Chris Brown kuipeleka Warner Bros. mahakamani kwa kuchapisha taarifa za uongo kwenye Documentary ya "Chris Brown: A History of Violence"

Chris Brown kuipeleka Warner Bros. mahakamani kwa kuchapisha taarifa za uongo kwenye Documentary ya "Chris Brown: A History of Violence"

Wild Flower

JF-Expert Member
Joined
Jul 20, 2023
Posts
378
Reaction score
766
Mwanamuziki Chris Brown amewasilisha kesi dhidi ya kampuni ya filamu, Warner Bros. Discovery akiidai kampuni hiyo kiasi cha Tshs. Trilioni 1.2, akidai kwamba kampuni hiyo imechapisha taarifa za uongo na zinazomdhalilisha kupitia "Documentary" ya "Chris Brown: A History of Violence"​

1737555712383.png

Ni baada ya Kampuni hiyo kutoa "Documentary" Oktoba 2024, ikielezea historia ya makosa na mashtaka ya Mwanamuziki huyo, ikijumuisha mashtaka ya Ubakaji aliyofunguliwa Januari 2022.

Katika mashtaka hayo "Breezy" anadaiwa kumdhalilisha kingono Mwanamke mmoja baada kumpa madawa ya kulevya, katika moja ya Sherehe za Sean Combs (P Diddy) mwaka 2020

Aidha, Mwanasheria wa Chris, Levi McCathern amesema "Kesi hii ni kuhusu kulinda ukweli. Licha ya kupewa ushahidi kuwa taarifa hizo si za kweli bado kampuni hiyo iliandaa "documentary" hiyo na kuichapisha kwa makusudi wakifahamu wako kinyume na majukumu yao kama waandishi wa habari."
 
Hao documentary sio wajinga kama Msiba wa Ccm! Na Chris Brown akishinda analogwa, fidia hakuna wakulipwa!
 
Hii inataka ifanane na ile ya "IN THE NAME OF......" ya somebody kaflag...
 
Hao documentary sio wajinga kama Msiba wa Ccm! Na Chris Brown akishinda analogwa, fidia hakuna wakulipwa!
ULaya hamna biashara za kulogwa and other mystical dark wishes
Warner ni kampuni ya muda mrefu sana na maarufu. Brown akishinda atalipwa pesa zake period
 
ULaya hamna biashara za kulogwa and other mystical dark wishes
Warner ni kampuni ya muda mrefu sana na maarufu. Brown akishinda atalipwa pesa zake period

Kwa hiyo you think I was serious? Kweli wewe ni mwehu!
 
Back
Top Bottom