Chris Mugalu simuelewi

Chris Mugalu simuelewi

pwilo

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2015
Posts
10,913
Reaction score
13,876
Habari zenu wakuu,

Mchezo Kati ya SIMBA SC dhidi ya Biashara United umemalizika kwa ushindi mnono baada ya Mnyama kumchakaza mtu kwa jumla ya mabao manne kwa nunge.

Ila Kuna huyu mchezaji mpya wa SIMBA aliyeingia kuchukua nafasi ya kagere naona kama hapa tumeingia Cha kike kwa sababu zifuatazo:-

1. yupo slow Sana -kwa nafasi anayocheza anatakiwa awe na quick movement ndani ya boksi anashindwa hata Luis pamoja na Morrison.

2. hana pressure-ukiangalia anavyo cheza kagere au John boko wapo tofauti Sana na MUGALU akipoteza mpira hakabi Wala hasaidii kutafuta mpira Kama wenzako.

3. goal scoring accuracy - kwa hizi mechi za karibuni nilizomuona jinsi anavyocheza ili afunge haitaji usumbufu wa aina yeyote either awe yeye na kipa au golini kusiwe na kipa he needs improvement.

4. Hana tofauti na hawa ma striker wetu wa bongo -kwa namna anavyocheza anasubiria mpira tu afunge wakati wenzake wanatoa mpaka assist za magoli.

Ni hayo tu wadau Ila ngoja tumpe mda anaweza kubadilika Ila kwa SIMBA Ile asipobadilika atakaa benchi mpaka counter book liishe.

N:B Bwalya ilichukua mechi moja tu kuonyesha ubora wake na kila mtu alikubali kiwango chake Ila MUGALU ananipa wasiwasi.
 
Mugalu.
Mechi mbili, goli mbili...
Ndugu yangu mpira haupo hivyo unavyofikiri...
Quick movements zipi unazosemea? Au ndo bora mradi umechambua?
Leo kapata clear chance moja na goli moja.....
Anaweza asiwe mzuri ila sio kama ulivyochambua wewe.
Wengine ni wachambuzi wa mchele tu mkuu wazoee!
 
Wengine ni wachambuzi wa mchele tu mkuu wazoee!
Mi sio mchambuzi nimetoa tu maoni na ww una ruhusiwa kuweka ya kwako bila kumtukana ama ku mkejeli mtu yeyote maana hili ni jukwaa huru mkuu
 
Mugalu.
Mechi mbili, goli mbili...
Ndugu yangu mpira haupo hivyo unavyofikiri...
Nadhani itakuwa umesoma title tu mkuu hujasoma nilichoandika mkuu kwa umakini
 
Jamaa nimemshangaa ananiambia Mugalu hana accuracy...
Tangu aje kacheza dakika 61 tu na goli mbili ( mechi ya kwanza 45 na hii 16)
Mchezaji mzuri hajifichi anaonekana tu Bwalya alicheza mechi moja tu kila mtu alikubali kiwango chake Ila Yule jamaa anacheza Kama kiungo kumbe striker
 
Habari zenu wakuu,

Mchezo Kati ya SIMBA SC dhidi ya BIASHARA UNITED umemalizika kwa ushindi mnono baada ya Mnyama kumchakaza mtu kwa jumla ya mabao manne kwa nunge...
Nilichogundua ni kua unakariri uchezaji wa watu, yaani wewe unataka acheza ka anavyocheza boko au kagere, ungekua na jicho la kuangalia kiufundi ungezugumzia ubora wake kwenye timu kuliko kuangalia acheze ka mtu flani acheze
 
He is a bull striker, he needs a time to cope with the teammates and playing styles of Simba Sc
 
Jinsi alivyopiga mpira na kufunga goli, ni kuonesha kuwa yeye ni mfungaji mzuri. Ndemla au Boko angeweza kuupeleka nje ya goli.
Kaunyoosha mpira down post, Pale anamfunga hata golikipa wa Bayen Munchen ya Ujerumani.

Ule mpira unapigwa na wajuzi tu, Kuhusu kasi, kocha wa viungo nadhani Ameliona hilo na atalifanyia kazi.

Pongezi Kwako Chris Mugalu.
 
Mbona yuko vizuri uyo jamaa.hao ni wale washambuliaji ambao hawataki mambo mengi uwanjani kazi yake ni kupiga mpira golini tu sio kutafuta mbwembwe na kukurukakara zisizo nalazima.Na namba anayocheza inamruhusu asiwe na mambo labda kama atakua anashindwa kujiposition vizuri.Tumpe muda.
 
Mbona yuko vizuri uyo jamaa.hao ni wale washambuliaji ambao hawataki mambo mengi uwanjani kazi yake ni kupiga mpira golini tu sio kutafuta mbwembwe na kukurukakara zisizo nalazima.Na namba anayocheza inamruhusu asiwe na mambo labda kama atakua anashindwa kujiposition vizuri.Tumpe muda.
ndivyo alivyofanya goli zake 2. atapokea anapiga. Hata jana kuna goli alikosa kwa kukutana na kipa,alipokea akasogeza kipa akamuwahi. Huyu ni striker
 
Back
Top Bottom