Chongolo: Kwa Afrika Mashariki, nchi ambayo haina mzigo wa mikopo kuliko nyingine zote ni Tanzania

Chongolo: Kwa Afrika Mashariki, nchi ambayo haina mzigo wa mikopo kuliko nyingine zote ni Tanzania

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Chongolo.jpg
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimesema Tanzania haina mzigo wa mikopo ikilinganishwa na nchi nyingine za Afrika Mashariki na kusema hakuna nchi duniani isiyo na mikopo. Katibu Mkuu wa CCM, Daniel Chongolo amesema baadhi ya watu wanapiga kelele kuwa Tanzania inakopa na akasema katika nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Tanzania ni nchi pekee isiyo na mzigo wa mikopo.

Chongolo aliyasema hayo wilayani Iramba akiwa katika ziara ya siku sita mkoani Singida akifuatana na Sekretarieti ya CCM kukagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya 2020-2025 na kuzungumza na wananchi. “Wapo baadhi ya watu wanakaza nyuso na shingo zao kutaka kuonesha nchi hii inakopa sana, niwaambie tu katika nchi za Afrika Mashariki, nchi ambayo haina mzigo wa mikopo kuliko zingine zote ni Tanzania,” alisema Katibu Mkuu wa CCM.

Chongolo alisema hakuna nchi duniani ambayo haikopi, akitoa mfano kuwa hivi karibuni Marekani ilikopa kwa China ili mambo yake yatatuliwe. “Wote mnajua Marekani ndo dunia nyingine, nendeni mkaangalie mjiridhishe mimi ni kiongozi mkuu wa chama siwezi danganya, nimetaja kwa jina kwa sababu ni ukweli, hapa kuna mtu hajui kukopa? Kuna mtu amewahi kufa kwa kukopa?” Alihoji Chongolo. Alisema mtu asiyetaka maendeleo hutengeneza mazingira ya kujifunga kama kisiwa na kusisitiza nchi zote zinakopa.


Chanzo: HabariLEO
 
kwani ni Mashindano?

... nani atashinda?
Ila tu...
Wasisahau, tunajua kukopa sio shida. Shida ni, nani mwenye mzigo wa kulipa! Wao wakiondoka madarakani wanavitita vyao, ziwe zimelipwa au lah!

Unyonge saa nyingine, yaani anatupumulia shingoni!
 
Maelezo meeengi kuhalalisha kushindwa kwao
 
Kumbe kulikuwa na mashindano ya kukopa pesa?🤣🤣🤣😍
 
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimesema Tanzania haina mzigo wa mikopo ikilinganishwa na nchi nyingine za Afrika Mashariki na kusema hakuna nchi duniani isiyo na mikopo. Katibu Mkuu wa CCM, Daniel Chongolo amesema baadhi ya watu wanapiga kelele kuwa Tanzania inakopa na akasema katika nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Tanzania ni nchi pekee isiyo na mzigo wa mikopo.

Chongolo aliyasema hayo wilayani Iramba akiwa katika ziara ya siku sita mkoani Singida akifuatana na Sekretarieti ya CCM kukagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya 2020-2025 na kuzungumza na wananchi. “Wapo baadhi ya watu wanakaza nyuso na shingo zao kutaka kuonesha nchi hii inakopa sana, niwaambie tu katika nchi za Afrika Mashariki, nchi ambayo haina mzigo wa mikopo kuliko zingine zote ni Tanzania,” alisema Katibu Mkuu wa CCM.

Chongolo alisema hakuna nchi duniani ambayo haikopi, akitoa mfano kuwa hivi karibuni Marekani ilikopa kwa China ili mambo yake yatatuliwe. “Wote mnajua Marekani ndo dunia nyingine, nendeni mkaangalie mjiridhishe mimi ni kiongozi mkuu wa chama siwezi danganya, nimetaja kwa jina kwa sababu ni ukweli, hapa kuna mtu hajui kukopa? Kuna mtu amewahi kufa kwa kukopa?” Alihoji Chongolo. Alisema mtu asiyetaka maendeleo hutengeneza mazingira ya kujifunga kama kisiwa na kusisitiza nchi zote zinakopa.


Chanzo: HabariLEO
Akawaulize hao walio kopa sana kama wana raha zaidi ya ugumu wa maisha.
 
Back
Top Bottom