Chuo cha Bagamoyo kimekufa? Wasanii hawakustahili kwenda Korea bali tulihitaji uwezeshaji hapa nchini

Chuo cha Bagamoyo kimekufa? Wasanii hawakustahili kwenda Korea bali tulihitaji uwezeshaji hapa nchini

robbyr

Senior Member
Joined
Apr 8, 2017
Posts
129
Reaction score
221
GRvDHmjXgAELLly.jpeg

Picha: Mtandaoni
Kwa heshima kubwa nampongeza rais na baraza la sanaa kwa kuona kuna kitu tunaweza kujifunza kutoka kwa jamii ya watu wa Korea Kusini

Ila niseme kuwa wizara ya sanaa imeshindwa kutafsiri maono ya rais juu ya sanaa yetu.

Ila wasani hawaendi kujifunza utamaduni wa Korea ili waje kuigiza hapa Bongo. Nahisi wengi watatumia kama sehemu ya kutalii

Limefanyika kosa kupeleka wasani korea bali Serikali ilipaswa kuwekeza kwenye chuo cha sanaa kwa kuajiri wataalamu wa sanaa kutoka korea ambao watafundisha uandishi bora wa stori na kuchukua muvi.

Kazi iwe kwetu kutumia taaluma hiyo kuandika stori zenye ubunifu wa mafunzo kutoka Korea unao akisi utamaduni wetu.

Pia, kuna naona walioenda Korea wengi ni wazee ingali kuna vijana walistahili maarifa hayo ili wawe chachu ya mabadiliko ya sanaa hapa nchini hapakuwa na malengo ya muda mrefu ya baraza la sana au wanataka kumfurahisha rais.

Hivyo, Hakuna haja ya baraza kupeleka wasani Korea bali kuwe na Darasa bora kwenye chuo cha Sanaa Bagamoyo na kuajiri wataalamu toka nchi mbalimbali kama tuna malengo ya muda mrefu wa kukuza sanaa yetu. Na pia watu wasome kwa vitendo na wahitimu

PIA SOMA
- Rais Samia Suluhu awasili nchini Korea Kusini kwa mwaliko wa Rais wa Jamhuri ya Korea, Yoon Suk Yeol
 
Hadi Mtumishi Irene kaenda, mbna mabwakuuu.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Hakuna sanaa zaidi ya watalii waliochoka akili na maisha. Tunahitaji malengo ya muda mrefu na yenye tija. Wameenda kuchezea kodi zetu tu.
 
Back
Top Bottom