Katika hali ya kusikitisha sisi wanachuo wa chuo cha Butimba TTC Tumenyimwa hela kwa ajili ya kununulia vifaa kwenye Mafunzo kwa vitendo(BTP).Pesa tayari zilikuwa zimeshatolewa na wizara ya elimu na kila tunapofuatilia tunatishiwa kufukuzwa chuo.Wenzetu wa mwaka wa 2 kipindi wanaondoka hawakuambiwa juu ya uwepo wa pesa hizo kiasi cha kutufanya tuamini hatutopewa pesa hiyo.Na hivyo ndivyo ilivyokuwa mpaka tunaondoka hatukupewa kabisa. Sisi wanachuo tunamuomba waziri mwenye dhamana na wizara ya Elimu atusaidie kupata hela zetu kwa ajili ya kununulia vifaa kwa ajili ya kufundishia