Chuki inakudhuru wewe mwenyewe

Chuki inakudhuru wewe mwenyewe

Etugrul Bey

JF-Expert Member
Joined
Aug 6, 2020
Posts
6,514
Reaction score
15,247
Utamsikia mtu anasema "hakika namchukia mtu fulani yaani sitaki hata kumwona "

Huyu hajui kuwa anajidhuru yeye mwenyewe,,, kwanza anaishi na nguvu hasi ambazo zina mwangamiza na kumtafuna yeye binafsi.

Hivi umeshawi kuwaona watu ambao wana roho ya korosho au kwa maana nyingine roho mbaya, hawa mara nyingi huwa wamenyauka kutokana na roho mbaya,, si kila mtu mwembamba ana roho mbaya hapana, ila wembamba wa watu hawa huwa tofauti sana kwakuwa wanatafunwa na nguvu hasi nyingi hivyo hukosa hata nuru.

Wewe unayeendekeza chuki tambua unajidhuru wewe mwenyewe kwakuwa kila utapokutana na yule unaye mchukia basi chuki inadhidi na kuzalisha kemikali mwilini mwako ambazo zinakudhuru wewe mwenyewe, na istoshe unakosa raha na amani moyoni mwako.

Na kibaya zaidi huyo unayemchukia haathiriki kama wewe kwakuwa yeye amekubali kuwa unamchukia na anaendelea na maisha yake,,, unabaki wewe unajishughulisha kwa kutaka kumuona anaharibikiwa, anaanguka na kupata madhira mbali mbali na kuanguamia,,, usichojuwa baraka zinatoka kwa Mwenyezi Mungu na humbariki amtakaye bila hesabu

Jifunze kuishi bila chuki hata vitabu vya dini vinasisitiza sana kusameheana na kugawa love kwa binadamu wenzetu.

Kwani asiye msamehe mwanadamu mwenzake hata huyo aliye juu zaidi na ambaye ni mkuu hatokusame pia.

Upendo ni nuru, upendo ni amani, upendo ni furaha, kuwa huru kwa kuepukana na chuki,,, siku zote chagua tabasamu.

Ni hayo tu!
 
Chuki lazima ziwepo na hauwezi kupenda au kupendwa na Kila MTU ...

Harafu Hakuna uhusiano WA kuwa mwembamba na kuwa na chuki ...

Unene Ni ugonjwa mtupu ndio maana Hakuna billionaire mnene hapa Duniani ...

Na Hakuna binadamu mwenye Akili timamu mnene ...
 
 
Chukua lazima ziwepo na hauwezi kupenda au kupendwa na Kila MTU ...

Harafu Hakuna uhusiano WA kuwa mwembamba na kuwa na chuki ...

Unene Ni ugonjwa mtupu ndio maana Hakuna billionaire mnene hapa Duniani ...

Na Hakuna binadamu mwenye Akili timamu mnene ...
Chief kama umekurupuka hivi,,, sijasema kila mtu mwembamba ana chuki
 
Ukiwa mvivu utaanza kuwa na wivu,, ukianza kuwa na wivu utaanza kuwa na makasiriko mda wote kwa sababu WIVU +UVIVU= MAKASIRIKO.

Ukianza kuwa na Makasiriko unaanza kuwa na Roho mbaya, ukianza kuwa na roho mbaya, unaanza kuwa na roho ya kukunja, sasa hapa unakuwa umefika stage mbaya kwa sababu utakuja kuwa MCHAWI MIXER MWANGA 😁😁
 
Ukiwa mvivu utaanza kuwa na wivu,, ukianza kuwa na wivu utaanza kuwa na makasiriko mda wote kwa sababu WIVU +UVIVU= MAKASIRIKO.

Ukianza kuwa na Makasiriko unaanza kuwa na Roho mbaya, ukianza kuwa na roho mbaya, unaanza kuwa na roho ya kukunja, sasa hapa unakuwa umefika stage mbaya kwa sababu utakuja kuwa MCHAWI MIXER MWANGA 😁😁
Nimeipenda hii
 
Chuki lazima iwepo ,hapa Duniani kama wote tukipendana harafu iweje sasa ?

Chuki ndio inafanya watu kuendelea kupambana na kujituma ...

Kukataliwa au kuchukiwa na kundi la watu ndio kunafanya watu wanakuwa wabunifu katika maisha Kwa kutafuta Namna nyingine ya kuishi ...

Chuki ndio inaleta maendeleo ...

Chuki ndio inafanya Dunia inazunguka ...

Maisha Bila kuchukiana hayana maana ,Ni sawa useme tuishi hapa Duniani Bila kuwa na changamoto yeyote yaani Kila kitu kiwe poa tu ...haiwezekani kamwe [emoji23]
 
Chukua lazima ziwepo na hauwezi kupenda au kupendwa na Kila MTU ...

Harafu Hakuna uhusiano WA kuwa mwembamba na kuwa na chuki ...

Unene Ni ugonjwa mtupu ndio maana Hakuna billionaire mnene hapa Duniani ...

Na Hakuna binadamu mwenye Akili timamu mnene ...
🤣🤣 mbona kama umekwazika?
 
Chuki lazima iwepo ,hapa Duniani kama wote tukipendana harafu iweje sasa ?

Chuki ndio inafanya watu kuendelea kupambana na kujituma ...

Kukataliwa au kuchukiwa na kundi la watu ndio kunafanya watu wanakuwa wabunifu katika maisha Kwa kutafuta Namna nyingine ya kuishi ...

Chuki ndio inaleta maendeleo ...

Chuki ndio inafanya Dunia inazunguka ...

Maisha Bila kuchukiana hayana maana ,Ni sawa useme tuishi hapa Duniani Bila kuwa na changamoto yeyote yaani Kila kitu kiwe poa tu ...haiwezekani kamwe [emoji23]
Utakubaliana na mm kwamba kutokana na comment yako,,,, kwamba mwenye kuchukiwa ndio anaweza kufanikiwa na kusonga mbele

Kwahiyo unakubaliana na mm kwamba mwenye kuchukia wengine ndio mhanga
 
Chuki lazima iwepo ,hapa Duniani kama wote tukipendana harafu iweje sasa ?

Chuki ndio inafanya watu kuendelea kupambana na kujituma ...

Kukataliwa au kuchukiwa na kundi la watu ndio kunafanya watu wanakuwa wabunifu katika maisha Kwa kutafuta Namna nyingine ya kuishi ...

Chuki ndio inaleta maendeleo ...

Chuki ndio inafanya Dunia inazunguka ...

Maisha Bila kuchukiana hayana maana ,Ni sawa useme tuishi hapa Duniani Bila kuwa na changamoto yeyote yaani Kila kitu kiwe poa tu ...haiwezekani kamwe [emoji23]
Umeelewa lakini ni chuki ya namna gani imezungumziwa na mtoa mada???
 
Na Hakuna binadamu mwenye Akili timamu mnene ...
Dah! 😁😁😁🏃🏿‍♂️🏃🏿‍♂️

Screenshot_20230615_154356_Instagram Lite.jpg
 
Utakubaliana na mm kwamba kutokana na comment yako,,,, kwamba mwenye kuchukiwa ndio anaweza kufanikiwa na kusonga mbele

Kwahiyo unakubaliana na mm kwamba mwenye kuchukia wengine ndio mhanga
Mzee siku zote Sifu anayekukimbiza pia ....

Bila Huyo kukuchukua usingekuwa na ubunifu na Akili ya kiupambanaji kukuijia mwilini mwako ...

Yule anayekuchukuia na yeye kuna watu wanamchukia na anapambana ....circle ina endelea hivo ...na Dunia ndio ilivo
 
Back
Top Bottom