwa rasmi!
Wageni hawakukaribishwa tena vizuri katika kijiji kile,ukipata mgeni unaenda kumtambulisha kwa mjumbe kwanza na unaulizwa anakaa siku ngapi?
JE NINI KITAENDELEA?USIKOSEEEE!


Chombezo………….BAO TATU ZA MGENI!
Mtunzi……………….Jack Mambo
Whtsp………………..0752761388
Call…………………….0716352102
Umri…………………..18+

Sehemu ya 59

Mzee Jomo alianza kuhangaika huku na kule akitafuta dawa ya kumfanyia ubaya Lukas,lakini kila alipoenda aliambiwa haiwezekani na wengine wakamtapeli tu!
Aliuza mpaka ng;ombe zake akasafiri mpaka Nigeria lakini hakuambulia kitu,kinga aliyoweka mzee Mtata ilikuwa kiboko!
Hatimaye mkewe alijifungua na binti zake wakajifungua pia,watoto ambao ukiwaona unasema huyu ni Lukas mtupu!
Hali ile ilimchefua zaidi mzee yule ambaye aliongeza juhudi za kutaka kumfanyia ubaya Lukas ambaye zote ziligonga mwamba!
Mzee Jomo hakula kwa amani,alikonda kwa mawazo na huzuni,miaka ikakatika watoto wakawa wanakuwa na kibaya walichukua sura ya baba yao mtupu!
Mawazo hayakumuacha salama Mzee Mtata alifariki miaka mitano baadae, na kumuacha mkewe akiwa analea familia!
Wake wa mzee Mtata waliondoka na kwenda kuishi kijiji cha jirani,ambako wengine walishaolewa huku kila mtu akiwa na chata ya Lukas!
Miaka kumi sasa imepita siyo Lukas,Selina wala Zubeda walioonekana kijijini,hakuna aliyewaona wala kupata tetesi za wapi walipo!
Historia ya mgeni ikawa imeishia hapo,mgeni alikuja mwenyewe kaondoka na watu wawili,hakuja na mtoto lakini kaacha watoto!
Mgeni kamuua shujaa wa kijiji hiki aliyeogopwa mpaka na sisimizi,mgeni kamuua mzee Jomo kabla hata ya siku zake!
Mgeni kafufua mizimu,mgeni kaleta mizimu mgeni kaleta taharuki,ni nani atampenda mgeni tena katika kijiji hiki?Nani atamkaribisha mtu hasiyemjua tena katika kijiji hiki?nani?nani atamuamini tena mgeni katika kijiji hiki!Hakuna hakuna hakuna!
MGENI ALISHUSHA THAMANI YA WAGENI KATIKA KIJIJI CHETU,VIJIJI VINGINE WANAFURAHI WAKIPATA WAGENI LAKINI HAPA MGENI ANATOA KUMBUKUMBU MBOVU SANA ILIYOWAHI KUTOKEA!

**************


“EFUUUUUUUUUUUUHHHHHHH!”
Nilishusha pumzi ndefu sana,hakika ilikuwa ni simulizi yenye kusisimua na kusikitisha sana,hata mimi nilikubali kwa namna ile ni haki wageni tuchukiwe!
“Ndiyo hivyo kaka!”
“Aiseeh poleni sana!”
“Tulishapoa ila ndo ivyo hatupendi wageni!”
“Kwahiyo na mimi unanichukia?”
“Kidogo maana umeonyesha utofauti!”
“lakini hujaniambia mwanzo kabisa ulisema ulimpoteza dada yako kisa mgeni!”
“Zahara alikuwa dada yangu,alifariki akijifungua yeye pamoja na mtoto!”
“Dah pole sana!”
Wakati tukiwa pale tunajadili walipita watoto watatu wanacheza ndipo Regina akanishtua!
“Eeeh unamuona yule mtoto?”
“Ndiyo!”
“Sasa yule mtoto wa Johari yule aliyekuwa anamchukia mgeni basi unaambiwa ndo kaizaa kopi yake yani ukimuona huyo wanasema ni sawa na Lukas kabisa kwa wanaomjua!”
“Ebhu muite!”
“Unataka ufanyeje?”
“We muite tu!”
Regina alimuita yule mtoto alipofika akatusalimia kisha nikachukua simu yangu nikampiga picha kama tatu hivi!
“Sasa mbona umempiga picha?”
“Aaah nimependa tu!”

Kiukweli nilikuwa sina sababu ya kubaki kijijini sababu nilikuwa nimemaliza utafiti wangu kwa asilimia zote,mbali na utafiti wangu lakini pia mbali na utafiti nilipata story nzuri ambayo nina uhakika itapendwa sana na wengi!
Niliomba nipelekwe kwa mama Zubeda wakafanya ivyo,haikuwa rahisi lakini kutokana na kwamba niliwaambia nataka niwasaidie kuwatafuta binti zao yaani Selina na Zubeda walikubali nikaongea nao kisha nikawapiga picha ya pamoja na picha moja moja!
Niliaga nikaondoka kijijini huku Regina akionekana kuhuzunika sana,hata mzee wake aliumia akinisihi nibaki lakini sikukubali!
Niliondoka nikiwaahidi kuwa nitarudi na Selina,Zubeda na pia nitamleta Lukas aje aombe msamaha kwa kijiji ili wageni tupokelewe tena kijijini!
Nilipanda gari asubuhi na mapema na kuanza safari ya kurejea Dar,safari yangu ilitawaliwa na tabasamu pana kwa kupata simulizi nzuri!
Lakini kichwani nilitamani kuyajua maisha ya Lukas baada ya kurudi mjini,je ni kweli wabaya wake walimsamehe au mzee Mtata alimuingiza choo cha kike!
Nilifika nikapumzika wiki nzima kisha nikachukua ile picha ya yule mtoto wa Lukas nikaitoa kisha nikamtafuta mchoraji hodari na maarufu sana kwa jina la Masoud Kipanya!
“Mdogo wangu mambo vipi?”
“Safi kaka shikamoo!”
“Ahh unaniona mzee,nilishakukataza kunizeesha nambie vipi hatuonani?”
“Kaka Masoud nina shida!”
“Ipi tena!”
“Nina picha hapa”,nilimpa ile picha akaiangalia kisha nikamuambia!”
“Kaka nataka iyo picha unichoree lakini huyo mtoto akiwa mtu mzima,yani uvute taswira huyo dogo akiwa mtu mzima atafananaje najua unaelewa cha kufanya we mzoefu!’
Nilimuelezea Masoud kwanini naitaka ile picha akakubali kunifanyia,baada ya wiki moja aliniita na kunikabidhi picha tatu zikiwa tofauti nyingine zina ndevu nyingine hazina!
Nilizichukua zile picha nikarudi nyumbani nikazihifadhi,nilitamani sana kumpata Lukas ili anipe stori yake na Selina mjini!
Bado namtafuta na hakika nikimpata nawaahidi nitawaletea simulizi nyingine ya Lukas kama season ya pili ya hadithi hii!
Bado nina shauku ya kumjua Lukas kiundani,nataka nimjue aliishije baada ya kutoka kijijini?

Nawashukuru sana kwa kuwa pamoja unaweza kutoa maoni yako kuhusu simulizi hii,mwisho wa hadithi hii ni mwanzo wa hadithi nyingine!TUTEGEMEE SEASON TWO KAMA NIKIMPATA NDUGU YETU LUKAS!


MWISHOOOOOOOOO**********
JACK MAMBO THE KING OF STORIES****
Story nzuri sana
 
Ewaaaah hatimae naimaliza leo story tamu sana mafunzo ni mengi ila nilidhan Regina nae atapitiwa kumbe hamna au ukirud kijijn ndo zamu yake 😀😀😀
 
Back
Top Bottom