Chombo cha NASA chafanikiwa kutua Sayari ya Mirihi (Mars), kitakusanya na kurudisha sampuli za mawe duniani

Chombo cha NASA chafanikiwa kutua Sayari ya Mirihi (Mars), kitakusanya na kurudisha sampuli za mawe duniani

Nimeona hii kitu CNN yaani wametumia miezi 6 kusafiri maili karibia milioni 300.
Haya mambo ya Sayari yapo kweli au usanii tu wa NASA?

Mkuu watu wanacho sahau ni kwamba Taifa la Urusi ndio lilikuwa la kwanza kutuma chombo kwenye sayari ya MARS mwaka 1976 kikafanikiwa kutua na kutuma picha za rangi Duniani, hilo NASA hawalisemi kabisa - hawasemi chochote kuhusu mananikio ya chombo cha Urusi aina ya VENERA.

Miaka 45 baadae ndio wanajifanya ni mapioneer! Kweli Duniani kuna mambo.
 
Bado nauliza, camera iliyopiga picha ya hiko vhombo wakati kinatua nayo ilirushwa kabla ya chombo au sambamba na chombo. Tuzingatie angleIyake.
Swali la msingi mkuu, naona watakuwa wanarudia usanii wao wa ku-animate project nzima - yanarudia yale yale ya kutua mwezini!! Hollywood GURUS bado wapo sana.
 
Cha muhimu waifanye dunia iwe na amani na upendo ndio italeta maana na chanjo ya ukimwi watoe
 
huko wamepeleka vyombo vingapi vya utafiti? Maana kwenye hizo picha naona ni vyombo viwili tofauti.
 
Wewe hapo umeona nini ? Mpaka unaniuliza kama nimeona?

Kwani hapo bibie kitu kimekufanya mpaka ukasidikisha hiyo habari? Je, hukuona haja ya kuhoji au hupaswi kuhoji?

Mimi mpaka hapo nina maswali zaidi ya matatu ya kuhoji juu ya habari hiyo. Huku ushahidi wa picha nikiudhohofisha sababu hata mimi naweza kubuni picha kama hiyo.

Tukirudi katika swali lako, hapo nimeona picha tu sijaona kipya. Ili niweze kuwaamini tu ni kuwa watuambie kwanini walituambia kuna mtu alienda mwezini na kwanini hawaendi tena?
Sas wewe hata nauli ya kufika 2 nasa huna unatak sisi tukusaidiaje? Wenzio wanaend wanashuhudia chombo inaondoka CNN wanarusha live we sijui unakuwaga wapi hapo. Hufanyi effort yyte ya tafiti.
 
Wamarekani uwaga ni waongo,, uwaga ni Photoshop.
Sawa wenzio wameleta ushahidi wa picha. Leta uthibitisho kuwa ile ni photoshop mbona simple 2. Kama hujui huko mbele kudetect pich iliyotengenezwa rahisi tu watu wangesema. Makao makuu ya NASA watu wanatembelea. We huko hapo bongo umepoa 2 unataka nasa wakusaidiaje?
 
Naanzia hapa,suala la budget waesema lini au umejiaje kama budget ni kubwa ? Umbali wa kwenda Mars na Mwezini unatofautiana vipi na changamoto ni zipi ? Bajeti hiyo ni kiasi gani wanayo

Kuna swali nilikuuliza wewe unahihikisha vipi ya kuwa kweli wameenda Mwezini au Mars ? Marejeo yako wewe ni yapi ? Hili swali hujalijibu. Kwamba je kwa kuona picha au kusikia habari ?

Hapa naona unawachoresha Wanasayansi na kuwafanya tuwaone wamebweteka. Kisayansi walitakiwa mpaka sasa hivi wawe wameshaenda zaidi ya mara kumi sababu ni zaidi ya miongo mitatu tangu tuambiwe Nail alikwenda mwezini. Maana yake walitakiwa wawe wameshabuni vifaa vyenyw ufanisi mkubwa na kwa gharama nafuu. Labda watuambie ya kuwa gharama imekuwa kubwa zaidi ya kuandaa movie kama hiyo, au wameshajua ya kuwa watu wameshawaona wao mazwazwa kwa kuigiza tukio hilo pale Area 51.

Lakini suala la uzandiki juu ya tukio la mwezini mbona limeshabatilishwa tangu zamani na husemwa pia sababu ya kifo cha John F. Kenedy ni kufichua siri au kutaka kufichua mbinu hiyo. Kihistoria husemwa ya kuwa hiyo ilikuwa ni vita baina ya USSR na Marekani katika kuonyeshana umwamba maendeleo ya kisayansi.

Mimi siyo kwamba nadhani bali nina uhakika kabisa.

Watuambie kwanza umbali wa kutoka katika uso wa dunia mpaka mwezini ni kiasi gani ? Bila kuweka Assumtions yoyote ile, wakiweka tu Assumptions wameharibu.

Pili, walitumia vigezo gani kutengeneza kifaa ambacho walijua fika kitawapeleka na kuwafikisha mwezini ? Hapa inabidi watuambie. Maana yake kabla inabidi ufanya ufanue utafiti, na utembelee sehemu husika. Tafiti hii ilifanyika wapi na kwa kutumia nini ?

Sasa unapohoji haya mambo ndipo unapoona ya kuwa hili ni igizo na wengine walithibitisha hilo.

Tatu, kiimani jambo hili hali wezekani, sababu hakuna anaejua ya kuwa Mwezi uko umbali gani toka mbingu ya kwanza ila kwa macho ukiangalia vizuri unaona ya kuwa mwezi uko karibu sana na mbingu ya kwanza kuliko ardhini, yaani duniani. Tunaambiwa umbali wa mbingu ya kwanza na dunia na mbingu na mbingu ni mwendo wa miaka 500. Hii ni kwa mwendo kasi wa juu zaidi (Rejea jaya katika kitabu kiitwacho "Qamus al Bida'ah" ). Maana chini ya muda huo hizo zinabaki kuwa stori tu na kufurahisha nafsi.

Tatu, zipo sababu za kisayansi zinazo pinga igizo hilo. Unaweza kuzifatilia Google ukazipata. Ukisearch "Did we land on the moon". Utaona mambo mengi wapo wanao thibitisha ya kuwa tukio hilo ni kweli na wale wanao kadhibisha tukio hilo, ukipima katika mzani utaona ya luwa hawa wapili wana hoja zenye nguvu mno kuliko wengin, na hao wa kwanza wameanza kuja kuandika hayo hivi karibuni.

Narudi kuendelea hapa nilipoishia...
Duu mwezi uliopo juu tu hapo ukaribie mbinguni? Na jua je? Sas wenzio waliogundua nuclear bombs hospitals wakatufundisha jinsi ya kuishi wakatoka kwao wakafanikiwa kufika kwetu wakafanikisha nasisi tuweze kwenda kwao wanasema wameenda mars. Je tukuamini wewe kwa lipi ulilofanya hapo. Mbona hata hesabu za kurusha ndege ni za makadirio lakini ndege imeruka kweli. Meli je density ya maji sio makadirio? Matumizi ya umeme sio makadirio mpaka kukawa na power factor? Ko we makadirio ya mars 2 ndo yanakutoa roho!?
 
Ngoja twende taratibu. Kwanza nipe marejeo yako juu ya hiki unachokiandika.

Pili, tunacho kiona angani ni mawingu au mbingu ? Maans mawingu huwa yanatembea, sasa jile kinachobaki huwa ni nini na je kinaonekana au kinyume chake ?

Ila watu mna vituko sana.
Ile ni ozone layer wewe huna uwezo wa kuona umbali mrefu kiasi hicho. Ile ozone layer ni reflection 2 ya mwanga there is nothing. Ungekuwa umewahi tumia telescope nadhani ungeshuhudia.
 
Shirika la Marekani la Utafiti wa Anga (NASA) limesema ndege yake ya utafiti imefanikiwa kutua katika Sayari ya Mirihi (Mars) imefanikiwa kutua salama na kushusha kifaa cha utafiti kilichopewa jina Perseverance katika sayari hiyo nyekundu.

View attachment 1705902

Hii ni hatua mpya katika utafiti wa anga za juu, ambapo kifaa hicho chenye ukubwa unaolingana na gari dogo kitakusanya sampuli za mawe kutoka katika sayari hiyo na kuyaleta duniani kwa mara ya kwanza katika historia ya mwanadamu.

Lengo la kutuma kifaa hicho cha utafiti ni kuangalia uwezekano wa kuwapo uhai katika sayari hiyo ya nne katika Sayari za Mfumo wa Jua, na kitapeleleza kwa muda wa miaka miwili.

Kwa sasa, wahandisi na wafanyakazi wa NASA wanashusha pumzi ya ahueni baada ya chombo hicho kufanikiwa kutua, kwani ni takriban nusu tu ya vyombo vya anga vilivyowahi kutumwa katika Sayari Nyekundu vimefanikiwa kutua salama!

Matokeo ya utafiti utakaofanywa na chombo Perseverance utamsogeza mwanadamu karibu zaidi na lengo la siku moja kuishi katika Sayari ya Mirihi. Licha ya kutumia gharama kubwa ya zaidi ya dola bilioni 3 (Sawa na zaidi ya Tsh. trilioni 6 na bilioni 900), NASA ina matumaini ya kupata matokeo yenye kulingana au zaidi ya thamani hiyo ya fedha kutokana na utafiti huo.

Chombo hicho kimetua karibu na eneo lililopewa jina Kreta ya Jezero, bonde lenye upana wa kilomita 12 lililopo karibu na Ikweta ya sayari hiyo. Eneo hilo linaaminika kuwahi kuwa na mto uliotengeneza delta zaidi ya miaka bilioni 3.6 iliyopita, hivyo kufanya uwezekano wa kuwapo viumbe hai au masalia ya viumbe hai kuwa mkubwa.


Marekani inapewa changamoto na mataifa ya China na Umoja wa Falme za Kiarabu ambao pia wametuma vyombo vyao vya anga katika Sayari hiyo Nyekundu kupeleleza uwezekano wa uwepo wa uhai. Wingi wa shughuli za anga katika sayari hiyo kunaifanya kuwa kitovu cha utafiti wa anga za juu kwa takriban kipindi cha karne ijayo.
Kwa mtu anayefkiria kwa akiri wala sio nyiiiingi kawaida tu, sio wale mashabiki hata wasioelewa wanacho kishabikia, ataona hizi ni polojo muve kbs! Et na picha kabisa zinaonyesha chombo kiki take place ardh ya mars, kweli kilahis hivi!! kwanza hivi nani aliepiga picha? nazipigwe kwa umbali kidogo,ajabu! kuna mengi yakuhoji ntajichosha tu nadhalia za kijinga kbs!
 
Wewe ndo unajibana.
Katika hizo sayari Tisa na dunia ikiwemo.ni moja Tu inayosapoti maisha.
Na hata ukiangalia mizunguko ya hizo sayari kulizunguka JUA.ni wazi dunia ndo ina afaa kuishi
Aliekufahamisha kwamba kuna sayari nyingine japo hazisupport maisha si ndo yupo kutafuta lead ya kupata maisha huko sas unampinga nn? 2litarajia utakuwa unaitafuta hata anga sahv kwenda kuthibitisha.
 
Kuna vitu mi nashindwa kuviamini hasa inapotokea nguvu kubwa yakutaka niamini... sasa hiyo picha kaipiga nani aliyekua katangulia huko chombo kinapotua?
Duu aisee? Yani mpaka leo unaamini picha mpaka akushikie mtu nd ipigwe? Ina maan huna idea yyte kuhusu sensors zinavyofanya kaz
 
Duu aisee? Yani mpaka leo unaamini picha mpaka akushikie mtu nd ipigwe? Ina maan huna idea yyte kuhusu sensors zinavyofanya kaz
sawa mtaalam, kwamaana hiyo hizo sensors ndio zimepiga hiyo picha, how? Tunaoeana elimu tuu. Enhe sensors hiyo ikitangulia au ilikua na chombo au haipo hata eneo la tukio? Msaada tafadhari ewe mtaalamu wa masuala ya upigwaji wa picha.
 
Nilikua nuaulisa Mbinguni ni Sayari ipi au ni mpaka uvuke sayari zote.
 
Huwa nawaona wajinga kwa sababu nyingi sana. Hizi ni miongoni mwazo.

1. Hamjui kuhoji na kutafuta ukweli juu ya habari mnazo zisikia, na hili wahusika wamefanikiwa sana, sababu wameona wengi wenu mnapenda kuona.

2. Hamjibu maswali ninayo wauliza zaisi ya ushabiki kwenye Sayansi.

3. Mnatakiwa kuvunja hoja na kuweka ukweli na si kinyume chake, kama mnavyofanya nyinyi. Mathalani nikikuuliza wewe unahakikisha vipi ukweli wa hizi habari ? Bila shaka kwenu nyinyi mnazipokea tu, hili ni tatizo lenu binafsi na ukameme wenu. Kuna mmoja niliwahi kumuuliza anadai ya kuwa Albart Einstein alikuwa na akili sana, nikamwambia nitajie mambo matano ambayo aliwahi kuyasema au kuyafanyia utafiti halafu yakawa kweli, kisha nikamwambia mimi binafsi Einstein hanifikii kwa akili, na hakuna atakaye weza kuthibitisha ys kuwa Einstein kanizi mimi akili.

4. Huwa mnatatizo au matatizo ya kulinganisha mambo hasa katika kutoa mifano. Mifabo yako yote ni mfu sababu unalinganisha uhalisia na na visivyo halisi, mangapi au vingapi hatujawahi kuvidiriki na tunaviamini ? Achilia mbali tu hapo Marekani. Mimi nina muamini Mtume na yote aliyokuja nayo lakini sijawahi kumuona, tunaamini uwepo wa kina Plato, Socrates, Anaksimenesi na wengine katika Wanafalsafa wa magharibi na wasio kuwa hao, lakini hatujawaona. Sasa mnapokosa hoja bora mnyamaze na mimi na nyinyi tunatofautiana pakubwa sana, mimi natafakari na kuhoji kwa usawa nyinyi ni mashabiki, na wakubwa zenu wanawapa kile mnachokitaka.

Mwisho kabisa nakuuliza swali dogo ambalo wenzako wamelikimbia, wewe umezihakiki vipi hizo habari za kwamba je ni kweli au umetosheka na kusikia au kuona tu ?
Kumbe ndo kilichokuponza wewe unashinda na watu hawajui mambo. Sasa kuna mtu anaejua field ya sayansi vizuri hajui einstein alichokifanya kweli? We umefanya nn ambacho hata kimetatua changamoto za bongo?
 
Naendelea kufurahu na kuwaona hamna mnachokijua, na unachokiandika ni dhana na laiti kama ungekuwa umesoma nilichokiandika usingeandika au kuhoji kitoto namna hii. Nakukumbusha tu japokuwa unadai ya kuwa umesoma nilichokiandika. Nimesema haya yafuatayo :

1. Ukiangalia kwa macho unaona ya kuwa Mwezi upo karibu sana na Mbingu kuliko dunia, nikahoji watuambie umbali halisi bila kuweka "Assumptions" zozote wa duniani mpaka mwezini.

2. Nikasema ya kuwa umbali mbingu moja kwenda mbingu nyingine na kutoka duniani kwenda mbingu ya kwanza kwa mwendo kasi wa juu zaidi ni miaka 500. Sasa kama una akili vizuri na kutafakari utaelewa nini nakusudia.

3. Kupanda ndege hakukufanyi ukajua mbingu iko mbali gani na Sayansi yenyewe haijui, ndiyo maana hata hao NASA wanaendelea kuleta maigizo. Kwahiyo hizi mada zinataka hoja na si viroja na kuimba mapambio.

4. Ninajua ninachokihoji, kama huamini tuendelee na mjadala.
Usichanganye mafile braza. Mbingu na dunia wapi na wapi? Ko unatak kunambia jua ambalo liko umbali mkubwa zaid kuliko mwezi Mungu na malaika wanaliota?
 
Kijana labda nikusaidie kitu kimoja ili usipoteze muda katika hakuna, usiniwekee mambo yenye "Assumptions" weka uhalisia wa mambo, haya mambo nimeishi nayo ila nilipoanza kutafakari kwa usahihi na kuhoji na kusoma vitabu vya wakubwa nikajua ya kuwa huo ni utoto.

Ngoja nikuoe maana tu ya "Assumptions" katika Sayansi hasa fizikia na anga, unapoona "Assumptions" ujue ya kuwa "..wameshindwa kupata jibu sahihi,kwahiyo wanaficha ujinga wao ili hesabu zikubali tu"

Maana yake wangekuwa wanajua hakika ya mambo wasingeweka "Assumptions". Sasa huu utoto usiulete kwangu.
Yani wewe ungezaliwa kipindi kile cha malaika waliozaa na binadamu huenda ungewaabudu wale. We unataka binadamu wenzio wajifanye Miungu kila ki2 wajue kinachofuata nd shida hyo.
 
Back
Top Bottom