Chunusi: Chanzo, tiba na jinsi ya kuepukana nazo

un



ungefafanua kwanza vitu ulivyotumia ili watu wajue sasa wakushauri utumie nini, maana tunaweza tukakuambia cha kutumia halafu yakawa yaleyale uliyowahi kupitia
 
Acha ama punguza vitu vya sukari na mafuta mf ice-cream karanga chocolate nk
Tumia sabuni ya zoazoa na lotion yake ya ngozi ya mafuta
 
Pia tumia pamba safi kujifuta uso kila siku na epuka nywele kugusa uso wako,pendelea kubana hadi utakapopona
 
Kwanza usiyaminye. USITUMBUE YANAACHA MADOA MEUSI.
1. Punguza kula vyakula vyenye sukari na mafuta kwa wingi.
2. Epuka sabuni au mafuta/ lotion au cream zenye kemikali
3. Usinawe uso kwa maji moto
4. Osha uso kwa limao au paka maji ya limao usoni acha kwa dk 10-15 kisha nawa uso na kupaka lotion baridi (zisizo na kemikali) mf nivea.
5. Fanya scrub ya limao na sukari mara 1 kila baada ya wiki 2. All the best. Nina njia nyingi ila hii naona uanze nayo for quick results.
 
Mimi ziliishaga zenyewe, ila naona tatizo ni kwamba ngozi yenye mafuta huwa inashambuliwa sana na bacteria huvyo huvyo kupelekea hizo chunusi.
Kucontrol hiyo hali jenga utaratibu wa kuosha uso na limao angalau mara mbili asubuhi na jioni, pia si vibaya ukawa na utaratibu wa kunywa juice ya limao ili healing ianzie ndani.

Pia achana na madawa yenye machemical maana yanaongeza tatizo kwa kuua kinga iliyopo katika ngozi hivyo kushindwa kupambana na bacteria katika ngozi yako.
 
Ahsante sn mkuu ntafanyia kaz
 
Nikitumia limao peke ake linanletea vitu vingne vipya kabsa km rashes zlizokomaa, kwa mbali km mba flan hv labda km alivyosema mdau mmoja nichanganye hyo limao na maji.
 
Stress pia hua zinaleta sana chunusi na pia kama hulali vizuri basi ndio kabisa uso hata kuungalia kwenye kioo hutatamani,kunywa maji mengi walau lita 3 kwa siku.
 
Tumia African Black soap, Alata samina. Hizi sabuni ni mwisho wa matatizo ukitaka na smooth finishing tumia unrefined raw Shea Butter. Bidhaa hizi ni Natural na organic na zote zinatoka Ghana. Zina msaada mkubwa. Ukihitaji ni PM
Nimeku-pm hata hujajibu [emoji17] [emoji17]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…