saidoo25
JF-Expert Member
- Jul 4, 2022
- 624
- 1,456
Katibu Mkuu wa CCM, Ndg. Daniel Chongolo amekunuliwa akionyesha kutoridhishwa na utendaji kazi wa Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe ambaye ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi.
Kwa ambao hamfahamu masuala ya CCM Bashe ndani ya Chama ni Kiongozi mkubwa kuliko Chongolo na anaweza kuendesha kampeni ya kuungana na WANEC wenzake kuishauri Kamati Kuu kutengua uteuzi wa Chongolo.
Watu wengi wamelalamikia maagizo hayo ya Chongolo kwa Bashe na wengine wakaenda mbali zaidi na kusema mawaziri wanaoongoza kwa kulalamikiwa na wananchi kwa utendaji usioridhisha ni watu wa karibu sana na Chongolo na ndio wanaotajwa kumuweka kwenye hiyo nafasi ya KM- CCM ili kulinda maslahi yao.
Mawaziri hao ni pamoja na Bashe, Januari Makamba, Mwigulu Nchemba na Nape Nauye ambao inatajwa kuwa Chongolo ndio aliwasimamia kuhakikisha vikao vya maamuzi ya Chama vinawateua majina yao na kusimamia kuhakikisha wanashinda nafasi hizo.
Leo Chongolo anapata wapi uhalali wa kulalamikia utendaji wa Waziri Bashe ikiwa wakati anampigania kuingia NEC alikuwa anafahamu watanzania wengi wanamlalamikia kwa kushindwa kudhibiti upandaji wa bei za chakula pamoja na mgogoro wa mbolea za ruzuku.
Kwa ambao hamfahamu masuala ya CCM Bashe ndani ya Chama ni Kiongozi mkubwa kuliko Chongolo na anaweza kuendesha kampeni ya kuungana na WANEC wenzake kuishauri Kamati Kuu kutengua uteuzi wa Chongolo.
Watu wengi wamelalamikia maagizo hayo ya Chongolo kwa Bashe na wengine wakaenda mbali zaidi na kusema mawaziri wanaoongoza kwa kulalamikiwa na wananchi kwa utendaji usioridhisha ni watu wa karibu sana na Chongolo na ndio wanaotajwa kumuweka kwenye hiyo nafasi ya KM- CCM ili kulinda maslahi yao.
Mawaziri hao ni pamoja na Bashe, Januari Makamba, Mwigulu Nchemba na Nape Nauye ambao inatajwa kuwa Chongolo ndio aliwasimamia kuhakikisha vikao vya maamuzi ya Chama vinawateua majina yao na kusimamia kuhakikisha wanashinda nafasi hizo.
Leo Chongolo anapata wapi uhalali wa kulalamikia utendaji wa Waziri Bashe ikiwa wakati anampigania kuingia NEC alikuwa anafahamu watanzania wengi wanamlalamikia kwa kushindwa kudhibiti upandaji wa bei za chakula pamoja na mgogoro wa mbolea za ruzuku.