KERO Chuo cha Maafisa Tabibu Kilosa na NACTVET kimeshindwa kuwapa vyeti wanafunzi waliounguliwa na vyeti vyao mwaka 2019

KERO Chuo cha Maafisa Tabibu Kilosa na NACTVET kimeshindwa kuwapa vyeti wanafunzi waliounguliwa na vyeti vyao mwaka 2019

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

christophermmassi

New Member
Joined
Jul 8, 2024
Posts
3
Reaction score
3
Mwaka 2019 chuo chetu kilipata janga la kuungua moto na Vyeti vyetu wanafunzi wahitimu 43 vikaungua, Tangu wakati huo tumepata usumbufu wa kutopata vyeti vyetu kutoka Chuo na NACTVET huku wote wakirushiana mpira kwa kusema ni uzumbe wa mwingine mpaka sasa sisi kutokupata vyeti vyetu.

Tunaomba JamiiForums kusaidia wadau mbalimbali kutoa mchango wao wa mawazo na ikiwezekana kama kuna msaada tunaweza kupatiwa kwani tunapitia changamoto ya kukosa ajira serikali na hata kwenye sekta binafsi kwani tunakosa sifa kutokana na kukosa vyeti.

Kilosa.png

Asante.


UFAFANUZI WA NACTVET
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Masoko wa Baraza la Taifa la Elimu ya ufundi na mafunzo ya ufundi stadi (NACTVET), Jeff Shellembi anafafanua:

Mawasiliano baina ya Chuo husika na NACTVET yalifanyika. Utaratibu wa vyeti vya wahusika unafanyika. Jambo hili litakamilika karibuni na wahusika watapewa vyeti vyao kwa utaratibu uliwekwa.
 
Aisee kama viliungua kabla ya kukabidhiwa basi ni haki yenu kupatiwa vipyaaaaa
 
Watumishi wasio wajibika ndio mzigo wa taifa hasa katika maendeleo ya wananchi. Mawaziri wenye dhamana inabidi wawachukulie hatua za kinidhamu watendaji hao maana ndio watakao mharibia sifa nzuri Rais katika utendaji wake
 
Poleni sana, miaka 5 imepita mkiwa hamjui hili wala lile.
 
Tumeteseka sana na hili hakuna ambaye alikuwa tayari kutusaidia asanteni sana Jamii forum kwa kutusaidia kufuatilia hilii kweli mnamchàngo mkubwa kwenye maendeleo ya jamii ýetu.
 
wanataka muwe wezi et mkiwa wezi tena hao hao ndo wanakuwa wa kwanza kuwahukim kumbe sabab ni wao hili swala wanatakiwa wawajibike ipsavyo usilete ujanja nchi hii imekaa kiwiz wiz tu wanatafuta lushwa tu hapo
 
Kwanza nawashukuru sana Uongozi wa JamiiForums katika kulisimamia hili. Na Pili, Naomba tushirikiane kupaza SAUTI KUU kwani sio Chuo hicho tu kuna na vingine vingi na hasa Chuo Cha Kibosho (Kibosho Institute of Health and Allied Sciences=KIBIHAS) zamani kilijulikana kama Kibosho School of Nursing kabla ya kupandishwa hadhi. Sisi wahitimu wa tangu 2018 hatujapewa vyeti vyetu, pamoja na kufuatilia mpaka kwa Katibu Mkuu Wizara ya Elimu kwa barua na mdomo lakini wapi tunaambulia majibu ya maneno tupu hivyo kuishia kukosa msaada na kupata mkwamo katika Soko la Ajira. NAOMBA MSAADA TUPAZE SAUTI ILI WAHUSIKA WAWAJIBIKE JAMANIII. Ahsanteni.
 
Mwaka 2019 chuo chetu kilipata janga la kuungua moto na Vyeti vyetu wanafunzi wahitimu 43 vikaungua, Tangu wakati huo tumepata usumbufu wa kutopata vyeti vyetu kutoka Chuo na NACTVET huku wote wakirushiana mpira kwa kusema ni uzumbe wa mwingine mpaka sasa sisi kutokupata vyeti vyetu.

Tunaomba JamiiForums kusaidia wadau mbalimbali kutoa mchango wao wa mawazo na ikiwezekana kama kuna msaada tunaweza kupatiwa kwani tunapitia changamoto ya kukosa ajira serikali na hata kwenye sekta binafsi kwani tunakosa sifa kutokana na kukosa vyeti.


Asante.


UFAFANUZI WA NACTVET
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Masoko wa Baraza la Taifa la Elimu ya ufundi na mafunzo ya ufundi stadi (NACTVET), Jeff Shellembi anafafanua:

Mawasiliano baina ya Chuo husika na NACTVET yalifanyika. Utaratibu wa vyeti vya wahusika unafanyika. Jambo hili litakamilika karibuni na wahusika watapewa vyeti vyao kwa utaratibu uliwekwa.
Asante kwa ufafanuzi tunaomba mwaka huu mtu kumbuke vijana wenu usipite mwaka huu tena
 
Kero: Habari za Leo! Mimi ni mdau wa
Mwaka 2019 chuo chetu kilipata janga la kuungua moto na Vyeti vyetu wanafunzi wahitimu 43 vikaungua, Tangu wakati huo tumepata usumbufu wa kutopata vyeti vyetu kutoka Chuo na NACTVET huku wote wakirushiana mpira kwa kusema ni uzumbe wa mwingine mpaka sasa sisi kutokupata vyeti vyetu...
Habari za wakati huu! Mimi ni mdau wa jamii Forum tarehe 9 July mwaka huu nilandika kero yangu kuhusu kukosa vyeti vyetu tukiwa wahitimu wa chuo cha kilosa COTC karibia wahitimu 43 hivi. Sasa kero ile tunashukuru uliweza kuipost kwenye mjadala na mtandao wa Facebook na tunashukuru kwa kulitafutia ufafanuzi zaidi kutoka kwenye ngazi zinazohusika na jambo hilo.

Kero: yangu bado ipo pale pale kwani mamlaka husika za NACTVET zilisema taarifa rasmi za kuungualiwa kwa vyeti wanazo na walikuwa kwenye hatua ya kushughuliki hilo lakini bado tupo gizani kwa bado tukiuliza kuhusu vyeti vitakuwa tayari lini bado tunapewa majibu yale yale ambayo tumekuwa tukipewa sikuzote mwaka wa 6 huu na mamlaka hizo, chuo wanasema hawana taarifa zozote kutoka baraza huku baraza NACTVET wakisema nao taarifa rasmi zipo Chuoni na wanafanya mawasiliano nao..kwa hiyo tunaishia kusubiri tu mpaka mienzi siku na miaka inasongaa tulikuwa tunaomba kupatiwa ufafanuzi wa kutosha vyeti vitatoka rasmi lini na kama kuna kitu kinachelewesha visitoke tuambiwe shida ni nini. Hilo litasaidia kwa wale ambao wameahaajiriwa kwenye sekta binafsi kuwapa waajiriwa wao taarifa rasmi lakini pia kwa wale ambao bado hatujaajiriwa kujua hatma rasmi ya vyeti vyetu itakuwa lini maana tuna taarifa za tangu mwaka jana mwezi Decemba kutoka chuoni kuwa taarifa zote za msingi zilishawasilishwa NACTVET kuhusu vyeti vilivyoungua na wakatuambia vitakuwa tayari karibuni, lakini leo ni karibia mwaka unaenda bado taarifa wanazotupa ni zile zile za kuturidhisha ilihali hazina matokeo yoyote.

Ombi letu tunaomba wadau wote waone hili na kama kuna taasisi za juu zinazoweza kutusaidia tutashukuru sana maana tumekuwa tukizungushwa na maneno ya kwamba subirini vyeti vitatoka karibuni tangu mwaka 2020 mpak leo bila matokeo yeyote.

Asante kwa muitikio mzuri kwa Kero iliyopita ni matumaini yangu hii pia mtaipa uangalifu.

Nimeambatanisha na barua iliyopostiwa wizara ya afya mwaka 2023 mwezi Aprili kutoka chuoni kuhusu kuungua kwa vyeti vyetu kuonyesha kwamba muda wa kusubiria kwetu umekuwa sio suluhisho kuna cha ziada kinachokwamisha kupatikana kwa vyeti vyetu.

Tunaomba ufafanuzi zaidi kwa taasisi husika zaidi ya kutuambia SUBIRINI TU VYETI VITAKUWA TAYARI KARIBUNI Tunatakwa watuambie lini vitakuwa rasmi
 
Back
Top Bottom