Ukwaju
JF-Expert Member
- Oct 19, 2010
- 13,383
- 11,197

ilishakuja thread hapa JF kuwa IT ya Chuo hiki haiko makini hasa katika kutoa Matokeo ya Wanachuo
Leo nimeamini kabisa kwani, matokea yanatoka mara mbilimbili licha ya kutanguliwa na Supplimentary zilizokuwa na utata
Yaani Mwanangu kaandikiwa SUPP 2 kwenye Mtandao baada ya kufika Chuoni kakuta SUPP 4 na kuingia kwenye Mtandao ni kweli 4
Leo matokeo wanatoa kwenye link 2 Namba za watahiniwa zilezile lakini matokeo ni tofauti
Tafadhalini MUJIHADHARI watoto wetu wakichukua uamuzi kama wa wale wa Form 4, kuambiwa wamefeli Div. 0 wakajiua baadaye mnarekebisha kuwa marehemu alikuwa na Div III ni UUAJI ambao maliopo yake sio hayo ya kumtoa Ndalichako Baraza la Mitihani, au Waziri wa Elimu kutojiuzulu
Annual Examination Results for Finalist 2012/2013
Annual Examination Results for Continuing Students 2012/2013
SASA NI IPI iko sahihi
Update:
Kuhusu hayo matokeo nimeshafahamishwa kumbe ni namba zinafanana za mitihani kuanzia Diploma hadi Certificate km upo Dip kwa Namba IRDP/DDP/EX 2700 na Certificate ni IRDP/CRP/EX 2700
Na kwa vile malalamiko yalishatolewa kuhusu ukamilifu wa huo utaratibu wao wa IT ndio nikasema wangeanza kurekebisha mitindo yao hakuna sababu ya kuzirejea namba
SAMAHANINI KWA USUMBUFU