Chuo cha Ustawi wa Jamii: Wanafunzi wanachagua wenyewe kusoma asubuhi au Mchana, tunawashauri wakae karibu na Chuo

 Chuo cha Ustawi wa Jamii: Wanafunzi wanachagua wenyewe kusoma asubuhi au Mchana, tunawashauri wakae karibu na Chuo

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Salaam,

Baada ya Mdau wa JamiiForums kulalamikia Ratiba ya Masomo ya Chuo cha ustawi wa jamii Kwamba Wanafunzi wanasoma hadi hadi saa 4 usiku kitu ambacho ni hatari kwa usalama wa wanafunzi, Chuo kimetoa Ufafanuzi.

Katia taarifa yao wameeleza hivi;

Tarehe 3 Novemba, 2024 ilisambaa taarifa katika mitandao ya kijamii yenye kichwa cha habari "Ratiba ya Masomo hadi saa 4 usiku Chuo cha ustawi wa jamii ni hatari kwa usalama wa wanafunzi".

Tunapenda kutoa ufafanuzi wa jambo hilo kwamba, upangaji wa ratiba ya masomo katika Chuo cha Ustawi wa Jamii unafanyika kwa kuangalia vigezo mbalimbali kama vile idadi ya wanafunzi katika programu husika na ukubwa wa vyumba vya mihadhara. Kutokana na idadi ya wanafunzi kuongezeka mwaka hadi mwaka, programu zenye wanafunzi wengi hulazimika kugawanywa katika makundi mawili au zaidi ili waweze kutosha katika vyumba vya mihadhara vilivyopo.

Katika mgawanyo huo wa makundi, baadhi ya wanafunzi huanza vipindi vyao mapema saa moja asubuhi na kumaliza wakati wa mchana. Makundi mengine huanza vipindi wakati wa mchana na kumaliza kati ya saa 12 jioni na saa nne usiku. Aidha, ieleweke kwamba mwanafunzi yeyote anakuwa huru kuchagua kuwa kwenye kundi la wale wanaoanza vipindi mapema asubuhi au wale wanaoanza vipindi vyao baadae mchana.

Kwa hiyo katika muktadha huo, kusoma vipindi vinavyoanza asubuhi au mchana ni uchaguzi wa mwanafunzi mwenyewe na Chuo kimekuwa na utaratibu wa kuwashirikisha wanafunzi kila rasimu ya ratiba ya masomo inayoandaliwa. Vilevile kwa wanafunzi wanaoishi mbali na eneo la Chuo, wamekuwa wakishauriwa kutafuta makazi karibu na Chuo ili waweze kuhudhuria vipindi mbalimbali vya masomo yao kwa ufanisi.

Hivyo, tunapenda kuujulisha Umma kwamba taarifa iliyotolewa ni ya upotoshaji na haina mantiki kwa vile utaratibu huu umekuwa ukifuatwa na vyuo mbalimbali hapa nchini.

Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano na Masoko
Ustawi.jpg
 
Ni vema mtu asijidahili katika programu ambayo muda wake wa mafunzo hawezi kuuhimili.
 
Watoto wetu( hasa wa kike)wanapitia mazingira magumu sana kwenye elimu yetu ya Tanzania
 
Kwa maana hiyo idadi ya wanafunzi inaongezeka, ila miundombinu iko vilevile! Hapo wakubali tu wanakosea. Saa nne usiku siyo muda rafiki kwa mwanafunzi kumaliza vipindi. Kwa level yao walitakiwa kuishia muda wa saa 12 au saa 1 jioni.
 
Salaam,

Baada ya Mdau wa JamiiForums kulalamikia Ratiba ya Masomo ya Chuo cha ustawi wa jamii Kwamba Wanafunzi wanasoma hadi hadi saa 4 usiku kitu ambacho ni hatari kwa usalama wa wanafunzi, Chuo kimetoa Ufafanuzi.

Katia taarifa yao wameeleza hivi;

Tarehe 3 Novemba, 2024 ilisambaa taarifa katika mitandao ya kijamii yenye kichwa cha habari "Ratiba ya Masomo hadi saa 4 usiku Chuo cha ustawi wa jamii ni hatari kwa usalama wa wanafunzi".

Tunapenda kutoa ufafanuzi wa jambo hilo kwamba, upangaji wa ratiba ya masomo katika Chuo cha Ustawi wa Jamii unafanyika kwa kuangalia vigezo mbalimbali kama vile idadi ya wanafunzi katika programu husika na ukubwa wa vyumba vya mihadhara. Kutokana na idadi ya wanafunzi kuongezeka mwaka hadi mwaka, programu zenye wanafunzi wengi hulazimika kugawanywa katika makundi mawili au zaidi ili waweze kutosha katika vyumba vya mihadhara vilivyopo.

Katika mgawanyo huo wa makundi, baadhi ya wanafunzi huanza vipindi vyao mapema saa moja asubuhi na kumaliza wakati wa mchana. Makundi mengine huanza vipindi wakati wa mchana na kumaliza kati ya saa 12 jioni na saa nne usiku. Aidha, ieleweke kwamba mwanafunzi yeyote anakuwa huru kuchagua kuwa kwenye kundi la wale wanaoanza vipindi mapema asubuhi au wale wanaoanza vipindi vyao baadae mchana.

Kwa hiyo katika muktadha huo, kusoma vipindi vinavyoanza asubuhi au mchana ni uchaguzi wa mwanafunzi mwenyewe na Chuo kimekuwa na utaratibu wa kuwashirikisha wanafunzi kila rasimu ya ratiba ya masomo inayoandaliwa. Vilevile kwa wanafunzi wanaoishi mbali na eneo la Chuo, wamekuwa wakishauriwa kutafuta makazi karibu na Chuo ili waweze kuhudhuria vipindi mbalimbali vya masomo yao kwa ufanisi.

Hivyo, tunapenda kuujulisha Umma kwamba taarifa iliyotolewa ni ya upotoshaji na haina mantiki kwa vile utaratibu huu umekuwa ukifuatwa na vyuo mbalimbali hapa nchini.

Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano na Masoko
Kwa nini isiwe hadi saa mbili usiku siyo saa nne usiku...tatizo la Tanzania ni viongozi wasio na akili ....masaa 6 ya masomo yanatosha sana ki akili mtu kwa siku anaweza kusoma kwa masaa 4 tu bila tatizo hata masomo yawe magumu kiasi gani...hata shule za secondary walitakiwa wasiruhusiwe kwenda shule siku ya jumamosi na jumapili ...kuna faida kubwa sana kielimu na kisaikolojia kupunguza shinikizo (pressure) ya masomo kwa wanafunzi kuliko kuiongeza ....siku mbili kwa week ziwe ni mapumziko kwa shule zote nchini tena iwe ni lazima ....pia NAKUMBUSHA KUONDOSHWA KWA VITU VYOTE VYA KIDINI MASHULENI IKIWEMO HIJABU NA IKABU HAPA SIPEPESI MACHO HATA KIDOGO (TUNAFARAKANISHA TAIFA KUKOSA UMOJA KWA SABABU ZA DINI) wanafunzi watambuane kama wanafunzi siyo kwa dini zao...
 
Jamii yenyewe haina ustawi wowote, hao wanafunzi wanapoteza muda wao
 
Unadahili vipi idadi kubwa ya wanafunzi wakati huongezi majengo.Saa nne usiku muda wa kulala na kujisomea mtu yupo class anapigwa lecture. Tamaa tuu ya pesa.
 
Kumaliza masomo saa nne usiku sio ustawi hii ni sawa na mtoto wa darasa la tatu kwenda shule hadi jumamosi
 
Kwa nini isiwe hsdi saa mbili udiku siyo saa nne usiku...tatizo la Tanzania ni viongozi wasio na akili ....masaa 6 ya masomo yanatosha sana ki akili mtu kwa siku anaweza kusoma kwa masaa 4 tu bila tatizo hata masomo yawe magumu kiasi gani...hata shule za secondary walitakiwa wasiruhusiwe kwenda shule siku ya jumamosi na jumapili ...kuna faida kubwa sana kielimu na kisaikolojia kupunguzs shinikizo (pressure) ya masomo kwa wanafunzi kuliko kuiongeza ....siku mbili kwa week ziwe ni mapumziko kwa shule zote nchini tena iwe ni lazima ....pia NAKUMBUSHA KUONDOSHWA KWA VITU VYOTE VYA KIDINI MASHULENI IKIWEMO HIJABU HAPA SIPEPESI MACHO HATA KIDOGO (TUNAFARAKANISHA TAIFA KUKOSA UMOJA KWA SABABU ZA DINI) wanafunzi watambuane kama wanafunzi siyo kwa dini zao...
Point kubwa sana hii! Masomo ya dini wakutane nayo siku za wikend za mapumziko. Watoto wadogo hadi Jumamosi na Jumapili wako shuleni ni upuuzi huu
 
Kwa nini isiwe hsdi saa mbili udiku siyo saa nne usiku...tatizo la Tanzania ni viongozi wasio na akili ....masaa 6 ya masomo yanatosha sana ki akili mtu kwa siku anaweza kusoma kwa masaa 4 tu bila tatizo hata masomo yawe magumu kiasi gani...hata shule za secondary walitakiwa wasiruhusiwe kwenda shule siku ya jumamosi na jumapili ...kuna faida kubwa sana kielimu na kisaikolojia kupunguzs shinikizo (pressure) ya masomo kwa wanafunzi kuliko kuiongeza ....siku mbili kwa week ziwe ni mapumziko kwa shule zote nchini tena iwe ni lazima ....pia NAKUMBUSHA KUONDOSHWA KWA VITU VYOTE VYA KIDINI MASHULENI IKIWEMO HIJABU HAPA SIPEPESI MACHO HATA KIDOGO (TUNAFARAKANISHA TAIFA KUKOSA UMOJA KWA SABABU ZA DINI) wanafunzi watambuane kama wanafunzi siyo kwa dini zao...
Kwa hiyo wanafunzi wasivae hijabu kwasababu ya dini yao,lakini wenye dini nyingine,siku zao za kuabudu,jumamosi na jumapili,wasiende kwenye masomo.Wataka kujifanya hujui kama Jumamosi na Jumapili,ni siku za Ibada za madhebu,mawili tofauti za dini moja.Ungesem siku pia za ibada za Jumamosi na Jumapili,ziondolewe,Iwekwe jumatatu na Jumanne,kusiwe na masomo,ili kuondoa utofauti wa dini.Na kama mavazi,sio kuondoa hijabu tu,hata mavazi ya nguo fupi na kuwa kichwa wazi,,ni ya dini pia.Kwa hiyo mavazi,ya nguo fupi na kichwa wazi,pia yaondolewe,pia ni mavazi ya dini,na ndio wanao
kwenda nao,kwenye nyumba zao za ibada.Kwa hiyo tuondoe mavazi ya dini zote mbili,na mavazi ya wasio na dini.Halafu useme wavae,mavazi gani.
 
Kwa hiyo wanafunzi wasivae hijabu kwasababu ya dini yao,lakini wenye dini nyingine,siku zao za kuabudu,jumamosi na jumapili,wasiende kwenye masomo.Wataka kujifanya hujui kama Jumamosi na Jumapili,ni siku za Ibada za madhebu,mawili tofauti za dini moja.Ungesemq siku pia za ibada za Jumamosi na Jumapili,ziondolewe,Iwekwe jumatatu na Junanne,kusiwe na masomo,ili kuondoa utofauti wa dini.Na kama mavazi,sio kuondoa hijabu tu,hata mavazi ya nguo fupi na kuwa kichwa wazi,,ni ya dini pia.Kwa hiyo mavazi,ya nguo fupi na kichwa wazi,pia yaondolewe,pia ni mavazi ya dini,na ndio wanaoj
kwenda nao,kwenye nyumba zao za ibada.
Nani kakuambia kuwa siku za mapumziko ni za dini tumia akili hijabu aijaleta uhadilifu wowote mashuleni tena kwa sasa wasichana ni malaya kuliko miaka tuliyo soma sisi ambapo hakukuwa na hizo hijabu ...mimi nimesema wapi kuwa jumamosi na jumapili ni siku za dini ...msingi wangu ni siku mbili za mapumziko....hatutakiwi kuweka siku za mapumziko au za kufunga shule kwa kuangalia dini za watu ...maana huo utakuwa ni udini wenye kuligawa taifa ...na kumbuka kuwa kuligawa taifa ni kufarakana ...na ufalme ulio farakana ni ngumu kusimama..
 
Hapa wanaonekana wakike tu as if wa kiume ni haki yao kupitia hayo mazingira?
Elimu ya tanzania ni ya mazingira magumu regardless jinsia, ni jukumu la mwanafunzi kufunga mkanda
Jaribu kufuatilia uone watoto wakike wanavyokumbana na vibaka usiku wanapotoka shule, wanaporwa simu, laptop nk. Na wanapojaribu kupambana wanaishia kuchomwa visu na kupoteza maisha. Inasikitisha sana
 
Jaribu kufuatilia uone watoto wakike wanavyokumbana na vibaka usiku wanapotoka shule, wanaporwa simu, laptop nk. Na wanapojaribu kupambana wanaishia kuchomwa visu na kupoteza maisha. Inasikitisha sana
Acha ubinafsi kwamba wakiume wao wanastahili?
Tunazungumzia jinsia zote sio kutetea kundi moja kama vile wao ni special sana
 
Jaribu kufuatilia uone watoto wakike wanavyokumbana na vibaka usiku wanapotoka shule, wanaporwa simu, laptop nk. Na wanapojaribu kupambana wanaishia kuchomwa visu na kupoteza maisha. Inasikitisha sana
Wote wanapitia changamoto sawa. Wewe umebebwa na propaganda za mafeminists wa Magharibi.
 
Salaam,

Baada ya Mdau wa JamiiForums kulalamikia Ratiba ya Masomo ya Chuo cha ustawi wa jamii Kwamba Wanafunzi wanasoma hadi hadi saa 4 usiku kitu ambacho ni hatari kwa usalama wa wanafunzi, Chuo kimetoa Ufafanuzi.

Katia taarifa yao wameeleza hivi;

Tarehe 3 Novemba, 2024 ilisambaa taarifa katika mitandao ya kijamii yenye kichwa cha habari "Ratiba ya Masomo hadi saa 4 usiku Chuo cha ustawi wa jamii ni hatari kwa usalama wa wanafunzi".

Tunapenda kutoa ufafanuzi wa jambo hilo kwamba, upangaji wa ratiba ya masomo katika Chuo cha Ustawi wa Jamii unafanyika kwa kuangalia vigezo mbalimbali kama vile idadi ya wanafunzi katika programu husika na ukubwa wa vyumba vya mihadhara. Kutokana na idadi ya wanafunzi kuongezeka mwaka hadi mwaka, programu zenye wanafunzi wengi hulazimika kugawanywa katika makundi mawili au zaidi ili waweze kutosha katika vyumba vya mihadhara vilivyopo.

Katika mgawanyo huo wa makundi, baadhi ya wanafunzi huanza vipindi vyao mapema saa moja asubuhi na kumaliza wakati wa mchana. Makundi mengine huanza vipindi wakati wa mchana na kumaliza kati ya saa 12 jioni na saa nne usiku. Aidha, ieleweke kwamba mwanafunzi yeyote anakuwa huru kuchagua kuwa kwenye kundi la wale wanaoanza vipindi mapema asubuhi au wale wanaoanza vipindi vyao baadae mchana.

Kwa hiyo katika muktadha huo, kusoma vipindi vinavyoanza asubuhi au mchana ni uchaguzi wa mwanafunzi mwenyewe na Chuo kimekuwa na utaratibu wa kuwashirikisha wanafunzi kila rasimu ya ratiba ya masomo inayoandaliwa. Vilevile kwa wanafunzi wanaoishi mbali na eneo la Chuo, wamekuwa wakishauriwa kutafuta makazi karibu na Chuo ili waweze kuhudhuria vipindi mbalimbali vya masomo yao kwa ufanisi.

Hivyo, tunapenda kuujulisha Umma kwamba taarifa iliyotolewa ni ya upotoshaji na haina mantiki kwa vile utaratibu huu umekuwa ukifuatwa na vyuo mbalimbali hapa nchini.

Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano na Masoko
Shule gani usiku? Vunjeni vipindi vya usiku muviache kwa ajili ya Executives siyo kwa ajili ya hao watoto, nyie hamuogopi?
 
Salaam,

Baada ya Mdau wa JamiiForums kulalamikia Ratiba ya Masomo ya Chuo cha ustawi wa jamii Kwamba Wanafunzi wanasoma hadi hadi saa 4 usiku kitu ambacho ni hatari kwa usalama wa wanafunzi, Chuo kimetoa Ufafanuzi.

Katia taarifa yao wameeleza hivi;

Tarehe 3 Novemba, 2024 ilisambaa taarifa katika mitandao ya kijamii yenye kichwa cha habari "Ratiba ya Masomo hadi saa 4 usiku Chuo cha ustawi wa jamii ni hatari kwa usalama wa wanafunzi".

Tunapenda kutoa ufafanuzi wa jambo hilo kwamba, upangaji wa ratiba ya masomo katika Chuo cha Ustawi wa Jamii unafanyika kwa kuangalia vigezo mbalimbali kama vile idadi ya wanafunzi katika programu husika na ukubwa wa vyumba vya mihadhara. Kutokana na idadi ya wanafunzi kuongezeka mwaka hadi mwaka, programu zenye wanafunzi wengi hulazimika kugawanywa katika makundi mawili au zaidi ili waweze kutosha katika vyumba vya mihadhara vilivyopo.

Katika mgawanyo huo wa makundi, baadhi ya wanafunzi huanza vipindi vyao mapema saa moja asubuhi na kumaliza wakati wa mchana. Makundi mengine huanza vipindi wakati wa mchana na kumaliza kati ya saa 12 jioni na saa nne usiku. Aidha, ieleweke kwamba mwanafunzi yeyote anakuwa huru kuchagua kuwa kwenye kundi la wale wanaoanza vipindi mapema asubuhi au wale wanaoanza vipindi vyao baadae mchana.

Kwa hiyo katika muktadha huo, kusoma vipindi vinavyoanza asubuhi au mchana ni uchaguzi wa mwanafunzi mwenyewe na Chuo kimekuwa na utaratibu wa kuwashirikisha wanafunzi kila rasimu ya ratiba ya masomo inayoandaliwa. Vilevile kwa wanafunzi wanaoishi mbali na eneo la Chuo, wamekuwa wakishauriwa kutafuta makazi karibu na Chuo ili waweze kuhudhuria vipindi mbalimbali vya masomo yao kwa ufanisi.

Hivyo, tunapenda kuujulisha Umma kwamba taarifa iliyotolewa ni ya upotoshaji na haina mantiki kwa vile utaratibu huu umekuwa ukifuatwa na vyuo mbalimbali hapa nchini.

Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano na Masoko
Wakiwapa uhuru wanafunzi kuchagua, ina maana wote wakichagua vipindi vya asubuhi maana yake si itabidi chuo kikate kundi hili asubuhi na kundi lile jioni!
 
Jaribu kufuatilia uone watoto wakike wanavyokumbana na vibaka usiku wanapotoka shule, wanaporwa simu, laptop nk. Na wanapojaribu kupambana wanaishia kuchomwa visu na kupoteza maisha. Inasikitisha sana
Man kwamba wanao kabwa na vibaka na kuchomwa visu ni wakike tu?
Wa kiume ahhh, hao watavumilia sababu ni wakiume?
Hii stigma inatoka wapi kwenye jamii hii?
 
Back
Top Bottom