Chumaulete kwenye Tigopesa; namshindaje huyu adui?

Chumaulete kwenye Tigopesa; namshindaje huyu adui?

WEKA NDIMU NA KIPANDE CHA MKAA KWENYE SANDUKU LA KUTUNZIA PESA
 
Nicheki hapa nikupe maujanja kwenye hii kazi mwaka 4 ungekuwa huku. Kijijin. Ungelia mkuu hali mbay sana nichek hapa. 0764616353
 
Pole. Tafuta mtu anayefanya kazi ya cashier bank akwambie jinsi ya kutatua hizo changamoto maana hata hao watu wa benki huwa wanakutana na hii kitu.
 
Ni umakini tu ndugu yangu, kama huna vile vitabu vyao vya tigo, tengeneza chat yako nzuri yenye jina la anayetuma au kutoa, kiasi namba yake ya simu ionyeshe kama anaweka au kutoa, ukiweza kuijaza hiyo chat kila siku itakusaidia atakama utakosea kwenye namba kurekebisha ni rahisi sana
 
Hakuna chuma ulete wala kuni ulete hapo, kichwa chako kinawaza ushirikina tu na hili jambo ndio linafanya wengi wafeli!
Na usipochunga, utadanganywa na utafilisiwa mtaji wako wote na atakayekuambia atakusaidia hayo machumaulete usemayo!
Acha uzwazwa kuwa makini...
Chuma ulete huijui...
Unafanyia kazi yako wapi?
 
Dawa yake kila ukifanya transaction hesabu pesa zako,uje na mrejesho hapa!
 
Back
Top Bottom