mamayeyo
Senior Member
- Apr 4, 2012
- 167
- 138
Kwa uchungu na masikitikomakubwa nasikia matokeo ya darasa la saba yalirekebishwa ili kufuta aibu kwani wengi walikuwa chini ya wastani unaotakiwa ambao ni 100/250. Habari za kuaminika toka wasahihishaji wa mitihani ya kidato cha pili ni kuwa wanafunzi wengi sana wamekosa wastani unaotakiwa kuingia kidato cha 3 mwakani ambao ni alama 30.
Nahofia kuwa wahusika watataka kuficha hii aibu kwa kuteremsha alama za ufaulu. Chonde chonde msifanye hivyo. Hao waliopata wastani wa 30 na kuendelea ndio watakaopambana na kitabu ili walau kupunguza division zero mwaka 2014. Na hao waliofeli na kurudia kidato watapambana zaidi na hatimaye pumba itachekechwa na mchele mzuri utabaki. Mimi nina hakika hao waliochakachua matokeo ya darasa la saba watachakachua na ya kidato cha pili pia. Nani anabisha?
Nahofia kuwa wahusika watataka kuficha hii aibu kwa kuteremsha alama za ufaulu. Chonde chonde msifanye hivyo. Hao waliopata wastani wa 30 na kuendelea ndio watakaopambana na kitabu ili walau kupunguza division zero mwaka 2014. Na hao waliofeli na kurudia kidato watapambana zaidi na hatimaye pumba itachekechwa na mchele mzuri utabaki. Mimi nina hakika hao waliochakachua matokeo ya darasa la saba watachakachua na ya kidato cha pili pia. Nani anabisha?